Hoja Mbadala: Katiba Ya Muungano Kuja Kabla ya Katiba ya Tanganyika (Tanzania Bara) ni Makosa!

Hoja Mbadala: Katiba Ya Muungano Kuja Kabla ya Katiba ya Tanganyika (Tanzania Bara) ni Makosa!

Mchambuzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2007
Posts
4,850
Reaction score
9,434
Sio sahihi kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuja kabla ya uwepo kwa ukamilifu – kwa Katiba za mataifa mawili yanayounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania – yani Jamhuri ya Watu Wa Zanzibar na Jamhuri ya Watu Wa Tanganyika (Tanzania Bara).

Kwa vile ndugu zetu wazanzibari ni waelewa zaidi juu ya unuhimu wa national identity and national sovereignity katika masuala ya mahusiano na pia mashirikiano ya kimataifa, miaka karibia 30 iliyopita (1984), ikiwa ni miaka saba tu baada ya katiba ya JMT (1977) kuzaliwa, walifanya juu chini na kushinikiza kuzaliwa kwa Katiba yao kamili bila ya kujalisha uwepo wa katiba ya JMT(1977), ambayo miongoni mwa mengineyo, walifutilia mbali jina batili walilopewa chini Katiba ya 1977 kwani katiba hii ilifuta jina halisi la "Zanzibar" na kuweka jina batili la "Tanzania Visiwani", huku Tanganyika ikibadilika na kuwa Tanzania Bara, jina ambalo kutokana na ukosefu wa umakini kwa upande wa watanganyika, wamebakia kutambulika kwa utambulisho batili wa "Watanzania Bara"; Wazanzibari walienda mbali na werevu wao ambapo mwaka 2010 na waliamua kuboresha katiba ya zanzibar (1984) ili kuweka bayana nia ya taifa la Zanzibar, kwanza ‘to maintain her sovereignty and national identity' kabla ya masuala mengine yoyote, likiwepo suala juu ya Muungano wake na Tanganyika (Tanzania Bara);

Kwa upande mwingine, Katiba ya sasa ya Tanzania (1977) imeendelea kuwa ndio Katiba kwa masuala ya Tanganyika huku pia ikiwa ni Katiba kwa masuala ya Muungano, suala ambalo linazidi kuleta utata juu ya muungano uliopo; Kuendelea kukosekana kwa ‘decleration of national sovereignty and national identity' kwa Tanganyika kwa mujibu wa Katiba ya Tanganyika (Tanzania Bara), huku upande mwingine wa muungano (Zanzibar) ukiwa tayari umefanya hivyo, ni utata unaohitaji ufumbuzi wa haraka;

Bila ya kujalisha iwapo muungano baina ya Zanzibar na Tanganyika (Tanzania Bara) utakuwa ni muungano wa mkataba au wa aina yoyote ile, kuna umuhimu kwa upande wa Tanganyika (Tanzania bara) kwanza kuja na Katiba yake iliyokamilika na inayoelezea bayana masuala ya national sovereignty na national identity kama ilivyofanya Zanzibar; Ndani ya katiba hizi ndio lizungumzwe suala juu ya jinsi gani pande zote mbili zinataka kushirikiana na mataifa mengine, ikiwa ni pamoja na nchi shirikishi za muungano – yani Tanganyika (Tanzania Bara) na Zanzibar, kama mataifa huru.

Kwa maana nyingine, Muungano wa Tanganyika (Tanzania bara) na Zanzibar) utokane na matakwa ya wananchi wa pande zote mbili, kwa mujibu ya yaliyomo ndani ya Katiba za pande hizi mbili – yani Katiba ya Tanganyika (Tanzania Bara) na Katiba ya Zanzibar; Nje ya hapo, kitendo cha tume ya Jaji Warioba kuja na Katiba ya Muungano bila ya uwepo wa Katiba za pande zote mbili yani – Katiba ya Tanganyika (Tanzania bara) na Katiba ya Zanzibar itakuwa ni kupoteza muda na fedha za walipa kodi, lakini mbaya zaidi, itaimarisha tatizo lililopo badala ya kulitafutia ufumbuzi wenye manufaa kwa nchi shirikishi za muungano;
 
Wazbr hawana shida na muungano,haja yao ni mamlaka kamili ya nchi yao,haijalishi kama tanganyika ipo au haipo,haiwahusu.
 
