Hizi drama kwenye treni ya SGR nadhani zina lengo ovu

Hizi drama kwenye treni ya SGR nadhani zina lengo ovu

Kwa muda sasa kumekuwa na shutuma kuhusu hujuma inayohusu treni ya SGR, tukumbuke huko nyuma kuliwahi kutolewa wazo la kuruhusu watu binafsi waweke vichwa na mabehewa yao kwenye huo mradi,

Wazo ambalo lilikuja mapema sana hata kabla treni hazijaanza kufanya kazi!

Nikiangalia tuhuma hizi za sasa naona kama zinatengenezwa ili ziwe kichocheo cha ajenda ya kuwa ili kuboresha ufanisi serikali iruhusu watu binafsi waingize injini na mabehewa yao kwenye SGR, tujiulize watu hao wanaopigiwa debe kabla ya wao kuomba ni akina nani?

Mimi ninadhani ni kati ya waliokuwa wanakwenda huko zilikotoka injini na mabehewa ya SGR, na je, wataleta mapya yapambane na haya yanayodaiwa kuwa ni mitumba?

Hebu tungoje kwani muda utajibu kitendawili hiki.
The end of the beginning.
Mkurugenzi wa TRC asimame imara, atajijengea heshima kubwa kabisa kwa mradi kama huu kusimama imara na kuonyesha dalili zote za kuingiza faida kubwa, tunafahamu wapo ambao hili wanaliona kwao ni hapana na wangependa mapato haya manono wayaingize mfukoni mwao, umefika wakati baada ya uwekezaji mkubwa TRC nayo ikatoa gawio nono la kustaajabisha kwa serekali yetu, wapo wengi kwa ulafi wao wanautamani mradi huu uwe wao, aidha serekali iwakodishe washenzi hao, badala ya mradi huu kusimamiwa na serekali yetu, tuwe imara tusichotwe mawazo, MAPUMBAVU yasiunase mradi huu kamwe!
 
waweke vibox vya maoni ya siri, watu wataje nani anafanya hujuma. wachunguzwe, na wakijulikana, huo ni uhujumu uchumi kama uhujumu uchumi mwingine tu. wanamchezea kizmkazi kwa sababu ni mwanamke. hivi angekuwa ni Magufuli, kungekuwa na ujinga kama huo? just imagine, wanamchezea uyo maza wapendavyo. nachelea basi kusema 2025 tunahitaji Rais mwanaume, kwetu sisi wa kijijini, mwanamke hata akienda kufukuza nyani wanaokula mahindi, nyani huwa hakimbii, ila mwanaume hata mdogo tu nyani anakimbia.
Samia kwa uanamke wake ameshafanya mengi sana ambayo wanaume watano waliyashindwa, huwezi ukayaona kwa sababu kichwani umeshatanguliza udhaifu wa kumtazama na kumhukumu kwa uanamke wake.

Kabla yake alikuwa mwanaume ambaye baadhi yetu walifanya sherehe siku kifo chake kilipotangazwa kwa umma, unajua kwanini kwa hao watu ilikuwa ni siku ya furaha?.
 
serikali ina watu wajinga..badala wabaki na jukumu la ulinzi wa miundombinu wao wanadhani ni sifa serikali kuisimamia TRC kwenye uendeshaji wa kila siku..tulishawaambia achia makampuni binafsi kwenye baadhi ya majukumu km ukatishaji tiketi na usimamizi wa abiria wakati wa kuingia na wakiwa safarini nk..wameshindwa DART ndio wataweza SGR..kulalamika hujuma ni ujinga, watafute wanaohujumu usilete excuse za reje reja..!
Huwezi ukaachia makampuni binafsi miradi kama hii nyeti ya kiuchumi.

Lazima "mkono" wa serikali uwepo.
 
una maana gani kusema hakuna wa kusimamia? hawapo wenye sifa kusimamia au uwezo? lkn kuwa na hisa si lazima uwe msimamizi wa mradi, mashirika yanaendeshwa kwa utaratibu ambao wanahisa wanataka, wakipendekeza MD apatikane kwa usaili na kwa ushindani..basi inakuwa hivyo..
KInachokoseka ni msimamizi mwenye uzalendo na uchu na mradi, visionary na mwenye jicho la kuona both long and short term of the project. Ili mirafi iwe endelevu even if it means working outside the books.
Ila sio hii ya kununu hisa na kupewa isimamizi wa mradi wanachofanya ni kutafta profit kwa walichokiweka.

Mfano TTCl wawekezaji walipata profit na kuondoka na chao. Pesa ilikuwepo ila Kilichokosekana ni mtu mwenye maono na kusamia miradi iwe endelevu isife. Ni bora mradi apewe mtu wa private sector au simamie atakua na uchungu nao kuliko shirika la serkali.
 
Private sector dunia nzima inaendeshwa kinyapara na results zinaonekana ,hii lazyfair ya serikali ni upuuzi ,bila mabadiriko ya kweli ya kimfumo kila siku kilio kitakuwa ni kile kile tu.
Ni sawa na kujenga ghorofa zuri kwenye msingi wa tofali za tope ,work done =zero
 
Huwezi ukaachia makampuni binafsi miradi kama hii nyeti ya kiuchumi.

