Ni siku ya 31 leo tangu nianze kutumia dawa za Kuzuia maambukizi ya Ukimwi kwa watu walio mazingira hatarishi kupata ugonjwa huo (PEP), Dozi hii nimeimaliza jana.Hofu niliyo nayo imenifanya nishndwe kufanya kitu chochote cha maana zaidi ya kuzorota mwili.
Binafsi nina utaratibu wa kupima afya kwa kila mwanamke mpya ninaekutana nae, lakini siku ya kufa nyani miti yote huteleza.
Huyu mdada sikuwahi kukutana nae katika maisha yangu, kwa mara ya kwanza nimekutana nae MALAIKA BEACH HOTEL MWANZA ilikuwa ni usiku wa Jumapili, Mimi nikiwa ni mgeni pale kwa siku kadhaa na huyu dada alikuwa na marafiki zake kwenye meza iliyokuwa pembeni yangu. Kwa umbo na uzuri wamebarikiwa haswa.
Alikuwa amevaa vazi ambalo ukichanganya umbo na rangi yake kwa namna yoyote ile mwanaume yeyote aliyekamilika lazma atatamani kuwa karibu, na vyombo vilikuwa vimeshanikolea kama saa 6 hivi usiku nikamuita kumuomba kampani ahamie kwenye meza yangu hakusita, huo ukawa mwanzo ambao mwisho wake tukawa wote kwenye room yangu niliyofkia pale hotelini. Siku hii sikuwa na vipimo, nilijaribu kutafuta pale hotelini nikakosa ilibidi nichukue condom, Tukafanya sikuwa na vurugu katkati ya mchezo mwenyewe nikaomba kuchomoa ile condom akakubali hata hivyo sikuchukua mda nikamaliza baada ya kumaliza nikawa najilaumu sana na sikurudia tena mpaka alivyoondoka tukapanga, tukutane kesho yake ili tuweze kupima tufanye mambo yetu kwa uhuru, Akakubali.
kesho yake Jumatatu Akaja, na mimi nikawa tayari nimeshanunua Vipimo. Mwenzangu akabadilika akagoma kupima baada ya kumbembeleza kwa mda mrefu akakubali kwa sharti nianze mimi na majibu yeye nisimpe nibaki nayo mimi. Baada ya kupima majibu yake yakawa na changamoto. Nilijihisi kufa na isitoshe kipindi tunapimana ile kujitoboa nilishika kile kidole chake bila tahadhari, Sehemu ya damu yake ikagusana na kidole chngu nilichojitoboa kutoa damu. Hapa nilichanganyikiwa zaidi.
Asubuhi ya Jumanne nimeamka mapema kazi ilikuwa ni kusaka hospital ambayo naweza Kupata dawa za PEP ili nianze dozi, nilizunguka na boda kama kichaa. Jana nimemaliza hii dozi na kila wiki tangu nianze kutumia hii dozi nacheki afya yangu. Mpaka mda huu bado sijapata maambukizi ila nina hofu sana.
Kila nikifikiria huu ugonjwa napata shida sana.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Wanaume tuna kazi sana.
Unasema siku ya kufa nyani miti huteleza.
Mkuu ondoa hofu,nakumbuka hiyo hali iliwahi kunikuta kipindi fulani hivi kuna binti nilimuonaga fb alikuwa anasoma chuo fulani hivi basi nikamfukuzia kwa muda mrefu akawa hasomeki sasa baadae alivyomaliza chuo akarudi dar ni baada ya miaka 3.
Nikajaribu kutupa ndoano mtoto akajaa nikaenda kumla kimasihara japo nilitumia kinga.
Ikapita kama miezi 3 hivi nikapata typhoid ikanisumbua sana na mimi sijawahi kuumwa typhoid serious kama kipindi kile maana nilimeza dawa nikahisi kama ndio inazidi.
Sasa wakati nimejilaza yule demu akanitext.
Demu:Mambo my
Mimi
😛owa niambie
Demu:Ndio nini kuniambukiza ukimwi mwenzio?
Mimi:Nilinyong'onyea Pumzi ikapanda nikajikaza kisha nikamjibu,una uhakika ni mimi
Demu:Ndio ni wewe maana mimi nina miezi 6 sijakutana na mwanamme mwingine.
Mimi:Mapigo ya moyo yakaongezeka nikajikaza na kumjibu,lakini mbona tulitumia kinga?
Demu:Hapana nakumbuka uliivua
Mimi:Una uhakika uyasemayo
Demu:Lakini Mungu anakuona,umeamua kuniua mtoto wa watu,sawa bhana,wewe si umenikomoa.
Majadiliano yaliishia hivi basi nikaishiwa nguvu nikalala usiku mzima nikifikiria dah itakuwaje sasa.
Basi unaambiwa kuanzia ile wiki nikaanza kukonda na kukata tamaa nikasema ndio basi tena kumbe hii homa kali inayonisumbua ni kwa ajili ya HIV.
Hiyo hali ikanitesa kama mwezi mmoja hivi,sasa baadae nikasema potelea mbali ngoja nikapime nijiandae tu kuanza kutumia ARV.
Nikaenda Hospitali ya wilaya nikaingia nikajiandikisha mapokezi nikaenda kukaa foleni,lakini nilionekana mnyonge sana kuliko watu wote yaani sikuwa na amani kabisa.
Baadae ikafika zamu yangu nikakutana na madokta wawili vijana wadogo wa kike na mwingine wa kiume wenye miaka kati ya 27 hadi 30.
Wakanikaribisha vizuri kisha wakaanza kunihoji sababu ya mimi kuamua kwenda kupima,endapo nitakutwa muathirika nitachukua hatua gani na stori nyingi za hapa na pale.
Walikuwa very charming wakanifanya ile huzuni yangu ipotee nikaanza kutabasamu.
Baadae wakaniuliza uko tayari kwa kupima nikawajibu ndio,wakanitoboa na kuchukua sampo ya damu.
Nikangoja kama dakika 5 hivi majibu yakawa tayari kisha wakaniuliza,upo tayari kupokea majibu?mimi nikasema ndio.
Wakanijibu"Majibu yako yanaonesha uko Negative yaani hauna maambukizi ya ukimwi.
Unaonekana wewe ulikuwa mtu makini huwa unazingatia kutumia zana wakati wa tendo na pia huwa huchukui wanawake ukiwa umelewa kupitiliza yaani wakati wote huwa unachukua mwanamke wakati upo katika hali ya kujitambua hicho ndicho kilichokusaidia.
Aisee nilipata furaha ya ajabu,nikaingiza mkono mfukoni nikatoa noti ya elfu 10 nikawapa wale madokta nikawaambia mtakunywa soda asanteni na kwaherini.
So nilivyoona kisa chako hiki nikakumbuka hii stori yangu ni kama zinaendana.[emoji38]