Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Katika maisha Ya mwanadamu hitaji moja wapo kubwa na la muhimu ni ulinzi.

hatuweza tukaacha kutoa mfano wa majambazi wakati ndio yanayotutushia uhai wetu...

nakuuliza tena, mimi niko tayari kuosha vyombo,kupika,kupiga deki n.k

sasa je, wewe uko tayari kupambana na hata vibaka waliokuja kutuvamia huku mimi nimejificha chini ya uvungu na watoto?

maana ndio mnachokitaka hasa kuwa sawa na mwanaume kwenye kila kitu.
mwanamke hawezi timiza majukumu ya mwanaume, mwanaume akaoshe vyomy,mwanamke akafungue spare tyre apige tumuone
 
Ni sawa ila mimi naona kama mara nyingi wanawake ndo tunaweza kufanya majukumu yote ambayo yapo ndani ya uwezo wetu ila wanaume kuna baadhi ya majukumu hawawezi kufanya hata kama yapo ndani ya uwezo wao eti kwa sababu tu kwenye jamii yamezoeleka kuwa ni majukumu ya kike na inaonekana ni aibu kwa mwanaume kuyafanya hii imekaaje?

Hapo itakuwa hakuna namna zaidi ya kufanya mwenyewe kama mwanamke,sometimes unaacha vitu vipite tu bila kubishana
 
You aren't serious are you? Halafu kwenye kutongoza mbona wanaume siku hizi mnatulazimisha tuwatongoze? Hamuoni kama hata hapo napo nyie ndo mnaotaka usawa?
wanaume wanawalazimisha wanaume wawatongoze,wapi huko??? mbona sijawahi ona hiyo
 
Kwamba mmoja akijisikia hawezi au hajisikii kufanya kitu anaacha sio??Mambo hayataenda labda mmoja ajifanye mjinga.Hii haina tofauti sana na kauli ya mwanamke mvivu anayejaribu kukataa majukumu yake kwa kauli/mbinu za kuzunguka.

Kwa mtazamo wangu inabidi mwanaume asimame kama kiongozi kwa busara kuhakikisha mambo yanaenda ipasavyo.
Hata mwanaume ni binadamu kuna muda anaweza kushindwa sehemu na akasaidiwa na mwanamke
 
Mimi naona hii haki sawa ilitokana na baadhi ya wanaume kutokutimiza majukumu yao kwa wake zao maana majukumu ya mwanaume ni kutafuta pesa na kuhudumia mke na watoto na majukumu ya mwanamke ni kufanya kazi za ndani na kulea mume na watoto ila kuna wanaume waliwanyanyasa wake zao kwa sababu walijua kuwa wake zao waliwategemea wao kwa kila kitu

Ndipo sasa wanawake wakaona kwanini wanyanyaswe wakati sisi wote ni binadamu basi na wao wakaona waanze kujitafutia pesa zao wenyewe ili wasinyanyaswe tena na ndipo haki sawa ilipoanzia sasa hii ni kwa upande wa kiuchumi

Haki sawa nyingine inayoongelewa ni ile ya kupendana, kuvumiliana, kusameheana na kuheshimiana na hii ilitokana na kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanataka wao tu ndo wapendwe, wavumiliwe, wasamehewe na waheshimiwe na wake zao ila wao hawana muda wa kufanya hayo kwa wake zao

Na wake zao wakikosea basi hao hao wanaume aidha watawapiga watawasaliti watawapa talaka au watawaongezea wake kwa kisingizio cha kuwa wao ndo wanatoa mahari kwahiyo wanaona wakishatoa tu hizo mahari kazi yao imekwisha kazi inabaki kwa mwanamke sasa kuhakikisha anafanya mengine yote kulinda ndoa je hiyo ni sawa?
Sasa kama ni kukwepa manyanyaso ya kifedha, swala la kushupaza shingo limetokea wapi
 