Free riders.. Wazanzbari wamebebwa ktk Muungano huu wao hawana cha kupoteza!!!
 
Wazbr hawana shida na muungano,haja yao ni mamlaka kamili ya nchi yao,haijalishi kama tanganyika ipo au haipo,haiwahusu.

Je hauoni kama ni muhimu kwa watanganyika (watanzania bara) kuwa na nchi yao yenye mamlaka kamili kwa mujibu wa katiba yao bila ya kujalisha zanzibar ipo au haipo? Kama umenisoma sawa katika bandiko namba moja, huo ndio msingi wa hoja yangu;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Je hauoni kama ni muhimu kwa watanganyika (watanzania bara) kuwa na nchi yao yenye mamlaka kamili kwa mujibu wa katiba yao bila ya kujalisha zanzibar ipo au haipo? Kama umenisoma sawa katika bandiko namba moja, huo ndio msingi wa hoja yangu;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Kwani ilikufaje?
 
Nani kakuambia bara wanautaka Muungano???


Je huoni kwamba aidha kwa kusudia au kutokusudia, hoja yako inakuweka upande wa hoja yangu ya msingi? Na je, huoni kwamba matumizi yako ya jina "bara" ni muendelezo wa political ignorance yetu watanganyika(unlike ndugu zetu wazanzibari) katika muktadha wa national sovereignty na national identity?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kwani ilikufaje?

Iwapo swali lako linalenga kujua Tanganyika ilikufaje, tembelea uzi wangu mwingine "Tundu Lissu na kiini macho cha muungano", huko suala hili limefafanuliwa kwa kina;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Iwapo swali lako linalenga kujua Tanganyika ilikufaje, tembelea uzi wangu mwingine "Tundu Lissu na kiini macho cha muungano", huko suala hili limefafanuliwa kwa kina;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Sawa nakubaliana na hoja yako ya kuifufua tanganyika,lakini unaonaje tanganyika mkaomba muungano na nchi nyengine kama vile kenya na uganda ili mpate marafiki wapya?coz zanzibr hawaitaji tena muungano.
 
Sawa nakubaliana na hoja yako ya kuifufua tanganyika,lakini unaonaje tanganyika mkaomba muungano na nchi nyengine kama vile kenya na uganda ili mpate marafiki wapya?coz zanzibr hawaitaji tena muungano.

Kwanza, matumizi yako ya neno "marafiki" inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa na upeo mdogo juu ya masuala ya muungano wa mataifa kwani urafiki huwa sio kigezo cha msingi; Pili na muhimu zaidi, inawezekana ukawa na hoja nzuri lakini suala la wazanzibari kutoutaka muungano ni muhimu wakaweka bayana kupitia a referendum na sio maneno ya mitaani, kwani hivyo ndivyo seriousness yao katika suala hili itabainika; hoja hii imejadiliwa kwa angles tofauti kwa kina sana na wadau kama mzee mwanakijiji, nguruvi3 na wengineo; vinginevyo hoja yangu ya msingi hapa ni juu ya umuhimu wa Tanganyika kujipatia katiba yake kwanza kabla ya suala la muungano kuchukua any prominence;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kwanza, matumizi yako ya neno "marafiki" inaonyesha jinsi gani ulivyokuwa na upeo mdogo juu ya masuala ya muungano wa mataifa kwani urafiki huwa sio kigezo cha msingi; Pili na muhimu zaidi, inawezekana ukawa na hoja nzuri lakini suala la wazanzibari kutoutaka muungano ni muhimu wakaweka bayana kupitia a referendum na sio maneno ya mitaani, kwani hivyo ndivyo seriousness yao katika suala hili itabainika; hoja hii imejadiliwa kwa angles tofauti kwa kina sana na wadau kama mzee mwanakijiji, nguruvi3 na wengineo; vinginevyo hoja yangu ya msingi hapa ni juu ya umuhimu wa Tanganyika kujipatia katiba yake kwanza kabla ya suala la muungano kuchukua any prominence;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Inawezekana kweli upeo wangu wa kufikiri ni mdogo lakini mm nilitaka kujua je mnampango wowote wa kuishawishi nchi nyengine kuingia kwenye muungano coz naona zile nchi nyengine za east africa (KKK)wameanza kuweka vikao bila ya kuishirikisha tanzania a.k.a tanzania bara a.k.a tanganyika.
 
