Hivi serikali haioni hawa wanawake wanaocheza Ngoma za Uchi maarufu kama Baikoko?

Sir John Roberts

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
12,835
Reaction score
23,584
Sijui ni Mimi mwenyewe naona au hata nyie watanzania wenzangu.naona hii michezo ya wanawake hasa mabinti wadogo wadogo kucheza Ngoma za Uchi maarufu kama Baikoko mitaani hasa kwa Jiji la daresalam ikizidi kukuwa kwa kasi .
Mkuu wa mkoa yupo , Wakuu wa wilaya wapo na viongozi wote wa serikali wapo wanaangalia.
Hivi ni maadili gani tunaifunza jamii yetu? Naomba serikali kudhibiti hii michezo huu ni upunguwani kabisa kama siyo ufirauni unataka kuzoeleka katika jamii yetu. Inanikera sana hii tabia. Mh waziri muhusika naomba ushughulikie hili suala ASAP
 
Zinachezwa hadharani huku watu wote wakishuhudia au zinachezwa ndani!?

Kama ni hadharani huko mitaani, wakuu wa kamati za ulinzi na usalama za mitaa hawatimizi majukumu yao.
 
Hayo ni mambo binafsi serikali Ina wajibu wakushughulika na Yale matatizo makubwa zaidi Kama ukosefu wa ajira,gharama za matibabu,ugumu wa maisha hayo mambo ya kulinda maadili kwenye michezo ya baikoko yashughulikiwe na watendaji wa kata na wajumbe nyumba kumi
 
Una waonea wivu mzee aya vaa na ww kibwebwe ukazicheze hizo ngoma
 
Kuna mambo hayawezekani kuzuilika, yalikuwepo tangu enzi na enzi.. tuishi navyo tu.. pia inatusaidia madomo zege
 
Mkuu we umeanza kuyaona leo?
Ushenzi huo uliletwa na Mwarabu!
Hautofautiani na vigodoro!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…