Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Ndio kielelezo cha utaifa wa Tanzania kinapotambulika kimataifa. Kwani Tanganyika na Zanzibar zipo mbinguni?.
Umesema hayo mambo mengine ni ufahari wa kidunia tu ila kwako muhimu ni Tanzania kuwa na kiti umoja wa mataifa ndiyo nimekuuliza huko umoja wa mataifa ni mbinguni siyo duniani? Hata hivyo nisikutwishe mzigo usiyohumudu maana inawezekana tunajadili vitu viwili tofauti.
 
Unajua ndugu Pascal Mayalla mzee kama wewe ikifikia mahali mtu akakuita "mjinga" na Kitambakwiri" labda itakuwa ni kukukosea heshima na adabu...
Lakini inakuwaje kama wewe mwenyewe umejipa hiyo sifa ya UJINGA na UPUMBAVU?
Bila shaka atakeyeitikia na kukufukuzia kwa tabia yako hiyo hatakuwa amekuvunjia heshima yoyote..
Mpaka hatua hii, bila shaka yoyote ni kuwa WEWE Pascal Mayalla ndiye hasa uliye MJINGA na KITIMBAKWIRI unayestahili kuelimishwa na kufundishwa kusikiliza na kuelewa mawazo ya watu wengine..
Neno!
Tunautaka muungano. Tunataka ushirikiano na watu au nchi zingine. Lakini muungano huo ni lazima uwe wenye usawa na kuheshimiana kwa pande zote zilizokubali kuunga/kushirikiana..
Na pia muungano huo uwe na faida kwa pande zote. Mfano, Tanzania inapokuwa na MoU na mataifa kama Marekani, UK, Ufaransa , China n.k. utajiuliza ni kwa vipi? Uchumi wa Miji ya Beijing, New York , California n.k. ni mkubwa kuliko wa Tanzania! swali ni kwanini wanatuhitaji? Jibu ni rahisi kuna kitu kinaitwa ''mutual benefit'.

Swali, Muungano wetu na Zanzibar, Watanganyika wana kitu gani cha kufaidika?
Hii haina maana hatuhitaji Muungano, lakini Muungano uliopo una investment isiyo na return au dividend.

Lakini pia tunajiuliza pamoja na kubeba muungano kwanini tutumie muda mwingi na gharama kubwa kuwabembeleza Zanzibar na si ku invest katika maeneo yatakayokuwa na tija kwa ustawi wa Tanganyika
KWA HIYO: Sio UJINGA wala u - TIMBAKWIRI watu kuzisema kasoro hizi kwa malengo ya kurekebisha. Ujinga na u - timbakwiri ni kule kung'ang'ania kuishi ktk makosa au kasoro. Na huyo mtu ni wewe na wenzako wote huko CCM...
Makosa ni kudhani kwamba wataweza kuendelea na ulaghai huo daima milele.
Kwasasa hali ya muungano ni mbaya kwasababu walioubeba wamechoka! Nani atazuia wimbi linalovuma
Swali ni moja tu: Mataweza kuwafanya Watanganyika kuishi ktk ujinga wenu hadi lini?
Hilo halikubaliki na ni LAZIMA TUCHUKUE HATUA KUREKEBISHA..
' The train has just left the train'' fursa ilikuwa kupitia Tume ya Warioba, wakaihujumu.
Tanganyika itarudi ni suala la muda na haiuziliki. Marekebisho yatakuwa na gharama kubwa sana

Walifanya makosa kutowahi marekebisho wakati Watanganyika wakiwa kimya! hatari kubwa wasiyo iona viongozi ni ' Tanganyika ina upper hand'' ndiyo iliyobeba Muungano, haina cha kupoteza.
Viongozi wanapuuza Watanganyika bila kujua kwamba wanaohitaji Muungano ni Zanzibar!
Tanganyika inatoa haipati kitu! ina nini cha kupoteza !

Hawa viongozi wasipofanya jambo ipo siku Watanganyika wataamka na kusema ''NO' na huo utakuwa mwisho. Hizi projo za ' tutalinda kwa gharama yoyote hazina maana , Nyerere alionja joto la G55''
Je, yupo Nyerere mwingine?
 
Mkuu Nguruvi3, unapoteza muda. Kwa bahati mbaya watu aina ya Pascal Mayalla wamejaaliwa kuwa na akili kubwa lakini zisizo za kawaida. Mtu kama huyu akiwa mwizi na akabahatika kuishi ndani ya taifa hili la wajinga ataiba hadi avimbiwe hadi kupasuka!

