Hivi sifa kubwa ya kuteuliwa na Rais kwenye nafasi za utumishi wa Umma ni kuwa kada kindaki ndaki wa CCM?

Hivi sifa kubwa ya kuteuliwa na Rais kwenye nafasi za utumishi wa Umma ni kuwa kada kindaki ndaki wa CCM?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tumemsikia mara kwa mara Rais Magufuli wakati akihutubia akisema kuwa maendeleo hayana vyama, akimaanisha kuwa serikali yake haina upendelo linapokuja suala la maendeleo ya nchi, kuwa kila mwananchi anayo haki sawa

Lakini, maneno hayo yana tofauti kubwa katika utendaji wake katika uteuzi wake wa nafasi za utumishi wa Umma katika nafasi kama vile maRC's maDC's, maRAS, maDAS, wakurugenzi wa wilaya, pamoja na nafasi zote za uteuzi katika nafasi kubwa za utumishi katika mashirika yote ya Umma, ambapo "qualification no 1" kwake Rais Magufuli, ni lazima uwe kada kindaki ndaki wa CCM.

Hivi Rais Magufuli haoni kuwa anafanya ubaguzi wa waiwazi kabisa, wakati Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, inasema kuwa nchi yetu ina mfumo wa vyama vingi?

Katika Katiba ya nchi inayoainisha hivyo, kwa Rais Magufuli kufanya ubaguzi wa waziwazi kabisa, haoni kuwa kwa kuangalia wale anaowateua katika nafasi hizo, kwa kuangalia uanachama wao wa kindaki ndaki kwa CCM, haoni kuwa anaivunja Katiba hiyo ya nchi?

Nawakaribisha wasomaji tuidadavue mada hii, kwa maslahi mapana ya Taifa hili.
 
Tafuta walipo chadema, wapige mitama na makofi.

Andika makala za kusifu na kuabudi

Uwe na kadi

Korido za chama uwe unapazungukia kila siku.


Mtafute mbowe au sugu au lema umlambe makofi.


Faster sana unakuwa DC
Ni kweli kabisa.

Inashangaza kuona wale ambao ni mabingwa wa kuwatukana wapinzani, ndiyo wanaopewa "priority" ya uteuzi!
 
Tafuta walipo chadema, wapige mitama na makofi.

Andika makala za kusifu na kuabudi

Uwe na kadi

Korido za chama uwe unapazungukia kila siku.


Mtafute mbowe au sugu au lema umlambe makofi.


Faster sana unakuwa DC
Au uache maadili ya kazi yako ugeuke mtu wa kumsifia tu Yesu wa CCM na ku critisize tu wapinzani kama mme wa Zwena Hassan Ngoma.
 
T

Lakini, maneno hayo yana tofauti kubwa katika utendaji wake katika uteuzi wake wa nafasi za utumishi wa Umma katika nafasi kama vile maRC's maDC's, maRAS, maDAS, wakurugenzi wa wilaya, pamoja na nafasi zote za uteuzi katika nafasi kubwa za utumishi katika mashirika yote ya Umma, ambapo "qualification no 1" kwake Rais Magufuli, ni lazima uwe kada kindaki ndaki wa CCM.
acha uongo mleta maada
Anna mugwira alituliwa akowa ACT WAZALENDO KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARIO ,Katambi aliteuliwa kuwa mkuu wa wilta Dodoma akiwa chadema,JULUSI MTATITIRO aliteu;iwa DAS akiwa Cuf nk uongo haukusaidii
 
Umeenda mbaliiii sana mkuu, hat kijiji kikiwa na harufu ya upinzani lazima huduma ya REA iwaruke hawawezi kupata umeme, kule kwa Wahaya alipofika kule wakamuomba Stendi...akawajibu hivi.....mlichagua vibaya....maana pale kuna CHADEMA.....Then unaambiwa Maendeleo hayana chama...chezea mkulu wewe
 
Umeenda mbaliiii sana mkuu, hat kijiji kikiwa na harufu ya upinzani lazima huduma ya REA iwaruke hawawezi kupata umeme, kule kwa Wahaya alipofika kule wakamuomba Stendi...akawajibu hivi.....mlichagua vibaya....maana pale kuna CHADEMA.....Then unaambiwa Maendeleo hayana chama...chezea mkulu wewe
Huu ubaguzi wa Jiwe,umevunja rekodi, kwa vile anawapita marais wote waliomtangulia!

Huwa najiuliza, hivi hayo maeneo ambayo hataki kuyapelekea maendeleo, wananchi wake pia wamekuwa "exempted" kulipa kodi?

