HOJA NDANI YA HOJA: Rais Magufuli na bahati nasibu ya korona - ITALIPA?

HOJA NDANI YA HOJA: Rais Magufuli na bahati nasibu ya korona - ITALIPA?


Nilipoandika makala yangu ya ILIYOPITA kuhusiana na ugonjwa utokanao na virusi vya korona (COVID-19) Tanzania ilikuwa haijtangaza kuwepo kwa mgonjwa yeyote nchini na kuwa makala ile ililenga katika kutoa shime ya kuwahi ugonjwa huo. Nchi zote zilizowahi kuutangaulia ugonjwa huo na kuchukua hatua kali mapema wameweza kudhibiti kusambaa kwake na hata kupunguza kasi ya maambukizi (rate of infections). Nchi zilizochelewa kuchukua hatua hizo au zimechukua hatua ambazo ni za taratibu sana zimejikuta leo hii zikihangaika kuokoa na kulinda maisha ya wananchi wao. Italia, Ufaransa na Uingereza kama ilivyo Marekani na Irani ni nchi ambazo zote leo zinajikuta zinakimbizana na muda. Muda hauko upande wao.

Kwa Tanzania hadi hivi sasa kuna kitu kinachoonekana si cha kawaida (an anomaly). Nchi zote ambazo zimepata wagonjwa wa kwanza tumeona idadi ya wanaoambukizwa ikiongezeka kwa kasi kubwa (exponentially). Karibu mwezi mmoja nyuma (Februari 15) Marekani ilikuwa na wagonjwa 15; leo hii Machi 26 Marekani ina wagonjwa karibu 70,000. Hii ni nyuma ya China tu na Italia. Kasi hiyo ya kusambaa kwa ugonjwa huu imeonekana karibu nchi zote ambazo ugonjwa huu umejikita. Kwa Afrika ni Afrika ya Kusini ambayo inaonekana ugonjwa huu kusambaa kwa kasi (sasa hivi wao wana kesi zaidi ya 900)

Je, namba zetu zinaweza kuaminika?
Nimesema hapo juu kuwa hali katika Tanzania inaonekana si ya kawaida (an anomaly). Kwamba, kweli nchi yetu inaweza kuwa na wagonjwa 13 tu wakati watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida? Je inawezekana serikali inaficha hali halisi na kuwa labda Rais Magufuli hataki watu waone kuwa Tanzania ina wagonjwa wengi? Ukifuatilia mitandao ya kijamii unaweza ukaamini hili. Lakini hiki “kinachoonekana” ni lazima tukipime (kwa tulio pembeni) kwa kulinganisha na nchi nyingine kama za kwetu. Hadi hivi sasa inaonekana ugonjwa wa COVID-19 haujalipuka kwa kasi kubwa katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama ilivyo kwa nchi nyingine.

Kufikia leo kwa baadhi ya nchi za Afrika hali ya wagonjwa (na namba za wagonjwa wapya kwenye mabano) ni kama ifuatavyo:

Nigeria (yenye watu milioni 190) - 51

Rwanda – 41

Kenya 31 (3)

Madagascar (4)

Zambia – 16 (4)

Uganda - 14

Ethiopia (yenye watu milioni 105) - 12

Congo DR (yenye watu milioni 81) – 4


Hivyo, tukiangalia takwimu hata za majirani zetu na nchi nyingine tunazoshabihiana nazo kwa mambo mengi utaona kuwa kasi ya maambukizi bado si kubwa na kama alivyosema Waziri Ummy Mwalimu leo ni kuwa wengi wa wagonjwa hawa ni wale waliopata COVID-19 wakitokea nje. Kwa hiyo, hatuna budi kukubaliana na kile tunachokiona; ugonjwa huu ni tishio lakini kwa nchi hizi za kwetu haujaweza kusambaa kwa haraka katika jamii (community spread). Hofu ya ugonjwa huu kusambaa kwa haraka ndio ulikuwa msingi wa hoja yangu.

Hatua Zilizochukuliwa Zinatosha?
Hadi hivi sasa serikali imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa haya maambukizi ya ndani kwa ndani kwenye jamii hayatokei. Kufungwa kwa shule, vyuo na kutoa elimu ya usafi na kupunguza mikusanyiko isiyo ya lazima ni njia sahihi. Katika mazingira ya kawaida tulitarajia baada ya Isabela kugundulika kule Arusha tungeona mlipuko Arusha lakini hilo halijatokea. Katika mazingira tunayoyaona kwenye nchi za wenzetu mgonjwa wa kwanza anapopatikana tu basi kuna uwezekano wa kuibuka kwa wagonjwa wengi zaidi.

Na namna pekee ya kuwapata wagonjwa hao ni kuchukua vipimo kwa watu wengi kwa kadiri inavyowezekana. Hili nalo Waziri Mwalimu amelielezea leo vizuri. Kwamba serikali inafanya vipimo na kuongeza uwezo wa kupima kwa haraka. Hii yote inasaidia kuweza kujua ni sehemu gani ya watu katika nchi wanaweza kuwa wameupata ugonjwa huu.

Bahati Nasibu ya Magufuli
Ni kutokana na hili Rais Magufuli – ambaye ni mwanasayansi ameona kuwa kwa sasa nchi nzima si lazima ifungwe kama walivyofanya nchi nyingine. Amewataka Watanzania kuzingatia kanuni za usafi na kupunguza migusano isiyo ya lazima lakini wakati huo huo kuendelea na shughuli zao. Hoja hii si kwa Magufuli peke yake; tumeona hata Marekani kuna mjadala mkubwa wa kutaka watu waanze kurudi makazini ifikapo Pasaka kwani uchumi wao hauwezi kwenda bila watu kurudi makazini. Hili nalo tumelisikia kwa Rais Bosanaro wa Brazili na baadhi ya wataalamu ambao wanataka kuona jamii inatengeneza kinga ya jamii (herd immunity) ambayo inatokea endapo watu wengi wanapata maambukizi na kupona na hivyo kupunguza mahali virusi hivyo vinaweza kuambukiza zaidi.

Endapo kasi hii ya maambukizi Tanzania itaendelea kuwa ndogo namna hii mambo mawili yanaweza kutokea. Kwanza, tunaweza kujikuta hatuna wagonjwa wapya ndani ya wiki chache zijazo kwa sababu tumeweza kuzuia maambukizi ya ndani kwa ndani kwenye jamii na pili tunaweza kuonesha kuwa hofu ya kuwa Afrika itakuwa ni kiini cha mlipuko haina msingi kwani nchi zetu katika umaskini wao wote wameweza kudhibiti ugonjwa huu kwa haraka bila kulazimika kufunga nchi. Hii itaokoa uchumi wetu na watu wataendelea na maisha yao kama kawaida na kutumia fursa mbalimbali ambazo zitakuwa zimejitokeza kiuchumi.

Bahati Nasibu Ikilipa

Huku kutakuwa ni kulipa kwa bahati nasibu ya korona ambacho Magufuli ameicheza. Na ikitokea hivyo, Rais Magufuli atakuwa ameonesha namna nyingine ya kukabiliana na tishio hili kinyume na viongozi wenzake wa Afrika kama Uhuru Kenyatta, Cyril Ramaphosa na Paul Kagame. Mabezo yote ambayo baadhi ya watu wameyarusha kwa Rais Magufuli kwenye mitandao yatawarudia kwani Watanzania kwa fahari wataanza kuyarudisha mabezo hayo. Magufuli atajionesha bado ni kiongozi wa aina yake katika Afrika; umpende au usimpende. Kwamba, siyo kiongozi wa kufuata mkumbo au upepo.