Wizi kama huu hujulikana kama wizi usio na staha. Yaani mtu anaanza kwa kuiba vya nje na ikiisha anaanza kufanya kufuru. Atawaibia ndugu zake, atawaibia wazazi wake, atamwibia mkewe, atawaibia watoto wake na mwisho ataanza kujiibia yeye mwenyewe.

Naam ndivyo walivyo na mimi binafsi nasita sana kuwa na mnakasha na watu wanaojiita wenye akili hizo huku wakitetea mambo ya kipuuzi na ya kijinga. Hizo si akili ni ugonjwa unaosababishwa na vitu vingi lakini viwili vikubwa ni tamaa na ulafi...tamaa na ulafi ni kama pete na kidole!
Mkuu nakuelewa sana
Hatari ninayo iona ni watu kuachwa wafanye '' exploitation' ya jamii yetu iliyojaa wengi wasio na maarifa ya kutafuta ukweli. Kwa mfano kuna kijana kaniambia eti natakiwa nijibu 'uadhimu na uadimu wa Muungano''
Tena anasisitiza kwamba Pascal kaeleze vizuri sana kuhusu Muugano wa 'Union na Federation'

Huyo kijana anaamini kwamba kuna federation ya '' Tanzania na Zanzibar' kutoka kwa Pascal, na si yeye, unapokuwa na vijana kama hawa kwa wingi iwe kwa ignorance au uchawa bado kama Taifa tuna tatizo

Nilipomuuliza huyo kijana Federation ya Tanzania na Zanzibar inatokeaje, hakuwa na jibu.

Upotoshaji unapewa nafasi katika media na media kuacha wajibu wao .
Hivi media house ikiwa na editorial board inashindwa vipi ku 'fact check' kuhusu contents wanazochapisha!

Watu wenye ushawishi katik jamii wanapoongozwa na tamaa na ulafi kuna madhara makubwa.
Si kwamba wanafanya exploitation lakini pia wanafanya intellectual abuse na wana najisi akili za watu. Tunakuwa na vicious circle ya chawa na wapuuzi.
 
Zanzibar ni ndogo sana kiasi cha kuzisumbua akili za watu wengi wa bara wakaacha kutafuta mkate wao wa kila siku na kuanza kuiwazia. Ni sawa na wilaya mbili tu za mkoa wa Morogoro au Tabora.
Lakini inapewa mapato kuliko Morogoro au Tabora! mapato yanayotoka Morogoro na Tabora.
Hulioni tatizo hapo?

Lini Wananchi wa Morogoro na Tabora waliwahi kulipiwa umeme na JMT? Zanzibar wanalipiwa. Huoni tatizo?

Nafasi za ajira za Morogoro na Tabora zipo wapi? Zanzibar wanazo!
Nafasi za elimu ya juu na mikopo za Tabora na Morogoro ziko wapi? Zanzibar wanazo! huoni tatizo?


Unaweza ku ignore ukatafute mkate lakini bei ya mkate huo ni pamoja na bill ya umeme ya watu waliopunzika ufkweni Zanzibar! Ni pamoja na mishahara ya Wazanzibar wanaolala pale Mjengoni wakisema si Watanzania. Kwahiyo katafute mkate na maji ili ujaze ndoo inayovuja
 
Lakini inapewa mapato kuliko Morogoro au Tabora! mapato yanayotoka Morogoro na Tabora.
Hulioni tatizo hapo?

Lini Wananchi wa Morogoro na Tabora waliwahi kulipiwa umeme na JMT? Zanzibar wanalipiwa. Huoni tatizo?

Nafasi za ajira za Morogoro na Tabora zipo wapi? Zanzibar wanazo!
Nafasi za elimu ya juu na mikopo za Tabora na Morogoro ziko wapi? Zanzibar wanazo! huoni tatizo?


Unaweza ku ignore ukatafute mkate lakini bei ya mkate huo ni pamoja na bill ya umeme ya watu waliopunzika ufkweni Zanzibar! Ni pamoja na mishahara ya Wazanzibar wanaolala pale Mjengoni wakisema si Watanzania. Kwahiyo katafute mkate na maji ili ujaze ndoo inayovuja
Inapewa mapato? haina vyanzo vyake vya mapato unataka kusema?. Tunajaribu kushusha thamani Zanzibar kwa maarifa yetu ambayo upatikanaji wake una walakini.

