Hizi ni biashara zinazolipa ila sio rafiki sana kwa mfanyabiashara anayeanza kujitafuta.

Hizi ni biashara zinazolipa ila sio rafiki sana kwa mfanyabiashara anayeanza kujitafuta.

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Watu wengi tumekuwa tukipeana ushauri wa biashara zinazolipa hasa kwa wale vijana wadogo wanaoanza pilika baada ya kutoka masomoni. Nimekumbuka biashara kadhaa nzuri ila sio rafiki kwa anayeanza biashara ambaye bado mtaji wake ni mdogo. Haya ni maoni yangu ila sio sheria.

1. Biashara ya kununua mazao wakati wa mavuno na kuyahifadhi kusubiria bei ipande.
Hii sio mbaya kwa watu wenye mtaji mkubwa na pesa nyingi. Tukiachana na risk za mazao kuharibika bali pia kuweka hela chini na kusubiri kwa miezi kadhaa bei ipande inahitaji misuli ya kifedha. Kwa mfanyabiashara anayejitafuta hii sio poa haitamfaa. Mbaya zaidi wakati mwingine bei inaweza isipande.

2. Biashara ya kuagiza vitu China au Dubai na kuviuza Tanzania.
Hii ni nzuri ila unayeanza bora ukazungusha hela yako kwa kununulia vitu kwa wauzaji wa jumla Kkoo na kwingineko hapahapa nchini ili ukuze mtaji. Baadae unaweza anza taratibu kwa kuagiza vitu kadhaa China bila kutumia mtaji wako wote. Tatizo kubwa kwenye hii biashara ni mizigo kuchelewa kufika na wakati mwingine kutumiwa vitu vilivyo chini ya kiwango.

3. Biashara za vitu vinavyoweza kuharibika kwa haraka.
Kwa mfano wale wanaonunua matunda na kwenda kuyauza viwandani hasa pale Mwandege huwa ni risk kubwa. Hata wanaonunua ndizi Moshi na kuziuza Mabibo wana risk sana.

4. Biashara za kampuni inayohitaji vibali vingi mwanzoni.
Kufungua kampuni sio jambo baya kama umejipanga. Ila kama mtaji ni mdogo anza na sole proprietorship badala ya kampuni. Hii itakusaidia kuepuka gharama nyingi za uendeshaji hasa mambo ya kodi. Na hata kama ni kampuni jiulize sana kabla kwasababu kuna kampuni zinahitaji uwe na vibali hadi vya TMDA na TBS.

ONGEZEA ZINGINE KWA FAIDA YA WAFANYABIASHARA WADOGO
 
Ungejazia jazia nyama hiyo ya no 2 mkuu
Kuagiza vitu China kama mtaji ni mdogo inachelewesha sana mtaji kukua. Kikwazo cha kwanza ni bei. Mzigo ukiwa mdogo bei inakuwa sio rafiki. Utakuta tofauti ya bei ya mzigo wa China na Dar ni kiasi kidogo mno. Hivyo ni bora kuzungusha mtaji hapahapa kwanza kwa sababu muda upo kasi sana.
 
Watu wengi tumekuwa tukipeana ushauri wa biashara zinazolipa hasa kwa wale vijana wadogo wanaoanza pilika baada ya kutoka masomoni. Nimekumbuka biashara kadhaa nzuri ila sio rafiki kwa anayeanza biashara ambaye bado mtaji wake ni mdogo. Haya ni maoni yangu ila sio sheria.

1. Biashara ya kununua mazao wakati wa mavuno na kuyahifadhi kusubiria bei ipande.
Hii sio mbaya kwa watu wenye mtaji mkubwa na pesa nyingi. Tukiachana na risk za mazao kuharibika bali pia kuweka hela chini na kusubiri kwa miezi kadhaa bei ipande inahitaji misuli ya kifedha. Kwa mfanyabiashara anayejitafuta hii sio poa haitamfaa. Mbaya zaidi wakati mwingine bei inaweza isipande.