Inawezekana kweli upeo wangu wa kufikiri ni mdogo lakini mm nilitaka kujua je mnampango wowote wa kuishawishi nchi nyengine kuingia kwenye muungano coz naona zile nchi nyengine za east africa (KKK)wameanza kuweka vikao bila ya kuishirikisha tanzania a.k.a tanzania bara a.k.a tanganyika.
Mkuu Bobwe,

Awali ya yote, sikusema una upeo mdogo wa kufikiri kwani hivyo ni kukuvunjia heshima;nilichomaanisha narudia tena ni upeo wako kuhusiana na masuala ya muhusiano na ushirikiano wa mataifa inawezekana ni mdogo kwani unaweka kigezo cha urafiki kama ndio kigezo cha msingi, suala ambalo kwa mtazamo wangu finyu, sidhani kama ni sahihi huku nikisimama to be corrected;pamoja na hayo, nikasema inawezekana una hoja ya msingi lakini mada yangu haikulenga huko kwani iwapo umekuwa unanisoma vizuri, ushirikiano wetu Tanganyika na nchi nyingine chini ya katiba ya sasa (1977) ambayo technically ni katiba ya tanganyika (tanzania bara) na hapo hapo katiba ya jamhuri ya muungano, is problematic;so kabla ya kuzungumza juu ya kujiunga katika union na kenya, burundi etc, tunahitaji katiba ya tanganyika (tanzania bara) kwanza, hence hoja yangu ya msingi; nadhani umenisoma na samahani kama maneno yangu yalikukwaza;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
  • Thanks
Reactions: PhD
Mchambuzi; Hoja yako ni maridhawa.

Hata hivyo, binafsi naamini kuwa bila kuzungumzia uwepo wa Muungano yote yanayofanyika bado yataleta matatizo mbeleni. Kitu cha kwanza kabla hatujaamua kuandika Katiba ya Muungano au ya Tanganyika for that matter wananchi wa Zanzibar walitakiwa wapige kura ya maoni kama wanataka kutoka kwenye Muungano au la. Uamuzi wa Wazanzibari ungeamua kama tunakuwa na serikali ya Tanganyika au vipi na kama tunaendelea na Muungano unakuwa vipi. Sasa hivi, Wazanzibari hata tukirudisha Tanganyika bado wataona wanaonewa.

Kabla ya kuamua kuhusu Katiba ya Muungano au ya Tanganyika ni lazima wananchi wa Zanzibar wangeamua kwanza kama wanataka Muungano. Kama wakitaka kutoka kwenye Muungano basi la kwanza ambalo linafanyika ni wao wanaweka tarehe ya siku ya kufungasha virago vyao halafu huku Tanganyika tunaamua tunataka kufanya nini. Kwa sababu hapo hakutakuwa na masuala ya Katiba ya Muungano.
 
Guys, don't you know how governments work? Msingi wa tatizo kubwa la Muungano wetu wa Zanzibar na Tanganyika ni malengo ya siri ya Muungano huo ambayo waliyajua Nyerere na Karume wake. Tena zaidi ni Nyerere ndiye aliyejua anachokifanya. Rejea kauli ya Mtikila kwamba "Marekani wana mkono wao kwenye Muungano wa Tanganyika na Zanzibar".

Allegedly, USA didn't want another Cuba in Africa. So, they influenced Nyerere to form the so called Muungano to control Zanzibar. Now, USA can allegedly support any effort to keep Muungano alive because of their fear for "terrorrism". Mkuu Mchambuzi nauakubali uwezo wako wa kuchambua hili suala la Muungano. But you are missing one important point ...

Muungano na "mbwembwe nyingi" zinazoendelea sasahivi kuhusu Muungano is a sham. Inasemekana kwamba lengo halisi la Muungano ni kulinda maslahi ya wakubwa "Marekani na washirika wake". Na hawa wakubwa wanaihonga serikali ya JMT kuulinda huo Muungano. Mengine yote ni "ngonjera" tu. Na mimi ninashawishika kuamini hivyo.
 