Muungano una faida zake za pande mbili tatizo unapofikiria kuhusu hasara ukitumia nguvu nyingi unapoteza uwezo wa kuuona upande wa faida.
 
Lakini inapewa mapato kuliko Morogoro au Tabora! mapato yanayotoka Morogoro na Tabora.
Hulioni tatizo hapo?

Lini Wananchi wa Morogoro na Tabora waliwahi kulipiwa umeme na JMT? Zanzibar wanalipiwa. Huoni tatizo?

Nafasi za ajira za Morogoro na Tabora zipo wapi? Zanzibar wanazo!
Nafasi za elimu ya juu na mikopo za Tabora na Morogoro ziko wapi? Zanzibar wanazo! huoni tatizo?


Unaweza ku ignore ukatafute mkate lakini bei ya mkate huo ni pamoja na bill ya umeme ya watu waliopunzika ufkweni Zanzibar! Ni pamoja na mishahara ya Wazanzibar wanaolala pale Mjengoni wakisema si Watanzania. Kwahiyo katafute mkate na maji ili ujaze ndoo inayovuja
Kupewa mapato ni makubaliano ya kikatiba yaliyoandikwa miaka mingi iliyopita. Nafasi za ajira za bara zipo nenda kwenye raasisi za kiserikali zinazotoa ajira watakupa mgawanyo wa kila eneo la Tanzania.

Nafasi za elimu pia zipo tena nyingi tu, hakuna kinachowagusa watu wa huku bara kisiwaguse wazenji pia.

Ni hulka zile zile za uchoyo, ubaguzi na umaskini pia. Tuna mamia kwa mamia ya fursa za kujiendeleza sisi wenyewe wa huku bara bila hata kugusa hicho wanachokipata ndugu wa visiwani.

Tembea tu na gari lako kutoka nje ya Dar kabla hujafika Morogoro utaona kushoto na kulia ardhi nzuri ambayo haijaguswa bado, bado haijatumika kuweza kuchangia pato kwa taifa. Tembea mikoani uone ardhi nzuri tu ambayo bado haijaguswa na hivyo haijaweza moja kwa moja kuweka mchango kwenye pato kuu la Taifa.

Ni aibu sana kwetu sisi wa huku bara kulia na hicho kidogo kinachokwenda huko viswani wakati tunao utajiri usioguswa leo hii miaka 63 baada ya uhuru.
 
Inapewa mapato? haina vyanzo vyake vya mapato unataka kusema?. Tunajaribu kushusha thamani Zanzibar kwa maarifa yetu ambayo upatikanaji wake una walakini.
Yes! tuonyeshe bajeti ya ulinzi, mambo ya ndani, nje katika bajeti ya SMZ.
Onyesha mikopo wanayopewa kama sehemu yao wapi wanarudisha wenyewe kama si JMT
Makusanyo ya kodi ya SMZ ni bilioni 60 kwa mwezi sawa na chini ya bilioni , bajeti ya 2023/2024 ni 2.4T!
Unajua ni kiasi gani 4.5% sasa ni 9% ya Bajeti ya JMT inakwenda Zanzibar! Morogoro na Tabora wanapata kiasi gani
Tuonyeshe wapi mapato ya TRA yamevuka kutoka SMZ kuja hazina Dar
Tuonyeshe wale Wabunge 80% wanalipiwa na bajeti ipi ya SMZ?
Kwanini mfuko wa Mbunge wa uende Zanzibar wakati hawana mchango wowote katika katika JMT
Kwanini Mbunge anayechaguliwa na watu 3,000 awe na haki sawa na Mbunge anayechaguliwa na watu 400,000
Kwanini wao wawe na kipaumbele zaidi ya raia mlipa kodi wa Tanganyika.
Muungano una faida zake za pande mbili tatizo unapofikiria kuhusu hasara ukitumia nguvu nyingi unapoteza uwezo wa kuuona upande wa faida.
Tuonyeshe na utushawishi kwamba Tanganyika inahitaji Muungano! hebu tushawishi ni kwa lipi au faida gani.
 
