Hoja Chokonozi: Hivi Rais anapowapita wananchi barabarani na Ulinzi mkali anaogopa kuwasalimia?

Hoja Chokonozi: Hivi Rais anapowapita wananchi barabarani na Ulinzi mkali anaogopa kuwasalimia?

Sir John Roberts

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
12,835
Reaction score
23,584
Kwanza niseme nakubali kabisa Rais anafanya kazi kwa ratiba alizopangiwa na wasaidizi wake. Siku 4 zilizopita Mh. Samia Suluhu Hassan katika ziara yake mkoani Katavi ameonekana katika msafara wake wa magari zaidi ya 100 akipita kwa kasi sana huku wananchi wakiwa wamejipanga barabarani kushangaa msafara wa Kiongozi wao.

Nimejiuliza maswali kadhaa kichwani kwangu huyu Rais tumemchagua sisi wananchi tuliosimama barabarani (ndio tumemchagua kwasababu wakati wa kupiga kura tulipiga kwa Marehemu magufuli na mgombea mwenza wake ambae ni huyu bibi samia).

Nimejiuliza anajisikiaje anapoona wananchi waliomchagua wapo barabarani yeye akipita kwa kasi bila kuwapa hata salamu huku akiwa na ulinzi wa kutisha kiasi cha kusema labda wananchi waliomchagua ndio tishio?

Jamani ieleweke sipingi ulinzi kwa Kiongozi wa nchi lakini nimeona tu kuwa waliomchagua wangepata faraja hata kupungiwa mkono tu na Kiongozi wao.

Kila la heri Rais samia Mungu akulinde afya njema na Hekma katika kuliongoza taifa letu.

Screenshot_20240718_210635_Instagram.jpg
 
Ukiona ulinzi ni mkubwa, jua kuwa, USALAMA ni mdogo.

Mwl Nyerere hakuwa na misafara ya aina hiyo, gari yake pia haikuwa na tinted, unamwona live.
Sishawishiki kuamini kuwa rais anawaogopa wakiomchagua .
 
Kwanza niseme nakubali kabisa Rais anafanya kazi kwa ratiba alizopangiwa na wasaidizi wake. Siku 4 zilizopita Mh. Samia Suluhu Hassan katika ziara yake mkoani Katavi ameonekana katika msafara wake wa magari zaidi ya 100 akipita kwa kasi sana huku wananchi wakiwa wamejipanga barabarani kushangaa msafara wa Kiongozi wao.

Nimejiuliza maswali kadhaa kichwani kwangu huyu Rais tumemchagua sisi wananchi tuliosimama barabarani (ndio tumemchagua kwasababu wakati wa kupiga kura tulipiga kwa Marehemu magufuli na mgombea mwenza wake ambae ni huyu bibi samia).

Nimejiuliza anajisikiaje anapoona wananchi waliomchagua wapo barabarani yeye akipita kwa kasi bila kuwapa hata salamu huku akiwa na ulinzi wa kutisha kiasi cha kusema labda wananchi waliomchagua ndio tishio?

Jamani ieleweke sipingi ulinzi kwa Kiongozi wa nchi lakini nimeona tu kuwa waliomchagua wangepata faraja hata kupungiwa mkono tu na Kiongozi wao.

Kila la heri Rais samia Mungu akulinde afya njema na Hekma katika kuliongoza taifa letu.

Waulize Ccm
..
 
Yaani asimame Kila Kijiji atafika kweli anakokwenda? Huwa yanachaguliwa maeneo Maalumu humo barabarani hasa kwenye eneo lenye watu wengi..hivyo wale wa vijiji/maeneo ya jirani wanaweza kwenda huko.
Aidha,kunakuwepo na mikutano rasmi ya hadhara kwa maeneo anayotembelea.
 
Ukiona ulinzi ni mkubwa, jua kuwa, USALAMA ni mdogo.

Mwl Nyerere hakuwa na misafara ya aina hiyo, gari yake pia haikuwa na tinted, unamwona live.

Mbwembwe tu za kijinga , hivi rais anapokuwa nje ya nchi usalama wake unakuwa mkubwa zaidi ndio maana anakuwa hana ulinzi mkubwa
 
Lazima awe na HOFU sababu anatumia Kodi za wananchi vibaya.

