Hivi Sungura anataga Mayai au Anazaa? Nimeulizwa na binti aliyetoka kufanya Usaili wa ualimu hivi karibuni

Hivi Sungura anataga Mayai au Anazaa? Nimeulizwa na binti aliyetoka kufanya Usaili wa ualimu hivi karibuni

🤓🤓😂😂

Inategemea na sungura yupi.
Kwenye Fasihi Sungura anaweza kutaga na kuzaa papo hapo
Hizo ni hadithi mkuu. Halafu sungura sio mnyama mgeni kabisa maana karibia Kila kabila Lina hadithi zake tangu utotoni hadithi za sungura na fisi au na kobe tumesimuliwa sana
 
Umeamua kuwavua nguo walimu sasa
Hapan mkuu huenda wapo wengi wa namna hii hivyo ni vyema sisi tukaangalia namna ya watoto wetu waweze kujifunza kwa vitendo kama nilivyo eleza.

Umewahi kuulizwa yesu alikuwa mwanamke au mwanaume? Jibu ni hujawahi maana viongozi wa dini wanapewa kipindi Kila ijumaa ama jtano
 
Huyo asifaulu hiyo interview atafanya vijana wetu wa kayumba kuwa vilaza walioshindikana.
Kabisa. Pia Kuna shida kwenye elimu yetu.Mwalimu anayefundisha biology hajawahi hata kuona viumbe anao wafundisha nayeye kakaririshwa vilevile
 
Kwanza kabisa kwa maelezo uliyoyatolea sijaona haja ya kuhusanisha kulaumu mfumo wa elimu bali ni ujinga wa mtu binafsi kuuliza kama mnyama anataga.
Pili wewe kwakuwa unajua kuwa sungura hatagi hakukupi nafasi ya kupata darasa la kufundisha kuhusu ufugaji wa sungura isitoshe umewapata siku chache kama ulivyosema. Lakini point ya kusema wafugaji (ambao siyo wewe) wapewe vipindi chuoni naafikiana na wewe,kuna wafugaji wanafuga kisasa kwa models ambazo hazifundishwi kwa vyuo vyetu ambapo wahitimu wanaotoka chuoni wakipata nafasi kwenye hizo farms wanaanza kufundishwa upya. Vyuo vinaweza shirikiana na hawa kwa kuwapa vipindi ili kupanua wigo wa ufahamu wa mambo mengi na mara nyingi huwa ni technlojia ya ulimwengu wote kwa ujumla na kuwawezesha wahitimu kuwa na wigo mpana wa ajira
 
Kwanza kabisa kwa maelezo uliyoyatolea sijaona haja ya kuhusanisha kulaumu mfumo wa elimu bali ni ujinga wa mtu binafsi kuuliza kama mnyama anataga.
Pili wewe kwakuwa unajua kuwa sungura hatagi hakukupi nafasi ya kupata darasa la kufundisha kuhusu ufugaji wa sungura isitoshe umewapata siku chache kama ulivyosema. Lakini point ya kusema wafugaji (ambao siyo wewe) wapewe vipindi chuoni naafikiana na wewe,kuna wafugaji wanafuga kisasa kwa models ambazo hazifundishwi kwa vyuo vyetu ambapo wahitimu wanaotoka chuoni wakipata nafasi kwenye hizo farms wanaanza kufundishwa upya. Vyuo vinaweza shirikiana na hawa kwa kuwapa vipindi ili kupanua wigo wa ufahamu wa mambo mengi na mara nyingi huwa ni technlojia ya ulimwengu wote kwa ujumla na kuwawezesha wahitimu kuwa na wigo mpana wa ajira
Sahihi mkuu ndio maana nimesema ni kitu kidogo sana........ mkuu kwa mfugaji yeyote wa muda mrefu anakuwa anajua vitu vingi sana kiuhalisia na tofauti na muhitimu wa kitengo husika.