Kupewa mapato ni makubaliano ya kikatiba yaliyoandikwa miaka mingi iliyopita.
Tuonyeshe wapi katika katiba imeelezwa hiyo!
Kumbuka wao ndio wanataka formaula ya kugawana rasilimali za Tanganyika! kama ipo kikatiba ni wapi?
Ni hulka zile zile za uchoyo, ubaguzi na umaskini pia.
Hkusikia wanataka passport kuingia Zanzibar! huo si ubaguzi
Hukuwasikia Wazanzibar hawataki Utanzania kwasababu ni Wazanzibar, huo si ubaguzi

Unashindwa kuelewa kwamba Ubaguzi wa Wazanzibar ndio chanzo cha matatizo na sasa ubaguzi huo itakula kwao. Watu wanaitaka Tanganyika yao ili Zanzibar ipate mamlaka kamili

Tunahitaji Tanganyika tusimamie mambo yetu, hatuna muda wa kubembelezana kila siku!

Ikiwa wanataka Muungano watasema wao , Tanganyika haina cha kupoteza wala kunufaika!

Narudia tena tuonyeshe au tueleze, kwanini Tanganyika inahitaji Muungano! ni kwasababu au faida gani
 
Narudia tena tuonyeshe au tueleze, kwanini Tanganyika inahitaji Muungano! ni kwasababu au faida gani
Karibu "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza
Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.

Anasema Zanzibar inafaidika sana na muungano, kisiasa, kiuchumi na kijamii, ikiwemo kufaidika kielimu, wakati wa muungano, Zanzibar haikuwa na chuo kikuu chake hivyo Wanzanzibari wote wa enzi hizo waliofika elimu ya vyuo vikuu, wamesomea bara.

Mama Samia amesema watu waachiwe kuujadili muungano kadri watakavyo na hata kutema nyongo kuhusu muungano, na serikali inazitumia hizo hoja zinazolalamikiwa kuimarisha muungano, akasema ni heri watu wafunguke na kusema hivyo kuyatoa madukuduku yao, kuliko kunyamaza na madukuduka ndani yao, siku wakilipuka moto utawaka, hivyo watu waachwe waseme.

Amesema Zanzibar ni visiwa hivyo viko wazi pande zote, hivyo faida kubwa kabisa ya muungano ni ulinzi usalamax amani na na utulivu wa Zanzibar, bila muungano, ilikuwa ni rahisi sana kuivamia Zanzibar na Zanzibar ikivamiwa ni rahisi sana kuivamia bara, hivyo muungano umeimarisha sana ulinzi na usalama, amani na utulivu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kuna kitu Mama Samia amekisema sikuwahi kukijua!. Kumbe Wizara ya Mambo ya Nje ilipokiwa ikiitwa Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa ndio ilikuwa ya Muungano iki handle issues zote za Zanzibar kimataifa, lakini , ilipobadilishwa jina na kuitwa Wizara ya Mambo, ya Nje na Ushirikiano wa Africa Mashariki, sasa ina handle mambo ya Zanzibar ndani ya Africa Mashariki tuu, lakini kimataifa, kwa yale mambo ambayo sio ya muungano, SMZ ya Zanzibar imepewa uhuru wa kunegotiate ufadhili, misaada, na mikopo na mikataba ya kimataifa kwaniaba ya Zanzibar, ila kwenye kutiliana saini, anayetia saini ni serikali ya JMT, kwasababu Zanzibar haina sovereignty, sovereignty ni moja tuu ambayo iko kwenye JMT pekee!.

Hili sikuwahi kulijua, hivyo kumbe sasa Zanzibar inaweza kupata misaada na mikopo ya kimataifa, sasa kwavile uwiano wa kugawana misaada ya kutoka nchi wafadhili na wahisani, Zanzibar inastahili kupata asilimia 4.5% ya misaada yote kwa Tanzania, sasa kwa vile Zanzibar nayo inaweza kuomba ufadhili wa kimataifa, jee hii misaada ya kimataifa ya Zanzibar inayoomba, Tanzania bara pia tunapewa ule mgao wa asilimia 95.5% ya misaada ya Zanzibar, au misaada ya Tanzania tuu, ndio Zanzibar inapaswa kugaiwa asilimia 4.5%, lakini kwa misaada ya Zanzibar, then misaada hiyo ni ya Zanzibar pekee?.

