Hivi umefanikiwa kusamehe kila jambo linalokutokea au lililokutokea kwenye maisha yako?

Hivi umefanikiwa kusamehe kila jambo linalokutokea au lililokutokea kwenye maisha yako?

Cha msingi ni wewe kujuwa kuishi jinsi ambavyo unataka,usitarajie mambo makubwa kutoka Kwa watu wengine,tarajia kutoka kwako,kama unataka wakusalimie Anza wewe kuwasalimia halafu utaona Kila mtu anaanza kutaka kukusalimia,kukujulia Hali kama hivyo. Usiogope kwamba watu wengine wanakuonaje,wakati ule utakapofikia mahali ukasema liwalo na liwe basi utakuwa huru katika nafsi. Unajuwa Kuna wakati unajikuta uko na watu lakini rohoni mwako unajuwa Hawa Niko nao TU sababu ya nidhamu ya uoga. Kataa uoga kuwa huru.

Sent using Jamii Forums mobile app
yani kuna watu hum duniani wanachotaka nibwasiklizwe wao, na hivyo wapo age kubwa baaas na ule msemo wa kinafki et mtu mzima hakosei, wtf!! mimi n mtu wa kujichanganga but once ukijiresi vibaya kwangu nikasema its enough ujue imeeenda hio sasa naambiwa usilipe baya kwa baya kwa hio mimi nitakua natenda wema tu wao wanilipe ubaya?? hakunaga biashara iso na faida kama haina faida unaachana nayo ndio hii ya hawa ndugu lawama
 
I totally agree with you,. Mtu akikufanyia ubaya unamsamehe, una take note, na kukaa naye mbali sana. Dunia ina mchanganyiko wa watu wema na wabaya, wako positioned in a way lazima ukutane nao, so you get rid of those wabaya kila unapokutana nao na kuendelea na safari. Ni zoezi endelevu.
Exactly brother 👏🏾👏🏾👏🏾👏🏾
 
Kwanza lazima ukubali toka awali ulikosea namna unavyohusiana nao,ulishindwa kubalance shobo,unawezaje kutembelea watu mfululizo hivyo wakati wao hawana time na wewe?
Why ulijua kujipa umuhimu mahali ambapo umuhimu wako watu hawauoni?
Usirudie hili kosa kwenye safari yako ya maisha la sivyo utateseka sana.
Mojawapo ya kanuni zangu zinazonisaidia sana ni kujua kubance shobo,yaani mahali ambapo sina umuhimu na sihitajiki huwa silazimishi nachukua 50% zangu kiroho safi.kwa sasa omba Mungu uweze kuwasamehe na usiruhusu ukaribu nao
 
Haya maisha haya, unakutana na mambo mengi sana ya kukuumiza moyo na kukufurahisha yes dunia imeumbwa hivyo.

je wewe umeweza kusamehe kila jambo lililokutokea au linalokutokea katika maisha yako? mimi nimeshindwa, kuna watu bwana nilikua nao very close, katika maisha yetu mimi ndie nilikua nakwenda kuwatembelea.

Nikisikia wanaumwa nishafunga safari, nikijua tu nina muda sijaonana nao najikuta nishafunga safari, ikumbukwe hapo ninapokaa ni karibu na barabara kuu, yani huwez kua una safari ya mjini au kurud bila kupita ninapokaa lakini hakujatokea hata mmoja kuja kunitembelea na ukiona umetembelewa ujue mtu alikua anakuja eneo la jiran ulilopo ndio mtu anapita.

Kisa kinakuja hapa kuna mambo flan flani niliyataka yafanyike kwao, hawa ni ndugu zangu upande wa baba, bas pia wakanipigisha danadana lisifanyike na maneno ya kejeli nikaona isiwe kesi jambo likafanyikia nyumban kwa wazazi wangu, since then nimekua na hasira nao kiasi nashindwa kumove on.

