Hizi Tuzo alizopewa Gabo Sijazielewa...........

Hizi Tuzo alizopewa Gabo Sijazielewa...........

Lady Ra

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2014
Posts
879
Reaction score
991
Za Usiku wakuu,

Jana kulikua pale Mlimani City na utoaji wa Tuzo za Sinema Zetu International Film Festival, au SZIFF kwa kifupi. Tuzo hizi ziliandaliwa na kuratibiwa na kituo cha Television cha Azam TV ambacho kinamiliki pia channel ya Sinema Zetu.

Katika tuzo hizi, Msanii Salim Ahmed (Gabo Zigamba) aliibuka mshindi katika categories mbali mbali. Binafsi sina shaka kabisa kua Gabo ni Msanii Mzuri, ila ambacho sijakielewa ni Filamu iliyotumika kumpatia Gabo tuzo hizi.

Gabo alichukua Tuzo hizo kupitia Filamu yake ya SAFARI YA GWALU ambayo aliigiza kama Mwanafunzi mwenye Umri mkubwa. Nachofahamu filamu hii ndio pia iliyompatia Tuzo Gabo mwaka jana. Yaani mpaka tunaingia kwenye Mchakato Gabo ndio alikua "Bingwa Mtetezi" kupitia filamu hiyo hiyo, sasa iweje tena itumike na mwaka huu?

Kama Tuzo ni zinatolewa kila mwaka, inakuaje miaka miwili mfululizo Gabo anatumia filamu moja hiyo hiyo kujipatia ushindi? Hivi hata kwenye Mziki zikitolewa tuzo si zinakua za kipindi cha mwaka mmoja tu nyuma uliopita? Ina maana Gabo atatumia miaka mingapi kuingia na Filamu hiyo hiyo moja tu ilhali kila siku zinazalishwa filamu mpya nyingi tu za kutosha??

Naomba kueleweshwa tafadhali
 
Ni kweli aiseee ila sijui ni nani atatuelewesha huku , kama hapo ulivyoomba
 
Za Usiku wakuu,

Jana kulikua pale Mlimani City na utoaji wa Tuzo za Sinema Zetu International Film Festival, au SZIFF kwa kifupi. Tuzo hizi ziliandaliwa na kuratibiwa na kituo cha Television cha Azam TV ambacho kinamiliki pia channel ya Sinema Zetu.

Katika tuzo hizi, Msanii Salim Ahmed (Gabo Zigamba) aliibuka mshindi katika categories mbali mbali. Binafsi sina shaka kabisa kua Gabo ni Msanii Mzuri, ila ambacho sijakielewa ni Filamu iliyotumika kumpatia Gabo tuzo hizi.

Gabo alichukua Tuzo hizo kupitia Filamu yake ya SAFARI YA GWALU ambayo aliigiza kama Mwanafunzi mwenye Umri mkubwa. Nachofahamu filamu hii ndio pia iliyompatia Tuzo Gabo mwaka jana. Yaani mpaka tunaingia kwenye Mchakato Gabo ndio alikua "Bingwa Mtetezi" kupitia filamu hiyo hiyo, sasa iweje tena itumike na mwaka huu?

Kama Tuzo ni zinatolewa kila mwaka, inakuaje miaka miwili mfululizo Gabo anatumia filamu moja hiyo hiyo kujipatia ushindi? Hivi hata kwenye Mziki zikitolewa tuzo si zinakua za kipindi cha mwaka mmoja tu nyuma uliopita? Ina maana Gabo atatumia miaka mingapi kuingia na Filamu hiyo hiyo moja tu ilhali kila siku zinazalishwa filamu mpya nyingi tu za kutosha??

Naomba kueleweshwa tafadhali
Hizo tuzo mbona ndio zinafanyika kwa mara ya kwanza
 
Ndio mwanzo watapata wasaa wakujifunza zaid.... Tujifunze kuwatia watu Moyo, nguvu ya kuanda aifanan na nguvu ya ukosoaj ata tonye
 
Bado mnaangalia utoaji wa Tuzo bongo???? Mimi nilishaacha kitambo mnoo
 
Angeshinda diamond ingekua sawa.
Ni kama nyimbo inaweza kuwa namba moja kwenye radio one_ magic na channel zingine kwasababu waandaaji tofauti ukimuona Gabo mpe hongera.
Nb. Gabo ameingizwa kwenye game na sajuki(rip) na Dada yetu mpendwa wastara
 
sijui kwenye movie ila kwenye muziki iyo ipo....Nyimbo ya dar stand up ya chid ilimpatia tuzo kwa miaka 5 mfululizo kama sijakosea
 
Hizi tuzo ni tofauti, waandaaji ni tofauti, so wako sahihi
Haya mashindano ni mara ya kwanza kufanyika tz.tofautisha yale ya zanzibar festival na haya yanayoratibiwa na azam tv,kama unazidi kubisha weka aina ya shindano ambalo gabo alishinda hiyo tuzo kwa hiyo filamu
Sawa, ndio kueleweshana kwenyewe huku nilikoomba,

Kwa hiyo swala la Tuzo hizi ni tofauti, ila swala la mwaka likoje?
Kama Filamu hii ilishinda mwaka Jana, si ina maana itakua na zaidi ya mwaka sokoni?
Si zilitakiwa kua Filamu zilizozalishwa kipind cha mwaka mmoja uliopita?
 
Sawa, ndio kueleweshana kwenyewe huku nilikoomba,

Kwa hiyo swala la Tuzo hizi ni tofauti, ila swala la mwaka likoje?
Kama Filamu hii ilishinda mwaka Jana, si ina maana itakua na zaidi ya mwaka sokoni?
Si zilitakiwa kua Filamu zilizozalishwa kipind cha mwaka mmoja uliopita?
Hutokea ukaingalia filam mara kwa mara sababu ni nzuri.Pia yy kapewa tuzo kwa filam hiyohiyo sbb haijatokea filam nzuri kama hiyo ktk miaka hiyo husika.Na anaweza akawa ametoa filamu nyingine lakini isiwe nzuri kama hiyo.pia kuna swala la upigaji kura kwa kutoka kwa watazamaji na wapenzi.
 
Back
Top Bottom