2. Biashara ya kuagiza vitu China au Dubai na kuviuza Tanzania.
Hii ni nzuri ila unayeanza bora ukazungusha hela yako kwa kununulia vitu kwa wauzaji wa jumla Kkoo na kwingineko hapahapa nchini ili ukuze mtaji. Baadae unaweza anza taratibu kwa kuagiza vitu kadhaa China bila kutumia mtaji wako wote. Tatizo kubwa kwenye hii biashara ni mizigo kuchelewa kufika na wakati mwingine kutumiwa vitu vilivyo chini ya kiwango.

3. Biashara za vitu vinavyoweza kuharibika kwa haraka.
Kwa mfano wale wanaonunua matunda na kwenda kuyauza viwandani hasa pale Mwandege huwa ni risk kubwa. Hata wanaonunua ndizi Moshi na kuziuza Mabibo wana risk sana.

4. Biashara za kampuni inayohitaji vibali vingi mwanzoni.
Kufungua kampuni sio jambo baya kama umejipanga. Ila kama mtaji ni mdogo anza na sole proprietorship badala ya kampuni. Hii itakusaidia kuepuka gharama nyingi za uendeshaji hasa mambo ya kodi. Na hata kama ni kampuni jiulize sana kabla kwasababu kuna kampuni zinahitaji uwe na vibali hadi vya TMDA na TBS.

ONGEZEA ZINGINE KWA FAIDA YA WAFANYABIASHARA WADOGO
Sikiliza wewe, pesa ni matokeo ya wewe kutatua changamoto fulani kwenye jamii au kwa mtu fuliani.
Tatua Changamoto yoyote uone kama pesa hazijakutafuta.

Hakuna cha hii biashara unalipa au hii hailipi, kinacho fanya upate pesa ni je kuna kitu una solve? tofauti na hapo utamaliza waganga kwa kupigiwa ramli
 
Watu wengi tumekuwa tukipeana ushauri wa biashara zinazolipa hasa kwa wale vijana wadogo wanaoanza pilika baada ya kutoka masomoni. Nimekumbuka biashara kadhaa nzuri ila sio rafiki kwa anayeanza biashara ambaye bado mtaji wake ni mdogo. Haya ni maoni yangu ila sio sheria.

1. Biashara ya kununua mazao wakati wa mavuno na kuyahifadhi kusubiria bei ipande.
Hii sio mbaya kwa watu wenye mtaji mkubwa na pesa nyingi. Tukiachana na risk za mazao kuharibika bali pia kuweka hela chini na kusubiri kwa miezi kadhaa bei ipande inahitaji misuli ya kifedha. Kwa mfanyabiashara anayejitafuta hii sio poa haitamfaa. Mbaya zaidi wakati mwingine bei inaweza isipande.

2. Biashara ya kuagiza vitu China au Dubai na kuviuza Tanzania.
Hii ni nzuri ila unayeanza bora ukazungusha hela yako kwa kununulia vitu kwa wauzaji wa jumla Kkoo na kwingineko hapahapa nchini ili ukuze mtaji. Baadae unaweza anza taratibu kwa kuagiza vitu kadhaa China bila kutumia mtaji wako wote. Tatizo kubwa kwenye hii biashara ni mizigo kuchelewa kufika na wakati mwingine kutumiwa vitu vilivyo chini ya kiwango.

3. Biashara za vitu vinavyoweza kuharibika kwa haraka.
Kwa mfano wale wanaonunua matunda na kwenda kuyauza viwandani hasa pale Mwandege huwa ni risk kubwa. Hata wanaonunua ndizi Moshi na kuziuza Mabibo wana risk sana.

4. Biashara za kampuni inayohitaji vibali vingi mwanzoni.
Kufungua kampuni sio jambo baya kama umejipanga. Ila kama mtaji ni mdogo anza na sole proprietorship badala ya kampuni. Hii itakusaidia kuepuka gharama nyingi za uendeshaji hasa mambo ya kodi. Na hata kama ni kampuni jiulize sana kabla kwasababu kuna kampuni zinahitaji uwe na vibali hadi vya TMDA na TBS.

ONGEZEA ZINGINE KWA FAIDA YA WAFANYABIASHARA WADOGO
Mawazo ya kichuuzi haya hizi ndio idea za Watanzania wengi hakuna anaye waza Productions, watu wanawaza jinsi ya kuinua uchumi wa China.
 
