Elections 2010 Hizi takwimu zinaakisi hali halisi?

Elections 2010 Hizi takwimu zinaakisi hali halisi?

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Unapoingia jf unakutana na mchakato wa kura dhidi ya wagombea wote wa ngazi ya urais. Kati ya wote, dr. Slaa anaongoza kwa %79 akifuatiwa na kikwete kwa %14. Hizi takwimu zinaakisi hali halisi ya upigaji kura? Tunaweza kusema tunayafananisha maoni haya na redet na synovate? Huu ushindi wa slaa wa mtandaoni unaweza vipi kushawishi hali halisi. Mwananchi wa kawaida anajua kuwa slaa anaongoza kura za maoni humu? Haya ni muhimu kuyafahamu na kuyanyumbulisha
 
Jf ni chadema club...
Ingawa sio rasmi..........

Tatizo watanzania wenye acces na internet
ni asilimia moja tu......
 
Ila hata DAILYNEWS iliwapambanisha Slaa na Kikwete na hali ikawa hiyo hiyo. Slaa 75%, Kikwete 20%.

Wanaosoma DAILYNEWS na kushiriki kwenye cyberspace ni wananchi waliosoma na kuelewa nini kinaendelea. Hao wanamweka Slaa mbele sana ya Kikwete. Does it matter? Yes; absolutely. These are opinionated people. They have influence. They are the movers and shakers of our nation.
 
Jf ni chadema club...
Ingawa sio rasmi..........

Tatizo watanzania wenye acces na internet
ni asilimia moja tu......

Ishi kwa matumaini mkuu kwa kujipa moyo kwamba 99% ya wananchi hawana access internet?, kaka hatuipendelei CHADEMA na DR Slaa bila vigezo, hizi statistics ni prove tosha weakness ya uongozi wa JK na CCM yenu iliyojaa ahadi lukuki, matumizi makubwa na fedha za umma na kuwakumbatia mafisadi.

Wait and see...
 
Cha msingi pia na hapa wakuu wa JF waendeshe utafiti nje ya jukwaa ili kulinganisha na takwimu hizi tulizo nazo sie watu wa mtandao. isije ikawa kweli kuwa watu wa mtandao ni wa chadema wakati hali halisi sio hivyo
 
Tambueni kuwa education level na exposure ndio vinachangia sana Dr slaa kuongoza watu wenye exposure wanajua hali halisi ya weakness katika uongozi wa kikwete, lakini kutokana na media ambazo zinawafikia wengi wasio na exposure kupamba na kuifagilia serikali iliyopo madarakani ndio maana basi wasio wa exposure na education bado wanaamini kwa kiasi kikubwa CCM na serikali yake ipo juu. Juhudi kubwa inatakiwa kufanya na vyama pinzani kujenga awereness through Radio kwa sababu ndio inawafikia watu wengi na ni rahisi kwa mkulima wa kijijini kuown radio kuliko kuwa na TV au kununua gazeti. nadhani kazi iliyopo kubwa kwa wapinzani ni Rural na ikumbukwe rural tanzaia ina chukua 73% ya population na ndio maana Redet na Synovate wakifanya tafiti mnaona Kikwete anaongoza ni kwasababu sisi wa mjini ambao ni 27% tunadhani wenzetu wa vijijini 79% wana fikra kama zetu. Pia kumbukeni watu wa vjijini ni wagumu saaana kubadilika so inatakiwa kazi kubwa ya ziada kutoka kwa upinzani kuwafumbua macho hawa wenzetu vijijini.
 
aaah wapi, not scientific and absolutely doesn't represent general population. Hata hivyo inaweza ikatupa idea ya mwelekeo wa wale watumishi, wasomi, wanafunzi na wenye access ya mtandao watakavyopiga kura (endapo watapiga kura). Otherwise, its purely for entertainment.
 
Tambueni kuwa education level na exposure ndio vinachangia sana Dr slaa kuongoza watu wenye exposure wanajua hali halisi ya weakness katika uongozi wa kikwete, lakini kutokana na media ambazo zinawafikia wengi wasio na exposure kupamba na kuifagilia serikali iliyopo madarakani ndio maana basi wasio wa exposure na education bado wanaamini kwa kiasi kikubwa CCM na serikali yake ipo juu. Juhudi kubwa inatakiwa kufanya na vyama pinzani kujenga awereness through Radio kwa sababu ndio inawafikia watu wengi na ni rahisi kwa mkulima wa kijijini kuown radio kuliko kuwa na TV au kununua gazeti. nadhani kazi iliyopo kubwa kwa wapinzani ni Rural na ikumbukwe rural tanzaia ina chukua 73% ya population na ndio maana Redet na Synovate wakifanya tafiti mnaona Kikwete anaongoza ni kwasababu sisi wa mjini ambao ni 27% tunadhani wenzetu wa vijijini 79% wana fikra kama zetu. Pia kumbukeni watu wa vjijini ni wagumu saaana kubadilika so inatakiwa kazi kubwa ya ziada kutoka kwa upinzani kuwafumbua macho hawa wenzetu vijijini.

