state agent
JF-Expert Member
- Jul 1, 2019
- 1,764
- 2,510
Mbona inaeleweka?
Mbowe kasema vituo vyote viligoma vikasema havitaweza kuonyesha mkutano wa CHADEMA kwa mazingira ya sasa, hivyo sio TBC peke yao.
Haijalishi, mlishatamka hamtaki kuwaona TBC kwenye event yenu yoyote, kinachowaliza saivi ni nini wakati mlishawakufukuza?Unajua chanzo cha kukataa kushiriikiana na TBC?
Ni kutokana na wao TBC kuipendela mno CCM, na kuviacha vyama vya upinzani kama watoto yatima
Sasa Mkurugenzi wa TBC afukuzwe kazi kwa kosa gani?Umtakii mema mkurugenzi kufanya hivo ni kosa kubwa Sana sawa na uhujumu uchumi yaani kodi za wananchi ziutangaze upinzani.
Kamuulize Tido,alitaka kuleta uprofesionalism kilichompataSasa Mkurugenzi wa TBC afukuzwe kazi kwa kosa gani?
Kuwapa coverage iliyo sawa wananchi wake ni wajibu wake.........
Juu ya hayo ni kuwa chimbo hicho cha habari kinaendeshwa kwa kodi zetu wananchi wote, wanachama wa CCM, vilevile wanachama wa Chadema
Ni makosa makubwa kwa Mkurugenzi wa TBC kuanza kufanya ubaguzi wa nani anastahili coverage na nani hastahili
Ubovu ni kwamba mwenye mamlaka ya mwisho anatoka kwenye hii nchi ni mwanachama wa chama tajwa, hivyo lazima wamfuate kokote aliko ili waweze kudumu katika nafasi zao walizonazo.Wanalipwa mishahara,kwa kodi zetu na wala hawapewi hizo pesa toka CCM
Katiba haibaguiUbovu ni kwamba mwenye mamlaka ya mwisho anatoka kwenye hii nchi ni mwanachama wa chama tajwa, hivyo lazima wamfuate kokote aliko ili waweze kudumu katika nafasi zao walizonazo.
Dr Rioba mkurugenzi mkuu wa TBC bado anayo kumbukumbu ya kutumbuliwa kwa Mhando hivyo hawezi kufanya kosa hilo.wangethubutu kufanya hivyo, leo hii mkurugenzi wao angekuwa ndani pamoja na kupoteza kibarua
"katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1877"Tunavyofahamu ni kuwa chombo cha habari cha TBC ni cha Watanzania wote na kinagharamiwa uendeshaji wake na kodi za wananchi wote, wana CCM na wana Chadema.
Kwa hiyo ni wajibu wa Mkurugenzi wa TBC, Ayoub Rioba, kuangalia ni kitu gani kina umuhimu mkubwa kwa Taifa na kukionyesha mubashara bila upendeleo wowote.
Vile vile Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1877, ibara ya 3(1( ) inatamka wazi kuwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakuwa nchi ya kidemokrasia na ni ya mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu.
Ndipo hapo ninapomuuliza Mkurugenzi wa TBC, ni kwanini waliamua kuonyesha tukio dogo la ufunguzi wa mahakama ya wilaya ya Chato na kuacha kuonyesha mubashara, tukio lenye umuhimu mkubwa kwa Taifa hili la mkutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema?
Tunajua pia TBC sio chombo cha habari cha CCM, na ni cha Taifa zima, kwa hiyo kufanya upendeleo kwa matukio yoyote ya ki-CCM ni makosa makubwa
Naomba mwenye kuelewa umuhimu wa TBC kuonyesha kila tukio analofanya Rais kwenye nchi hii lionyeshwe mubashara, na kutoweza kuonyesha matukio mengine yenye umuhumu mkubwa sana kwa Taifa hili aweze kunijibu.
Hahaha nawewe ulikuwa ukifuatilia kama Sumaye kajitosa au ulikuwa ukichungulia number za Cecil Mwambe?!