Hizi hapa taasisi zilizorudisha rushwa kwa kasi ya ajabu awamu ya sita

Magufuli alisema rushwa ya traffic ni ela ya kupiga viatu rangi. Au ushasahau?
Bora ya hao tubukubuku, buku mbili mpaka buku tano haziumizi ingawa anakusanya kwa wengi na anapata nyingi kwa siku. Kuna watu wanapiga rushwa mishindo mpaka unajiuliza huyu ana akili kweli?!

T.R.A huko mtu anataka umpe laki tano mpaka milioni na zaidi, Bandari, uhamiaji na wizara zinginezo... hao ndo wala rushwa nguli

Hao matrafiki kwa kweli wana maisha magumu wacha wajikusanyie vitakasa nafsi ingawa wapunguze kidogo
 
Rushwa ipo popote wakati wowote, tena kipindi chake ndio watu wanalikua wanapiga ela kimya kimya bila kelele yeye akiwa kinara wao, maana vyanzo vya kutoa habari vilikua vimebanwa, mtu ukitoa taarifa ya rushwa unatafutwa wewe, ukitoa taarifa ya mradi m'bovu unakamatwa wewe, nadhani mnakumbuka alietoa taarifa ya ubora wa majengo ya mlimani cuty kilichomkuta

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walishaagizwa kuwa wale rushwa na kufanya ufisadi
Your browser is not able to display this video.
 
Awamu dhaifu, mama anaupiga mwingi hadi kwenye matope!.
Awamu ya 4 (JK) = Awamu ya 6 (Sa100)

Allahu akbar,Mungu aepushie mbali fikra za watu wa hovyo kama hizi,leo mnatamani kweli yule Jamaa angekuwapo madarakani??

Ni watu wenye roho ngumu kama za waana wa israel watanzania
 
Kuhusu vibaka mbezi malamba mawili saa 3 tu usiku vibaka wanavamia nyumba na kupora,hivi vitendo vilishasahaulika ila vimerudi kwa kasi mno!
Tuweke ulinzi shirikishi maana polisi walikuwa wanajitahidi sana kutupatia huduma ya ulinzi ila Watz tulivyomafala hatuthamini kwamba wenzetu(polisi) wanahatarisha maisha yao kwa ujira mdogo,sasa mwishowe ndio kama hivi mapolisi wanatususia kiaina ili tuonje joto la jiwe. Huku mtaani mali zetu na uhai wetu havipo salama.
 
Ukiwa summoned na Mamlaka husika unaweza kuthibitisha haya?

Pili Kati ya Samia na Mwendazake nani aliwaruhusu Polisi kula Rushwa?

Kati ya Samia na Mwendazake nani amekuwa anaitaka Mahakama kutenda Haki?

Mwisho kama kote huko Kuna Rushwa inakuaje Serikali awamu hii Ina mapato mara 2 ya mapato ya Mwendazake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…