Hivi wafanyakazi wa TRA mna matatizo gani? Mnaomba omba hela za rushwa kila huduma kwa mteja!

CCM inatesa sana wananchi, rushwa,ufisadi, unyanga'anyi inavilea sana
 
Iyo biashara yako ina mda gani?
Unataka kujua ili iweje? Wewe changia achana na maswali yasiyo na kichwa wala miguu! Wewe kama unapenda kuanika mambo yako ni wewe sio kila mtu!
 
Unataka kujua ili iweje? Wewe changia achana na maswali yasiyo na kichwa wala miguu! Wewe kama unapenda kuanika mambo yako ni wewe sio kila mtu!
Kama ina mwaka au mwaka mmoja nikitaka kujua kama ulishafungua uzi kipindi Magu yuko hai ukalalamikia kudai rushwa tena ofisini kabisa hapo TRA? Kwanini unadaiwe sasa umsingizie Magu?
 
Kama ina mwaka au mwaka mmoja nikitaka kujua kama ulishafungua uzi kipindi Magu yuko hai ukalalamikia kudai rushwa tena ofisini kabisa hapo TRA? Kwanini unadaiwe sasa umsingizie Magu?
Kwa ujumla suala la Rushwa lipo siku zote hata kipindi cha nyuma naanza biashara niliombwa rushwa na ilikuwa kipindi cha Magu! Ni mwendelezo wa tabia za wafanyakazi wa TRA wao kitu kidogo ni kawaida ila shida ni kuwa kwa mtu asiye na kitu kupata huduma na hii hupelekea picha mbaya sana kwa serkali!
 
Nilichoona TRA hasa kitengo cha kubadilisha umiliki wa Gari, kuna mama pale hafanyi kazi kama hujamuwekea pesa kwenye document zako kupata Control namba ilinichukua massa 7 lakini kuna vishoka wanamuita mama nae anaitika na kuwapa control namba ilibidi niwe Mkali ndipo akanitolea kwa kweli wafanyakazi wa kitengo kile wamejiwekea malengo ya kukusanya pesa za hongo kwa siku na kama kazi haina hongo haifanywi sijui tunaelekea wapi??!! Hebu vyombo husika fuatilieni hapo
 
Hivi hawa watu hawasimamiwi? Why hawajafungiwa camera kwenye maeneo yao ya kazi? Serikali mnafeli wapi?
 
Hio kazi ya watoza ushuru sijui ina laana,hata kwenye biblia watoza ushuru walikuwa watu wa ovyo.
Kaja Raisi Mkapa kawafukuza wengi na kuajiri wapya lakini mambo ni hayo hayo.
Kuna wakati TRA hupanga kwenye majengo binafsi au ya umma, LAKINI wapangaji wengine wanakuwa na wasiwasi wa jengo kuunguwa kama alivyonidokeza jamaa mmoja siku chache baada ya jengo la NASACO kuungua.
Nikamuuliza kulikoni akasema walipanga jengo la NASACO,enzi hizo lilikuwa ndio jengo la kisasa liko karibu na police traffic .
Kasema TRA nayo ilikuwa na ofisi humo,mara ukatokea moto katika ofisi ya TRA lakini wakawahi kuuzima.Lakini haikupita muda labda miezi 6 hivi, jengo zima liliteketea kwa moto,akishauri wajenge yao na wakae wao tu ni nuksi.
 
Tatizo siyo TRA bali tatizo nchi inaongozwa na Rais fisadi ambae anahamasisha ufisadi kwenye serikali yake tena kupitia TV ya Taifa🤡🤡🤡
Your browser is not able to display this video.
 
Nenda kwa branch manager mwambie shida yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…