Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

mwanamke hawezi timiza majukumu ya mwanaume, mwanaume akaoshe vyomy,mwanamke akafungue spare tyre apige tumuone
 

Hapo itakuwa hakuna namna zaidi ya kufanya mwenyewe kama mwanamke,sometimes unaacha vitu vipite tu bila kubishana
 
You aren't serious are you? Halafu kwenye kutongoza mbona wanaume siku hizi mnatulazimisha tuwatongoze? Hamuoni kama hata hapo napo nyie ndo mnaotaka usawa?
wanaume wanawalazimisha wanaume wawatongoze,wapi huko??? mbona sijawahi ona hiyo
 
Hata mwanaume ni binadamu kuna muda anaweza kushindwa sehemu na akasaidiwa na mwanamke
 
Sasa kama ni kukwepa manyanyaso ya kifedha, swala la kushupaza shingo limetokea wapi
 
Hahahha umeongea point kubwa sana.Kitu ambacho wazungu na watu wa haki za binadamu wanajaribu kuwaaminisha wanawake ni kwamba they are not strong enough kwamba watafute position kubwa zaidi ya hiyo bahati mbaya ndo wanatoka kwenye ukubwa wanawapeleka kwenye udogo..

Wao wanaaminishwa ili uwe strong lazima ufanye yote anayofanya mwanaume ubebe zege,uhudumie na wewe,uteseke na makazi magumu.Swali Ni Je mbona idadi ya wanaume wanaotamani kubeba mimba nakufanya majukumu kama mwanamke bado ipo chini??

Mwanamke hatakiwi kufanya kile mwanaume anachoweza,mwanamke anatakiwa kufanya kile mwanaume asichoweza.

Ila kitaeleweka tu [emoji3][emoji3]
 
Ndo ujiulize hicho kimbelembele kawapa nani mbona sisi hatuna?????????hamna mwanaume mwenye MDA wakufanya majukumu ya kike ila nyie mpo busy kung"'ang'ania majukumu yetu ili muwe strong woman...Tukiwapa hayo majukumu mnalalamika[emoji3][emoji3][emoji3]. Eti Wanaume siku hizi hawafanyi majukumu Yao, Nani kakutuma ufanye??????
 
Hivi kwani bado unaongelea usawa au unaongelea mgawanyo wa majukumu? Kwani nani kasema wanaume na wanawake tuko sawa? Hebu nukuu hiyo sehemu niliyosema hivyo nikufafanulie vizuri, wanaume na wanawake hatuko sawa ila inapokuja kwenye swala la majukumu usiniambie maswala ya kujikinga na majambazi kitu ambacho ni tendo la dharura tu na siyo tendo la kila siku

Kwanza ulishakubaliana na mimi hapo juu kuwa ndoa ambazo mwanamke ndo anafanya majukumu mengi kuliko mwanaume hazifai yaani ilitakiwa mjadala uishie pale huku kwingine tunatafuta ligi tu yaani mimi mashaka yangu makubwa ni pale ninapoona mwanamke anafanya majukumu mengi kuliko mume wake yaani hiyo tu ndo hoja yangu ya msingi na hapa ndipo wanaume wengi wanapobisha
 
kwenye nini hasa!? actually you control us sexually na hapo ndio sehemu pekee ulipo na nguvu ya ushawishi.
Unadhani ni kwanini Mungu alimwambia mwanaume amtawale mwanamke baada ya kula tunda na siyo kabla ya kula tunda?
 
nauliza hivi,baba ako kuosha vyombo, kukata nyanya na vitunguu,kufagia uwanja,kukuna nazi, kupiga deki,wewe unaona sawa????
Anafanya hayo katika mazingira gani? Uliza vizuri swali lako ndo nitakujibu maana naona wewe unataka ligi tu hapa kama hauna hoja basi kaa kimya waachie wenye hoja.
 
Equity.
Equality.

Haitakuja tokea wanawake wakawa equal na wanaume, ki2 ambacho wanawake wanatakiwa kukipigania ni equity. Kuongelea mambo ya equality ni propaganda tu zisizo na mashiko yeyote.

-Equality means ME na KE mgawane miezi ya kubeba ujauzito.
-Equality means ME na KE wagawane miezi ya kunyonyesha mtoto.
- Equality means KE na mimba yake akatafute chakula. na mahitaji mengine ya kifamilia.
-Equality means KE na ME wawe na same physics.
-Equality means ME na KE wawe na same biology.
-Equality means ME na Ke wawe na same psychology.

Ukiangalia kiuhalisia hakuna term ya usawa unapoongelea wanawake na wanaume. Fighting a war against nature ni moja kati ya vitu vinavyo prove kwamba KE mna akili fupi.

Mwanamke anatakiwa atreatiwe with fairness katika majukumu yake kama mwanamke. Majukumu ya mwanamke hayakuwekwa na mwanaume au majukumu ya mwanaume hayakuwekwa na mwanaume bali nature ndio inaprovide majukumu.
(Mfano) jukumu la kubeba mimba na kunyonyesha litabaki kuwa la mwanamke hata mkeshe mwaka mzima barabarani na mabango yenu.
 
kwenye kuzaa unazaa na wanawake wenzako au???
Yaani unafananisha zoezi la kumwaga mbegu tu na zoezi la kubeba mimba, kuzaa watoto na kunyoyesha watoto? Wewe hebu nenda kabishane na wavulana wenzio huko mimi hapa nabishana na wanaume tu.
 
wanaume wanawalazimisha wanaume wawatongoze,wapi huko??? mbona sijawahi ona hiyo
Kuna mada ilianzishwa humu kuwa je ni sawa mwanamke kumtongoza mwanaume? Niliona wanaume wengi walisema ndiyo eti kama tumewapenda tusiogope kuwatongoza ila wanawake wengi walisema hapana kutokana na tamaduni za Africa mwanaume ndo anayetongoza

Na hata mtaani pia naona wanaume wengi wanataka na wanawake tuanze kutongoza kama wao ila wanawake wengi wanaona aibu na hata wanaotongoza wenyewe wanatongoza kwa ishara na siyo moja kwa moja nikajiuliza sasa hawa si ndo wanasema hawataki usawa? Sasa na wanawake tukianza kutongoza kama wanaume hakutakuwa na usawa kweli hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…