Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

mnajidharau wenyewe kiasi kwamba mnanekana mna akili fupi,kwa mfano unamhonga mwanamke kwa 20k,kwa hiyo umemnunua kwa 20 k,sasa kwa nini usimdharau
Huyo mwanamke unayetembea naye unakuwa na mpango wa kumuoa na kutokumsaliti?
 
Habari za usiku huu wana JF?

Mie wala siyo mwingi wa habari ila nilitaka tu kuwauliza ninyi kaka zetu hili swali kama kichwa cha mada kinavyojieleza hapo juu.

Swali: Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha usawa kivipi yaani kwenye mambo yepi haswa?

Swali la nyongeza: Je, mnataka wanawake tusifanye makosa ila wanaume mfanye makosa halafu wanawake tukae kimya tusiwaambie na wala tusiwafanye chochote au mnatakaje?

Naombeni majibu yenu tafadhali na hata wanawake wenzangu pia mnaweza kujibu chochote mnachojua kuhusiana na hayo maswali maana mimi sina majibu kabisa.
Tatizo hawa wenzetu Wanaongozwa na ubinafsi zaidi...mfano mwanaume akichepuka anaona ni halali yake kuchepuka ila mwanamke akichepuka ataambiwa ni malaya.... Mwanaume akizingua ndoa ikavunjika mke wake ataambiwa siyo mvumilivu,,, Mara sijui unatakiwa kumuombea mume wako..ila mwanamke akizingua ndoa ikavunjika ataambiwa ana tabia mbaya na mwanaume hataambiwa anatakiwa kumvumilia na kumuombea mwenzake


wanaume wanapenda wanawake wasiohoji kabisa hata pale wakiona mambo hayakai sawa....ukihoji unaambiwa unashindana na mwanaume, unataka usawa n.k. but mwanaume nani aliwaambia sisi siyo wanadamu? Sisi siyo wa kuhoji? Kwamba tukihoji ni kutaka usawa? Kwamba ninyi mna haki ya kukosea ila sisi hatuna? Kwamba ninyi ni bora kuliko sisi?

Siku mkiacha ubinafsi mtaacha na huu msemo wa kwamba wanawake tunapenda usawa



N.B Sisi kama binadamu tuko sawa humanly lakini mwanamke hawezi kuwa mwanaume na mwanaume hawezi kuwa mwanamke. Kila mtu atambue haki za mwenzake katika familia, ndoa na jamii kwa ujumla.
 
Sasa kama ni kukwepa manyanyaso ya kifedha, swala la kushupaza shingo limetokea wapi
Kwa sababu tayari wanawake wameingilia majukumu ya wanaume yaani kwa kifupi hiyo ni kama message kuwa wanawake wanatakiwa kuhudumiwa wakianza kujihudumia wenyewe au kuhudumia wanaume zao basi lazima wakae kwenye nafasi za wanaume zao tu hakuna namna hiyo ni nature
 
Hahahha umeongea point kubwa sana.Kitu ambacho wazungu na watu wa haki za binadamu wanajaribu kuwaaminisha wanawake ni kwamba they are not strong enough kwamba watafute position kubwa zaidi ya hiyo bahati mbaya ndo wanatoka kwenye ukubwa wanawapeleka kwenye udogo..

Wao wanaaminishwa ili uwe strong lazima ufanye yote anayofanya mwanaume ubebe zege,uhudumie na wewe,uteseke na makazi magumu.Swali Ni Je mbona idadi ya wanaume wanaotamani kubeba mimba nakufanya majukumu kama mwanamke bado ipo chini??

Mwanamke hatakiwi kufanya kile mwanaume anachoweza,mwanamke anatakiwa kufanya kile mwanaume asichoweza.

Ila kitaeleweka tu [emoji3][emoji3]
Hilo mbona linaeleweka mkuu? Sema sasa tatizo linakuja wanawake wasipofanya hizo kazi za kujitafutia kipato chao je wanaume mtawahudumia mahitaji yao yote kiuchumi bila kuwanyanyasa wala kusimanga?
 
hahaaaaaa[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]!! wanawake mna akili gani kwa mfano???
Nipe definition yako ya akili halafu ndo nitakwambia tuna akili gani
 
This is a FEMINISM THEORY formulated in EUROPE and AMERICA when a WOMEN started demanding women's rights on the grounds of political, social, and economic equality to men.
Equality feminism and American liberalism seek equality for every individual.
But this concept are suitable to western countries and America because they know how to practice in its and not to our most of African countries including Tanzania.
 