Mama Samia amezungumzia kero za muungano na kusema kero nyingi zimeisha tatuliwa ila utekelezaji ndio unasua sua, na kutolea mfano deni lililokuwa la umeme la Tanesco, deni hilo lilisababishwa na double taxation, kwa Tanesco kuwachaji SMZ VAT huku shirika la umeme la Zanzibar, Zesco nalo likiwachaji kodi ya ongezeko la thamani Vat, wateja watumiaji wa umeme zao nao wakilipishwa Vat, kero hiyo imetatuliwa kwa Tenesco hawaichaji tena Vat kwa SMZ, hivyo Zanzibar haidaiwi tena deni lolote la umeme na Tanesco.

Ninachokumbuka kwenye deni la umeme la Zanzibar, lilitokana na Tenesco kuuza umeme kwa bei ya juu kwa Zesco, halafu Zesco wanauza umeme huo kwa bei ya chini Zanzibar, kumbe ilikuwa ni issue ya VAT!.

Pia amezungumzia kero za muungano kadri zinavyotatuliwa, kero nyingine zinaibuka, hivyo issue za kero za muungano ni issue endelevu.

Amezungumza mengi na kumalizia kwa kusisitiza Muungano ni jambo jema, tuulinde na kuuenzi.

Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?. Hili mnalionaje?.

Paskali
Natumaini umeelimika
P
 

Rais SSH aliyesema wakati akiwa VP, muda hauongopi rangi zipo wazi hata maua ya Zambarau anapewa. Ukipendwa na Zambarau kuna jambo unafanya dhidi ya Tanganyika kwasababu wana chuki nayo. Niishie hapo

Pili, alichosema kuhusu manufaa kwa upande wa Zanzibar ni kweli.
Hoja ni kwamba Tanganyika inapoteza nini ikiwa Wazanzibar hawataki muungano!

Tatu kuhusu Wizara ya mambo ya nje, ni kweli Jakaya Kikwete aliwapa ruhusu ya kukopa.
Kelele unazosikia wanataka kukopa kupitia jina la JMT halafu hawalipideni linalipwa na Hazina Tanganyika inayoitwa Hazina Tanzania. Ikiwa wanakopa na wanalipa wenyewe sioni kama ni tatizo! sivyo! wao wanataka kupitia JMT !

Kuhusu misaada, nimewasikia Wazanzibar wengine na ma-digrii wakiishi nje ya nchi wakilizungumzia hili.
Misaada inayokuja ni fadhila wala haina 'guarantee' hivyo kuiongelea ni ukosefu tu wa elimu.

Bajeti ya ulinzi ni 3.3T ambayo Zanzibar haichangii hata senti!
Bajeti ya Mambo ya ndani na Taasisi za Muungano ni zaidi ya 2.5 Trilioni, Zanzibar haichangii hata senti tano.

Gharama za Wabunge wanaochaguliwa na watu 3,000 na mfuko wa jimbo la watu 3,000 zinatoka Tanganyika
Mishahara , marupu rupu na pensheni za Watumishi wa Muungano zinatoka Hazina Tanganyika

Kuna 4.5% sasa (9%) kwa mujibu wa mwenezi CCM Zanzibar, msaada wa kibajeti kutoka 49T za Bajeti ya Tanganyika

Mwaka 2023/2024 Bajeti ya Zanzibar isiyo na ulinzi , usalama , mambo ya nje na Muungano ilikuwa 2.8T.
Makusanyo ya Zanzibar kwa miezi 5 ni takribani 270 Bilioni ikiwa ni takribani 50 Bilioni kwa mwezi

Pia, Tanganyika imebeba Wazanzibar wengi kuliko wanaoishi Zanzibar , wanatumia resources za Tanganyika bila kubaguliwa iwe shuleni , Hospitali n.k. kwa jina la Tanzania kwasababu ile ile wao ni Watanzania na Wazanzibar

Hoja hapa ni kwamba gharama za Muungano na SMZ zinabebwa na kodi za Watanganyika , wanaposema misaada ni upuuzi tu maana wanapewa kuliko wanachoweza kukusanya au kutengeneza. Ni ukosefu wa matumizi ya elimu.

Tatu, kuhusu deni la umeme kutotozwa VAT na Tanesco si sawa. Ikiwa Tanesco ni shirika la Tanzania kwanini kuna ZESCO. Kukiwa na mashirika mawili tayari Tanesco inakuwa ya Tanganyika.

Kutotoza VAT ni kuwabebesha mzigo Watanganyika kwasababu gharama za uendeshaji Tanesco zinabebewa na Watanganyika, si Wazanzibar!