Hivyo ukubali ukatae wanafunzi wakipelekwa shamba wakiwa na mkufuzi wao pamoja na mkulima/mfugaji watapata elimu na majibu ya maswali Yao.

Hata kama hujui kma sungura anazaa au anataga ukifika shambani utaambiwa hawa sungura Wana mimba na wapo karibu kuzaa....na badae mtaonyeshwa watoto wa sungura hivyo utaelewa vizuri.

Sikupingi nakubaliana nawewe.
 
Hukuwa na sababu ya kuandika hayo yote. Nyie mngemjibu tu kuwa "Sungura anazaa".
Kutokujua hilo haimanisi hana elimu na kwamba hafai kuwa mwalimu.
Yapo mambo mengi sana watu hawayajui ila siju ikiwapasa kuyajua huyajua kuanzia hapo na wanaweza hata kuwaelekeza wengine.
 
Leo mida ya mchana wife akiwa anatoka kanisani alikuwa ameongozana na binti muhitimu wa chuo cha ualimu.
Hapa nyumbani nimefuga sungura wapo watatu nimenunua hivi karibuni baada ya madogo kuwapeleka kwa mfugaji mwenzangu wakawapenda sana nikaamua kuwanunulia .Muda ule walinikuta nahangaika kuwaingiza badani baada ya kutoka bandani.

Alipowaona alifurahi sana na baada ya kukamata sungura mmoja alitamani na yeye amshike nikawa nimempa
Swali alilo niuliza liliniacha mdomo wazi "HIVI SUNGURA ANATAGA MAYAI AU ANAZAA?" Nikijua labda sijasikia vizuri akarudia tena swali lile lile. Nikamjibu sungura anazaa kama wanavyo zaa paka na mbuzi au nguruwe anazaa na hatagi mayai

Nikamuuliza kwani shuleni mlifundishwa kuwa anataga ? akajibu hata hajui yeye siku zote anajua sungura anataga mayai kama bata au kuku!!

Ni kitu kidogo sana hiki lakini mimi kimeniacha na maswali mengi sana.Tazamia huyu apate ajira tofauti na a e i o u alizo karirishwa chuoni ana vitu gani vingine vya kufundisha watoto wetu kama viumbe wa kawaida kabisa kama sungura hajui kama anazaa.Mtu kafika level ya chuo na bado hajui.

Nimejifunza elimu yetu pia ni kimeo sana hivyo uwepo ulazima wa kwenda kujifunza kwa vitendo kwa wafugaji walio karibu na shule au wafugaji waombwe waende shuleni wakafundishe kwa vitendo hasa wakiulizwa maswali.Na kumbuka kipindi chetu kulikuwa na somo stadi za kazi moja ya mada ilikuwa ufugaji mwalimu wetu(rip)alitupeleka kwa mfugaji wa kuku,ng'ombe na mbuzi.Tuliuliza maswali mengi na yote tulijibiwa japo mfugaji yule alikuwa anafuga kienyeji tu.

Mfugaji au mkulima ni rahisi sana kujibu swali na kueleweka maana yeye ana fanya kazi kwa vitendo.Haya mabadiriko ya mitaala yazingatie sana elimu kwa vitendo na iwe kipaumbele.

Mbona kwenye kipindi cha dini wachungaji na mashekh huwa wanakuja kufundisha itashindikana vipi sisi wakulima na wafugaji kwenda kuwafundisha watoto/wadogo zetu ? Naimani tukipewa muda hakuna atakaye kataa kuwafundisha watoto wetu kwa vitendo.

Mwalimu hata kama umesomea masomo ya sanaa pekee yake ndo usijue kama sungura ni mnyama na sifa ya mnyama ni kuzaa?
Nilishakutana na vituko kàma hivi toka mwalimu graduate, nilishangaa sana. Ikabidi niulize rafiki zake kama ni kweli ana degree ya ualimu.
Kuna majanga ya kutisha kwenye mfumo wa elimu nchini.
 
Back
Top Bottom