Mimi msimamo wangu nilidhani kabla hata ya kuwepo na rasimu ya katiba hii ya muungano, wananchi wote wangeulizwa kwa njia ya kura ya maoni kama wanataka muungano. Kama wengi watasema wanataka muungano, basi pia waseme ni muungano wa aina gani.

Kwa kufanya hivyo, kungetoa fursa kwa tume kuanza kuandika rasimu ya katiba ikiwa inafahamu ni serikali gani zitakuwepo na hivyo kuwarahisishia kazi wao na wananchi kwa ujumla.

Nikirudi kwenye hoja yako. unachokisema kilikuwa hakiwezekani kwa sababu hata tume ya Jaji Warioba haina uhakika kama wananchi kwa kupitia mabaraza, asasi mbali mbali na bunge la katiba wanaweza kukubali serikali tatu. Si umesikia CCM wao wanataka waendelee na serikali mbili!.

Kama wangeandika rasmu ya katiba ya serikali ya Tanganyika na Zanzibar basi ingeonekana wameisha BAKA (STEAL) jukumu la wananchi kujiamulia aina gani ya muungano wanataka uwepo ikichukuliwa kuwa mpaka sasa haijulikani kama kutakuwepo na serikali tatu. Ndiyo maana jaji Warioba na wajumbe wake wakapendekeza kwanza wananchi waipitishe rasimu hii ya katiba ili zoezi la kuandika rasimu ya katiba ya serikali hizi mbili lianze tena.

Hoja yako ni sawa na kuanza kununua nguo za mtoto wakati mimba inaweza kuharibika wakati wowote achilia mbali aina ya mtoto atakayezaliwa.

Waziri wa katiba na sheria alisema, haitachukua muda mrefu kuandika rasimu ya katiba ya serikali hizi mbili kama wananchi wataridhia hii rasimu ya katiba na kuwa katiba ya muungano. Hata hivyo, naona kama muda unakuwa haurusu kufika August 2015 tukiwa na katiba zote "Tatu". Kuna uwezekano wa kuongezwa kwa muda utawala wa Rais Kikwete ili zoezi likamilike.
 
Mchambuzi; Hoja yako ni maridhawa.

Hata hivyo, binafsi naamini kuwa bila kuzungumzia uwepo wa Muungano yote yanayofanyika bado yataleta matatizo mbeleni. Kitu cha kwanza kabla hatujaamua kuandika Katiba ya Muungano au ya Tanganyika for that matter wananchi wa Zanzibar walitakiwa wapige kura ya maoni kama wanataka kutoka kwenye Muungano au la. Uamuzi wa Wazanzibari ungeamua kama tunakuwa na serikali ya Tanganyika au vipi na kama tunaendelea na Muungano unakuwa vipi. Sasa hivi, Wazanzibari hata tukirudisha Tanganyika bado wataona wanaonewa.

Kabla ya kuamua kuhusu Katiba ya Muungano au ya Tanganyika ni lazima wananchi wa Zanzibar wangeamua kwanza kama wanataka Muungano. Kama wakitaka kutoka kwenye Muungano basi la kwanza ambalo linafanyika ni wao wanaweka tarehe ya siku ya kufungasha virago vyao halafu huku Tanganyika tunaamua tunataka kufanya nini. Kwa sababu hapo hakutakuwa na masuala ya Katiba ya Muungano.
Mzee Mwanakijiji,

Karibu katika mjadala; Ni kweli kwamba msuguano wa muungano revolves around the autonomy of Zanzibar, lakini sababu juu ya hili ni obvious; Sababu za msingi kwanini muungano survived chini ya Karume bila ya misiguano ni mbili (1) Zanzibar ilikuwa na chama chake cha Siasa (ASP) (2) Karume alipuuzia constitutional restrictions on his power.

Vinginevyo suala la Wazanzibari kudai their autonomy lazima lingejitokeza tu na mantiki juu ya hili ni obvious, na nadhani unalielewa hilo. Vinginevyo baada ya kifo cha karume power struggles zikajitokeza huko Zanzibar na Aboud Jumbe akaibuka kama mshindi kwa msaada wa bara ingawa ASP die hards waliendeleza vita vyao juu ya autonomy of Zanzibar katika suala zima la muungano.