Hoja kwamba eti ni nchi moja ni ya kipuuzi kwasababu huwezi kuwa na ZESCO inayoongeza gharama za uendeshaji wakati Tanesco ingefanya peke yake. Lakini pia nchi moja ipi ikiwa Wabunge wa Zanzibar wanasema si Watanzania?

Kufuta deni la umeme ni kuwaumiza Watanganyika kwasababu Tanesco ikipata hasara anayefidia ni Mtanganyika.

Swali linabaki pale pale, Kwa kubebeshwa zigo la Bilioni 60 za umeme, Tanganyika inafadika nini na Muungano na ingepoteza nini kama isingepeleka umeme Zanzibar !

Nne, suala la kero ni la ajabu maana Zanzibar inalalamika dhidi ya nani?

Tanganyika haina structure ya gov. Zanzibar haiwezi kulalamika dhidi ya Tanzania kwasababu kanuni za asili zinasema '' huwezi kuwa mlalamikaji, halafu ukawa mwedesha mashtaka na kisha Hakimu''.

Leo SMZ inakuja na Kero dhidi ya Tanganyika. Mwendesha mashtaka ni VP wa JMT ambayo Wazanzibar wamo. Hakimu ni Rais wa JMT ambayo Wazanzibar wamo. Tanganyika inayolalamikiwa haina mwakilishi mahakamani, wala mahakama haitambui uwepo wake ingawa hukumu ni dhidi ya Tanganyika! all nonesense

Ndicho kilichopo sasa hivi na mwisho wa siku losers ni Watanganyika.

Kuna tatizo la waandishi wa habari wa Tanzania. Hakuna anayehoji maswali magumu na muhimu nadhani ni mapungufu ya kutojua au kujisomea . Mfano, sijasiki mtu akiuliza viongozi wa Zanzibar mambo haya
1. Mchango wa Zanzibar ni upi katika kuendesha Muungano
2. Kero za Tanganyika ni zipi zinazojadiliwa kwa upande wa Tanganyika
3. Formula la kugawana rasilimali za Tanganyika kwa jina la Tanzania zinazingatia nini
4. Ni wapi Bajeti ya SMZ inaonyesha wanalipa mikopo kupitia JMT na kwanini wasiruhusiwe kukop na kulipa wenyewe
5. Nani anasimamia masilahi ya Tanganyika ndani ya Muungano
6. Wazanzibar wanataka Muungano au la, na kama hawataki nini kinawazuia wakiwa na nyenzo na taasisi zote
7. Kwanini wasitumie taasisi zao, BLW au Wabunge kudai kura ya maoni kama Eritrea, Scotland, Timor, Quebec n.k
8. Wazanzibar wanadhani wapi wanadhulumiwa na Tanganyika, na Tanganyika inanufaika na nini katika muungano

Waandishi lazima wawe na uwezo wa kuuliza maswali si kukaa na kusikiliza hadithi kama wale wa ITV na ipad !
 
Yes! tuonyeshe bajeti ya ulinzi, mambo ya ndani, nje katika bajeti ya SMZ.
Onyesha mikopo wanayopewa kama sehemu yao wapi wanarudisha wenyewe kama si JMT
Makusanyo ya kodi ya SMZ ni bilioni 60 kwa mwezi sawa na chini ya bilioni , bajeti ya 2023/2024 ni 2.4T!
Unajua ni kiasi gani 4.5% sasa ni 9% ya Bajeti ya JMT inakwenda Zanzibar! Morogoro na Tabora wanapata kiasi gani
Tuonyeshe wapi mapato ya TRA yamevuka kutoka SMZ kuja hazina Dar
Tuonyeshe wale Wabunge 80% wanalipiwa na bajeti ipi ya SMZ?
Kwanini mfuko wa Mbunge wa uende Zanzibar wakati hawana mchango wowote katika katika JMT
Kwanini Mbunge anayechaguliwa na watu 3,000 awe na haki sawa na Mbunge anayechaguliwa na watu 400,000
Kwanini wao wawe na kipaumbele zaidi ya raia mlipa kodi wa Tanganyika.

Tuonyeshe na utushawishi kwamba Tanganyika inahitaji Muungano! hebu tushawishi ni kwa lipi au faida gani.
Punguza chuki na roho mbaya. Zanzibar ni sehemu ndogo sana kulinganisha na ukubwa wa Bara.
 
