HOJA NDANI YA HOJA: Rais Magufuli na bahati nasibu ya korona - ITALIPA?

Kufunga mipaka sio kujikinga na korona ingekua ivyo mpaka sasahivi urus isingekuwa na mgonjwa Mana waligunga mapema Sana Yan kabla hata haujasambaa Sana kutoka China
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmk tatizo kubwa ni uwaxi
Mmk tatizo letu accurate information. Je data tunazopewa ni sahihi?
Mbeya, dom tayar kuna wagonjwa na hawajaripotiwa bado
 
Ni uchambuzi mzuri mno na wa kina.Uchambuzi kama huu ulifanywa na mwandishi wa gazeti la Mwananchi na akaishia kufukuzwa kazi.
Mpaka sasa tunamshukuru Mungu kwa hali ilivyo,iwe ni kwa mkakati wa Rais wetu na wataalamu wake au ni "nature" imetuhifadhi yote kwa yote shukrani ni za Mwenyezi Mungu.
Uthubutu wa Raisi wetu hauna mfano bahati mbaya kubwa ni kuwa pale mambo yanapokwenda kombo uwazi unakuwa tatizo.Mimi naamini mfumo uliopo Tanzania wa serikali mpaka vitongojini ndio nguzo kubwa.Nipo kijijini kabisa lakini huwezi amini kuwa hata viduka mkoba vina ndooya maji na sabuni na watu wananawa kwelikweli.
Hata mikakati hii iki back fire bado Magufuli atasimama kama shujaa!!!!
 

Mzee tunakushukuru kwa hii makala ndefu ya bahati nasibu ilipayo au itiayo hasara. Kiukweli alichofanya rais sio kucheza bahati nasibu, ila kiuhslisua ugonjwa huu hauna nguvu kwenye nchi zenye hali kama ya kwetu. Hakuna cha tahadhari wala nini, bali ni ugonjwa usioweza kujimwambafy kwenye hizi nchi zetu fullstop.
 
watu watakufa Sana,???

hiyo tu, ndio imeondoa kabisa uzuri wote wa mawazo yako
 
Nimekusoma kamanda mwanzo mwisho,
Nachangia hivi
Wazungu pamoja na kuwa na madaktari wengi, vifaa tiba vya kutosha, Mapesa kibao kuna sehemu kidogo wameteleza katika kutoa elimu kwa wananchi wao

Kuhusu maambukizi ya corona
Sisi watanzania tumetulia kwanza tukausoma mchezo tukafanya sub

Elimu elimu elimu
Katazo,, hapa ndio wazungu na wachina walipofeli ndio maana maambukizi yakawa makubwa

Msivae mask kwa sababu zenyewe ndio chanzo cha maambukizi
nimeona wachina na wazungu wanavaa mask muda wote na kisha wanazishika shika mara wanashusha kidevuni, mara wanashika pale mbele bila kujua madhara yake

Mask wanatakiwa kuvaa wagonjwa na madaktari au wahudumu wa kuhudumia wagonjwa au zivaliwe kwenye mikusanyiko ya watu kisha ukitoka mahala hapo tupa mask yako kwenye dustbin

Wachina na wazungu walifundishwa kuvaa muda wote mask mbaka chumbani

Sisi watanzania baada ya kupata elimu ya madhara ya kuvaa mask tumepotezea kabisa kuzivaa hizo mask zenyewe na tunadunda tu,

Watanzania tumefundishwa kunawa na sabuni au kujipaka sanitizer tunanawa hatari mikono na kujipaka sanitizer kama tumevurugwa

Watanzania tumeondoa ile hofu ya corona baada ya kuambiwa corona ni mafua tu yanapona yenyewe na watanzania awana sifa ya kufa kwa mafua

Kifupi upo uwezekano mkubwa wa watanzania walio wengi mtaani wakawa na dalili za corona lakini wanameza tu panadol kisha wanachukulia poa kwa sababu historia ya kufa kwa mafua hatuna

Mfano dada isabela na mwana F A
Sio kwamba walizidiwa sanaa laah ila kwa sababu walitoka nje ya nchi na uko ndio kuna corona walijijengea hofu kutokana na kelele za mitandao na vyombo vya habari

Lakini kama isingekuwa kutoka huko nje ya nchi wangekula zao panadol na tungekuwa nao mtaani kama tulivyokuwa nao wengine

Kuna watu wengi sana mtaani wanaishi na dalili za corona lakini awaendi kupima
Na kama wataamua kwenda kupima Muhimbili Patakuwa apatoshi

Mwisho watanzania corona tunayo tunatembea nayo hao watu 13 wamejistukia wenyewe na kutokana na ile taharuki ya ugonjwa wamejipeleka wenyewe serikalini lakini wagonjwa mtaani awakosekani...


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hali hii utatumia kigezo gani kujua kama bahati nasibu ililipa au kutokulipa kama taarifa tunazopewa haziaminiki?!

Sent using Jamii Forums mobile app

Mbona kaelezea vizuri viashiria tunvyotakiwa kutumia kujua kama Bahati nasibu imelipa ama kutolipa! Italipa pale janga hili litakapoisha bila ya kuwa na mlipuko kwenye nchi yetu kiasi cha kushindwa kuimudu, Haitalipa pale hali ya maambukizi itakapochukua kasi na kuwa na wagonjwa wengi kiasi cha vituo vya huduma kuzidiwa.

Hajasema haamini taarifa, lakini kaongelea dhana iliyojingeka miongoni mwetu kwamba kuna namna takwimu zinafichwa, ni dhana hatuna uhakika nayo.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Serikali ipo vizuri, imeweka mikakati thabiti ya kuzuia kusambaa na kuingia ugonjwa huu. Sanitizers zipo zakutosha, mask zipo za kutosha, elimu imetolewa yakutosha.. Serikali ya awamu ya tano inawajali na kuwalinda sana wananchi wake..
 

Marekani kama nchi utapataje statement yake? Amesema wanawaza kulift lock down, hajasema wametangaza tayari. Hata mmoja akitamka ambae anasauti kwenye maamuzi inatafsiriwa kwamba tayari wanawaza kuhusu hilo.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mbeya, dom tayar kuna wagonjwa na hawajaripotiwa bado

Unaweza kutusaidia dondoo kuhusu wagonjwa hawa ili itusaidie kuishinikiza serikali kutoa taarifa sahihi, kama wamethibitika kwanini tunafichwa.
Tutajie angalau hospitali walipopatikana, najua kuna watu humu watatumia platforms zao kuhoji.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Umeandika kipropaganda zaidi. Umetaja idadi ya wananchi wa Nigeria kwa kuwa ya kwanza lakini hujaweka population ya Rwanda pamoja na kwamba wana karibiana na hao Nigeria uliotoa population number yao. Be honest in your analysis.
 
 
Covid-19 facts:
1.Corona Virus ni kirusi hatari kwa ustawi wa binadamu kokote duniani.
2.Mlipuko huo umesimamisha uchumi wa dunia mzima.
3.Social distancing ni mbinu rahisi ya kupunguza maambukizi mapya ya Corona virus.
4.Magufuli approach is hypotheses not a law,time will tell.
 

Mkuu unapokuwa kiongozi ni jukumu lako kuweka maono yako katika Imani ya kile unachokiamini. Sasa iwapo unachokiamini kikiwa vizuri na matarajio yako basi utakuwa umeponya wengi sana lakini pia kikiwa kunyume na ulivyotarajia pia wengi wataangamia kwa kuamini kwako lakini yote na yote utakuwa ni kiongozi uliye bora kwa sababu umesimamia ulichokiamini bila kuyumbishwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…