Hivi vitu wanavyovalishwa Watoto Wachanga wa Kiafrika mikononi, viunoni na miguuni mbona navitafuta kwa wa Kizungu sivioni?

Hizo ni Imani
Hata wanaowekewa njiti za kuzuia Mimba ni Hirizi za wazungu.
Sema zetu hatuzikubali tu
Wanaovaa Lzari je sio hirizi?
Hata wanaochomwa sindano ili dawa iingie hakuna tofaouti na anaepigwa chale,ila ndo vile tunathamini ngozi nyeupe kuliko sisi na tunajizarau sana tunataka tufanye kitu chenye kufanana nao hali ya kuwa njia zipo tofauti na matokeo mamoja tu.
 
Hakuna shida ndio ufahamu wako umegotea hapo.
 
Hakuna shida ndio ufahamu wako umegotea hapo.
Kufunga watoto shingoni, viunoni, kichwani, tumboni, vifuani, miguuni, na tena wengine huchanjiwa kwenye ndimi, mahirizi ni kukosa maarifa sahihi.

Tuanzie hapa:-
1) Nani anayetengeneza hizo ndumba?

2). Maarifa ya kutengeneza hizo juju yalianzia kwa nani na ilikuwaje?

Naomba jibu kwa uvumilivu. Lengo hapa ni kusaidiana.
 
Ngoja nikukanushe mkuu,kwanza hizo sio ndumba hizo ni tiba kama tiba nyingine. Suala kuwa zilianzia wapi embu rejea huko kijijini ambako kuna chimbuko lenu tiba za asili hazikuwepo? Labda niulize swali huko kwenye asili yenu unataka kuniambia kuwa tiba za asili hazipo? Watu walikuwa wanatibiwa kwenye hospital hizi za kizungu ama! Kwa iyo usiseme wanaovaa hizo vidudu si kukosa maarifa wale Wana akili timamu kama wewe.
 
Jibu swali kiongozi, uwepo ama kutokuwepo, iwe tiba iwe kinga kama unavyoweza kuivalisha suti, haiondoi ushetani wake.

Ninataka tujadiliane siyo kunipa kazi ya kufanay research mimi wakati mimi hadi nasema haya ninayo research ya kutosha kuliko kawaida. Ili tujadiliane jibu swali lla mwongozo wa mjadala. Hujui mijadala ya kitaaluma, hakuna kosa wala sababu ya mihemuko na ushabiki. Kaa kando subiri wanaofahamu na waliotayari kujadiliana kwa uwazi waje wajibu, tuzungumze. Shetani ni shetani hata ukimvalisha kanzu nyeupe.
 
1:unaposema ndumba sijajua unaamanisha nini?!!kama unamaanisha dawa hilo anaweza kutengeneza yoyote mwenye maarifa na hiyo ndumba kutokana na tatizo husika.2;unaposema maarifa ya kutengeneza hizo juju hapa tena unaamanisha uchawi kwa tafsiri yetu ya kiswahili chetu,kama unaamanisha pia hizo dawa maarifa yake yametoka wapi na kwa nani hayo ni maarifa kutoka kwa watu wenye ujuzi,kwa mfano sisi kwetu kuna kitu huwa kinaitwa kimeo na wengi huwa wanakatwa tiba yao,Ila kwengine huwa kuna dawa huwa wanapaka na kinasagika kinakwisha!! Mfano usukumani hawakati.halafu jiulize hivi kati ya hizi tiba za kzungu( hospital ) na tiba za jadi zipi zilizoanza na kipi kinapaswa kiitwe Tiba mbadala.?!!kuna tiba nyingi za asili ambazo hazina ithibati za moja kwa moja lakini zina matokeo ya asilimia 100,halali au sio halali hiyo inategemea umesoma kutoka wapi,kwetu degdege mtoto ananing'inizwa kwenye tundu LA choo kichwa chini miguu juu baada ya hapo inabaki history kwenye degdege,ni mengi Tena mengi .
 
Wewe unachanganya imani na tiba ,hilo ni tatizo kwako,tiba haihusiani na imani
 
Ule ni ulozi tu...mtoto anaingizwa kwenye maagano ya kimizimu mapema kabisa.
 
Jamani watoto wachanga kawaida kuharisha na kama tumbo pia limejaa ni gesi,na wengine wanakuwa mpaka na COLIC na mtoto anakuwa
analia mfululizo au bila sababu.Inasababishwa na vitu tofauti kama digestive system haipo fully developed,hakuna bacteria wakutosha tumboni,allergies n.k
 
Sawa bana ila wengine wanapigwa vijicho
 
Tuma na kapicha
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
 
Kuna Mama Mmoja nilimkuta Kamvalisha Mwanae na nilipojaribu Kumuelimisha kwa Kumuambia kuwa huo ni 'Upuuzi' na kutaka Kumvua alinitishia kuwa nikithubutu tu nakuwa Chura Maji muda huo huo nikasalimu Amri.

Nashukuru Mungu sikuvalishwa kabisa.
Una elimu gani? Mbona swali la kitoto!
Unafahamu nini kuhusu mila na desturi?! Pia tofauti za kijamii.?
Hivi huko mashuleni mlienda somea ujinga!!?
 
Ni sawa na mengine mengi zaidi ya hayo yapo pia,ndio maana tunawafunga mvuje wasistukestuke usiku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…