Na inawezekana tukashuhudia kuwa kudhibitiwa kwa ugonjwa huu Tanzania kunaweza kutoa fursa mbalimbali za kiuchumi kwa viwanda vyetu na wajasiriamali mbalimbali. Baadhi ya nafasi zinazoweza au kupaswa kutumika mara ugonjwa huu ukidhibitiwa:

  • Utengenezaji wa vitakasa mikono (hand sanitizers)
  • Utengenezaji wa vifaa vya mtu kujikinga (PPEs) kama magauni, glovu, maski na vilemba. Viwanda vyetu vya nguo vinaweza kuchangamkia fursa hii
  • Utengenezaji wa vitanda na vifaa mbalimbali vya kitabibu (Kama dawa, maji ya wagonjwa n.k) ambavyo vinaweza kutoa nafasi kwa viwanda vyetu.
  • Kutoa mchango katika utafiti wa chanjo ya ugonjwa huu kwa wataalamu wetu (hatuwezi kuwa watu tunaosubiri wengine tu watuletee chanjo!)
Bahati Nasibu Isipolipa

Hata hivyo, bahati nasibu hii inaweza isilipe. Hili litatokea endapo vitu viwili vitatokea. Kwanza, endapo idadi ya wagonjwa wapya itaanza kuongezeka kwa kasi kama ilivyotokea nchi nyingine na kusababisha mfumo wetu wa tiba (healthcare system) kushindwa kuhimili na kubomoka (collapse). Pili, endapo itagundulika kuwa kwa makusudi serikali na taasisi zake wamekuwa hawaripoti kwa usahihi idadi ya wagonjwa na matokeo yake na hivyo kuwaacha watu wenye maambuziki kuendelea kuzurura mitaani na kusababisha hilo jambo la kwanza. Kwa vile hadi hivi sasa idadi yetu ya wagonjwa haina tofauti sana na baadhi ya nchi kama za wetu; suala la kuficha namba (under reporting) ni vigumu sana kuaminika isipokuwa kama kweli nchi nyingine zote kama za kwetu zingekuwa zinaripoti namba kubwa zaidi kulinganisha na za kwetu. Kwa nchi zetu za Afrika utaona kuwa tuoka katika wastani ukiondoa Afrika ya Kusini ambayo iko pembezoni kweli kweli (outlier).

Lakini endapo jambo la kwanza likitokea na Tanzania ikajikuta kwenye mlipuko mkubwa wa korona baadhi ya mambo ambayo yanaweza kutokea ni haya:

  • Magufuli atabebeshwa lawama binafsi za kusababisha hilo. Sidhani kama ataeleweka kama atakuja kuwalaumu Watanzania kuwa hawakumsikiliza.
  • Tanzania na Watanzania wote wanaweza kujikuta wanapigwa marufuku kwenda nchi nyingine hadi hali itakapotengemaa. Endapo mlipuko wa korona ukatokea wakati nchi nyingine zimedhibiti basi viongozi wa Tanzania watanyoshewa vidole na dunia nzima kwani wenzao walipokuwa wananyolewa wao walikuwa wanaweka kalikiti!
  • Mfumo wa afya wa Tanzania unaweza kujikuta ukiporomoka kuliko tunavyoweza kudhania. Tumeona jinsi nchi za daraja la kwanza (Italia, Ufaransa, Marekani na China) zikipata shida kukabiliana na ugonjwa huu. Imefikia mahali serikali za nchi hizo zimeomba na zinategemea misaada kutoka makampuni binafsi kupata dawa na vitendea kazi mbalimbali. Kuna hospitali Marekani manesi wake walijikuta wakitumia mifuko ya plastiki ya takataka kama mavazi ya kujikina! Marekani hiyo! Tumeona Hispania, wazee wakiachwa wajifie wenyewe kwani manesi na wahudumu wengine wamekimbia! Tumeona Italia madaktari na manesi wakifa kutokana na ugonjwa huu. Kama hili linatokea kwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti mkavu! Kama limetokea kwa chuma cha pua, itakuwaje kwa chuma chakavu!
  • Kama hali itakuwa mbaya zaidi ya nchi hizo basi mtafaruku wa kijamii (social unrest) unaoweza kutokea utatisha. Huko Marekani sasa hivi watu pamoja na utulivu unaoonekana kwa nje lakini watu wako katika hali ya msongo mkubwa wa mawazo. Tayari takwimu zinaonesha kuwa Wamarekani wananunua bunduki na silaha ndogondogo kwa kiasi kikubwa ili kujilinda endapo utatokea mtafaruku. Ununuzi wa bunduki umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 300 nchini Marekani kutokana na hofu ya kuvunjika kwa utawala wa sheria sababu ya korona.
Yapo na mengine ambayo yanaweza kusemwa. Lakini vyovyote vile ilivyo, swali kubwa ni je hii ni bahati nasibu holela au ni bahati nasibu inayotokana na fikra za kisayansi. Kwamba, Rais Magufuli badala ya kuangalia mambo kijamii anaongozwa na ujuzi wake wa kisayansi na hivyo anapima mambo kwa uzito wa ushahidi ulio mbele yake (empirical evidence). Kwamba, Rais Magufuli ameona kuwa uwezekano (chance) ya Tanzania kupata mlipuko mkubwa endapo tunaweza kudhibiti maambukizi yaliyopo hadi hivi sasa ni mdogo sana. Na hii ndio sababu amewataka Watanzania kutotishika na kuendelea na shughuli zao. Siyo kwamba, anapuuzia au hajali kinachotokea duniani bali hataki watu wake wajifungie ndani, waache kazi, na kuombea “siku ya mwisho ifike”. Magufuli anasema “tusitishane”. Kwamba, tunaweza kudhibiti hali iliyopo bila kulazimika kuifunga nchi nzima. Kiukweli, hayuko peke yake duniani.

Kama nilivyosema hapo mwanzoni, tayari nchi kama Marekani imeanza kufikiria namna gani ya kufungua nchi ili watu waanze kurudi makazini. Hata ndani ya Marekani yenyewe baadhi ya majimbo bado hayajatangaza kufunga shughuli zote kwa sababu hawajapata maambukizi mengi (kumbuka nusu ya kesi zote za korona Marekani zinatokea Jimbo la New York). Wenzetu Marekani kutokana na utajiri wao licha ya kuifunga nchi wameweza kutenga dola trilioni 2.2 kwa ajili ya kulinda ajira, wafanyakazi na kusaidia sekta mbalimbali ili zisilipe gharama kubwa kutokana na ugonjwa huu. Kiasi hicho ni sawa na bajeti ya sasa ya Tanzania kwa karibu miaka 75!

Ni wazi basi kila mmoja wetu afanye anachotakiwa kufanya kujikinga na ugonjwa huu. Serikali iendelee kuwa muwazi na kwa namna yeyote isiwafiche au kuonekana inawaficha Watanzania hali ilivyo. Wahenga waliposema “mficha maradhi kifo kitamfichua” walisema ukweli. Na kwa vile tumeona kuwa hadi hivi sasa hakuna sababu ya kudhania serikali haisemi ukweli ni muhimu basi Waziri Mwalimu na Waziri Mkuu kutoa taarifa za hali ilivyo kwa haraka na kwa uwazi. Katika ulimwengu wa mitandao ya kijamii, habari za uongo zinasambaa haraka na hatuwezi kuwafunga watu wote wenye kuandika au kuanzisha mijadala hiyo. La maana ni kuliwahi treni la uongo kabla yalijafika kituo cha kwanza.