Sikiliza wewe, pesa ni matokeo ya wewe kutatua changamoto fulani kwenye jamii au kwa mtu fuliani.
Tatua Changamoto yoyote uone kama pesa hazijakutafuta.

Hakuna cha hii biashara unalipa au hii hailipi, kinacho fanya upate pesa ni je kuna kitu una solve? tofauti na hapo utamaliza waganga kwa kupigiwa ramli
Umesoma vitabu vya Kiyosaki unakuja kuharisha kwenye huu uzi. Haiko hivyo unavyodhani.
 
Mawazo ya kichuuzi haya hizi ndio idea za Watanzania wengi hakuna anaye waza Productions, watu wanawaza jinsi ya kuinua uchumi wa China.
Unajua skilled labour, technology, machines na raw materials za kufanya productions ili uweze kushindana na China? Ulishawahi ku-produce nini?
 
Sikiliza wewe, pesa ni matokeo ya wewe kutatua changamoto fulani kwenye jamii au kwa mtu fuliani.
Tatua Changamoto yoyote uone kama pesa hazijakutafuta.

Hakuna cha hii biashara unalipa au hii hailipi, kinacho fanya upate pesa ni je kuna kitu una solve? tofauti na hapo utamaliza waganga kwa kupigiwa ramli
Wewe umewahi kutatua changamoto ipi? Vijana munadanganyana mno
 
Binafsi biashara zina changamoto zake.Kikubwa ni kuwa focused bila kuyumba kwa kusikia mawazo ya waliokwama au wanaotamani ukwame.Mfa yabiashara mzuri ni yule mwnye consistent kwenye kile anachokifanya
 
Mawazo ya kichuuzi haya hizi ndio idea za Watanzania wengi hakuna anaye waza Productions, watu wanawaza jinsi ya kuinua uchumi wa China.
Shida ni elimu yatu ndio imetufikisha hapo muhitimu akimaliza masomo anawaza kuajiliwa au kufanya uchuuzi hakuna anayefikiria Production Kwa sababu ni kitu ambacho hajawahi kukisikia akiwa darasani

Ila katika swala la production Mimi nairaumu VETA , SIDO na DIT
Yani wanashindwa hata kutengeneza mashine ya kuchonga vijiti vya kuchokonyolea meno Ili wajasilia mali wanunue wachonge vijiti wafungashe wauze ndani ya nchi na nje ya nchi

Yani hata vijiti vya kuchokonyolea meno na kutunga mishikaki tunaagiza kutoka china?

VETA, SIDO na DIT sijui wanafaida gani katika hili Taifa
 
shida
Shida ni elimu yatu ndio imetufikisha hapo muhitimu akimaliza masomo anawaza kuajiliwa au kufanya uchuuzi hakuna anayefikiria Production Kwa sababu ni kitu ambacho hajawahi kukisikia akiwa darasani

Ila katika swala la production Mimi nairaumu VETA , SIDO na DIT
Yani wanashindwa hata kutengeneza mashine ya kuchonga vijiti vya kuchokonyolea meno Ili wajasilia mali wanunue wachonge vijiti wafungashe wauze ndani ya nchi na nje ya nchi

Yani hata vijiti vya kuchokonyolea meno na kutunga mishikaki tunaagiza kutoka china?

VETA, SIDO na DIT sijui wanafaida gani katika hili Taifa
shida ni reward system zilizopo. mtu anapata u-Prof wakati uku kitaani kwenye maisha ya kawaida yeye mwenyewe anaendesha baa. wavumbuzi hawatambuliki.
 
Umesoma vitabu vya Kiyosaki unakuja kuharisha kwenye huu uzi. Haiko hivyo unavyodhani.
Yupo sahihi mno... Wala siyo vitabu vya kiyosaki ni fact!
Kwa mfano, hivi aliyegundua vile vijiti vya kuwashia moto, si wanapiga Hela wale?
Kuna mwamba mmoja alikuta Shule ya kata ipo remote sana, watoto wanatembea umbali mrefu mno, akapata wazo la kujenga nyumba jirani na Shule, alipowaomba wenyeji wakampa ardhi, akajenga nyumba, sasa hivi ni Hostel maarufu. Anapiga Hela. Je, hawa hawapigi pesa kwa kutatua changamoto halisi za watu?
 
Back
Top Bottom