Yaani hata ile kwenda kuwatembelea sifanyi tena na mimi naweza kuwa nnashida na maeneo waliyopo nahata nisiende na naweza kupanga kabisa ngoja niende moyo wangu ukawa mzito mpaka naghairisha kuna mmoja nilikutana naye ananiuliza mbona huji siku hizi nilimjibu tu nimechoka kufatafata watu ambo sioni umuhim wao kwangu nikampa ukweli wa moyo lakini bado nafsi yangu kama ina kinyongo dhidi yao nifanyeje iniepuke hii hali?
Simple tu.Unaposali waombee halafu wabariki kwa mema unayoyajua wanatenda.Yale mabaya jifunze kuelewa kuwa hawajui kuwa wanayafanya[emoji16]
 
Tupate burudani kidogo 😊🤓

Hiki kipande nakipenda......

Bora ni Enjoy (Mmmmmh)
Maisha mafupi ni simple
Yanini niteseke roho
Jiunge nami upoze koo
Bora ni Enjoy
Maisha mafupi ni simple
Yanini niteseke roho (Ooh yanini yanini)
Jiunge nami upoze koo (Mmmh khoo khoo khoo khoo)

Kama kupendaaa
Bora nimpende mama yangu (Mmmh)
Kama kupendwaa mimi iih
Nitajipenda peke yangu (Ooooh)
Kilichoniponza ufala
Kujiona simba kumbe swala
Nikazama kwenye penzi uchwala
Badala ya kusaka miamala
Aiii yooooooo oh
Toka ni date pesa (Enhee)
Sa napendeza (Enhee)
Na tena naenjoy (Enhee)
Na wanangu ma homeboy (Enhee)
Ooooh account inasoma (Enhee)
Na kamwili kananona (Enhee)
We mwenyewe si unaona yani (Enhee)
Ai nasema boraaaa
kaimba nani
 
😂😂Basi komaa na nafsi yako km huwategemei kula wala kwa chochote achana nao futa mbwa hao
na ndio kitu nilikua nafanya nadeal na mambo yangu nikikutana nao salam lakini kama mwanzo kuwafuata sitaki sasa hapo tu ndio wameona ninakosea wapuuzi wale
 
Kwanza lazima ukubali toka awali ulikosea namna unavyohusiana nao,ulishindwa kubalance shobo,unawezaje kutembelea watu mfululizo hivyo wakati wao hawana time na wewe?
Why ulijua kujipa umuhimu mahali ambapo umuhimu wako watu hawauoni?
Usirudie hili kosa kwenye safari yako ya maisha la sivyo utateseka sana.
Mojawapo ya kanuni zangu zinazonisaidia sana ni kujua kubance shobo,yaani mahali ambapo sina umuhimu na sihitajiki huwa silazimishi nachukua 50% zangu kiroho safi.kwa sasa omba Mungu uweze kuwasamehe na usiruhusu ukaribu nao
tangu nijitambue kwamba mimi ndio nachapa kwato kuwafuata nikaacha sasa kitendo cha kutowafata fata tena naonekana mm ndio mbaya wanasahau yao ijapokua hayaniumizi kichwa lakini moyo umekua mzito kuchangamana nao tena huku wazaz wakinikalia kooni nisitende baya kwa baya na maisha sio hivo najiuliza vitu vingi wao waliona namna ilivyokua mpaka kufikia hapo why wanifanye mtumwavwa kua down to earth wakat nafsi yangu imegoma kabisa
 
wazazi wangu hawanielewi, wananambia ubaya hulipwi kwaubya na kunilazimisha niendeleze mambo za kuwafata fata ambapo n kitu kimenishinda


Wazazi wako wapo sahihi, ni wajibu wao kukukumbusha mambo Kama hayo na kusisitiza umoja kati yenu, ninyi ni ndugu wa damu.

Lakini sio kila alisemalo mzazi ulifanye, samehe saba mara sabini huku ukikumbuka kwamba hata wewe sio mkamilifu na kuna watu pia unawakosea ama wameumizwa nawe hata sasa.

Badiri routine yako, acha kuwatembelea na ukiulizwa kwanini kuwa muwazi, sema Ukweli wa vile unavyojisikia juu ya mahusiano yenu.

Husithubutu kuishi na kinyongo rohoni, ni source ya maradhi mengi mwilini na Kama ni chuki kali basi kansa haitokuacha.

Tujifunze kuuishi Ukweli uliopo ndani yetu na kusimama imara juu ya maamuzi yetu bila kuyumbishwa na matendo na maneno ya wengine juu yetu.

Be [emoji817] % YOU and the rest of the World will adjust.
 
Back
Top Bottom