Hivi ungejaaliwa kuipata blioni moja ungeitumiaje?.

AbouZakariya

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2013
Posts
1,646
Reaction score
2,378
Habari wanajamvi, kwanza kabisa nitumie fursa hii kumpa pole ndugu yetu na mtanzania mwenzetu bwana Mohamed Dewji kwa mtihani ulompata, na pia naipa pole familia nzima ya wakina Dewji na watanzania kwa ujumla kwa fazaa iliyowapata baada ya kusikia taarifa za kutekwa kwa bwana Mo.

Niende sasa kwenye lengo na swali la uzi huu , baada ya Mo kutekwa familia ilitangaza donge nono la shilingi BILIONI MOJA kama zawadi kwa atakayefanikisha kupatikana kwake.

Swali langu kwako JE KAMA WEWE UNGEFANIKIWA KUIPATA ZAWADI HIYO UNGEITUMIAJE ILI KUIZALISHA ZAIDI?.
Hilo ndio swali langu kwako karibu jamvini tujadili.
 
Billion moja kwanza ningenunua NYUMBA ya Kama million 400, hapo inabaki 600m. Natoa 100m napeleka Kanisani (fungu LA kumi), 10 msikitini, 20M Ocean Road, 20M nyingine kuna kituo cha watoto yatima naendaga napeleka hull iwasaidie, 200m naenda kununulia bonds za serikali. 100M nafanyia kitu Fulani hivi cha hela, 50M namuwekea mwanangu fixed account, Mama nampa 50M Na yeye afanye yake, 10M naenda nayo Maldives Na bby kwa gharama yangu. Inayobaki tutaitumia taratibu mpaka iishe
 
Hahhahahhahaaa umetishaaaaa halafu mm na Shunie ungetupeleka makao makuu ya Heineken tukaogelee woiii
 
Kwa kweli mimi ningeiga mfumo wa china!! Sababu serikali inapenda mikopo basi ningeikopesha, alafu bondi nataka waweke rehani uwanja wa chato ili wakishindwa kulipa ni upige mnada!!
 
Nimesahau. Nyie nitawapeleka Zanzibar mkanywe mpaka muombe poo
Imebidi nicheke sana kuona hilo neno Zanzibar, weekend hii tulienda kujifungia znj sehem sehem na rafiki zangu kula bata, kurudi leo jioni boat ya mwisho, pale bandarini TRA aisee wanasachi mikoba kama wameahidiwa kuongezwa mishahara vile, ni wasumbufu mpaka kero.

Mi nliwatolea mpaka nguo za ndani boxer nikawapangia juu ya meza kwa kero zao. Nikabaki najiuliza hizi ni nchi mbili tofauti au ni nchi moja kweli!!!!
 
Mkuu sasa unadhani Yale mapato yaTRA tutafikiaje malengo bila kutafuta mianya Kama hiyo ya nyie wala bata wa Zanzibar? Siku nikutane nao wanifanyie huo usumbufu Na hiki kigugumizi changu naweza watukana
 
Sina uhakika kama mipango yote hiyo ingekamilika....maana mipango si matumizi
 
Mkuu sasa unadhani Yale mapato yaTRA tutafikiaje malengo bila kutafuta mianya Kama hiyo ya nyie wala bata wa Zanzibar? Siku nikutane nao wanifanyie huo usumbufu Na hiki kigugumizi changu naweza watukana
Kuna dada nlimkuta kanunua pasi ya nguo wanamdai risiti na kule znj wenzetu hawatumii risiti za electronic, kachambuliwa begi hatari.[emoji120] Jamaa hawana stara hata kwa wakina mama, mtu anatolewa mpaka sidiria za ndani (wengine hata kufua unakuta hajafua, sidiria chafu ukiisimamisha inasimama dede yenyewe bila sapoti yoyote).
 
Cha kwanza kabisa nabet timu mbili za uhakika kwa kuweka dau la 500million halo sikose 1.5 billion plus na 500million iliyobakia inakuwa 2billion ..

Naificha hiyo hela kwenye kibubu mpaka niwe mkubwa nianze kuitumia
 
Sio Haki sasa hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…