Mimi ninahisi uwezo aliopewa mwanamke Ni mkubwa Sana kulinganisha na mwanaume. Mwanamke ndiye mwenye uwezo wa kuuhifadhi uhai wa binadamu kwa miezi 9 na pia kuutunza kwa miaka mingi zaidi. Mwanamke ni safe keeper wa jamii, mwanamke Ni chombo Cha manung'uniko ya dunia hii kwa nafasi Kama mke na Kama mama. Pepo ya dunia hii ipo kwenye miguu ya mwanamke

Huwa nasikitika nikiona mwanamke akijaribu kuwa Kama mwanaume ili ajihisi superior. MWANAMKE YOYOTE ANAYETAFUTA USAWA NA MWANAUME HUPOTEZA NGUVU YAKE KAMA MWANAMKE.
Hahahha umeongea point kubwa sana.Kitu ambacho wazungu na watu wa haki za binadamu wanajaribu kuwaaminisha wanawake ni kwamba they are not strong enough kwamba watafute position kubwa zaidi ya hiyo bahati mbaya ndo wanatoka kwenye ukubwa wanawapeleka kwenye udogo..

Wao wanaaminishwa ili uwe strong lazima ufanye yote anayofanya mwanaume ubebe zege,uhudumie na wewe,uteseke na makazi magumu.Swali Ni Je mbona idadi ya wanaume wanaotamani kubeba mimba nakufanya majukumu kama mwanamke bado ipo chini??

Mwanamke hatakiwi kufanya kile mwanaume anachoweza,mwanamke anatakiwa kufanya kile mwanaume asichoweza.

Ila kitaeleweka tu [emoji3][emoji3]
 
Ni sawa ila mimi naona kama mara nyingi wanawake ndo tunaweza kufanya majukumu yote ambayo yapo ndani ya uwezo wetu ila wanaume kuna baadhi ya majukumu hawawezi kufanya hata kama yapo ndani ya uwezo wao eti kwa sababu tu kwenye jamii yamezoeleka kuwa ni majukumu ya kike na inaonekana ni aibu kwa mwanaume kuyafanya hii imekaaje?
Ndo ujiulize hicho kimbelembele kawapa nani mbona sisi hatuna?????????hamna mwanaume mwenye MDA wakufanya majukumu ya kike ila nyie mpo busy kung"'ang'ania majukumu yetu ili muwe strong woman...Tukiwapa hayo majukumu mnalalamika[emoji3][emoji3][emoji3]. Eti Wanaume siku hizi hawafanyi majukumu Yao, Nani kakutuma ufanye??????
 
my statements are still in logical table.

Suala la ulinzi wala hata sio jukumu la kibailojia, ni jikumu ambalo jinsia yoyote anafanya vizuri kabisa. Ndio maana siku hizi mnakuwa mpaka mageneral wa jeshi, ukienda kwenye jeshi la marekani hadi vitengo vigumu kama navy seal kuna wanawake wapo.

Hii inatuonyesha kuwa tofauti zetu za kibailojia hazikufanyi wewe ushindwe kuwa mlinzi wa familia.

Naona wewe ndio unaingiza masuala ya kuzaa kitu ambacho ni irrelevant kabisa hapa.

Nakuuliza tena, kuosha vyombo, kupiga deki n.k mimi niko tayari, je wewe uko tayari kuniokoa kwenye hatari yoyote ile hasa dhidi ya maadui wenye silaha kali?

ukishindwa kujibu hili swali basi mjadala unaishia hapa, na utakuwa umekubali kuwa mwananke kamwe hawezi kuwa sawa na mwanaume.
Hivi kwani bado unaongelea usawa au unaongelea mgawanyo wa majukumu? Kwani nani kasema wanaume na wanawake tuko sawa? Hebu nukuu hiyo sehemu niliyosema hivyo nikufafanulie vizuri, wanaume na wanawake hatuko sawa ila inapokuja kwenye swala la majukumu usiniambie maswala ya kujikinga na majambazi kitu ambacho ni tendo la dharura tu na siyo tendo la kila siku