Ndipo hapo ninapomuona mkulu, kama vile "upstairs" hayupo sawa
 
acha uongo mleta maada
Anna mugwira alituliwa akowa ACT WAZALENDO KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARIO ,Katambi aliteuliwa kuwa mkuu wa wilta Dodoma akiwa chadema,JULUSI MTATITIRO aliteu;iwa DAS akiwa Cuf nk uongo haukusaidii
Hao uliowataja, wakati wapo ndani ya upinzani, walikuwa viwiliwili vyao vipo upinzani, lakini nlmioyo yao ilikuwa ndani ya CCM!
 
acha uongo mleta maada
Anna mugwira alituliwa akowa ACT WAZALENDO KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARIO ,Katambi aliteuliwa kuwa mkuu wa wilta Dodoma akiwa chadema,JULUSI MTATITIRO aliteu;iwa DAS akiwa Cuf nk uongo haukusaidii
Yaani kweli ukiwa mwanaccm unakuwa huwezi kuwa na ufahamu wa kutosha kichwani...Katambi aliteuliwa mkuu wa wilaya akiwa chadema?? Mtatiro alichaguliwa akiwa cuf ?? Hata Mgwira alishakuwa ccm kivitendo, lkn kinadharia alikuwa Act wazalendo
 
Watumishi wa umma hawatakiwi kuwa wanachama wa chama chochote ila wanapaswa kufuata sera za serikali iliyoko madarakani.
Umejielekeza vibaya. Watumishi wa umma wanaruhusiwa kuwa wanachama wa chama chochote cha siasa, isipokuwa hawapaswi kupata nafasi za uongozi katika vyama wala kufanya shughuli za chama muda wa kazi.

Pia marekebisho kidogo, watumishi wa umma wanatekeleza sera za serikali. Nafikiri ulitaka kumaanisha chama kilichopo madarakani na sio serikali iliyopo madarakani.
 
Ndio. Au uwe tayari kuukana upinzani
Kabisa........

Ukisikia mpinzani kateuliwa kwenye nafasi za uteuzi za Mheshimiwa Rais, aidha mpinzani huyo yupo njiani kuekekea CCM, au mpinzani huyo ni kiwiliwili tu chake kipo upinzani lakini moyo wake upo CCM!
 
Huwezi kuteua watu wa kukukwamisha hata siku moja,hayo mambo tuwaachie wazungu tu walio na uzalendo na nchi zao.Uteue mtu aina ya tundu lissu au zitto unategemea nini?Uzalendo kwa upinzani ni sifuri kabisa waendelee kupiga kelele tu ndio kazi wanayoweza
 
Huwezi kuteua watu wa kukukwamisha hata siku moja,hayo mambo tuwaachie wazungu tu walio na uzalendo na nchi zao.Uteue mtu aina ya tundu lissu au zitto unategemea nini?Uzalendo kwa upinzani ni sifuri kabisa waendelee kupiga kelele tu ndio kazi wanayoweza
Hata hivyo huwezi ukaona ajabu kwa Mheshimiwa Rais, kumteua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi, ambaye ni kada kindakindaki wa CCM?

Hapo unategemea kweli huyo Mwenyekiti anaweza akawa "fair" na asipendelee chama chake cha CCM kweli?

Refer kwa yaliyotokea Zanzibar, kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salum Jecha, ambaye hivi karibuni alionyesha sura yake halisi, kwa kuchukua fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM!
 
Tumemsikia mara kwa mara Rais Magufuli wakati akihutubia akisema kuwa maendeleo hayana vyama, akimaanisha kuwa serikali yake haina upendelo linapokuja suala la maendeleo ya nchi, kuwa kila mwananchi anayo haki sawa

Lakini, maneno hayo yana tofauti kubwa katika utendaji wake katika uteuzi wake wa nafasi za utumishi wa Umma katika nafasi kama vile maRC's maDC's, maRAS, maDAS, wakurugenzi wa wilaya, pamoja na nafasi zote za uteuzi katika nafasi kubwa za utumishi katika mashirika yote ya Umma, ambapo "qualification no 1" kwake Rais Magufuli, ni lazima uwe kada kindaki ndaki wa CCM.

Hivi Rais Magufuli haoni kuwa anafanya ubaguzi wa waiwazi kabisa, wakati Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, inasema kuwa nchi yetu ina mfumo wa vyama vingi?

Katika Katiba ya nchi inayoainisha hivyo, kwa Rais Magufuli kufanya ubaguzi wa waziwazi kabisa, haoni kuwa kwa kuangalia wale anaowateua katika nafasi hizo, kwa kuangalia uanachama wao wa kindaki ndaki kwa CCM, haoni kuwa anaivunja Katiba hiyo ya nchi?

Nawakaribisha wasomaji tuidadavue mada hii, kwa maslahi mapana ya Taifa hili.
Kama unauweza UNAFIKI basi ni rahisi tu.
 
Back
Top Bottom