Hivi TBC wameona kitu cha maana cha kutuonyesha mubashara ni ufunguzi wa mahakama Chato na wala sio mkutano mkuu wa Chadema!

Hivi TBC wameona kitu cha maana cha kutuonyesha mubashara ni ufunguzi wa mahakama Chato na wala sio mkutano mkuu wa Chadema!

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Tunavyofahamu ni kuwa chombo cha habari cha TBC ni cha Watanzania wote na kinagharamiwa uendeshaji wake na kodi za wananchi wote, wana CCM na wana Chadema.

Kwa hiyo ni wajibu wa Mkurugenzi wa TBC, Ayoub Rioba, kuangalia ni kitu gani kina umuhimu mkubwa kwa Taifa na kukionyesha mubashara bila upendeleo wowote.

Vile vile Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 3(1( ) inatamka wazi kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa nchi ya kidemokrasia na ni ya mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu.

Ndipo hapo ninapomuuliza Mkurugenzi wa TBC, ni kwanini waliamua kuonyesha tukio dogo la ufunguzi wa mahakama ya wilaya ya Chato na kuacha kuonyesha mubashara, tukio lenye umuhimu mkubwa kwa Taifa hili la mkutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema?

Tunajua pia TBC sio chombo cha habari cha CCM, na ni cha Taifa zima, kwa hiyo kufanya upendeleo kwa matukio yoyote ya ki-CCM ni makosa makubwa

Naomba mwenye kuelewa umuhimu wa TBC kuonyesha kila tukio analofanya Rais kwenye nchi hii lionyeshwe mubashara, na kutoweza kuonyesha matukio mengine yenye umuhumu mkubwa sana kwa Taifa hili aweze kunijibu.
 
Ila kwa kweli viongozi wa CCM na serikali eitha hawajui mapambano ya kisiasa yakoje au wanafanya makusudi kuipaisha Chadema. Haya mazuio katika haki zao wanadhani kwa mtu asiye chama au hata kama yuko ccm lakini mpenda haki ataacha kuipenda Chadema?

Kumfanyia mtu au taasisi ukatili inabaki ni furaha yako wewe unaye tenda, lakini kwa wengine wanapata huruma na kuongeza mapenzi yao kwa muathirika. Ona Jana kikosi cha polisi kung'oa bendera kilikuwepo lakini polisi wa kuwatawanya kuokoa watu waliokwama kwenye mafuriko hakuna. CCM inajimaliza yenyewe kwa chuki zao za kichawi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uzinduzi wa miradi ya maendeleo na makusanyiko ya CHADEMA bora ni kipi? Chadema mna nini cha chamaana hadi tuwaangalie?
 
Ila kwa kweli viongozi wa CCM na serikali eitha hawajui mapambano ya kisiasa yakoje au wanafanya makusudi kuipaisha Chadema. Haya mazuio katika haki zao wanadhani kwa mtu asiye chama au hata kama yuko ccm lakini mpenda haki ataacha kuipenda Chadema?
Kumfanyia mtu au taasisi ukatili inabaki ni furaha yako wewe unaye tenda, lakini kwa wengine wanapata huruma na kuongeza mapenzi yao kwa muathirika. Ona Jana kikosi cha polisi kung'oa bendera kilikuwepo lakini polisi wa kuwatawanya kuokoa watu waliokwama kwenye mafuriko hakuna. CCM inajimaliza yenyewe kwa chuki zao za kichawi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa kweli CCM wanajimaliza wenyewe

Hivi chama cha CCM, ambacho kama wenyewe wanavyodai wanakubalika sana nchini Tanzania na kuzoa kura zaidi ya asilimia 99.9 kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, hivi inakuwaje kukiogopa chama cha upinzani cha Chadema, ambacho kwa Maelezo yao ni kama kimeshakufa tayari?
 
CDM walishatamka hadharani hawataki ushirikiano na TBC , mmesuswa huko kwingine saivi mnajiliza kwa nini TBC hawakuonyesha tukio lenu, kweli nyumbu ni nyumbu tu ...
 
CDM walishatamka hadharani hawataki ushirikiano na TBC , mmesuswa huko kwingine saivi mnajiliza kwa nini TBC hawakuonyesha tukio lenu, kweli nyumbu ni nyumbu tu ...
Hiyo ni Television ya Taifa, kwa hiyo msiifanye kuwa sawasawa na television ya CCM
 
Uzinduzi wa miradi ya maendeleo na makusanyiko ya CHADEMA bora ni kipi? Chadema mna nini cha chamaana hadi tuwaangalie?
Hivi wewe kada wa Lumumba hujaona umuhimu wa kukionyesha chama kikuu cha upinzani nchini cha nchni cha Chadema, kikifanya mkutano wake Mkuu?
 
Tunavyofahamu ni kuwa chombo cha habari cha TBC ni cha Watanzania wote na kinagharamiwa uendeshaji wake na kodi za wananchi wote, wana CCM na wana Chadema.

Kwa hiyo ni wajibu wa Mkurugenzi wa TBC, Ayoub Rioba, kuangalia ni kitu gani kina umuhimu mkubwa kwa Taifa na kukionyesha mubashara bila upendeleo wowote.

Vile vile Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1877, ibara ya 3(1( ) inatamka wazi kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa nchi ya kidemokrasia na ni ya mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu.

Ndipo hapo ninapomuuliza Mkurugenzi wa TBC, ni kwanini waliamua kuonyesha tukio dogo la ufunguzi wa mahakama ya wilaya ya Chato na kuacha kuonyesha mubashara, tukio lenye umuhimu mkubwa kwa Taifa hili la mikutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema?

Tunajua pia TBC sio chombo cha habari cha CCM, na ni cha Taifa zima, kwa hiyo kufanya upendeleo kwa matukio yoyote ya ki-CCM ni makosa makubwa

Naomba mwenye kuelewa umuhimu wa TBC kuonyesha kila tukio analofanya Rais kwenye nchi hii lionyeshwe mubashara, na kutoweza kuonyesha matukio mengine yenye umuhumu mkubwa sana kwa Taifa hili aweze kunijibu.
Ni makosa makubwa binadamu kujilinganisha na aliyemtangulia. Cha maana ni kujitahidi kumfikia ili nawe upate uhondo anaoufaidi.
 
Si ni CDM wenyewe walikataa ushirikiano wowote na TBC , sasa kinachowaliza hapa ni nini ?
Unajua chanzo cha kukataa kushiriikiana na TBC?

Ni kutokana na wao TBC kuipendela mno CCM, na kuviacha vyama vya upinzani kama watoto yatima
 
Back
Top Bottom