Uchaguzi 2020 Hoja ya kufuta sheria zinazonyima watu dhamana Ni turufu kwa CHADEMA

Uchaguzi 2020 Hoja ya kufuta sheria zinazonyima watu dhamana Ni turufu kwa CHADEMA

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Hii hoja ya kufuta sheria kandamizi zinazonyima watu dhamana Ni yakuungwa mkono na kila MTANZANIA, wapo Wana CCM inawaumiza na kuwanyamazisha, wapo wapinzani na wapo wafanyabiashara ambao leo CCM ikitaka ikufilisi inakupeleka mahakaman kwa makosa yakusadikika na hatma yake unaozea jela bila kesi yako kusikilizwa.

Kama Kuna hoja ambayo hata wana CCM wangepaswa kuona inatosha kuwapa Uhuru Ni hoja ya kuwanyima watu dhamana.

CCM wanashindwa hata kupambana ndani ya chama kwa kuofia kubambikiwa kesi, Leo hii hata ukiwa na ugomvi binafsi na kiongozi wa CCM au serikali anachofanya nikuelekeza upewe kesi isiyo na dhamana...huu ni utumwa.

Kama Zanzibar tu wamepiga marufuku hii sheria sisi bara tunashindwa nn? Nchi nyingi zinazowaza kuhusu maendeleo ya watu zinawaza kuhusu kufuta sheria kandamini lakini nchi zinazoongozwa kwa maendeleo ya vitu na mtu zinawaza kuwazuia watu wasiwaze tofauti, wasiendelee na wasiendeleze vizazi vyao ili iwe rahisi kuwatawala.

Tuing'oe miziz ya sheria hizi zinazokandamiza watu. Watu wapewe dhamana mahakama ipokee ushahidi iwafunge
 
Back
Top Bottom