Hivi Vitambulisho vya Magufuli vina lengo gani?

Hii elfu ishirini ni kwa mwaka au ukishanunua hicho kitambulisho ndo basi?
 
Kodi ya kichwa hiyo muulize babu yako enzi ya ukoloni ilikuwepo, mwaka wa kwanza rahisi, mwaka wa pili TRA wakiingia kijijini wote manakimbilia msituni
 
Ninachowaza hapa ni kwamba anataka kwanza hawa wafanyabiashara wadogo wadogo wasibugudhiwe.

Pili serikali itaweza kujua, ni wananchi wangapi biashara zao zipo katika level ya chini. Hili litasaidia serikali kutengeneza program maalumu za kuwaendeleza ili waweze kukuza mitaji yao na hatimaye kulipa kodi
 
Kuna watu hapa watakuwa na fremu wanapanga vitu vichache dukani mzigo wa maana unakaa store , ,afu wanavaa na Vitambulisho vyao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…