Tukifanya hivyo, na kweli tukadhibiti maambukizi ya ugonjwa huu na kuhakikisha uchumi wetu hauyumbi kwa kiasi kikubwa basi bahati hii nasibu ya Magufuli; italipa na italipa na kulipa.

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Unaweza kufuatilia takwimu za kasi ya uambukizaji wa virusi vya korona nchi mbalimbali duniani kwa KUBONYEZA HAPA
Umedadavua vr sana mkuu nimekuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu huo ndio ukweli, ila hawataki kuukubali, jamaa kaangalia Hali ya kipato Cha mtanzania na halingumu ya maisha akaona nibora ajifunge bomu shingoni likilipuka kilamtu atajuwa Ni jinsigani ya kujiokoa
 

Nilipoandika makala yangu ya ILIYOPITA kuhusiana na ugonjwa utokanao na virusi vya korona (COVID-19) Tanzania ilikuwa haijtangaza kuwepo kwa mgonjwa yeyote nchini na kuwa makala ile ililenga katika kutoa shime ya kuwahi ugonjwa huo. Nchi zote zilizowahi kuutangaulia ugonjwa huo na kuchukua hatua kali mapema wameweza kudhibiti kusambaa kwake na hata kupunguza kasi ya maambukizi (rate of infections). Nchi zilizochelewa kuchukua hatua hizo au zimechukua hatua ambazo ni za taratibu sana zimejikuta leo hii zikihangaika kuokoa na kulinda maisha ya wananchi wao. Italia, Ufaransa na Uingereza kama ilivyo Marekani na Irani ni nchi ambazo zote leo zinajikuta zinakimbizana na muda. Muda hauko upande wao.

Kwa Tanzania hadi hivi sasa kuna kitu kinachoonekana si cha kawaida (an anomaly). Nchi zote ambazo zimepata wagonjwa wa kwanza tumeona idadi ya wanaoambukizwa ikiongezeka kwa kasi kubwa (exponentially). Karibu mwezi mmoja nyuma (Februari 15) Marekani ilikuwa na wagonjwa 15; leo hii Machi 26 Marekani ina wagonjwa karibu 70,000. Hii ni nyuma ya China tu na Italia. Kasi hiyo ya kusambaa kwa ugonjwa huu imeonekana karibu nchi zote ambazo ugonjwa huu umejikita. Kwa Afrika ni Afrika ya Kusini ambayo inaonekana ugonjwa huu kusambaa kwa kasi (sasa hivi wao wana kesi zaidi ya 900)

Je, namba zetu zinaweza kuaminika?
Nimesema hapo juu kuwa hali katika Tanzania inaonekana si ya kawaida (an anomaly). Kwamba, kweli nchi yetu inaweza kuwa na wagonjwa 13 tu wakati watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida? Je inawezekana serikali inaficha hali halisi na kuwa labda Rais Magufuli hataki watu waone kuwa Tanzania ina wagonjwa wengi? Ukifuatilia mitandao ya kijamii unaweza ukaamini hili. Lakini hiki “kinachoonekana” ni lazima tukipime (kwa tulio pembeni) kwa kulinganisha na nchi nyingine kama za kwetu. Hadi hivi sasa inaonekana ugonjwa wa COVID-19 haujalipuka kwa kasi kubwa katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama ilivyo kwa nchi nyingine.

Kufikia leo kwa baadhi ya nchi za Afrika hali ya wagonjwa (na namba za wagonjwa wapya kwenye mabano) ni kama ifuatavyo:

Nigeria (yenye watu milioni 190) - 51

Rwanda – 41

Kenya 31 (3)

Madagascar (4)

Zambia – 16 (4)

Uganda - 14

Ethiopia (yenye watu milioni 105) - 12

Congo DR (yenye watu milioni 81) – 4


Hivyo, tukiangalia takwimu hata za majirani zetu na nchi nyingine tunazoshabihiana nazo kwa mambo mengi utaona kuwa kasi ya maambukizi bado si kubwa na kama alivyosema Waziri Ummy Mwalimu leo ni kuwa wengi wa wagonjwa hawa ni wale waliopata COVID-19 wakitokea nje. Kwa hiyo, hatuna budi kukubaliana na kile tunachokiona; ugonjwa huu ni tishio lakini kwa nchi hizi za kwetu haujaweza kusambaa kwa haraka katika jamii (community spread). Hofu ya ugonjwa huu kusambaa kwa haraka ndio ulikuwa msingi wa hoja yangu.

Hatua Zilizochukuliwa Zinatosha?
Hadi hivi sasa serikali imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa haya maambukizi ya ndani kwa ndani kwenye jamii hayatokei. Kufungwa kwa shule, vyuo na kutoa elimu ya usafi na kupunguza mikusanyiko isiyo ya lazima ni njia sahihi. Katika mazingira ya kawaida tulitarajia baada ya Isabela kugundulika kule Arusha tungeona mlipuko Arusha lakini hilo halijatokea. Katika mazingira tunayoyaona kwenye nchi za wenzetu mgonjwa wa kwanza anapopatikana tu basi kuna uwezekano wa kuibuka kwa wagonjwa wengi zaidi.

Na namna pekee ya kuwapata wagonjwa hao ni kuchukua vipimo kwa watu wengi kwa kadiri inavyowezekana. Hili nalo Waziri Mwalimu amelielezea leo vizuri. Kwamba serikali inafanya vipimo na kuongeza uwezo wa kupima kwa haraka. Hii yote inasaidia kuweza kujua ni sehemu gani ya watu katika nchi wanaweza kuwa wameupata ugonjwa huu.

Bahati Nasibu ya Magufuli
Ni kutokana na hili Rais Magufuli – ambaye ni mwanasayansi ameona kuwa kwa sasa nchi nzima si lazima ifungwe kama walivyofanya nchi nyingine. Amewataka Watanzania kuzingatia kanuni za usafi na kupunguza migusano isiyo ya lazima lakini wakati huo huo kuendelea na shughuli zao. Hoja hii si kwa Magufuli peke yake; tumeona hata Marekani kuna mjadala mkubwa wa kutaka watu waanze kurudi makazini ifikapo Pasaka kwani uchumi wao hauwezi kwenda bila watu kurudi makazini. Hili nalo tumelisikia kwa Rais Bosanaro wa Brazili na baadhi ya wataalamu ambao wanataka kuona jamii inatengeneza kinga ya jamii (herd immunity) ambayo inatokea endapo watu wengi wanapata maambukizi na kupona na hivyo kupunguza mahali virusi hivyo vinaweza kuambukiza zaidi.

Endapo kasi hii ya maambukizi Tanzania itaendelea kuwa ndogo namna hii mambo mawili yanaweza kutokea. Kwanza, tunaweza kujikuta hatuna wagonjwa wapya ndani ya wiki chache zijazo kwa sababu tumeweza kuzuia maambukizi ya ndani kwa ndani kwenye jamii na pili tunaweza kuonesha kuwa hofu ya kuwa Afrika itakuwa ni kiini cha mlipuko haina msingi kwani nchi zetu katika umaskini wao wote wameweza kudhibiti ugonjwa huu kwa haraka bila kulazimika kufunga nchi. Hii itaokoa uchumi wetu na watu wataendelea na maisha yao kama kawaida na kutumia fursa mbalimbali ambazo zitakuwa zimejitokeza kiuchumi.