Lazima "mkono" wa serikali uwepo.
Halafu usipotoshe kusema UKAACHIA..sina maana hiyo, mfano wanaochimba madini migodini ni serikali?? au madini si miradi nyeti kwa maana yako..? kwa maana ya kuwa na ufanisi serikali ielekeze nguvu nyingi kwenye kulinda na kusimamia miundombinu, mambo ya uendeshaji baadhi ya kazi wa-sub contract sekta binafsi, serikali hawana uwezo wa kubeba majukumu yote kwa utimilifu!
 
Unahisi kwanini taasisi kama Berkshire Hathaway, investment groups au holding companies hazimiliki kampuni moja 100%. Unakuta wanagawa mitaji kwenye makampuni tofauti hata elfu moja, kwanini wasiweke kampuni kubwa moja au mbili?

Mashirika ya hifadhi ya jamii hayawezi fanya betting eti yawekeze kwenye bandari hela zote. Ikitokea tsunami investment yao yote ipotee kwa pamoja. Sheria moja kuu ya uwekezaji, kuna FAIDA na HASARA. Wewe unafanya assumption kwamba bandarini hakuwezekani kutokea hasara. Kosa hilo
Hakuna aliyesema kuwa ni lazima wawekeze kwenye bandari pekee ni kwamba wanayo nafasi ya kuwekeza sehemu mbali mbali zinazo lipa kwa mtindo ule ule wa mgawanyo wa portfolio walizochagua.
 
Kwa muda sasa kumekuwa na shutuma kuhusu hujuma inayohusu treni ya SGR, tukumbuke huko nyuma kuliwahi kutolewa wazo la kuruhusu watu binafsi waweke vichwa na mabehewa yao kwenye huo mradi,

Wazo ambalo lilikuja mapema sana hata kabla treni hazijaanza kufanya kazi!

Nikiangalia tuhuma hizi za sasa naona kama zinatengenezwa ili ziwe kichocheo cha ajenda ya kuwa ili kuboresha ufanisi serikali iruhusu watu binafsi waingize injini na mabehewa yao kwenye SGR, tujiulize watu hao wanaopigiwa debe kabla ya wao kuomba ni akina nani?

Mimi ninadhani ni kati ya waliokuwa wanakwenda huko zilikotoka injini na mabehewa ya SGR, na je, wataleta mapya yapambane na haya yanayodaiwa kuwa ni mitumba?

Hebu tungoje kwani muda utajibu kitendawili hiki.
The end of the beginning.
Ni wanaccm ndiyo wanafanya huo upumbavu
 
Wazo la kununua vichwa mtumba lilikuwa la kijinga sana, sijui tuliwaza nini. Mwendokasi inavotupeleka puta nahofia yasije kufikia kwenye mradi wa maana na mzuri kama huu
Matrioni ya fedha za umma yamepigwa na mafisadi ya CCM
 
Hakuna aliyesema kuwa ni lazima wawekeze kwenye bandari pekee ni kamba wanayo nafasi ya kuwekeza sehemu mbali mbali zinazo lipa kwa mtindo ule ule wa mgawanyo wa portfolio walizochagua.
Kuhusu portfolio nakubali ila kwa umakini mkubwa mno. Kuna sababu kwanini mashirika mengi ya hifadhi ya jamii duniani huwa hayawekezi, mifumo mingi imejaribiwa na ikachukuliwa iliyo safe zaidi.

Shirika la hifadhi ya jamii hata lisipopata faida ni sawa, kazi yake kubwa lisipate hasara maana litaua vibaya sana uchumi wa nchi.
 
Huko wanakotumbukiza kwenye portfolio wanapata nini?? mbona hata kulipa mafao wenye hela zao walioweka wanashindwa? mfano, hizo nyumba za kigamboni zinawapa nini NSSF kwa sasa..
Sasa walioshindwa kwenye portfolio ndio wataweza kwa kuwekeza kitu kimoja?

Wasomi uchwara haohao wameshindwa kupata hela kwenye uwekezaji wa manyumba ambao hata vilaza wasiojua kusoma na kuandika wakiotea hela wanajenga na kupangisha na kupata faida. Watu haohao mnataka wawekeze kwenye bandari ambayo ni ngumu sana kuliko kuendesha na tangu tupate uhuru haijawahi kuwa efficient?
 
Sasa walioshindwa kwenye portfolio ndio wataweza kwa kuwekeza kitu kimoja?

Wasomi uchwara haohao wameshindwa kupata hela kwenye uwekezaji wa manyumba ambao hata vilaza wasiojua kusoma na kuandika wakiotea hela wanajenga na kupangisha na kupata faida. Watu haohao mnataka wawekeze kwenye bandari ambayo ni ngumu sana kuliko kuendesha na tangu tupate uhuru haijawahi kuwa efficient?
Labda hujaelewa toka mwanzo, uwekezaji tunaosema ni wa mifuko ya jamii kutumia pesa za wanachama kununua hisa kwenye kampuni zilizowekeza miradi mikubwa hapa ndani km zile za madini au kwenye usafirishaji..hata bandari pia km inawekwa kwenye soko la hisa ili watanzania washiriki kumiliki na kuendesha uchumi kwa faida yao..
 