katika hili ndo maana nikasema jf wapate na utafiti mwingine wa kulinganisha na huu kabla ya 31st oct ili tujue kuwa sio entertainment kama alivyosema mzee mwanakijiji. Labda tuwaulize pia na wadau wengine waliopiga kura humu kama walikuwa wanajiburudisha tu
 
Ishi kwa matumaini mkuu kwa kujipa moyo kwamba 99% ya wananchi hawana access internet?, kaka hatuipendelei CHADEMA na DR Slaa bila vigezo, hizi statistics ni prove tosha weakness ya uongozi wa JK na CCM yenu iliyojaa ahadi lukuki, matumizi makubwa na fedha za umma na kuwakumbatia mafisadi.

Wait and see...

wapi hamna lolote, mbona nyinyi mna ahadi kibao tena za kutisha kuliko hata CCM mnasema mtasomesha hadi form six bure, mnasema mtawalipa mshahara zaidi ya laki tatu kima cha chini, katiba mtabadilisha kwa siku mia (mkisahau kuwa katiba ni jambo zito na hasa ya muungano maana wazanzibari wako macho si sauli la kuota) na mengine mengi.

Jee hili hamuoni kuwa Slaa(Padri alieiba mke wa watu) anatoa ahadi hewa
 
wapi hamna lolote, mbona nyinyi mna ahadi kibao tena za kutisha kuliko hata CCM mnasema mtasomesha hadi form six bure, mnasema mtawalipa mshahara zaidi ya laki tatu kima cha chini, katiba mtabadilisha kwa siku mia (mkisahau kuwa katiba ni jambo zito na hasa ya muungano maana wazanzibari wako macho si sauli la kuota) na mengine mengi.

Jee hili hamuoni kuwa Slaa(Padri alieiba mke wa watu) anatoa ahadi hewa

Nadhani Mtu wa pwani humu hatuko ki haiba ya mtu wala chama na kila mtu humu kwa janvi la JF anachama chake anachoki support ila wewe kila mara huja na vitu vyako as if umekurupushwa na vya kishabiki sana ivi naomba niujue umri wako wewe kwa sasa na kama ni kijana una mtazamo upi katika nchi hii na inavyokwenda? Najua umesoma ila sasa sielewi somewhere along the road umekosea njia?

Nadhani kuana haja ya ku base in facts kama mtu anafanya kazi zake kwa manuufaa ya nchi lets recognize it na kama mtu anaboronga tumwambie na tuseme wazi bila ku base one side.

Hizi ahadi zilipaswa ziwe na kiujumla au kimikoa?au maana utekelezani wake kwa kweli sijui utatekelzwaje? au Mikoa ibadiliki iwe majimbo na mifumo mipya ya kimaendeleo mie nadhani ndio tutakwenda kwa speed kali katika maendeleo

 
kwakweli takwimu hizi ni za watu wenye access na mitandao ambao wengi ni wa mijini...ndio maana tunaposema kuwa CCM inakubalika vijijini na kwa wananchi wa kawaida watu wanakasirika bila kujua ukweli huu..watanzania wengi hata gazeti hapa mjini wanalisoma kwenye mbao za wauzaji...wanaopiga hiyo kura ya Oktoba kuchagua viongozi huwa wachache so hii haireflect kabisa population ya TZ so tujipe moyo tu ila ukweli unapojidhihiri ndipo tunadai tumeibiwa kura kumbe tulisahau kutazama wengi(wasio na access) wanasemaje.
 
Jf ni chadema club...
Ingawa sio rasmi..........

Tatizo watanzania wenye acces na internet
ni asilimia moja tu......

Kwa taarifa yako hata magazeti ya Uhuru, Rai, mtanzania na yale ya Shigongo yakifanya hii study na yakawa siyo biased, statistics zitakuwa hivyo hivyo na hata actual results zitakuwa hivyo hivyo kama hakuna mchakachuo.
 
kwakweli takwimu hizi ni za watu wenye access na mitandao ambao wengi ni wa mijini...ndio maana tunaposema kuwa CCM inakubalika vijijini na kwa wananchi wa kawaida watu wanakasirika bila kujua ukweli huu..watanzania wengi hata gazeti hapa mjini wanalisoma kwenye mbao za wauzaji...wanaopiga hiyo kura ya Oktoba kuchagua viongozi huwa wachache so hii haireflect kabisa population ya TZ so tujipe moyo tu ila ukweli unapojidhihiri ndipo tunadai tumeibiwa kura kumbe tulisahau kutazama wengi(wasio na access) wanasemaje.
sasa hapo ndio unapopata picha ya upumbavu wa watanzania walio wengi tena walio vijijini. Bora sie wa mjini tunajua maisha yanaendaje, hela inatafutwaje, nani anaiba nini na vipi, siasa ni mchezo wa aina gani. Hao hao walio na maisha duni ndio hao wanaosahau dhiki zao kwa muda kwa ulaghai wa mwezi mmoja na kuirudisha serikali ya awali madarakani. Sie wachache wa mjini tunazidiwa nguvu na hao wengi. Maisha ya huko vijijini yanatisha ila hawaoni hilo. Labda tuamini kuwa si akili zao zinazotumika wakati wa upigaji kura
 