Bahati Nasibu Ikilipa

Huku kutakuwa ni kulipa kwa bahati nasibu ya korona ambacho Magufuli ameicheza. Na ikitokea hivyo, Rais Magufuli atakuwa ameonesha namna nyingine ya kukabiliana na tishio hili kinyume na viongozi wenzake wa Afrika kama Uhuru Kenyatta, Cyril Ramaphosa na Paul Kagame. Mabezo yote ambayo baadhi ya watu wameyarusha kwa Rais Magufuli kwenye mitandao yatawarudia kwani Watanzania kwa fahari wataanza kuyarudisha mabezo hayo. Magufuli atajionesha bado ni kiongozi wa aina yake katika Afrika; umpende au usimpende. Kwamba, siyo kiongozi wa kufuata mkumbo au upepo.

Na inawezekana tukashuhudia kuwa kudhibitiwa kwa ugonjwa huu Tanzania kunaweza kutoa fursa mbalimbali za kiuchumi kwa viwanda vyetu na wajasiriamali mbalimbali. Baadhi ya nafasi zinazoweza au kupaswa kutumika mara ugonjwa huu ukidhibitiwa:

  • Utengenezaji wa vitakasa mikono (hand sanitizers)
  • Utengenezaji wa vifaa vya mtu kujikinga (PPEs) kama magauni, glovu, maski na vilemba. Viwanda vyetu vya nguo vinaweza kuchangamkia fursa hii
  • Utengenezaji wa vitanda na vifaa mbalimbali vya kitabibu (Kama dawa, maji ya wagonjwa n.k) ambavyo vinaweza kutoa nafasi kwa viwanda vyetu.
  • Kutoa mchango katika utafiti wa chanjo ya ugonjwa huu kwa wataalamu wetu (hatuwezi kuwa watu tunaosubiri wengine tu watuletee chanjo!)
Bahati Nasibu Isipolipa

Hata hivyo, bahati nasibu hii inaweza isilipe. Hili litatokea endapo vitu viwili vitatokea. Kwanza, endapo idadi ya wagonjwa wapya itaanza kuongezeka kwa kasi kama ilivyotokea nchi nyingine na kusababisha mfumo wetu wa tiba (healthcare system) kushindwa kuhimili na kubomoka (collapse). Pili, endapo itagundulika kuwa kwa makusudi serikali na taasisi zake wamekuwa hawaripoti kwa usahihi idadi ya wagonjwa na matokeo yake na hivyo kuwaacha watu wenye maambuziki kuendelea kuzurura mitaani na kusababisha hilo jambo la kwanza. Kwa vile hadi hivi sasa idadi yetu ya wagonjwa haina tofauti sana na baadhi ya nchi kama za wetu; suala la kuficha namba (under reporting) ni vigumu sana kuaminika isipokuwa kama kweli nchi nyingine zote kama za kwetu zingekuwa zinaripoti namba kubwa zaidi kulinganisha na za kwetu. Kwa nchi zetu za Afrika utaona kuwa tuoka katika wastani ukiondoa Afrika ya Kusini ambayo iko pembezoni kweli kweli (outlier).

Lakini endapo jambo la kwanza likitokea na Tanzania ikajikuta kwenye mlipuko mkubwa wa korona baadhi ya mambo ambayo yanaweza kutokea ni haya:

  • Magufuli atabebeshwa lawama binafsi za kusababisha hilo. Sidhani kama ataeleweka kama atakuja kuwalaumu Watanzania kuwa hawakumsikiliza.
  • Tanzania na Watanzania wote wanaweza kujikuta wanapigwa marufuku kwenda nchi nyingine hadi hali itakapotengemaa. Endapo mlipuko wa korona ukatokea wakati nchi nyingine zimedhibiti basi viongozi wa Tanzania watanyoshewa vidole na dunia nzima kwani wenzao walipokuwa wananyolewa wao walikuwa wanaweka kalikiti!
  • Mfumo wa afya wa Tanzania unaweza kujikuta ukiporomoka kuliko tunavyoweza kudhania. Tumeona jinsi nchi za daraja la kwanza (Italia, Ufaransa, Marekani na China) zikipata shida kukabiliana na ugonjwa huu. Imefikia mahali serikali za nchi hizo zimeomba na zinategemea misaada kutoka makampuni binafsi kupata dawa na vitendea kazi mbalimbali. Kuna hospitali Marekani manesi wake walijikuta wakitumia mifuko ya plastiki ya takataka kama mavazi ya kujikina! Marekani hiyo! Tumeona Hispania, wazee wakiachwa wajifie wenyewe kwani manesi na wahudumu wengine wamekimbia! Tumeona Italia madaktari na manesi wakifa kutokana na ugonjwa huu. Kama hili linatokea kwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti mkavu! Kama limetokea kwa chuma cha pua, itakuwaje kwa chuma chakavu!
  • Kama hali itakuwa mbaya zaidi ya nchi hizo basi mtafaruku wa kijamii (social unrest) unaoweza kutokea utatisha. Huko Marekani sasa hivi watu pamoja na utulivu unaoonekana kwa nje lakini watu wako katika hali ya msongo mkubwa wa mawazo. Tayari takwimu zinaonesha kuwa Wamarekani wananunua bunduki na silaha ndogondogo kwa kiasi kikubwa ili kujilinda endapo utatokea mtafaruku. Ununuzi wa bunduki umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 300 nchini Marekani kutokana na hofu ya kuvunjika kwa utawala wa sheria sababu ya korona.
Yapo na mengine ambayo yanaweza kusemwa. Lakini vyovyote vile ilivyo, swali kubwa ni je hii ni bahati nasibu holela au ni bahati nasibu inayotokana na fikra za kisayansi. Kwamba, Rais Magufuli badala ya kuangalia mambo kijamii anaongozwa na ujuzi wake wa kisayansi na hivyo anapima mambo kwa uzito wa ushahidi ulio mbele yake (empirical evidence). Kwamba, Rais Magufuli ameona kuwa uwezekano (chance) ya Tanzania kupata mlipuko mkubwa endapo tunaweza kudhibiti maambukizi yaliyopo hadi hivi sasa ni mdogo sana. Na hii ndio sababu amewataka Watanzania kutotishika na kuendelea na shughuli zao. Siyo kwamba, anapuuzia au hajali kinachotokea duniani bali hataki watu wake wajifungie ndani, waache kazi, na kuombea “siku ya mwisho ifike”. Magufuli anasema “tusitishane”. Kwamba, tunaweza kudhibiti hali iliyopo bila kulazimika kuifunga nchi nzima. Kiukweli, hayuko peke yake duniani.

Kama nilivyosema hapo mwanzoni, tayari nchi kama Marekani imeanza kufikiria namna gani ya kufungua nchi ili watu waanze kurudi makazini. Hata ndani ya Marekani yenyewe baadhi ya majimbo bado hayajatangaza kufunga shughuli zote kwa sababu hawajapata maambukizi mengi (kumbuka nusu ya kesi zote za korona Marekani zinatokea Jimbo la New York). Wenzetu Marekani kutokana na utajiri wao licha ya kuifunga nchi wameweza kutenga dola trilioni 2.2 kwa ajili ya kulinda ajira, wafanyakazi na kusaidia sekta mbalimbali ili zisilipe gharama kubwa kutokana na ugonjwa huu. Kiasi hicho ni sawa na bajeti ya sasa ya Tanzania kwa karibu miaka 75!

Ni wazi basi kila mmoja wetu afanye anachotakiwa kufanya kujikinga na ugonjwa huu. Serikali iendelee kuwa muwazi na kwa namna yeyote isiwafiche au kuonekana inawaficha Watanzania hali ilivyo. Wahenga waliposema “mficha maradhi kifo kitamfichua” walisema ukweli. Na kwa vile tumeona kuwa hadi hivi sasa hakuna sababu ya kudhania serikali haisemi ukweli ni muhimu basi Waziri Mwalimu na Waziri Mkuu kutoa taarifa za hali ilivyo kwa haraka na kwa uwazi. Katika ulimwengu wa mitandao ya kijamii, habari za uongo zinasambaa haraka na hatuwezi kuwafunga watu wote wenye kuandika au kuanzisha mijadala hiyo. La maana ni kuliwahi treni la uongo kabla yalijafika kituo cha kwanza.