Kwanza ulishakubaliana na mimi hapo juu kuwa ndoa ambazo mwanamke ndo anafanya majukumu mengi kuliko mwanaume hazifai yaani ilitakiwa mjadala uishie pale huku kwingine tunatafuta ligi tu yaani mimi mashaka yangu makubwa ni pale ninapoona mwanamke anafanya majukumu mengi kuliko mume wake yaani hiyo tu ndo hoja yangu ya msingi na hapa ndipo wanaume wengi wanapobisha
 
kwenye nini hasa!? actually you control us sexually na hapo ndio sehemu pekee ulipo na nguvu ya ushawishi.
Unadhani ni kwanini Mungu alimwambia mwanaume amtawale mwanamke baada ya kula tunda na siyo kabla ya kula tunda?
 
nauliza hivi,baba ako kuosha vyombo, kukata nyanya na vitunguu,kufagia uwanja,kukuna nazi, kupiga deki,wewe unaona sawa????
Anafanya hayo katika mazingira gani? Uliza vizuri swali lako ndo nitakujibu maana naona wewe unataka ligi tu hapa kama hauna hoja basi kaa kimya waachie wenye hoja.
 
Habari za usiku huu wana JF?

Mie wala siyo mwingi wa habari ila nilitaka tu kuwauliza ninyi kaka zetu hili swali kama kichwa cha mada kinavyojieleza hapo juu.

Swali: Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha usawa kivipi yaani kwenye mambo yepi haswa?

Swali la nyongeza: Je, mnataka wanawake tusifanye makosa ila wanaume mfanye makosa halafu wanawake tukae kimya tusiwaambie na wala tusiwafanye chochote au mnatakaje?

Naombeni majibu yenu tafadhali na hata wanawake wenzangu pia mnaweza kujibu chochote mnachojua kuhusiana na hayo maswali maana mimi sina majibu kabisa.
Equity.
Equality.

Haitakuja tokea wanawake wakawa equal na wanaume, ki2 ambacho wanawake wanatakiwa kukipigania ni equity. Kuongelea mambo ya equality ni propaganda tu zisizo na mashiko yeyote.

-Equality means ME na KE mgawane miezi ya kubeba ujauzito.
-Equality means ME na KE wagawane miezi ya kunyonyesha mtoto.
- Equality means KE na mimba yake akatafute chakula. na mahitaji mengine ya kifamilia.
-Equality means KE na ME wawe na same physics.
-Equality means ME na KE wawe na same biology.
-Equality means ME na Ke wawe na same psychology.

Ukiangalia kiuhalisia hakuna term ya usawa unapoongelea wanawake na wanaume. Fighting a war against nature ni moja kati ya vitu vinavyo prove kwamba KE mna akili fupi.

Mwanamke anatakiwa atreatiwe with fairness katika majukumu yake kama mwanamke. Majukumu ya mwanamke hayakuwekwa na mwanaume au majukumu ya mwanaume hayakuwekwa na mwanaume bali nature ndio inaprovide majukumu.
(Mfano) jukumu la kubeba mimba na kunyonyesha litabaki kuwa la mwanamke hata mkeshe mwaka mzima barabarani na mabango yenu.
 
kwenye kuzaa unazaa na wanawake wenzako au???
Yaani unafananisha zoezi la kumwaga mbegu tu na zoezi la kubeba mimba, kuzaa watoto na kunyoyesha watoto? Wewe hebu nenda kabishane na wavulana wenzio huko mimi hapa nabishana na wanaume tu.
 
wanaume wanawalazimisha wanaume wawatongoze,wapi huko??? mbona sijawahi ona hiyo
Kuna mada ilianzishwa humu kuwa je ni sawa mwanamke kumtongoza mwanaume? Niliona wanaume wengi walisema ndiyo eti kama tumewapenda tusiogope kuwatongoza ila wanawake wengi walisema hapana kutokana na tamaduni za Africa mwanaume ndo anayetongoza

Na hata mtaani pia naona wanaume wengi wanataka na wanawake tuanze kutongoza kama wao ila wanawake wengi wanaona aibu na hata wanaotongoza wenyewe wanatongoza kwa ishara na siyo moja kwa moja nikajiuliza sasa hawa si ndo wanasema hawataki usawa? Sasa na wanawake tukianza kutongoza kama wanaume hakutakuwa na usawa kweli hapo?
 
Back
Top Bottom