Hivi Urusi husubiri nini kuivamia jirani Finland ukizingatia kachokozwa na kuchokonolewa kwenye mapua na masikio

Hivi tunaposema putin kafeli..Tunamaanisha ukraine kavuka mipaka kaingia urus? Au anafumuliwa huko huko kwake?..Kashndwa hata kurusha bomu la mkono ndan ya urus? Me naona vita hii mrus hatak uharbifu na kuu maelfu ya raia la sivyo hyo ukraine ingeshafutwa yote kwa makombora mazito
 

Tulitegema Urusi aifumue Ukraine ndani ya masaa, maana Putin kasema ni special operation na ukizingatia miaka yote tulijua Urusi ni super power, sasa miezi imepita bado hamna kikubwa zaidi ya kulipua majengo na kuua raia na mwenyewe Urusi amepoteza hadi bonge la meli baba lao.
Ukraine hapo kataifa jirani, yaani hata Kiev imemshinda Urusi kuiteka.

Leo hii Liverpool akija kucheza na Kagera sugar, dakika ya tisini Kagera hajafungwa mabao 200, kafungwa mabao matatu tu kwa moja, na Liverpool amehema uwanja wote, amebadilisha wachezaji hadi basi lakini wapi, tutasema ushindi upo kwa Kagera maana kuhimili mapigo huo ni ushindi.

Huyo Urusi ndiye alikua tegemeo la waarabu dhidi ya Marekani, na ndio maana wote wa dini ile mnamshabikia sana Putin Bwana Utam
 
Nasidhanii kama hayo yamataifa yanaweza kuingia VITABI na RUSSIA ila acha tuone !!!!!
 
ufini kaonyesha nia ya kujiunga Nato ila na ameanza mipango ya mazungumzo kwa hatua tu alizofikia fini, URUSi kaonyesha ni reaction ikiwa ni pamoja na kupeleka mifumo ya kuzuiya mashambulizi kutoka huko kwenye nchi fini na mwenzake vivyo hivyo inawezekana kuna hatua urusi anazisubiri hizo nchi zitangaze zimeifikia kuhusu hili jambo basi nae atoe msimamo wake kwa vitendo
 
Ataingiza majeshi na kule kweli Putin karukwa na akili ama anatimiza unabii
 

Aha! Kwanza ujue mkataba ukitiwa saini kwamba Finland amejiunga NATO ndio basi, haguswi tena maana wababe wa NATO wamebanwa kimkataba, hivyo kama amekaa anasubiri Finland atangaze amejiunga basi atakua amechelewa, vitendo vyake atabaki akivifanyia nje huko.
 
Nyie kenya mbona mmeshindwa kuimaliza al shabab wakati hawafiki buku
Wale wanampigania Allah mkuu mbona hata Saudi kashindwa kuwamaliza wanamgambo wa Yemen wakati pesa,jeshi na support vyote yuko navyo
 
Ukraine hakuchokoza, yeye kakutwa kwake nyumbani, ila Finland anayoyafanya kapitiliza uchokozi......yaani Mrusi ni nguvu ya soda, hovyo sana.
Sababu zipi zimefanya Ukraine akutwe nyumbani kwake na Russia? Finland amefanya kipi ambacho Ukraine hajakifanya?
 
Wewe umewahi kwenda shule kweli au hata kuhudhuria masomo katika ngazi yoyote, unafahamu ulicho andika lakini au umempigisha mtu imla. Poor you.
 
Mwaka 1939-1940 ni kitu gani kilifanyika kati ya hayo mataifa mawili. Mwenye kumbukumbu atukumbushe maanake waingereza wana msemo wao moja unaosema kwamba, History always repeats itself.
 
Weka records sawa, baada ya mkataba na Urusi walikabidhi silaha zote za nuclear kwenda Urusi na hawakuendelea na uzalishaji wa silaha za nuclear.
 
Kwa sasa kashikwa pabaya, aliahidi wakifanya vile anadogeza karibu silaha za nuclear hana cha zaidi cha kufanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…