Hizi fake ID za JF kidogo ziniletee balaa

Hizi fake ID za JF kidogo ziniletee balaa

Katika kutimiza haja zangu za kirijali leo nimejikuta namtupia mistari binti mmoja maarufu humu ukumbini kwa mfumo wa PM. Sikupata adha ya kuporomoshewa mitusi Kama wadau wengine wanavyolalamikaga kuwa ukimPM binti humu ndani anakumwagia mitusi. Hali ilikuwa shwari mpaka ulipowadia Muda wa kubadilishana contact. Nilipoiweka namba yake kwenye kisemeo changu, lahaula...kumbe ni ni ndugu kabisaaaa...Hali kadhalika na kwake. Tumeombana misamaha na ninaamini yatabaki pale pale. Tuwe makini wadau unaweza tongoza Mkeo. Naamini anaisoma hii sredi, sister..nimeiweka hapa ili iwe fundisho kwa wengine.
ok, Niunganishie mkuu , mimi nataka niwe shemeji yako
 
Ndiyo raha/karaha ya mtandao. Kule Zambia mke na mume ambao walikuwa wameshashindana ndani ya ndoa yao na kila mmoja akitaka kuikimbia walitongozana mtandaoni na kujenga penzi zito sana hadi kuamua siku moja kukutana rasmi na hivyo kupanga sehemu ya kukutana. Lahaula! Walipofika pale ndiyo kufahamu kumbe ni wewe adui yangu mkubwa!!! Mume alikuwa kabeba na flowers kama zawadi kwa mrembo wake mpya.

Katika kutimiza haja zangu za kirijali leo nimejikuta namtupia mistari binti mmoja maarufu humu ukumbini kwa mfumo wa PM. Sikupata adha ya kuporomoshewa mitusi Kama wadau wengine wanavyolalamikaga kuwa ukimPM binti humu ndani anakumwagia mitusi. Hali ilikuwa shwari mpaka ulipowadia Muda wa kubadilishana contact. Nilipoiweka namba yake kwenye kisemeo changu, lahaula...kumbe ni ni ndugu kabisaaaa...Hali kadhalika na kwake. Tumeombana misamaha na ninaamini yatabaki pale pale. Tuwe makini wadau unaweza tongoza Mkeo. Naamini anaisoma hii sredi, sister..nimeiweka hapa ili iwe fundisho kwa wengine.
 
Mkuu USA baby habari yako!

Shwari kabisa bwana loya.

Umeshindaje leo?

USA baby
images
images
images
 
He,heh...ukistaajabu ya musa,utayaona ya firauni.poke kakangu weeee...sipati picha angekua mwanao
 
Back
Top Bottom