Mvutano huu ukawa suspended angalau superficially baada ya muungano wa vyama vya TANU na ASP ambapo Tanzania ikawa ni nchi ya chama kimoja cha siasa rasmi kuanzia mwaka 1977, huku katiba ya CCM Pia ikizaliwa kipindi hicho hicho ambapo CCM sasa ikashika hatamu sio katika muungano tu, bali pia katika serikali zake shiriki. Kwa maana hii, leo hii nazidi kuamini kwamba wazanzibari walio wengi hawana shida na muungano, shida yao ni autonomy ambayo ilikuwa compromised kwa miaka mingi kwa mfano maamuzi mengi juu ya masuala ya muungano kufanyika "Dodoma".

Suala hili pia limeanza kujitokeza katika umoja wa Ulaya ambapo nchi ndogo ndogo ndani ya umoja huo zimeanza kuhisi autonomy yao inakuwa compromised kutokana na maamuzi mengi juu ya maisha yao kufanyika Brussels, lakini hii ni hoja nje ya mada husika. Vinginevyo nina amini kabisa kwamba hata hiyo kura ya maoni ikipigwa, walio wengi watapendelea muungano uwepo kwani suala la ‘autonomy' wameshalitatua kupitia katiba yao mpya. Baada ya kusema haya, nina Swali ambalo ningependa kusikia maoni yako juu yake: Je, when it comes to muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar, suala la autonomy ni ‘relative' au absolute'?

Pia ningependa kurekebisha hoja yangu katika bandiko la kwanza kwamba katiba ya kwanza ya Zanzibar ilikuwa mwaka 1979 na sio 1984;
 
Mimi msimamo wangu nilidhani kabla hata ya kuwepo na rasimu ya katiba hii ya muungano, wananchi wote wangeulizwa kwa njia ya kura ya maoni kama wanataka muungano. Kama wengi watasema wanataka muungano, basi pia waseme ni muungano wa aina gani.

Kwa kufanya hivyo, kungetoa fursa kwa tume kuanza kuandika rasimu ya katiba ikiwa inafahamu ni serikali gani zitakuwepo na hivyo kuwarahisishia kazi wao na wananchi kwa ujumla.

Nikirudi kwenye hoja yako. unachokisema kilikuwa hakiwezekani kwa sababu hata tume ya Jaji Warioba haina uhakika kama wananchi kwa kupitia mabaraza, asasi mbali mbali na bunge la katiba wanaweza kukubali serikali tatu. Si umesikia CCM wao wanataka waendelee na serikali mbili!.

Kama wangeandika rasmu ya katiba ya serikali ya Tanganyika na Zanzibar basi ingeonekana wameisha BAKA (STEAL) jukumu la wananchi kujiamulia aina gani ya muungano wanataka uwepo ikichukuliwa kuwa mpaka sasa haijulikani kama kutakuwepo na serikali tatu. Ndiyo maana jaji Warioba na wajumbe wake wakapendekeza kwanza wananchi waipitishe rasimu hii ya katiba ili zoezi la kuandika rasimu ya katiba ya serikali hizi mbili lianze tena.

Hoja yako ni sawa na kuanza kununua nguo za mtoto wakati mimba inaweza kuharibika wakati wowote achilia mbali aina ya mtoto atakayezaliwa.

Waziri wa katiba na sheria alisema, haitachukua muda mrefu kuandika rasimu ya katiba ya serikali hizi mbili kama wananchi wataridhia hii rasimu ya katiba na kuwa katiba ya muungano. Hata hivyo, naona kama muda unakuwa haurusu kufika August 2015 tukiwa na katiba zote "Tatu". Kuna uwezekano wa kuongezwa kwa muda utawala wa Rais Kikwete ili zoezi likamilike.

Ng'wamapalala,

Karibu sana katika mjadala; nadhani suala ambalo tunapishana hapa ni moja - msimamo wangu ni kwamba, kabla ya suala juu ya muungano, ushirikiano, urafiki, whatsoever baina ya taifa moja na lingine, ni lazima kwanza mataifa husika yawe na national sovereignty na national identity kwa mujibu wa katiba za nchi zao. Sisi tuna treat suala la muungano kama vile ni suala ambalo halikwepeki kutokana na natural forces wakati hiyo sio kweli. Ni muhimu kwa katiba ya Tanganyika ipatikane kwanza na humo ndio itaje muungano kama ambavyo katiba ya zanzibar inavyofanya; baada ya hapo, Katiba ya muungano ndio ije.

