Uchaguzi 2020 Hoja ya CHADEMA kwamba wahudhuriaji wa mikutano ya CCM kwamba wanabebwa kwenye magari naifananisha msemo wa usilolijua sawa na usiku wa giza

Uchaguzi 2020 Hoja ya CHADEMA kwamba wahudhuriaji wa mikutano ya CCM kwamba wanabebwa kwenye magari naifananisha msemo wa usilolijua sawa na usiku wa giza

Mimi na rafiki zangu huwa tunaenda kwenye mikutano ya CCM kumwangalia konde boy pamoja na Diamond platinum kwa sababu ni bure
 
Kwa mfano limejenga uwanja wa ndege nyumbani kwake chattle

sasa huo ndo ufisadi? lijamaa lenu bado ni mbunge, anapokea ela kama mbunge wa hai, alafu pia ni mwenyekiti wa chama, na pia anapokea michango ya wabunge wenzake pamoja na wananchi 😂 😂 😂 😂 , yupi nuksi apa
 
1961ata baba yako alikuwa hajazaliwa unajua nyie watoto 2000's mnajifanya mnaijua sana CCM.
Waambie CCM waache kuwaibia Watanzania wasio na hatia. Wizi wa vitambulisho vya wajasiliamali, wizi wa Rambirambi. Kila Kona ni wizi tu. Mtajibu siku ya kiama
 
sasa huo ndo ufisadi? lijamaa lenu bado ni mbunge, anapokea ela kama mbunge wa hai, alafu pia ni mwenyekiti wa chama, na pia anapokea michango ya wabunge wenzake pamoja na wananchi 😂 😂 😂 😂 , yupi nuksi apa
BUNGENI mmekwapua 1.5 trilioni hazionekani
 
Ina maana Hashimu Rungwe nae akiwapelekea magari watapanda kwenda kwenye kampeni za Chauma?
 
Kwanza niwaulize hao wanaouzulia mikutano yenu wanatokea umbali gani? Kama wanatokea nje ya miji au katikati ya miji wanatumia nauli zao au zenu?

Mna uhakika gani kama wamejiandikisha au lah!, mnajuaje kama wote wamekuja kwa lengo la kuwapenda maana watanzania ni kawaida yao kuhudhuria kila jambo baya au zuri.

Niwafaamishe tu kuwa CCM ina wanachama wanaotambulika kindakindaki, CCM damu kila kitongoji, kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa, kanda na Taifa wapatao Milioni 18 wakati huo huo waliojiandikisha wapo Milioni29.

Mnaweza kuona hesabu rahisi kabisa hivyo sisi tunawawezesha wanachama wetu kufika kwenye kampeni kwa wakati na tunaobeba tunajua wazi ni wanachama hai na wana kadi na kama hamuamini subirieni 28/10/2020.

Hhamjiulizi kwanini watu wanavaa sare na wanakubali kubebwa. Zimwi likujualo halikuli likakumaliza hivyo msije kujidanganya ni umaskini wenu ndio unaowafanya mshindwe kusomba wapiga kura na ingekuwa inaruhusiwa kuwabeba wanachama siku ya kupiga kura ndio mngezimia zaidi.

Chama chochote kinachojitambua kamwe hakiwezi kuacha kuwajali wanachama wake wanaowaweka madarakani, nasisitiza hapa tutawabeba wanachama wetu hai nchi nzima hatuwezi kuwasikiliza watu walioishiwa hoja.

Huwezi kujisifia kuwa watu wanakupenda na huku unashindwa kuwapa usafiri wa kufika mikutanoni. Chama chochote mtaji wake ni wanachama sio wahuni au watu wasiotabilika kama mnaamini siasa ni imani basi sisi tuna wanaotuamini Milioni 18 na wana kadi na watampigia Rais kura na tutashinda kwa kishindo, nyie endeleeni kusema tunabeba watu kwenye mikutano ilihali mnashindwa kujua ndio wanachama kindakindaki na ndio wapiga kura wa uhakika.
Milioni 18?????watatoka wapi wewe taga..2015 mliiba kijinga
 
Back
Top Bottom