Hivi wanaume kwenye hii mikoba huwa wanaweka nini?

Hivi wanaume kwenye hii mikoba huwa wanaweka nini?

Mmh. Nimejikuta napatwa na mshangao. Kazi ipo lakini sababu tunakoelekea watatupita sisi wanawake.

Pia niseme jibu halitapatikana sababu sidhani kama itatokea Me wa jf aseme huwa anabebaga kapochi. Hahaaaa.


Mie nnabeba kabegi kama hako japo sio kila mahali. Inategemea na nnachotakiwa kwenda nacho.
 
Mie nnabeba kabegi kama hako japo sio kila mahali. Inategemea na nnachotakiwa kwenda nacho.
Doooh kaka yangu mkubwa alikua anabeba ka kishikaji anaweka hela, simu, sigara zake na kila kolokolo maana alikua mtu wa tungiiiiiii na hiyo tabia alikua nayo alipotoka nje huko kwa trampuuuu ila enzi zile za rais bush...ila now sioni tena naona amekua, hizo kubeba pochi ni tabia za umama umama kuzidi
 
[emoji44][emoji44][emoji44] unakutana na tissue pamoja na brush ya viatu kweeeeli wanaume.
 
Watu mnakua wajinga wajinga na washamba. Haya mimi binafsi nikibeba begi aina hiyo nakua na power bank, nakua na antibacterial wipes, vitambaa ziada sababu na sweat profusely, nakua na kitabu (hii ni lazima) cha kusoma napokua ndani ya daladala. Badala ya kuchat au kukaa idle napokua ndani ya daladala nakua nasoma. Au natoa simu nasoma soft copy ya kitabu.
 
Ukiwa inje ndo uta jua umuhim wake , like kubeba passport, power bank kama mnavo jua smartphone nying hazikai na charge, wengine wana Weka camera ndogo, earphones, Busines card wallet, some receipts za madukan kama ume weka Oder kwa wafanya biashara nk.
 
Back
Top Bottom