Ndo ujiulize hicho kimbelembele kawapa nani mbona sisi hatuna?????????hamna mwanaume mwenye MDA wakufanya majukumu ya kike ila nyie mpo busy kung"'ang'ania majukumu yetu ili muwe strong woman...Tukiwapa hayo majukumu mnalalamika[emoji3][emoji3][emoji3]. Eti Wanaume siku hizi hawafanyi majukumu Yao, Nani kakutuma ufanye??????
Hivi siyo nyie wanaume mnaosema mnataka wanawake wenye akili ya maisha na wanaojua kutafuta pesa? Tena si ndo mnasemaga hamtaki wanawake wenye njaa wanaowaomba pesa? Sasa kama mwanamke hatafuti pesa anatoa wapi pesa za kujikimu? Hapo maana yake si kwamba mnataka wanawake wanaotafuta pesa?
 
This is a FEMINISM THEORY and was formulated in AMERICA and WESTERN EUROPEAN COUNTRIES. This advocacy of women's rights on the grounds of POLITICAL, SOCIAL, and ECONOMIC EQUALITY to MEN.
EQUALITY FEMINISM and AMERICAN LIBERILISM SEEK EQUALITY FOR EVERY INDIVIDUAL.
Dhana hii katika nchi zetu za Kiafrika imekuwa na changamoto hasa katika kutafsiri maana halisi ya maneno mawili HAKI na WAJIBU.
Wanawake walio wengi wa kiafrika wanapenda kuona wanatendewa na wanaume HAKI lakini wanashindwa kutambua ni haki zipi ambazo wanapaswa kutendewa?
Pia wananwake walio wengi wa kiafrika wanapenda kuona wanaume wanatimiza WAJIBU lakini wanashindwa kutambua ni wajibu upi ambao wanapaswa kutekelezewa?
 
Equity.
Equality.

Haitakuja tokea wanawake wakawa equal na wanaume, ki2 ambacho wanawake wanatakiwa kukipigania ni equity. Kuongelea mambo ya equality ni propaganda tu zisizo na mashiko yeyote.

-Equality means ME na KE mgawane miezi ya kubeba ujauzito.
-Equality means ME na KE wagawane miezi ya kunyonyesha mtoto.
- Equality means KE na mimba yake akatafute chakula. na mahitaji mengine ya kifamilia.
-Equality means KE na ME wawe na same physics.
-Equality means ME na KE wawe na same biology.
-Equality means ME na Ke wawe na same psychology.

Ukiangalia kiuhalisia hakuna term ya usawa unapoongelea wanawake na wanaume. Fighting a war against nature ni moja kati ya vitu vinavyo prove kwamba KE mna akili fupi.

Mwanamke anatakiwa atreatiwe with fairness katika majukumu yake kama mwanamke. Majukumu ya mwanamke hayakuwekwa na mwanaume au majukumu ya mwanaume hayakuwekwa na mwanaume bali nature ndio inaprovide majukumu.
(Mfano) jukumu la kubeba mimba na kunyonyesha litabaki kuwa la mwanamke hata mkeshe mwaka mzima barabarani na mabango yenu.
Hata wanaume nadhani mnashindwa kuelewa ni usawa upi tunaoutaka mkuu usawa tunaoutaka siyo kimaumbile wala kimajukumu ila tunataka usawa kwenye mambo kama vile kupendana, kuheshimiana, kusameheana na kuvumiliana

Jamii nyingi za kiafrika zinataka mwanamke tu ndo ampende, amheshimu, amsamehe na amvumilie mwanaume ila mwanaume hatakiwi kufanya hayo eti kwa sababu tu ya mahari anayotoa kuoa kitu ambacho siyo sahihi

Yaani jamii zetu zinataka mwanaume akikosea aachwe tu na asifanywe chochote ila mwanamke akikosea apigwe, asalitiwe, apewe talaka au aongezewe mke sasa hiyo ni haki kweli?

