Hivi Serikali ina habari juu ya upandaji hovyo ya bei ya vitu?

Hivi Serikali ina habari juu ya upandaji hovyo ya bei ya vitu?

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Nina masikitiko sana kuhusu kupanda hovyo kwa bei ya bidhaa mbalimbali hapa nchini. Nitoe tu mifano michache niliyoyaona.

Kwa siku za karibuni nilikuwa nanunua gesi ya kupikia kilo 15 kwa Tshs.51,000 leo gesi ilipoisha nikaenda kununua na nikaambiwa bei ya gesi ya kilo 15 ni Tshs.59,000.

Sasa ukija kwenye bidhaa za ujenzi ndiyo ngoma nzito. Juzi nimenunua gypsum powder kwa Tshs.28,000 leo nilipoenda kununua kwa mara ya pili nikakutabei yake ni Tshs.32,000. Bei ya nondo, mabati, saruji na bidhaa zingine za ujenzi ndo usiseme.

Hivi Serikali inajua yote haya?. Mzunguko wa fedha haupo kabisa, kila kukicha wananchi wanazidi kuwa masikini. Hivi tukimbilie wapi?.

Na hali hii haina muda mrefu ni kama imeanza miezi miwili iliyopita. Ni wajibu wa Serikali kusaidia wananchi wake.
 
Bei ya gesi ulimwenguni imepanda sana ambayo inatishia sekta mbalimbali kilimo ikiwa kimojawapo. Siku za karibuni kulikuwa na mdau akilalamikia bei ya mbolea hapa jukwaani na kwamba now mfuko wa mbolea umefikia 140,000. Majibu ya hayo panoja na hili la kwako ni kama hapo chini!

 
Kuna mazingira serikali inatakiwa itupe macho yake yote mathalani vifaa na pembejeo za kilimo,vifaa vya ujenzi,bei za mafuta n.k tofauti na kufanya hivyo wenye taifa tutaendelea kuathiriwa pakubwa sana,viongozi wetu ambao pia ndio wawakilishi wetu tunajua baadhi yenu ni ma~economists wazuri na mnatambua TZ ina mixed economic system kwa maana ya kuwa baadhi ya vitu viko under control of the government please fanyeni ku~regurate hayo mambo.
 
watapataje habari za kupanda bei ya bidhaa wakati wao wanajua tuko uchumi wa kati wa viwanda😁 hali ya umasikini imeshuka🙄
 
Nina masikitiko sana kuhusu kupanda hovyo kwa bei ya bidhaa mbalimbali hapa nchini. Nitoe tu mifano michache niliyoyaona. Kwa siku za karibuni nilikuwa nanunua gesi ya kupikia kilo 15 kwa Tshs.51,000 leo gesi ilipoisha nikaenda kununua na nikaambiwa bei ya gesi ya kilo 15 ni Tshs.59,000. Sasa ukija kwenye bidhaa za ujenzi ndiyo ngoma nzito. Juzi nimenunua gypsum powder kwa Tshs.28,000 leo nilipoenda kununua kwa mara ya pili nikakutabei yake ni Tshs.32,000. Bei ya nondo, mabati, saruji na bidhaa zingine za ujenzi ndo usiseme. Hivi Serikali inajua yote haya?. Mzunguko wa fedha haupo kabisa, kila kukicha wananchi wanazidi kuwa masikini. Hivi tukimbilie wapi?. Na hali hii haina muda mrefu ni kama imeanza miezi miwili iliyopita. Ni wajibu wa Serikali kusaidia wananchi wake.
Gas zinapanda kuanzia kesho mkuu leo wamekuonea tu. 15 kg ORYX 59,000 au 58,000 =/
 
Leo nimenunua gas ya Oryx 15 kgs kwaTShs.59,000.
 
Hangaya anasemaje kwanza? Si mfumko wa bei sio mkubwa saannaaaaaaaaa. Pia umaskini umepungua from 28% to 26 [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hii nchi bila kupachimbisha hakuna kitu kitabadilika. Tutaendelea kupigwa na maCCM mpaka tuchakae.
 
Hakuna vitu ambavyo ni mahitaji muhimu ya kila siku kwa Mtanzania vilivyopanda bei
 
Back
Top Bottom