Tukifanya hivyo, na kweli tukadhibiti maambukizi ya ugonjwa huu na kuhakikisha uchumi wetu hauyumbi kwa kiasi kikubwa basi bahati hii nasibu ya Magufuli; italipa na italipa na kulipa.

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Unaweza kufuatilia takwimu za kasi ya uambukizaji wa virusi vya korona nchi mbalimbali duniani kwa KUBONYEZA HAPA
Siku hizi umepatwa na nini???
Maana unajikopa. Mpaka aibu jiwe ana bahati ipi sasa hapa???


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je, namba zetu zinaweza kuaminika?
Nimesema hapo juu kuwa hali katika Tanzania inaonekana si ya kawaida (an anomaly). Kwamba, kweli nchi yetu inaweza kuwa na wagonjwa 13 tu wakati watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida? Je inawezekana serikali inaficha hali halisi na kuwa labda Rais Magufuli hataki watu waone kuwa Tanzania ina wagonjwa wengi? Ukifuatilia mitandao ya kijamii unaweza ukaamini hili. Lakini hiki “kinachoonekana” ni lazima tukipime (kwa tulio pembeni) kwa kulinganisha na nchi nyingine kama za kwetu. Hadi hivi sasa inaonekana ugonjwa wa COVID-19 haujalipuka kwa kasi kubwa katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama ilivyo kwa nchi nyingine.
Sisi ligi yetu ni Burundi na Sudan Kusini kwa kila hali.

Tumekwishatoka kwenye kundi la nchi nyingi kama hizo ulizoorodhesha hapo.

Hii ndio Tanzania yetu ya leo.

Sasa, niseme tu, siku hizi napata shida sana kusoma makala hizi ndefu ndefu zenye mizunguko.

Hapo nilipoishia, "Bahati Nasibu" ilikuwa bado kabisa..., sasa sijui bahati nasibu gani inayomsubiri!

Nitasoma michango ya wengine huko chini, labda kuna jibu la swali langu!
 
Acha uongo na propaganda Mzee. Marekani kama nchi haijaamua ni lini wananchi watarudi makazini wakati maambukizi yakiendelea kuongezeka. Huo uliousema ni uongo. In fact Wamarekani wengi, kwa mujibu wa polls/surveys wanapinga kuruhusu watu kuchangamana sasahivi wakati maambukizi yakiendelea kukua. True, ni Trump ndiye aliyeleta hadharani pendekezo lake kuwa watu warudi kazini mapema kuliko Wanasayasi wake wanavyoshauri. Kwahiyo acha kupotosha kwamba eti "hata Marekani" wanafikiria ... In fact, hata mjumbe wa "task force" ya Coronavirus ya serikali ya Marekani Dr. Fauci amesema kitakachoamua ni lini utaondolewa mwongozo na sharti la "social distance" ni Coronavirus yenyewe, na siyo mtu mwingine yeyote kwa hisia zake. Acha uongo Mzee.
Mweeh.. hivi kusoma nako ni kugumu; mbona sijasema wameamua? Mjadala upo ndiyo upo na usishangae ukapamba moto ndani ya wiki mbili zijazo.
 
Ndugu yangu wakati mwengine mambo unayotetea ni magumu sana.
Kwanza eleza kwanini baadhi ya nchi umeweka idadi ya watu na baadhi ya nchi hujaweka idadi ya watu wa nchi hiyo.

Kuchagua Nigeria and Ethiopia and DRC kuweka idadi ya wagonjwa na idadi ya watu inaonyesha upo DISHONEST. Ungeweka nchi zote na Idadi ya watu na idadi ya wagonjwa. Halafu umeona South Africa? Idadi ya watu? Idadi ya wagonjwa?

Kaka sayansi inataka objectivity.
Kiufupi ni kuwa Tanzania INAFICHA takwimu za Watu wenye Corona waliopimwa. Lakini pia Tanzania hakuna vipimo mpaka juzi tulipopata vya Jack Ma. Huwezi kujua idadi kama hupimi.

Mwisho kauli ya Rais kanisani jumapili iliyopita ni kauli mbaya Sana kwa Kiongozi na imeaminiwa na baadhi ya watu. Watu watakufa sana

Kuna factors mbalimbali kwenye kila nchi na kundi la watu; objectivity haina maana kila kitu kiko sawa. Dishonest ni kujikuta "crying wolf" ili kuwatisha watu wapanic kila linapotokea jambo dogo au ambalo si kubwa kivile.. mwisho wa siku tutajikuta tunalia "wolf" na watu wasisikillize tena.
 
Mmk tatizo kubwa ni uwaxi

Mmk tatizo letu accurate information. Je data tunazopewa ni sahihi?
Mbeya, dom tayar kuna wagonjwa na hawajaripotiwa bado
Jamani, mbona taarifa za ugonjwa ndiyo ziko hivi? wagonjwa wanapimwa, vipimo vinapelekwa kupata matokeo.. matokeo yakija ndio namba zinakuwa adjusted. Hili ni kweli hata hapa na mara nyingi matokeo yanakuwa nyuma ya siku kulinganisha na muda waliopimwa. Ndio maana unaona leo Marekani ina wagonjwa wengi kweli kweli. Kubwa ni vipimo. Sasa inawezekana kabisa wagonjwa wameongezeka lakini matokeo ya vipimo bado hayajatoka.. nchi nyingi bado hazijaweza kupima hapo hapo na kutoa matokeo hapo hapo. Huko si kuficha ndio hali halisi.
 
Mbona kaelezea vizuri viashiria tunvyotakiwa kutumia kujua kama Bahati nasibu imelipa ama kutolipa! Italipa pale janga hili litakapoisha bila ya kuwa na mlipuko kwenye nchi yetu kiasi cha kushindwa kuimudu, Haitalipa pale hali ya maambukizi itakapochukua kasi na kuwa na wagonjwa wengi kiasi cha vituo vya huduma kuzidiwa.

Hajasema haamini taarifa, lakini kaongelea dhana iliyojingeka miongoni mwetu kwamba kuna namna takwimu zinafichwa, ni dhana hatuna uhakika nayo.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Asante, kumbe nimeeleweka... nilidhani labda niliandika kwa Kigagagigikoko...
 
Takwimu za DRC umepotosha maksudi au vipi? maana mpaka sasa wana wagonjwa 51 na vifo 3.
Pia sijajua kwa nini hujazigusia Burkina Faso yenye maambukizi 152 na vifo saba, Ghana maambikizi 136 na vifo 4, Senegal yenye maambukii 105, Ivory Coast 96, Cameroon 88 na vifo 2, Tuombe tu kwamba base ya virusi isitanuke maana ikitanuka maambukizi yanaana kuongeeka exponentially.
Bado sidhani kama umenipata; bado ugonjwa haujalipuka Afrika kama watu walivyokuwa wanahofia ukiondoa Afrika ya Kusini...
 
Kwa nature ya maambukizi yalivyo ni mwendawazimu pekee anayeamini data za serikali.

1.Kwanza, wanaripoti wale waliowapima, hawaripoti wasio wapima

Sasa unaweza vipi kuripoti usiowapima?