Kwani ina maana kwenye ndoa ni mwanaume tu ndo anakosea mwanamke hakosei? Na kwanini mwanaume akikosea aachwe ila mwanamke akikosea aadhibiwe? Kwani wanaume makosa yenu ni madogo sana kuliko ya wanawake?
 
Tatizo hawa wenzetu Wanaongozwa na ubinafsi zaidi...mfano mwanaume akichepuka anaona ni halali yake kuchepuka ila mwanamke akichepuka ataambiwa ni malaya.... Mwanaume akizingua ndoa ikavunjika mke wake ataambiwa siyo mvumilivu,,, Mara sijui unatakiwa kumuombea mume wako..ila mwanamke akizingua ndoa ikavunjika ataambiwa ana tabia mbaya na mwanaume hataambiwa anatakiwa kumvumilia na kumuombea mwenzake


wanaume wanapenda wanawake wasiohoji kabisa hata pale wakiona mambo hayakai sawa....ukihoji unaambiwa unashindana na mwanaume, unataka usawa n.k. but mwanaume nani aliwaambia sisi siyo wanadamu? Sisi siyo wa kuhoji? Kwamba tukihoji ni kutaka usawa? Kwamba ninyi mna haki ya kukosea ila sisi hatuna? Kwamba ninyi ni bora kuliko sisi?

Siku mkiacha ubinafsi mtaacha na huu msemo wa kwamba wanawake tunapenda usawa



N.B Sisi kama binadamu tuko sawa humanly lakini mwanamke hawezi kuwa mwanaume na mwanaume hawezi kuwa mwanamke. Kila mtu atambue haki za mwenzake katika familia, ndoa na jamii kwa ujumla.
Aise nimekosa hata cha kuongezea ndugu yangu yaani umeenda mule mule hadi nimehisi kama nikiongezea hoja yangu naweza jikuta naharibu comment yako daah umemaliza kila kitu na natamani wanaume wote wangesoma hii comment yako wakaelewa ninachomaanisha
 
Hata wanaume nadhani mnashindwa kuelewa ni usawa upi tunaoutaka mkuu usawa tunaoutaka siyo kimaumbile wala kimajukumu ila tunataka usawa kwenye mambo kama vile kupendana, kuheshimiana, kusameheana na kuvumiliana

Jamii nyingi za kiafrika zinataka mwanamke tu ndo ampende, amheshimu, amsamehe na amvumilie mwanaume ila mwanaume hatakiwi kufanya hayo eti kwa sababu tu ya mahari anayotoa kuoa kitu ambacho siyo sahihi

Yaani jamii zetu zinataka mwanaume akikosea aachwe tu na asifanywe chochote ila mwanamke akikosea apigwe, asalitiwe, apewe talaka au aongezewe mke sasa hiyo ni haki kweli?

Kwani ina maana kwenye ndoa ni mwanaume tu ndo anakosea mwanamke hakosei? Na kwanini mwanaume akikosea aachwe ila mwanamke akikosea aadhibiwe? Kwani wanaume makosa yenu ni madogo sana kuliko ya wanawake?
kupendana, kuheshimiana, kusameheana na kuvumiliana... nikiangalia hivi vyote mnavyovililia ni EMOTIONAL DERIVED (mtu kama hakupendi hakupendi na hawezi kukuheshimu na kukuvumilia, an nothing can change that)

Bahati nzuri karne hii 99% ya wanawake hawachaguliwi wanaume wa kuwaoa. Ni vyema kuwa na mwanamme anaye kupenda, kuheshimu, kukusamehe unapokosea, na anaye weza kukuvumilia.
Mnafanya wrong personal choices alafu baadae mnalalamika kwamba waume zenu wanawanyanyasa[emoji1][emoji1][emoji1]
Kuwa on the safe side hakikisha mnatumia mapenzi kama kigezo cha kupata wenza na sio ki2 kingine.
 
Nahisi nipo nje ya mada kidogo lakini sometimes wanawake tunajichanganya

Tunataka haki sawa kwa wote wakati huo huo tuna ile kauli mbiu yetu eti wanawake tukiwezeshwa tunaweza...SMH!😔😔

Kwanini tuhitaji kuwezeshwa wakati tuko na mikono na miguu miwili mixer ubongo kama wanaume
Briliant,jibu limenyooka halina utata...
 