Na pia hatukuwahi kumchagua sa100 kama Rais,

Bali mgombea mwenza wa Magu, na ndio maana mgombea mwenza wa Samia alipogombea Urais hajawahi kuwepo.
Kwa mujibu wa katiba Samia ni rais halali na wananchi waliomchagua kuwa makamu wa Rais wanajua kwa mujibu wa katiba yetu kuwa Rais atakapofia madarakani basi Makamu wake ataongoza Katika kipindi kilichobakia.
 
Yaani asimame Kila Kijiji atafika kweli anakokwenda? Huwa yanachaguliwa maeneo Maalumu humo barabarani hasa kwenye eneo lenye watu wengi..hivyo wale wa vijiji/maeneo ya jirani wanaweza kwenda huko.
Aidha,kunakuwepo na mikutano rasmi ya hadhara kwa maeneo anayotembelea.
Ni sawaa ila hata kuwapungia mkono wapiga kura haiwezekani? Kwamba muda hautoshi? Kwenye kuomba kura mbona wanakuja kulala mpaka kwenye vitongoji?
 
Mbona hata Mbowe ana bodyguards? Au na yeye anawaogopa nyumbu waliompa uenyekiti wa maisha?
 
Siyo rahisi kwa Rais kusimama kila penye watu barabarani asalimie.
Kama ambavyo wewe huwezi kusimama usalimie kila mtu mtaani unapopita hata kama unatembea kwa miguu.
 
Kwanza niseme nakubali kabisa Rais anafanya kazi kwa ratiba alizopangiwa na wasaidizi wake. Siku 4 zilizopita Mh. Samia Suluhu Hassan katika ziara yake mkoani Katavi ameonekana katika msafara wake wa magari zaidi ya 100 akipita kwa kasi sana huku wananchi wakiwa wamejipanga barabarani kushangaa msafara wa Kiongozi wao.

Nimejiuliza maswali kadhaa kichwani kwangu huyu Rais tumemchagua sisi wananchi tuliosimama barabarani (ndio tumemchagua kwasababu wakati wa kupiga kura tulipiga kwa Marehemu magufuli na mgombea mwenza wake ambae ni huyu bibi samia).

Nimejiuliza anajisikiaje anapoona wananchi waliomchagua wapo barabarani yeye akipita kwa kasi bila kuwapa hata salamu huku akiwa na ulinzi wa kutisha kiasi cha kusema labda wananchi waliomchagua ndio tishio?

Jamani ieleweke sipingi ulinzi kwa Kiongozi wa nchi lakini nimeona tu kuwa waliomchagua wangepata faraja hata kupungiwa mkono tu na Kiongozi wao.

Kila la heri Rais samia Mungu akulinde afya njema na Hekma katika kuliongoza taifa letu.

Huu mtindo wa ulinzi wa kutisha alianzisha dhalimu magu, huyu mama kacopy na kupaste tu. kimsingi huyu mama na mtangulizi wake hawana cha kujivunia chochote kwenye kura maana uchaguzi wa 2020 ulikuwa wa kipuuzi mno.

Hapo kwenye kutembea na msafara wa zaidi ya magari 100 huku serekali ikishindwa hata kulipa wakandarasi wa ndani ndio inaonyesha kwa jinsi gani tuna viongozi wasiojali shida za wananchi. Cha kushangaza viongozi wetu wakienda kwenye nchi ambazo hawana hata mpiga kura mmoja hawana ulinzi wa hivyo, ama msafara mrefu hivyo!
Lucas Mwashambwa
 
Siyo rahisi kwa Rais kusimama kila penye watu barabarani asalimie.
Kama ambavyo wewe huwezi kusimama usalimie kila mtu mtaani unapopita hata kama unatembea kwa miguu.
Sasa kuna haja gani ya kulazimisha hao wananchi wajitokeze barabarani kuhadaa umma kuwa unakubalika, kisha ushindwe kusimama na kuwapa ahadi hewa? Nakumbuka kipindi cha dhalimu yeye alikuwa anatengeneza nyomi fake, kisha wananchi wanapangwa ionekane wamezuia msafara wake, lakini unashangaa hiyo sehemu aliyosimamishwa bahati mbaya, kuna vyombo vya habari vilivyojipanga kabisa!
 
CCM ni dubwasha kubwaaa .kuwa specific
Ni kweli ni dubwasha kubwa,ila si dubwasha bora. Mjinga tu ndio husifia ukubwa na sio ubora. Kwa maneno marahisi ni chama analogia kwenye ulimwengu wa kidigital.
 
Back
Top Bottom