Hivi wanawake pesa zenu mnapelekaga wapi? Badilikeni!

Hivi wanawake pesa zenu mnapelekaga wapi? Badilikeni!

Poker

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
5,445
Reaction score
14,828
Kuna jamaa yangu ni mtumishi na mkewe pia ni mtumishi. Jamaa analipwa 900k na mkewe analipwa 1.3m ila sasa kodi ya nyumba, bili za umeme na maji analipa mwanaume, na bado ujenzi wa nyumba ni mwanaume apambane, ada ya shule ni mwanaume.

Hivi majuzi imebidi mwanaume amlipie vikoba mwanamke maana alikuwa anadaiwa na watu washatimba home kubeba vyao. Chanzo cha ugomvi kikaanza baada ya jamaa kumnyima mwanamke hela ya saloon kwa kuhoji wewe hela zako unapelekaga wapi?

Navyozungumza kesi ipo dawatini na ndoa ina ning'inia. Wanawake mmezidi badilikeni jueni saivi maisha ni 50/50 sio kuwa mzigo kama panya nyumbani huna faida kazi kuharibu tuu!
 
Wanawake ni wabinafsi, wanaishi nasi kwa mfumo wa CHANGU changu na CHAKO changu.

Pesa yake ni kwaajili ya kusaidia ndugu na jamaa zake tu ili wampongeze na kumsifu tu. Huku mwanaume ukipigika kuendesha familia.

Ndio maana sikuhizi wanawake wanamiliki pesa ndefu kuliko wanaume. Kwasababu pesa zao wanazihifadhi wakati za mwanaume zinatumika kwenye familia.
 
Wanawake ni wabinafsi, wanaishi nasi kwa mfumo wa CHANGU changu na CHAKO changu.
Pesa yake ni kwaajili ya kusaidia ndugu na jamaa zake tu ili wampongeze na kumsifu tu. Huku mwanaume ukipigika kuendesha familia.
Ndio maana sikuhizi wanawake wanamiliki pesa ndefu kuliko wanaume. Kwasababu pesa zao wanazihifadhi wakati za mwanaume zinatumika kwenye familia.
Sure mkuu!
 
Inabidi kama mwanaume uvunje ukimya, umkalishe chini mkeo mgawane majukumu, siyo wewe ubebe majukumu yote ya familia, Sasa yeye unaishi naye ili nini? Ni ngono tu?
Amekuja kuishi nawe ili kwa pamoja mshirikiane kujenga familia yeye ni msaidizi wako?
Haya maisha si yakuegemeana au kukomoana.
 
Kama anafanya kazi na mshahara wake hausaidii chochote kwenye familia, na unamhudumia pia mpaka pesa ya kusuka, condition inakuwa moja tu, kaa nyumbani ulee watoto nikuhudumie wewe na watoto, kinyume na hapo hana maana kuwepo kwenye familia, maana watoto hawapati malezi stahiki kutokana na ubize wa wazazi, bora angalau mama awe available kwa watoto then baba atafute kwa jasho!
 
Discuss about money mpangiane majukumu
Japo mwanaume lazima alishe familia na awe mstari wa mbele

Na Mwanamke lazima pia ujali gharama flani za familia yako
Wasomi wengi wanawake no wajuwaji ndo shida inaanzia Apo,wanasaidia familia ya kwao kuliko ata watoto wa kuwazaa,mzigo unabaki kwa mwanaume,huu ndo ukweli
 
Back
Top Bottom