Hiyo Tarehe 29 Hali itakavyokua huko staff

Hiyo Tarehe 29 Hali itakavyokua huko staff

Kwenye kikao saa 4
Mtaaluma:
*MUONGOZO WA SERIKARI KUHUSU MUHULA WA I NA II 2020 BAADA YA UGONJWA WA KORONA.*

*1. MUHULA WA KWANZA UTAANZA TAREHE 29.06.2020 MPAKA TAREHE 28.08.2020*

*2. LIKIZO FUPI ITAKUWA KUANZIA TAREHE 29.08.2020 MPAKA 06.09.2020*

*3. MUHULA WA PILI UTAANZA TAREHE 07.09.2020 MPAKA TAREHE 18.12.2020*

*3. SIKU TULIZOSOMA KABLA YA KUFUNGA SHULE KWAAJILI YA CORONA NI 52,SIKU ZILIZOBAKI KUKAMILISHA SIKU ZA MASOMO KWA MWAKA MZIMA NI 142,SIKU ZILIZOTOLEWA NA WIZARA KUFUNDISHA BAADA YA CORONA NI 125, HIVYO BASI ZITABAKI SIKU 17 KUKAMILISHA SIKU 194 ZA MASOMO KWA MWAKA MZIMA .*
*SIKU HIZO 17 ZITAFIDIWA KWA MASAA MAWILI YALIYOONGEZWA,AMBAPO JUMLA YA MASAA YA NYONGEZA NI 250 AMBAYO NI SAWA NA SIKU 30 ZA KAZI.(HIVYO BASI WANAFUNZI WATATOKA SAA 11 JIONI).*

*ZINGATIO.*
*HAKUNA SIKU ZILIZOPOTEA, SIKU ZOTE ZIMEFIDIWA.*

*4.ILI KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA KILA MWANAFUNZI MWENYE UMRI WA MIAKA MITANO NA KUENDELEA ANATAKIWA KUVAA BARAKOA.*

*6. MWANAFUNZI ASHONEWE BARAKOA YA KITAMBAA CHA PAMBA* *RANGI YA BLUU(BLUE), ANGALAU AWENAZO MBILI KILA SIKU KWAAJILI YA DHARURA.*

*7. MAJI NA SABUNI KWAAJILI YA KUNAWA MIKONO ATAPATA SHULENI.(MTOTO HARUHUSIWI KUPAKA AU KUJA NA VITAKASA MIKONO(SANITIZERS) KWASABABU ZINA HATARI YA KULIPUKA).*

*ASANTENI.*


Cc Smart911
 
Mwalimu mkuu : hivi Mr Mlevi mmoja ndo muda gani wa kuripoti shule mpaka kikao tumemaliza we haupo hivi ni shule gani umeona kuna utaratibu wa hovyo kiasi hicho .


Huku pombe zikiwa bado zipo kichwani akiwa anayumba yumba kidogo huku amevaa shati lake limejikunja halijapigwa pasi na suruali nyeusi iliyopauka anajibu


Mr mlevi mmoja :hii shule au kichuguu .tusichoshane hapa


Mwalimu mkuu: halafu unakujaje umelewa hayo sio maadili ya kazi kwanza utafundishaje


Mr mlevi : hizi ng'ombe unadhani zinaelewa basi halafu mbona mi sijalewa na hata nikinywa pombe huo ni mshahara wangu we haukuhusu .we mbona unanunua chipsi funga na hatusemi

Mwalimu mkuu : kausha basi we mtu ni mtu mzima ( akimbembeleza kwa sauti ndogo)

Mara madam Anna anadakia maongezi


Madam Anna : jamani sio vizuri Mr mlevi unachofanya unajishushia heshima hata wanafunzi wanakucheka huoni una jina zuri lakini wanafunzi washakupa nick name mwalimu mlevi


Mr mlevi : hakuna mwalimu ambae hana nick name we mwenyewe wanakuita madam cha wote .eti unajijushia heshima ( huku akiigiza sauti ya madam Anna kwa kebehi ) .kama ungekuwa unaijua heshima usingekuwa unagongwa na kila mwalimu wa field anaye kuja unadhani hatujui





Mr mlevi anatoka ofsini akipiga mluzi akielekea darasa la saba kufundisha hesabu


Akiwa darasani

Wanafunzi : shikamoo mwalimuuuu

Mr mlevi: sitaki salamu zenu na siku nikija kugundua ananiita mlevi nitakuja kumpiga mabanzi *****

Wanafunzi wanacheka


Mr mlevi : halafu Merry nilikwambia unione haukuja hii ni dharau kwahyo mi ni ng'ombe sio
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
PICHA LINAANZA
"Yule Mwalimu aliyezoea kuwahi kama kawaida saa 12:30 tayari yupo shuleni"

MUDA UNAZIDI KWENDA
Walimu karibu wote wameshafika staff

MARA GHAFLA
"Kanaingia kale ka madam kazuri kuliko wote staff. Kanaonekana kamekonda kidogo tofauti na mwanzo. Kanasalimia"
Miss staff: habari zenu walimu
Wanaitikia walimu wawili tu kati ya walimu 15

WABIASHARA NAO WAPO

Madam Asha: Jamani walimu nauza barakoa
"Walimu wote wanacheka kwa sauti wakuropoka nae karopoka.... Hee hee hee barakoa hizo kwiooo..."

KWA MBALI
Anaonekana mwalim Masamela ndo anaingia shuleni.. walimu wawili wa kike wanamuona kupitia dirisha..
Madam Joy: muoneni yule baba ananikera na suruali lake Lile kama kung'utio la mashineni
Madam Linda: muache baba wa watu kwa raha zake

MTAALUMA NAE
"Jamani walimu kumbukeni kuleta maandalio yenu kabla hamjaingia darasani"
Madam Eliza: we nawe una kihere here Yani watu hata hatujapumua umeanza na maandalio yako...

HUKU MWALIMU MNEMELE NAE ANAMWITA MWANAFUNZI
Mwl MNEMELE: "Hebu ng'ombe mmoja aje hapa nimtume"
MARA MWALIMU MKUU KAINGIA STAFF..
"Jamani walimu sa nne tutakua na kikao kwa hiyo msiondoke"...
Sir adam: chai ipo boss?
Mkuu: chai ipo ila vitafunwa mtajitegemea
Madam Tunu: Yani niache kwenda kunywa chai ya maziwa kwangu ninywe michai ya rangi iyo kazi sifanyi Mimi

SIR MADENGE NAYE ANAONEKANA ANAPEKUA KWENYE MABOX KISHA ANAANZA KULALAMA
"Yani hii staff bwanaa cku tunafunga shule niliacha vifaa vyangu vyote hapa sijui kuku gani kaja kuvihamisha sivioni
Mwl mkuu: "mwl MADENGE vifaa vyako nilivihamishia maana hapo niliona hapako salama sana"...

NAYE CHAPOMBE WA SHULE ANAWAZA KIMOYOMOYO
"Yani ngoja niombe ruhusa tu niseme naenda hospital nikapumzike nyumbani mie akili yangu Leo haipo sawa"

WALIMU
" wanaanza kuingia darasani mmoja mmoja hatimae ofisini wanabaki walimu wawili tu madam Anne na sir Chande
Madam Anne: niliku miss bebe wangu
Sir chande: mi mwenyewe nilikumiss kweli..

NB: Nawatakia maandaliza mema
"Kung'utio la mashineni" [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ng'ombe mmoja aje nimtume😀😀😀
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Tuko hapa
JamiiForums1034708099.jpg


Jr[emoji769]
 
Back
Top Bottom