Hivi vitu wanavyovalishwa Watoto Wachanga wa Kiafrika mikononi, viunoni na miguuni mbona navitafuta kwa wa Kizungu sivioni?

Waafrica na akili zao wanazijua wenyewe na wahidi pia Wana hii mitabia ya kijinga kuvalisha watoto mizigo isiyokuwa na maana..
 
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
Imani na mila hizi ni za Waafrika, Waarab, na Wahindi pamoja na Wayahudi pia.
 
Mnavyojikuta wazungu..kumbe waafrika mablak pure nywele kipiripiri..wakati utotoni mlifungwa hizo na chale mnazo mwili mzima..brainwashed creatures.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio wote wenye kuamini hizi za mahirizi na kuchanjwa chale.....kutokuamini hayo ni kila mtu na imani zake kuwa watu waliyaignore hayo muda mrefu baada ya kuona hayana maaana, kwa mfano iyo irizi mbona anafungwa mtu Ila akiugua hospital anapelekwa, chanjo zote za clinic anapata, kwanini iyo irizi isiwe kinga kiujumla hata hizi chanjo wanazopewa hospital asiende kupata?
 
Mbona wewe unavaa rozali na hospitali unaena ukiugua.?

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tayari umeonyesha kweli mwafrika yupo gizani, sio kila mtu mnene ana pressure na sio kila mwembaba hana pressure, tuanzie hapo kwako mkuu.
Ni kweli sisi tuko gizani hatuna elimu ndo maana hatuna akili.mfano mtu mnene kafariki ghafla kijijini kumbe alikuwa na pressure ila kijiji kizima wataamini kalogwa na huku hawajampima chochote
 
Nchi ambayo watu wake wanaishi katika imani au dini yao ya asili hawana mgogoro wa nafsi juu ya kile wanachoamini???lakin nchi ambazo tunaamini katika dini ( ambazo tuliletewa) tunahangaika sana na imani zetu..
Nchi za mashariki na mashariki kuna dini ambazo hata sisi tukiwatazama wanavyoabudu tunaweza pata mashaka..lakini wanaishi na amani mioyoni mwao.
 
Kwani Kunatatizo lipi limetokea lililosababishwa na ivyo vitu?

Ni vyema kama unataka kujua wako sahihi au hapana, ni wachawi au washirikina ukatafiti nasio kuja kulalamikia kitu ambacho hukijui.

Binafsi sijui ni kwann wanavalishwa ila sitapingana nao kwa style hii.

Anaesema ni ushirikina atufafanulie hapa,
Anaesema ni wajinga kinachofanyika hakina umuhimu wowote nae atoe ufafanuzi hapa.
 
Pumbavu zako wwπŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 
Waafrica na akili zao wanazijua wenyewe na wahidi pia Wana hii mitabia ya kijinga kuvalisha watoto mizigo isiyokuwa na maana..
Wazungu hawana muda wa kijinga wa kurogana kipuuzi thus why huwezi kuta kwao hayo mambo ya kufungana vitambaa! Ila kibongo bongo mtu kupiga hatua kimaisha ni nongwa hata kumiliki mtoto wengine hawapendi labda kama unaishi Masaki huko ila kama upo buza mwanao watampiga zongo tu unashangaa mtoto anaharisha bila sababu na kulia ovyo!
 
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
Kama unaishi ushuani kama Masaki, Oysterbay au Upanga huna haja ya kumfunga vidude hivyo mtoto! Wachawi hawakanyagi maeneo kama yale πŸ˜‚ ila kama upo uswahilini jiandae na zongo tu! Waafrika ni washirikina sana tena wanaweza kukulogea mtoto bila sababu ya msingi kabisa. Binafsi mie nimezaliwa Aga Khan na utoto ulinikutia Upanga kwetu wote hatujawahi kuvalishwa hayo mataka taka mpaka tumekuwa watu wazima ila huku uswahilini nilipo sasa kwa ushirikina uliopo siwezi shangaa mtu akimvalisha mwanae hivyo vitambaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…