Hizi ni kona kali na milima, kwa barabara nchini, taja nyingine

Hizi ni kona kali na milima, kwa barabara nchini, taja nyingine

Mkuu funga safari utoke iringa kwenda dodoma au dodoma kwenda iringa via Mtera utakuja kuelezea hiyo kitonga ni cha mtoto
Kitonga imezidi mi nishapita iringa to Dodoma ,songea to dar.njia ya kwenda Dodoma kun kona ila sio nyingi japo ni hatari pia ila kitonga naogopa hadi leo
 
Habari jamvi?, kwa wale wazurulaji nchini

Ukizunguka nchini utakutana na sehemu maarufu , kimandhari na kimuonekano.

Leo naongelea sehemu za barabara nchini ambazo Zina Kona Kali na sehemu ya milima, nataja chache nyingine ongeza
1. Kona za Iyovi - ukitoka tu mikumi kuelekea Iringa utaziona Kona hizi, ni Tamu Sana
2. Kona za kitonga - hizi zinapatikana kutoka Moro kwenda iringa.

3. Kona za Kolo- hizi zinapatikana kutoka kondoa kuelekea babati

4.kona za Nyang'olo - hizi zinapatikana unapokaribia kufika iringa kutokea dodoma

5. Kona za Lukumbulu songea huko

6. Kona za msambiazi, korogwe kuelekea mombo
7. Kona za Mombo kuelekea Soni - Lushoto
8.Kona za Mbeya kwenda Chunya
9. Kona za Ugara - Babati kwenda Mbulu - hapa kitonga chamtoto Cha ngedele
10. Kona za Hedaru - Vunta , Same


Ni Kona hatari lakini Tamu Sana, na mabasi huwa wanalala na Kona hizi kwa speed ya 120 yaani shaa.

Ongeza Kona Kali nyingine
Kona ya Bwiru
 
Habari jamvi?, kwa wale wazurulaji nchini

Ukizunguka nchini utakutana na sehemu maarufu , kimandhari na kimuonekano.

Leo naongelea sehemu za barabara nchini ambazo Zina Kona Kali na sehemu ya milima, nataja chache nyingine ongeza
1. Kona za Iyovi - ukitoka tu mikumi kuelekea Iringa utaziona Kona hizi, ni Tamu Sana
2. Kona za kitonga - hizi zinapatikana kutoka Moro kwenda iringa.

3. Kona za Kolo- hizi zinapatikana kutoka kondoa kuelekea babati

4.kona za Nyang'olo - hizi zinapatikana unapokaribia kufika iringa kutokea dodoma

5. Kona za Lukumbulu songea huko

6. Kona za msambiazi, korogwe kuelekea mombo
7. Kona za Mombo kuelekea Soni - Lushoto
8.Kona za Mbeya kwenda Chunya
9. Kona za Ugara - Babati kwenda Mbulu - hapa kitonga chamtoto Cha ngedele
10. Kona za Hedaru - Vunta , Same


Ni Kona hatari lakini Tamu Sana, na mabasi huwa wanalala na Kona hizi kwa speed ya 120 yaani shaa.

Ongeza Kona Kali nyingine

Barabara ya kutoka Sumbawanga mjini kwenda Bonde la Ziwa Rukwa katika vijiji vya Muze, Mtowisa, n.k. Hebu jaribu kupita barabara hiyo uonee! Huyarudia tena milele! Ndiyo barabara ya hatari kabisa kuliko zote zilizotajwa humu! Moto wa kuotea mbali. Nimesema hivi kwa sababu karibu kona zote za barabara na miteremko iliyotajwa humu naifahamu pamoja na hiyo bsrabara ya Sumbawanga-Muze bonde la Rukwa! Huko si mchezo hata mara moja aisee!
 
This road is amazing
Mnazunguka hapohapo tu[emoji1787]
Screenshot_20210501-083609.jpg
 
Nyang'oro Kona za kawaida sana hizo nilishawahi kushuka na gar ambayo haina uhakika wa brek na nikatoboa
 
Mleta mada acha utani. Ebu zitendee haki kona Kali sana za kawetire (kona za mkoa), kutoka Mbeye mjini kwenda Chunya. Ndiyo sehemu yenye "high elevation" kushinda kona zote za bara bara kuu Tanzania. Kutoka kileleni mwa bara bara mpaka chini ya bonde la usangu ni umbali wa "Kilometers".

Pale juu yaani peak ya hiyo barabara urefu wake ni nusu ya urefu wa mlima Kilimanjaro toka usawa wa bahari. Pana kibao kimeandika mwinuko ni meta 2950 kutoka usawa wa bahari na kuongeza kuwa ule mwinuko ambapo barabara imepita ndiyo mwinuko mrefu zaidi kuliko mwinuko wa barabara yoyote katika Tanzania. Nakubali kabisa hoja yako!
 
Hapo tatizo huwa ni maporomoko ya ardhi (landslides) wakati wa mvua. Ni hatari sana
 
Narudia kusisitiza

Mteremko wa kushuka Bondeni Rukwa kutoka Sumbawanga kwenda MUZE ni #1 kwa hatari.

Nimeambatanisha picha ya kutokea angani.

Mteremko gradient yake ni almost 45 degrees, Bus za kawwida ama Fuso za kawaida haziwezi kupita isipokuwa zile fupi fupi. Kuna kona kali almost nyuzi miatatu hamsini hivi.

Bàadhi ya madereva wapo radhi wwzunguke 180km plus kufika Muze kutokea Sumbawanga kuliko kukatisha hapo ambapo ni chini ya km 60.

Kwa madereva walio safiri sehemu mbalimbali Tz na wamepita njia hiyo watakubaliana nami, pia kwa abiria ambao wanaujua mlima huo na wanazijua njia nyingine ikiwemo ile ya Tukuyu, Makete, Lushoto na Manyara watashuhudia kuwa kushuka MUZE ni namba moja.

Ingawaje kwa picha hiyo huwezi kuona vizuri lakini ukipita utajuwa kwa nini nasema ni hatari.

Kitonga, Kigoma, Lukubulu, Gangitoroli kote ni cha mtoto.View attachment 1765386

Upo sahihi asilimia 100, hakuna barabara chafu kama hiyo! Na huko bondeni sijui binadamu walifikaje na kuishi huko bondeni huku maana kuna vijiji vingi sana huko! Ila bila kupepesa macho mimi nimewahi kufika bodeni huko mara tano! Hakuna sehemu kama hiyo Tanzania nzima na pengine East and Central Africa nzima!
 
Kuelekea Tarakea/Rongai kuanzia Kibolo je?
 
Kuna kona moja inaitwa KWA SHETANI, njia ya Njombe - Ludewa, hatari sana. Jina linasadifu kona hiyo.

Sijui siku hizi pakoje maana nasikia barabara inakarabatiwa, na sijapita njia hiyo miaka mingi.
 
Back
Top Bottom