Hivi wale wakaguzi wa shule bado wapo?

Hivi wale wakaguzi wa shule bado wapo?

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Zamani enzi zetu, kila mwaka tulikuwa tunaona gari la waguzi wanakuja na kukaa shuleni walau siku tatu hadi wiki wakifuatilia maendeleo mbalimbali (sifa za waalimu, vifaa, majengo nk nk)

Nimejiuliza kwa sababu, kwa miaka hii unaweza kusikia Muandishi wa habari anaripoti madarasa yanataka kuangukia wanafunzi, au yame ezekwa viwango duni kabisa, au wanafunzi wamekalia mawe, au shule ina waalimu wawili nk nk nk taarifa hizo zikitoka kila mtu wakiwepo walipewa jukumu la kusimamia nao wanashangaa na kuanza kukurupuka...

Kama bado wapo hata kama wangeweza kupitia shule zote ndani ya miaka miwili walau kwa siku mbili kwa shule...nafikiri wakiwa na macho ya kuona wangekuwa wa msaada sana
 
Wapo tena Wana jina jipya, "Wadhibiti ubora". Suala ni je wanatoka ofisini? Na kama wakitoka je, wanaweza kuiandikia serikali hati mbaya na kulazimisha wafungue shule?
 
Watakwambiaa shule za nn wakati makanisa yanalipa na yanakupa njia ya uzimaa..
FB_IMG_1722541036731.jpg
 
Back
Top Bottom