2. Pili hata hao waliowapima mostly likely wanaundereport hii ni kutokana na ego ya bwana mkubwa kumess up kutochukua hatua mapema. Na kwa jinsi inavyoonekana hii kitu iko underreported 10 times
Mimi wakiniambia kuna cases 12 wanazozijua mimi nazidisha na 10, maana yake ni cases 120 wanazozijua.
Hizi ni hisia tu...
 
Hili huwa linanishtuaga; na wasipokufa 'sana'?
Mkuu tunaviongozi wengi ambao huamini kwamba wakisema kitu hakuna challenges kutoka Kwa wanao waongoza, wanajiona wako juu kuliko wengine wote

Kumbe sifa ambayo wengi wameikosa ni Ile Hekima ya kutamka nini na Kwa Wakati gani na mahali gani

Huwezi mtu ukawa ni wa kujitamkia tu bila kupima Kwanza unachokitamka,

Viongozi wa Aina hii ni hataree na hawafai, huwezi kuwatakia kifo Watanzania, ni kukosa hekima
 
Mweeh.. hivi kusoma nako ni kugumu; mbona sijasema wameamua? Mjadala upo ndiyo upo na usishangae ukapamba moto ndani ya wiki mbili zijazo.

..Bahati nasibu siyo neno sahihi.

..Neno ulilopaswa kutumia ni KAMARI / GAMBLE.

.. sidhani kama Tanzania ina CAPACITY [ vifaa, wataalamu, fedha, miundombinu] ya kupima, kuhifadhi, na kuwatibu waathirika.

..pia MFUMO wa maisha ya waTz hauruhusu kuchukua hatua ngumu za kujikinga [ isolation, social distancing, lockdown] na hatari ya mlipuko wa Corona.

..Kwa hiyo Raisi kusisitiza kwamba tumuombe MUNGU atuepushe na janga la Corona amekuwa mkweli. Serikali haina uwezo wa ku-deal na tatizo hili. Na hata wajomba / mabeberu ambao wangeweza kutusaidia na wenyewe wameelemewa.
 

Nilipoandika makala yangu ya ILIYOPITA kuhusiana na ugonjwa utokanao na virusi vya korona (COVID-19) Tanzania ilikuwa haijtangaza kuwepo kwa mgonjwa yeyote nchini na kuwa makala ile ililenga katika kutoa shime ya kuwahi ugonjwa huo. Nchi zote zilizowahi kuutangaulia ugonjwa huo na kuchukua hatua kali mapema wameweza kudhibiti kusambaa kwake na hata kupunguza kasi ya maambukizi (rate of infections). Nchi zilizochelewa kuchukua hatua hizo au zimechukua hatua ambazo ni za taratibu sana zimejikuta leo hii zikihangaika kuokoa na kulinda maisha ya wananchi wao. Italia, Ufaransa na Uingereza kama ilivyo Marekani na Irani ni nchi ambazo zote leo zinajikuta zinakimbizana na muda. Muda hauko upande wao.

Kwa Tanzania hadi hivi sasa kuna kitu kinachoonekana si cha kawaida (an anomaly). Nchi zote ambazo zimepata wagonjwa wa kwanza tumeona idadi ya wanaoambukizwa ikiongezeka kwa kasi kubwa (exponentially). Karibu mwezi mmoja nyuma (Februari 15) Marekani ilikuwa na wagonjwa 15; leo hii Machi 26 Marekani ina wagonjwa karibu 70,000. Hii ni nyuma ya China tu na Italia. Kasi hiyo ya kusambaa kwa ugonjwa huu imeonekana karibu nchi zote ambazo ugonjwa huu umejikita. Kwa Afrika ni Afrika ya Kusini ambayo inaonekana ugonjwa huu kusambaa kwa kasi (sasa hivi wao wana kesi zaidi ya 900)

Je, namba zetu zinaweza kuaminika?
Nimesema hapo juu kuwa hali katika Tanzania inaonekana si ya kawaida (an anomaly). Kwamba, kweli nchi yetu inaweza kuwa na wagonjwa 13 tu wakati watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida? Je inawezekana serikali inaficha hali halisi na kuwa labda Rais Magufuli hataki watu waone kuwa Tanzania ina wagonjwa wengi? Ukifuatilia mitandao ya kijamii unaweza ukaamini hili. Lakini hiki “kinachoonekana” ni lazima tukipime (kwa tulio pembeni) kwa kulinganisha na nchi nyingine kama za kwetu. Hadi hivi sasa inaonekana ugonjwa wa COVID-19 haujalipuka kwa kasi kubwa katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kama ilivyo kwa nchi nyingine.

Kufikia leo kwa baadhi ya nchi za Afrika hali ya wagonjwa (na namba za wagonjwa wapya kwenye mabano) ni kama ifuatavyo:

Nigeria (yenye watu milioni 190) - 51

Rwanda – 41

Kenya 31 (3)

Madagascar (4)

Zambia – 16 (4)

Uganda - 14

Ethiopia (yenye watu milioni 105) - 12

Congo DR (yenye watu milioni 81) – 4


Hivyo, tukiangalia takwimu hata za majirani zetu na nchi nyingine tunazoshabihiana nazo kwa mambo mengi utaona kuwa kasi ya maambukizi bado si kubwa na kama alivyosema Waziri Ummy Mwalimu leo ni kuwa wengi wa wagonjwa hawa ni wale waliopata COVID-19 wakitokea nje. Kwa hiyo, hatuna budi kukubaliana na kile tunachokiona; ugonjwa huu ni tishio lakini kwa nchi hizi za kwetu haujaweza kusambaa kwa haraka katika jamii (community spread). Hofu ya ugonjwa huu kusambaa kwa haraka ndio ulikuwa msingi wa hoja yangu.

Hatua Zilizochukuliwa Zinatosha?
Hadi hivi sasa serikali imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa haya maambukizi ya ndani kwa ndani kwenye jamii hayatokei. Kufungwa kwa shule, vyuo na kutoa elimu ya usafi na kupunguza mikusanyiko isiyo ya lazima ni njia sahihi. Katika mazingira ya kawaida tulitarajia baada ya Isabela kugundulika kule Arusha tungeona mlipuko Arusha lakini hilo halijatokea. Katika mazingira tunayoyaona kwenye nchi za wenzetu mgonjwa wa kwanza anapopatikana tu basi kuna uwezekano wa kuibuka kwa wagonjwa wengi zaidi.

Na namna pekee ya kuwapata wagonjwa hao ni kuchukua vipimo kwa watu wengi kwa kadiri inavyowezekana. Hili nalo Waziri Mwalimu amelielezea leo vizuri. Kwamba serikali inafanya vipimo na kuongeza uwezo wa kupima kwa haraka. Hii yote inasaidia kuweza kujua ni sehemu gani ya watu katika nchi wanaweza kuwa wameupata ugonjwa huu.

Bahati Nasibu ya Magufuli
Ni kutokana na hili Rais Magufuli – ambaye ni mwanasayansi ameona kuwa kwa sasa nchi nzima si lazima ifungwe kama walivyofanya nchi nyingine. Amewataka Watanzania kuzingatia kanuni za usafi na kupunguza migusano isiyo ya lazima lakini wakati huo huo kuendelea na shughuli zao. Hoja hii si kwa Magufuli peke yake; tumeona hata Marekani kuna mjadala mkubwa wa kutaka watu waanze kurudi makazini ifikapo Pasaka kwani uchumi wao hauwezi kwenda bila watu kurudi makazini. Hili nalo tumelisikia kwa Rais Bosanaro wa Brazili na baadhi ya wataalamu ambao wanataka kuona jamii inatengeneza kinga ya jamii (herd immunity) ambayo inatokea endapo watu wengi wanapata maambukizi na kupona na hivyo kupunguza mahali virusi hivyo vinaweza kuambukiza zaidi.

