Hizi SALON za kiume za massage na Kushave balaa

Hizi SALON za kiume za massage na Kushave balaa

haya ya Saloon na scrubs tuyaache tu, maana......................
 
hii biashara inakua kwa kasi ya ajabu,na nyingi zinakuwaga na wadada walivyo na mbwembwe sasa..nenda na mke wako,kama hamtarudi na topaz...
 
Achaneni na hizo "Baba Shopu", mbona kwenye zile "hea kating salun" ambazo tunanyoa kwa jero tu uswahilini hakuna hao "wajasiria mwili"?
Mkuu unataka tuchekwe mjini ? pamoja na hali kuwa ngumu inabidi tu-maintain lifestyle ya kiwango flani hapa mjini, unavaa vizuri, elfu 10 ya barber shop kwa wiki,simu bei mbaya hata kama unapanda daladala na`mfukoni yamejaa makaratasi lol!
 
Kuanzia Sinza Bamaga hadi Shekilango kwa haraka haraka kuna BarberShop zinazofika 20 au zaidi ya hapo
 
Kuanzia Sinza Bamaga hadi Shekilango kwa haraka haraka kuna BarberShop zinazofika 20 au zaidi ya hapo

Ukija kinondoni sasa, afu zote zinataka kukaa barabarani kama matawi ya Benki.
Jamaa amenikumbusha wakati inaanzishwa BM! Waigizaji wote walitaka kuigizia pale
 
mi tangu nimeoa, sweetie ananifanyia yoote hayo nyumbani lol
 
ila jaman wale wadada ni wazuri karibia wote ile kibiashara tunaiita marketing techniques,,,,ful majaribu mle saloon,kwa waislam safi kama mimi huwa tunapita kwa mbaliiii tu
 
vitu vingine havina msingi lakini ndivyo tuvikumbatiavyo. mitego hiyo inagusa asili ya mwanadamu hasa sisi wanaume kutokana na kwamba wanaume tunatawaliwa na macho wakati wanawake wanatawaliwa na msikio ktk saikolojia ya mapenzi. hivyo basi wale wenye saloon wanacho kitaka ni faida wanawaweka kinadada ili macho yetu yatushawishi kurudi tena na tena tunapohitaji huduma hiyo. lakini hakuna ulazima wowote wa wasichana hao kufanya beyond responsibilities.
 
hizi salon kazi kweli kweli....nilikwenda wakati mmoja na my numero uno..akieda kunyolewa....yaani mzee mmoja babake mtu...amelala usingizi akisikizia sijui ni massage ya kichwa..halafu the gal places the clients head btn her boobs eh!!!! weee nikasema mweh!!!!
 
Mwenye ujuzi na zile za kike pia atujuze, je ni kusukwa tu!
Za kike mara nyingi huwa ni kwa ajili ya umbea nani anatembea na mume wa mtu, nani kufulia, na anajishebedua ndio maana mara nyingi unawakuta wakongo wanafanya kazi mule na wanawatafutana kweli wamama na wake za watu
 
Kwa vijana wa zamani watakumbuka jinsi huduma ya kunyoa nywele ilivyokuwa ikitolewa.

Kama siyo chini ya mti mkubwa wenye kivuli basi ilikuwa ni kwenye vibanda vidogo vidogo ambavyo kulikuwepo na kinyozi mmoja mwanaume.

Taratibu kwa kadri muda ulivyoendelea na utandawazi kushika hatamu, sasa tunashuhudia naweza kusema nyumba za kisasa kabisa zimejengwa ama kugeuzwa kuwa maeneo ya kunyolea nywele huku huduma nyingine za kuosha nywele,uso, kucha na nyingine kama hizo zikifanywa na akina dada tena warembo kweli kweli.

Baadhi ya hawa akina dada wamekuwa wanavaa nguo ambazo wakati mwingine zinaacha maswali mengi kwamba je ni huduma hii ya kufanya usafi wa nywele na uso ama ni zaidi ya hapo. Na zaidi ya hapo wakati wa hizi huduma wana minjonjo mingi tu kama kufungua vifungo vya shati ili waweke taulo/kitambaa, wasugue masikio, shingo,..nk.

Nawaulizeni wana-JF wenzangu, je kama uko na mai waifu wako akaona unayofanyiwa na hawa akina dada atakuruhusu uwe unakwenda peke yako? Au kama maiwaifu wako angekuwa anafanya kazi huko, ungemruhusu awafanyie wanaume wengine vile hawa akina dada wanafanya?

Na tujadili!

Hivi massage room ni lazima iwe an bafu
 
Ni kama ambavyo huwezi ambatana na wife akienda kusuguliwa kucha mwenge...
 
Haya mambo haya akikuingizia vidole masikioni huwa kuna hali flani hivi kiukweli nilijiuzulu sitaki tena kuna majaribu ya kujitakiwa wana makusudi hao!
 
Back
Top Bottom