Hivi kwa mtazamo wako, do you believe kwamba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania is a state? Is the Union president the head of state? Binafsi siamini katika hilo in practice ingawa inawezekana ikawa hivyo in theory. Vinginevyo component members of the union (Tanganyika na Zanzibar) ndio wenye real attributes of the state - wana head of state, head of government n.k, huku head of the state and government of Tanganyika akiwa amefichwa ndani ya kiini macho, vinginevyo tangia muungano uzaliwe, amekuwepo akiendesha masuala ya muungano na masuala yasiyokuwa ya muungano. Kama unanifuatilia vizuri, kinachohitajika hapa ni kuondoa hiki kiini macho kwa kuhakikisha kwamba nchi shiriki zinaingia katika mjadala juu ya muungano huku zikiwa na katiba zao mkononi.
 
Si umesikia CCM wao wanataka waendelee na serikali mbili!.

Nguzo kuu za CCM zimekuwa ni tatu:

1)Muungano;
2)Ujamaa na Kujitegemea;
3)Amani na Utulivu;

Nguzo namba mbili hapo juu sote tunajua imeshaanguka; nguzo namba tatu sote tunajua inazidi kumomonyoka, na nguzo namba moja (muungano) ndio kete ya mwisho ya chama kwa maana moja - CCM ni muungano wa TANU na ASP, na muungano wa vyama hivi viwili ndio uliotatua complications za muungano baina ya tanganyika na zanzibar kwani chini ya chama kimoja, CCM sasa ikashika hatamu katika masuala ya muungano na pia ya serikali shiriki [rejea sababu kwanini muungano uliendeshwa na katiba ya muda kwa niaka kumi na mbili (1965 to 1977)]; hivyo ndivyo CCM inaendelea kuwa na nguvu hadi hivi sasa. Kuvunja muungano au kuleta serikali tatu ni tishio kwa uhai wa ccm kwani uhalali wake ambao ni muungano baina ya vyama viwili vya tanganyika na zanzibar hautakuwepo tena;serikali mbili ni njia pekee ya kuendeleza legitimacy ya ccm huku serikali moja ikiwa ndio preference.

Nikirudi kwenye hoja ya msingi - mabadiliko yoyote ya mfumo wa muungano yatapelekea ASP die hards ambao bado wapo - kurudisha dhamira zao za kimapinduzi n.k, hivyo kutaka ndoa na ccm ife kwani kwa mujibu wa katiba ya 1977, wahusika wa muungano uliopo ambao umekuwa na utata ni ASP ya Jumbe na TANU ya Mwalimu;hilo likitokea zanzibar maana yake ni kwamba hata kwa tanganyika, wapo watakaotaka TANU irudi na kuwaondoa wazanzibari wote katika nafasi sio tu za uongozi, bali pia uanachama.

Huo ndio utakuwa mwisho wa CCM kushika hatamu na utamu; ni kwa mantiki hii, ccm kamwe haiwezi kukubali hoja ya serikali tatu!
 
Iwapo swali lako linalenga kujua Tanganyika ilikufaje, tembelea uzi wangu mwingine "Tundu Lissu na kiini macho cha muungano", huko suala hili limefafanuliwa kwa kina;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mara kwa mara anapokuwa anaongea Warioba anapata kigugumizi kutamka Tanganyika ilhali akitamka Zanzibar bila shida. Utamsikia akisema Zanzibar na kisha Tanzania Bara? Kwa nini hasemi Tanzania Visiwani anapokuwa anazungumzia Zanzibar? There is a really problem kwenye huu muungano. Ni nchi zipi ziliungana? Pasipo kuzifahamu itakuwa vigumu kujadili muungano. Warioba wewe ni mwanasheria. Please tell us! Mchanganyiko huu umesababisha watu na akili zao kusherehekea uhuru wa Tanzania Bara 9/12 nchi ambayo haipo. Hiyo ni tarehe ambayo Tanganyika ilipata uhuru. Anything Tanzania ni kuanzia 26/4//64.

Tusidanganyane na kupotosha historia kwa vizazi vijavyo.
 
Back
Top Bottom