Kwa sababu tayari wanawake wameingilia majukumu ya wanaume yaani kwa kifupi hiyo ni kama message kuwa wanawake wanatakiwa kuhudumiwa wakianza kujihudumia wenyewe au kuhudumia wanaume zao basi lazima wakae kwenye nafasi za wanaume zao tu hakuna namna hiyo ni nature
Hivi huwa mnawachukuliaje wanawake wenzenu ambao japo wanajitafutia vihela vyao binafsi ila ifikapo kwenye majukumu ya kifamilia wapo very active and responsible. Kuanzia mume watoto na nyumba kwa ujumla. How do you feel kuona kuna wanawake wenzenu wa namna hio na wanaishi freshi na waume zao tu bila kujitutumua.
 
kupendana, kuheshimiana, kusameheana na kuvumiliana... nikiangalia hivi vyote mnavyovililia ni EMOTIONAL DERIVED (mtu kama hakupendi hakupendi na hawezi kukuheshimu na kukuvumilia, an nothing can change that)

Bahati nzuri karne hii 99% ya wanawake hawachaguliwi wanaume wa kuwaoa. Ni vyema kuwa na mwanamme anaye kupenda, kuheshimu, kukusamehe unapokosea, na anaye weza kukuvumilia.
Mnafanya wrong personal choices alafu baadae mnalalamika kwamba waume zenu wanawanyanyasa[emoji1][emoji1][emoji1]
Kuwa on the safe side hakikisha mnatumia mapenzi kama kigezo cha kupata wenza na sio ki2 kingine.
Sasa kama mwanaume hampendi na hamheshimu mwanamke husika kwanini anafikia hatua ya kumuoa? Kwani kuna wanaume wanalazimishwa kuoa?
 
This is a FEMINISM THEORY and was formulated in AMERICA and WESTERN EUROPEAN COUNTRIES. This advocacy of women's rights on the grounds of POLITICAL, SOCIAL, and ECONOMIC EQUALITY to MEN.
EQUALITY FEMINISM and AMERICAN LIBERILISM SEEK EQUALITY FOR EVERY INDIVIDUAL.
Dhana hii katika nchi zetu za Kiafrika imekuwa na changamoto hasa katika kutafsiri maana halisi ya maneno mawili HAKI na WAJIBU.
Wanawake walio wengi wa kiafrika wanapenda kuona wanatendewa na wanaume HAKI lakini wanashindwa kutambua ni haki zipi ambazo wanapaswa kutendewa?
Pia wananwake walio wengi wa kiafrika wanapenda kuona wanaume wanatimiza WAJIBU lakini wanashindwa kutambua ni wajibu upi ambao wanapaswa kutekelezewa?
Kwahiyo kwa mtazamo wako mkuu unaona ni haki zipi ambazo mwanamke anatakiwa kupewa na mwanaume wake na ni majukumu yepi ambayo mwanamke anatakiwa kutekelezewa na mwanaume wake?
 
Hivi huwa mnawachukuliaje wanawake wenzenu ambao japo wanajitafutia vihela vyao binafsi ila ifikapo kwenye majukumu ya kifamilia wapo very active and responsible. Kuanzia mume watoto na nyumba kwa ujumla. How do you feel kuona kuna wanawake wenzenu wa namna hio na wanaishi freshi na waume zao tu bila kujitutumua.
Kwani mbona wapo wanaume ambao pamoja na kutimiza majukumu yao ya kutafuta pesa bado wanawasaidia wake zao kufanya kazi za ndani na wanaishi vizuri tu? Ninyi wanaume wengine ambao hamfanyi hivyo mnajisikiaje? Exceptions lazima ziwepo tu kwa sababu in every general rule there is always an exception ila tuongelee kile kilicho sahihi kabisa
 
Hivi huwa mnawachukuliaje wanawake wenzenu ambao japo wanajitafutia vihela vyao binafsi ila ifikapo kwenye majukumu ya kifamilia wapo very active and responsible. Kuanzia mume watoto na nyumba kwa ujumla. How do you feel kuona kuna wanawake wenzenu wa namna hio na wanaishi freshi na waume zao tu bila kujitutumua.

Ndivyo wanavyotakiwa kuwa ila huu usawa unatuaribu sana
 
Back
Top Bottom