Endapo kasi hii ya maambukizi Tanzania itaendelea kuwa ndogo namna hii mambo mawili yanaweza kutokea. Kwanza, tunaweza kujikuta hatuna wagonjwa wapya ndani ya wiki chache zijazo kwa sababu tumeweza kuzuia maambukizi ya ndani kwa ndani kwenye jamii na pili tunaweza kuonesha kuwa hofu ya kuwa Afrika itakuwa ni kiini cha mlipuko haina msingi kwani nchi zetu katika umaskini wao wote wameweza kudhibiti ugonjwa huu kwa haraka bila kulazimika kufunga nchi. Hii itaokoa uchumi wetu na watu wataendelea na maisha yao kama kawaida na kutumia fursa mbalimbali ambazo zitakuwa zimejitokeza kiuchumi.

Bahati Nasibu Ikilipa

Huku kutakuwa ni kulipa kwa bahati nasibu ya korona ambacho Magufuli ameicheza. Na ikitokea hivyo, Rais Magufuli atakuwa ameonesha namna nyingine ya kukabiliana na tishio hili kinyume na viongozi wenzake wa Afrika kama Uhuru Kenyatta, Cyril Ramaphosa na Paul Kagame. Mabezo yote ambayo baadhi ya watu wameyarusha kwa Rais Magufuli kwenye mitandao yatawarudia kwani Watanzania kwa fahari wataanza kuyarudisha mabezo hayo. Magufuli atajionesha bado ni kiongozi wa aina yake katika Afrika; umpende au usimpende. Kwamba, siyo kiongozi wa kufuata mkumbo au upepo.

Na inawezekana tukashuhudia kuwa kudhibitiwa kwa ugonjwa huu Tanzania kunaweza kutoa fursa mbalimbali za kiuchumi kwa viwanda vyetu na wajasiriamali mbalimbali. Baadhi ya nafasi zinazoweza au kupaswa kutumika mara ugonjwa huu ukidhibitiwa:

  • Utengenezaji wa vitakasa mikono (hand sanitizers)
  • Utengenezaji wa vifaa vya mtu kujikinga (PPEs) kama magauni, glovu, maski na vilemba. Viwanda vyetu vya nguo vinaweza kuchangamkia fursa hii
  • Utengenezaji wa vitanda na vifaa mbalimbali vya kitabibu (Kama dawa, maji ya wagonjwa n.k) ambavyo vinaweza kutoa nafasi kwa viwanda vyetu.
  • Kutoa mchango katika utafiti wa chanjo ya ugonjwa huu kwa wataalamu wetu (hatuwezi kuwa watu tunaosubiri wengine tu watuletee chanjo!)
Bahati Nasibu Isipolipa

Hata hivyo, bahati nasibu hii inaweza isilipe. Hili litatokea endapo vitu viwili vitatokea. Kwanza, endapo idadi ya wagonjwa wapya itaanza kuongezeka kwa kasi kama ilivyotokea nchi nyingine na kusababisha mfumo wetu wa tiba (healthcare system) kushindwa kuhimili na kubomoka (collapse). Pili, endapo itagundulika kuwa kwa makusudi serikali na taasisi zake wamekuwa hawaripoti kwa usahihi idadi ya wagonjwa na matokeo yake na hivyo kuwaacha watu wenye maambuziki kuendelea kuzurura mitaani na kusababisha hilo jambo la kwanza. Kwa vile hadi hivi sasa idadi yetu ya wagonjwa haina tofauti sana na baadhi ya nchi kama za wetu; suala la kuficha namba (under reporting) ni vigumu sana kuaminika isipokuwa kama kweli nchi nyingine zote kama za kwetu zingekuwa zinaripoti namba kubwa zaidi kulinganisha na za kwetu. Kwa nchi zetu za Afrika utaona kuwa tuoka katika wastani ukiondoa Afrika ya Kusini ambayo iko pembezoni kweli kweli (outlier).

Lakini endapo jambo la kwanza likitokea na Tanzania ikajikuta kwenye mlipuko mkubwa wa korona baadhi ya mambo ambayo yanaweza kutokea ni haya:

  • Magufuli atabebeshwa lawama binafsi za kusababisha hilo. Sidhani kama ataeleweka kama atakuja kuwalaumu Watanzania kuwa hawakumsikiliza.
  • Tanzania na Watanzania wote wanaweza kujikuta wanapigwa marufuku kwenda nchi nyingine hadi hali itakapotengemaa. Endapo mlipuko wa korona ukatokea wakati nchi nyingine zimedhibiti basi viongozi wa Tanzania watanyoshewa vidole na dunia nzima kwani wenzao walipokuwa wananyolewa wao walikuwa wanaweka kalikiti!
  • Mfumo wa afya wa Tanzania unaweza kujikuta ukiporomoka kuliko tunavyoweza kudhania. Tumeona jinsi nchi za daraja la kwanza (Italia, Ufaransa, Marekani na China) zikipata shida kukabiliana na ugonjwa huu. Imefikia mahali serikali za nchi hizo zimeomba na zinategemea misaada kutoka makampuni binafsi kupata dawa na vitendea kazi mbalimbali. Kuna hospitali Marekani manesi wake walijikuta wakitumia mifuko ya plastiki ya takataka kama mavazi ya kujikina! Marekani hiyo! Tumeona Hispania, wazee wakiachwa wajifie wenyewe kwani manesi na wahudumu wengine wamekimbia! Tumeona Italia madaktari na manesi wakifa kutokana na ugonjwa huu. Kama hili linatokea kwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti mkavu! Kama limetokea kwa chuma cha pua, itakuwaje kwa chuma chakavu!
  • Kama hali itakuwa mbaya zaidi ya nchi hizo basi mtafaruku wa kijamii (social unrest) unaoweza kutokea utatisha. Huko Marekani sasa hivi watu pamoja na utulivu unaoonekana kwa nje lakini watu wako katika hali ya msongo mkubwa wa mawazo. Tayari takwimu zinaonesha kuwa Wamarekani wananunua bunduki na silaha ndogondogo kwa kiasi kikubwa ili kujilinda endapo utatokea mtafaruku. Ununuzi wa bunduki umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 300 nchini Marekani kutokana na hofu ya kuvunjika kwa utawala wa sheria sababu ya korona.
Yapo na mengine ambayo yanaweza kusemwa. Lakini vyovyote vile ilivyo, swali kubwa ni je hii ni bahati nasibu holela au ni bahati nasibu inayotokana na fikra za kisayansi. Kwamba, Rais Magufuli badala ya kuangalia mambo kijamii anaongozwa na ujuzi wake wa kisayansi na hivyo anapima mambo kwa uzito wa ushahidi ulio mbele yake (empirical evidence). Kwamba, Rais Magufuli ameona kuwa uwezekano (chance) ya Tanzania kupata mlipuko mkubwa endapo tunaweza kudhibiti maambukizi yaliyopo hadi hivi sasa ni mdogo sana. Na hii ndio sababu amewataka Watanzania kutotishika na kuendelea na shughuli zao. Siyo kwamba, anapuuzia au hajali kinachotokea duniani bali hataki watu wake wajifungie ndani, waache kazi, na kuombea “siku ya mwisho ifike”. Magufuli anasema “tusitishane”. Kwamba, tunaweza kudhibiti hali iliyopo bila kulazimika kuifunga nchi nzima. Kiukweli, hayuko peke yake duniani.