tambueni kuwa education level na exposure ndio vinachangia sana dr slaa kuongoza watu wenye exposure wanajua hali halisi ya weakness katika uongozi wa kikwete, lakini kutokana na media ambazo zinawafikia wengi wasio na exposure kupamba na kuifagilia serikali iliyopo madarakani ndio maana basi wasio wa exposure na education bado wanaamini kwa kiasi kikubwa ccm na serikali yake ipo juu. Juhudi kubwa inatakiwa kufanya na vyama pinzani kujenga awereness through radio kwa sababu ndio inawafikia watu wengi na ni rahisi kwa mkulima wa kijijini kuown radio kuliko kuwa na tv au kununua gazeti. Nadhani kazi iliyopo kubwa kwa wapinzani ni rural na ikumbukwe rural tanzaia ina chukua 73% ya population na ndio maana redet na synovate wakifanya tafiti mnaona kikwete anaongoza ni kwasababu sisi wa mjini ambao ni 27% tunadhani wenzetu wa vijijini 79% wana fikra kama zetu. Pia kumbukeni watu wa vjijini ni wagumu saaana kubadilika so inatakiwa kazi kubwa ya ziada kutoka kwa upinzani kuwafumbua macho hawa wenzetu vijijini.

nakubaliana na wewe watu waliopo jf wengi wao wanauelewa mkubwa sana!!
 
aaah wapi, not scientific and absolutely doesn't represent general population. Hata hivyo inaweza ikatupa idea ya mwelekeo wa wale watumishi, wasomi, wanafunzi na wenye access ya mtandao watakavyopiga kura (endapo watapiga kura). Otherwise, its purely for entertainment.

That's right! I've said it before that this is an unscientific poll and it doesn't tell much. Kwanza kuna watu kibao humu wenye multiple IDs ambao sitashangaa kama wamepiga hiyo kura zaidi ya mara moja....
 
Mlioweka hii poll mnatuambiaje maana people say it is unscientific and purely entertainment. I do not want to believe either of the above bearing in mind the content of jf in terms of thinking, contributing and analyzing issues
 
Jf ni chadema club...
Ingawa sio rasmi..........

Tatizo watanzania wenye acces na internet
ni asilimia moja tu......

Nimeshasema tena hili jambo. Kwa maoni yangu, wana JF wengi ni wale wenye mapenzi ya dhati na taifa la Tanzania na hawatetei vitendo vyovyote vile ambavyo vinaturudisha nyuma. Vitendo hivyo ni wizi wa mali ya umma, upendeleo, ubinafsi, udini na mengine mengi ya aina hiyo, ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda mrefu chini ya ccm. Ingekuwa Chadema CUF, TLP NCCR na wengine wangekuwa wanafanya hivyo, nina hakika kuwa wangepata pingamizi kubwa kama inavyoonekana sasa kwa ccm. Mimi binafsi sio mwanachama wa chama chochote. ccm leo ikibadilisha muelekeo wake na kuthamini Watanzania ipasavyo, nitaishabikia CCM hiyo. Mpaka hapo watakapofanya hivyo, nitaendelea kutokubaliana nao. Nadhani maoni ya hao wana 'JF Club wa Chadema' wana mawazo kama yangu.
 
Unapoingia jf unakutana na mchakato wa kura dhidi ya wagombea wote wa ngazi ya urais. Kati ya wote, dr. Slaa anaongoza kwa %79 akifuatiwa na kikwete kwa %14. Hizi takwimu zinaakisi hali halisi ya upigaji kura? Tunaweza kusema tunayafananisha maoni haya na redet na synovate? Huu ushindi wa slaa wa mtandaoni unaweza vipi kushawishi hali halisi. Mwananchi wa kawaida anajua kuwa slaa anaongoza kura za maoni humu? Haya ni muhimu kuyafahamu na kuyanyumbulisha

Hapana hayaakisi maoni ya watanzania wote.

lakini yanaakisi maoni ya kada zifuatazo:

Wasomi (Diploma onwards) ambao ni zaidi ya kama 2 Million
Walio mijini ambao wana access ya TV, Radio na Magazeti. Hawa wanajua mapungufu ya serikali na kelele za upinzani hata kabla ya uchaguzi.

Nina wasiwasi kwamba kwa watanzania wa vijijini % zinaweza kuwa tofauti.
 
Back
Top Bottom