Mkurugenzi wa TRC asimame imara, atajijengea heshima kubwa kabisa kwa mradi kama huu kusimama imara na kuonyesha dalili zote za kuingiza faida kubwa, tunafahamu wapo ambao hili wanaliona kwao ni hapana na wangependa mapato haya manono wayaingize mfukoni mwao, umefika wakati baada ya uwekezaji mkubwa TRC nayo ikatoa gawio nono la kustaajabisha kwa serekali yetu, wapo wengi kwa ulafi wao wanautamani mradi huu uwe wao, aidha serekali iwakodishe washenzi hao, badala ya mradi huu kusimamiwa na serekali yetu, tuwe imara tusichotwe mawazo, MAPUMBAVU yasiunase mradi huu kamwe!

Alichokisema Mkurugenzi. Mkurugenzi TRC: Tutaruhusu Wawekezaji binafsi kwenye Mradi wa SGR kuingiza Vichwa vya Treni na mabehewa yao.​

 
waweke vibox vya maoni ya siri, watu wataje nani anafanya hujuma. wachunguzwe, na wakijulikana, huo ni uhujumu uchumi kama uhujumu uchumi mwingine tu. wanamchezea kizmkazi kwa sababu ni mwanamke. hivi angekuwa ni Magufuli, kungekuwa na ujinga kama huo? just imagine, wanamchezea uyo maza wapendavyo. nachelea basi kusema 2025 tunahitaji Rais mwanaume, kwetu sisi wa kijijini, mwanamke hata akienda kufukuza nyani wanaokula mahindi, nyani huwa hakimbii, ila mwanaume hata mdogo tu nyani anakimbia.
Unamwamini atakayevifungua hivyo vibox?
 
Hawa Trc hawako serious kabisa mimi juzi nilibooking tickets ya jumapili nikatumiwa control no nikafanya malipo nikabaki na sms ya muamala na Tickets no jumapili imefika nakwenda kituoni naonyesha Ticket yangu naambiwa haitambuliki mara sijui ilicanceliwa kitu ambacho kama wangecancel wangerudisha mesej ya muamala nilipandwa na hasira sana
 
Hawa Trc hawako serious kabisa mimi juzi nilibooking tickets ya jumapili nikatumiwa control no nikafanya malipo nikabaki na sms ya muamala na Tickets no jumapili imefika nakwenda kituoni naonyesha Ticket yangu naambiwa haitambuliki mara sijui ilicanceliwa kitu ambacho kama wangecancel wangerudisha mesej ya muamala nilipandwa na hasira sana
Usiamini biashara ya booking, kama unania ya kusafiri kata tikiti yako kwa kuilipia kabisa, kuhusu hilo lako mwenye pesa mkononi ndiye anathiniwa.
 
Mafanikio ya SGR sio swala la Kadogosa.

Kadogosa ni msimamizi tu wa shirika.

Ufanisi wa SGR ni swala la national interest.

Kufeli kwa SGR ni ishara ya kuwa, tuna serikali mbovu.

Hilo sio swala la Kadogosa tu, yeye ajaweka hela zake; serikali ndio uliyoweka hela na inatakiwa kuwa na kila sababu ya kuona mafanikio yake SGR kwa malengo ya mradi wa muda mrefu.

Hakuna mtu wa kupokea lawama kwa ku-fail mradi wa SGR zaidi ya serikali, huo sio mradi wa Kadogosa, bali serikali,
Unaweza kutuonyesha huyo serikali?
Kama una muondoa kadogosa
 
kwakweli wabongo wa ajabu sana ntu anapanda treni na sanduku sijui limebeba spear za howo? zito kweli hadi sehemu za kuwekea mabegi zinapinda, ipo haja ya kuwela limit ya kg za kubeba, lia ziletwe behewa zenye booty kama kilimanjaro express mabegi yawekwe huko

kuhusu kudhibiti mifuko ya rambo na watu kupanda na makande hongera sana, kwakweli hali ya usafi ni ya hali ga juu sana
 
Tanzania ndo nchi pekee ukiwa tajiri ni km laana maana kila sku matajiri wanaonekana wabay

Baba yangu aliwai kunambia neno moja Wenye Nyumba za nyasi wao huwa hawaonei ? wao kila sku wanaonewa ! na hii ilitokana. Kuna wanakijiji walijenga nyumba kwenye viwanja vya mzee sasa pind anashugulika kurudisha maeneo yake ndo akasema ivyo

Maskini wao kila sku wanaonewa wao huwa hawaonei

Tupunguze majungu na vijimaneno maneno visivyo na maana huu mradi ni mpya na inawezekana bado mamlaka ya usimamizi haijajua vzr jinsi ya kupambana na kuepuka changamoto wanazokutana nazo kwa sasa tuwape muda
 
Back
Top Bottom