Kama nilivyosema hapo mwanzoni, tayari nchi kama Marekani imeanza kufikiria namna gani ya kufungua nchi ili watu waanze kurudi makazini. Hata ndani ya Marekani yenyewe baadhi ya majimbo bado hayajatangaza kufunga shughuli zote kwa sababu hawajapata maambukizi mengi (kumbuka nusu ya kesi zote za korona Marekani zinatokea Jimbo la New York). Wenzetu Marekani kutokana na utajiri wao licha ya kuifunga nchi wameweza kutenga dola trilioni 2.2 kwa ajili ya kulinda ajira, wafanyakazi na kusaidia sekta mbalimbali ili zisilipe gharama kubwa kutokana na ugonjwa huu. Kiasi hicho ni sawa na bajeti ya sasa ya Tanzania kwa karibu miaka 75!

Ni wazi basi kila mmoja wetu afanye anachotakiwa kufanya kujikinga na ugonjwa huu. Serikali iendelee kuwa muwazi na kwa namna yeyote isiwafiche au kuonekana inawaficha Watanzania hali ilivyo. Wahenga waliposema “mficha maradhi kifo kitamfichua” walisema ukweli. Na kwa vile tumeona kuwa hadi hivi sasa hakuna sababu ya kudhania serikali haisemi ukweli ni muhimu basi Waziri Mwalimu na Waziri Mkuu kutoa taarifa za hali ilivyo kwa haraka na kwa uwazi. Katika ulimwengu wa mitandao ya kijamii, habari za uongo zinasambaa haraka na hatuwezi kuwafunga watu wote wenye kuandika au kuanzisha mijadala hiyo. La maana ni kuliwahi treni la uongo kabla yalijafika kituo cha kwanza.

Tukifanya hivyo, na kweli tukadhibiti maambukizi ya ugonjwa huu na kuhakikisha uchumi wetu hauyumbi kwa kiasi kikubwa basi bahati hii nasibu ya Magufuli; italipa na italipa na kulipa.

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Unaweza kufuatilia takwimu za kasi ya uambukizaji wa virusi vya korona nchi mbalimbali duniani kwa KUBONYEZA HAPA
Namuomba Mungu atuepushe na lolote kati ya hizo bashiri zako zote mbili Mkuu Mwanakijiji kwa sababu mbili muhimu.

BAHATI NASIBU IKIFANIKIWA
Haina haja ya kuwa na furaha ndani ya nyumba yako ilihali jirani zako wote wameshika tama.

BAHATI NASIBU IKIBUMA
Askari akifia vitani hahesabiwi kama msaliti bali mzalendo, Dr. Magufuli akishindwa vita hivi atakua ni Askari aliyefia vitani hivyo kiungwana heshima yake itabaki pale pale.

MY TAKE
Swali ni je! Nchi kama Uganda walifunga mipaka kabla hata ya ugonjwa kuingia mhona sasa nao wanazo kesi za COVID - 19?

Italia pamoja na kuwa miongoni mwa nchi za ulimwengu huo wa kwanza mbona imefikia wakati Waziri Mkuu kanyosha Mikono kusalimu amri?

USA, UK, IRAN na kwengimeko pamoja na kuchukua kwao extremely measure kujikinga na ugonjwa huu mbona wana maambukizi mengi zaidi?

KWA UJUMLA WATU TUPIGE GOTI TUMWOMBE KARIMA ATUEPUSHE NA GONJWA HILI KWAKUA JITIHADA ZA MWANADAMU HAZIZIDI KUDRA.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado sidhani kama umenipata; bado ugonjwa haujalipuka Afrika kama watu walivyokuwa wanahofia ukiondoa Afrika ya Kusini...
ni kweli haujalipuka ila tahadhari za kiafya zilitakiwa zichukuliwe mapema kuliko kucheza na bahati nasibu. Kwa tabia ya ugonjwa huu ongezeko huanza taratibu sana na ghafla hupanda pale ambapo hamtegemei. DRC walikaa na case zao 3 kwa zaidi ya wiki tatu, ilipoanza kupanda ndo hiyo imekwenda kwenye 51 na vifo. USA the same hivi sasa wanazungumia maambukizi zaidi ya 17000 kwa siku. Hivyo tusione kama tuko unique sana kuliko wazungu na kuendeleza ukawaida wetu
 
ASILIMIA KUBWA YA WATANZANIA NI MASKINI WA KUTUPWA, AKITOKA NJE ANAENDA KUTAFUTA CHAKULA CHA KULA SIKU HIYO PAMOJA NA ASUBUHI IFUATAYO IKIWEZEKANA, SASA ASIPOTOKA NJE KWENDA KUTAFUTA UJUE ATASHINDA NJAA SIKU HIYO.
UNATAKA RAIS AZUIE WANANCHI WAKE WASITOKE NJE KUTAFUTA CHAKULA ILI WAISHI WEWE UTAKUWA NI MCHAWI, UNA UBINAFSI WA MOYO WAKO. RAIS ATAANGALIA NAMNA NYINGINE AMBAYO ANAONA ITAFAA ZAIDI KWA WATU WAKE, NA ATAWASIHII WATU WAKE WAMTEGEMEE MUNGU KWA IMANI ZAO HUKU NAYE AKIJITAHIDI KUTAFUTA JIBU LA UHAKIKA LA KUDHIBITI GONJWA HILO.

NAMPONGEZA RAIS WANGU, MUNGU AMLINDE NA AMBARIKI. MUNGU AKIMLINDA RAIS NA AKAMBARIKI ITAKUWA NI NEEMA KWA WANANCHI AWAONGOZAYE AMEEN!!
 
Kwa nature ya maambukizi yalivyo ni mwendawazimu pekee anayeamini data za serikali.

1.Kwanza, wanaripoti wale waliowapima, hawaripoti wasio wapima

2. Pili hata hao waliowapima mostly likely wanaundereport hii ni kutokana na ego ya bwana mkubwa kumess up kutochukua hatua mapema. Na kwa jinsi inavyoonekana hii kitu iko underreported 10 times
Mimi wakiniambia kuna cases 12 wanazozijua mimi nazidisha na 10, maana yake ni cases 120 wanazozijua.

Kudanganya data kuna matatizo makubwa nako ni kuwafanya watu warelax

Huyu bwana mkubwa afunge mipaka, hana uwezo wa kuenforce karantini ya siku 14 huku akiwa na uhakika kuwa hakutakuwa na violation.

Just imagine kawaachia wachina kuingia nchini miezi yote ile ya mlipuko, leo Wachina wameamua kutufungia vioo kwa kufuta residence permit za wageni wote bila kujali taifa gani liliwapokea kipindi wanahaha.

Stubborness ya mtu mmoja itaangamiza Taifa, Baraza la Usalama la Taifa inabidi limkatalie huyo mzee kwa kumwambia bila woga kuwa measures zake zimekaa kihatari mno.

Kikubwa sasa ni Kufunga hiyo mipaka
Zuia mikusanyiko isiyo ya lazima na iincourage watu waliokatika vyombo vya usafiri kuvaa mask badala ya kuzipiga vita mask, kuvaa mask kwenye mikusanyiko ni muhimu maana hujui nani kaambukizwa
Tusaidie mkuu, Je, kwenye ukoo wenu kunaaliye na maambukizi?

Na ole useme hakuna, maana yake ungependa uone maambukizi yakizidi kuenea Kwa wengine tu Ila sio kwenu??
Unataka kuona Serikali ikiendelea kuripot ongezeko la wagonjwa ambalo miongoni mwao ukoo wenu hakuna?

Ukiwa mpinzani kwani ni lazima ujivike ushetwani?

Kama kwenye ukoo wenu hakuna hata mmoja aliyeathirika,unataka waongezeke kutoka wapi sasa?😉
 
Back
Top Bottom