Hivi wabongo hawafahamu Afrika Kusini ina makabila mengine zaidi ya Wazulu?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Sijawahi kuelewa kwanini Wabongo wengi wanaichukulia Afrika Kusini kama nchi ya Wazulu wakati wazulu wanakadiriwa kuwa milioni 12 tu kati ya watu milioni 60.

Kuna mtu nimekutana naye anasema Wazulu wamechachama kupeleka wanajeshi wengi zaidi Congo asijue hata Ramaphosa mwenyewe sio Mzulu.

Ushamba mtupu.
 
Ni mazoea tu kama ambavyo zamani kila pikipiki tulikuwa tunaita Honda au kuna mji daladala wanaita vi Ford
 
hiyo south si ndiyo inaitwa ZULULAND?
 
Ni mazoea tu kama ambavyo zamani kila pikipiki tulikuwa tunaita Honda au kuna mji daladala wanaita vi Ford
Mazoea mengine ni kutokana na ushamba au kutokufahamu, ni sawa na mtu atuite Watanzania wote Wamasai au Wasukuma kwa sababu ndio kabila analolifahamu tu.
 
bongo wengi wetu vichwa vitupu, cha kuisikitisha zaidi ni too much know.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…