G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,795
- 36,704
Kiukweli Rais Magufuli ni Rais wetu ndiyo ila ana udhaifu mmoja mkubwa sana. Ni mtu wa kufika bei haraka kama utamfanyia vitu viwili tu
1. Mpe sifa na ukuu
2. Mpe fedha
1. Sifa na Ukuu
Ukitaka kuamini rejea majina yote yaliyokatwa kwenye ubunge utagundua ni wengi ambao walikuwa "nyutro" na yeye hataki kabisa mwanaccm uwe "nyutro" Unatakiwa kusifia miradi kuipamba na kumpamba na yeye. Fanya kuitembelea na kusema "Haijawahi tokea" Ukifanya hayo wewe kwake utakuwa mchapa kazi na muadilifu.
Rais Magufuli hataki kabisa mwanaccm anayeipa Chadema kipaumbele chochote kile. Huo ni utakuwa ugomvi mkubwa sana kati yenu. Pia kushirikiana na upinzani wa kweli jihesabie huna lako ndani ya utawala wake. Hapendi kabisa kabisa kukosolewa kwa jambo lolote lile hata kama amefanya makosa makubwa.
2. Mpe hela
Huwezi kuamini kuwa sasa rafiki mkubwa wa Rais Magufuli ni kama kina Rostm Azizi maana wanatoa mpunga unaomzidishia sifa. Vimilioni 20 vya harambee mbona safi tu.
Mtu kama Mwanyika leo ni super pamoja na kuharibu kule ACACIA. Jiulize kwanini kina Harbinder na Rugemarila bado wapo mahabusu! Ni kwasababu wamegoma!
Kwa kutambua hayo wengi wa watanzania wasaka tonge wameamua kucheza ngoma yake kwa kishindo kweli kweli. Yani hawa watafanya lolote jambo ilimradi waneemeke kwani wamesha mjulia mkuu wao na habadiliki hivyo ni rahisi sana kuishi naye.
Huwezi kuamini, kama wewe ni msaka tonge basi hakuna kiongozi rahisi kuwahi kutokea kuishi naye kama Rais Magufuli.
1. Mpe sifa na ukuu
2. Mpe fedha
1. Sifa na Ukuu
Ukitaka kuamini rejea majina yote yaliyokatwa kwenye ubunge utagundua ni wengi ambao walikuwa "nyutro" na yeye hataki kabisa mwanaccm uwe "nyutro" Unatakiwa kusifia miradi kuipamba na kumpamba na yeye. Fanya kuitembelea na kusema "Haijawahi tokea" Ukifanya hayo wewe kwake utakuwa mchapa kazi na muadilifu.
Rais Magufuli hataki kabisa mwanaccm anayeipa Chadema kipaumbele chochote kile. Huo ni utakuwa ugomvi mkubwa sana kati yenu. Pia kushirikiana na upinzani wa kweli jihesabie huna lako ndani ya utawala wake. Hapendi kabisa kabisa kukosolewa kwa jambo lolote lile hata kama amefanya makosa makubwa.
2. Mpe hela
Huwezi kuamini kuwa sasa rafiki mkubwa wa Rais Magufuli ni kama kina Rostm Azizi maana wanatoa mpunga unaomzidishia sifa. Vimilioni 20 vya harambee mbona safi tu.
Mtu kama Mwanyika leo ni super pamoja na kuharibu kule ACACIA. Jiulize kwanini kina Harbinder na Rugemarila bado wapo mahabusu! Ni kwasababu wamegoma!
Kwa kutambua hayo wengi wa watanzania wasaka tonge wameamua kucheza ngoma yake kwa kishindo kweli kweli. Yani hawa watafanya lolote jambo ilimradi waneemeke kwani wamesha mjulia mkuu wao na habadiliki hivyo ni rahisi sana kuishi naye.
Huwezi kuamini, kama wewe ni msaka tonge basi hakuna kiongozi rahisi kuwahi kutokea kuishi naye kama Rais Magufuli.