Tuonyeshe wapi katika katiba imeelezwa hiyo!
Kumbuka wao ndio wanataka formaula ya kugawana rasilimali za Tanganyika! kama ipo kikatiba ni wapi?

Hkusikia wanataka passport kuingia Zanzibar! huo si ubaguzi
Hukuwasikia Wazanzibar hawataki Utanzania kwasababu ni Wazanzibar, huo si ubaguzi

Unashindwa kuelewa kwamba Ubaguzi wa Wazanzibar ndio chanzo cha matatizo na sasa ubaguzi huo itakula kwao. Watu wanaitaka Tanganyika yao ili Zanzibar ipate mamlaka kamili

Tunahitaji Tanganyika tusimamie mambo yetu, hatuna muda wa kubembelezana kila siku!

Ikiwa wanataka Muungano watasema wao , Tanganyika haina cha kupoteza wala kunufaika!

Narudia tena tuonyeshe au tueleze, kwanini Tanganyika inahitaji Muungano! ni kwasababu au faida gani
Tanganyika kwa sababu ya hasira ya uzanzibari haitadumu huo ni wosia wa Mwalimu Nyerere. Tusijione eti tupo salama sana kuweza kuwa peke yetu.

Umoja ndio kila kitu kwa nchi hizi za kiafrika, huu usalama wa Tanganyika ni kwa sababu tupo ndani ya muungano nje yake kuna ubaguzi mwingine unaokwenda kuzaliwa baina yetu sisi kwa sisi.

Tupunguze hasira na akili za kukomoana, hata Baba na Mama wanaoishi miaka 70 pamoja haina maana siku zote kwao ni sherehe tu, tupunguze hizi jazba zina madhara kwetu sis wenyewe tunaojiona tuna kila haki.
 
Chuki dhidi ya urais wa Samia inasumbua baadhi yetu hakuna jema atakalolifanya likaonekana ni la maana kwa ustawi wa Tanzania. Hizi hoja za utanganyika zinakuzwa kwa sababu ya uzanzibari wa Samia sio zaidi ya hapo.

JPM hata angefanya makosa makubwa kiasi gani hakuna ambaye angesema chochote. Nyerere pia hakuna ambaye aliweza kusema chochote, SSH akifanya chochote japo ni kidogo kulinganisha na walivyofanya watangulizi wake zinaanza nongwa za kila aina!.

Walijaribu kupiga kelele kisa mkataba wa kibiashara na DP World na ukichunguza kwa umakini wahusika wanaohoji masuala ya muungano ndio wale wale waliopinga bandari zetu kuwa na uwekezaji utakaopanua wigo wa ufanisi.

Lakini misukosuko ndio sifa ya uhusiano wenye maisha yanayodumu.
 
Tanganyika kwa sababu ya hasira ya uzanzibari haitadumu huo ni wosia wa Mwalimu Nyerere. Tusijione eti tupo salama sana kuweza kuwa peke yetu.

Umoja ndio kila kitu kwa nchi hizi za kiafrika, huu usalama wa Tanganyika ni kwa sababu tupo ndani ya muungano nje yake kuna ubaguzi mwingine unaokwenda kuzaliwa baina yetu sisi kwa sisi.

Tupunguze hasira na akili za kukomoana, hata Baba na Mama wanaoishi miaka 70 pamoja haina maana siku zote kwao ni sherehe tu, tupunguze hizi jazba zina madhara kwetu sis wenyewe tunaojiona tuna kila haki.
Hapana! Ubaguzi wameanza wao! kwani si miaka yote wanasema Tanganyika imevaa koti la Muungano?
Husikii wakisema wao siyo Watanzania! Huwasikii wakidai Watanganyika waende kwao na passport

Akisema Mtanganyika ni tatizo, akisema Duni, Jussa na OMO ni halali! huu upuuzi umefika mwisho.
Tunawaambia wazi bila kumung'unya maneno, wao ndio wanauhitaji Muungano! shut up or put up

Hatuhitaji malumbano yasiyo na mwisho, Zanzibar inachukua rasilimali nyingi sana kuliko mkoa wowote na haichangi chochote. Tunahitaji kusonga mbele, hatuwezi kuishi kwa ku please watu milioni.
Tunachukua resources Simiyu, Geita na Njombe mikoa michanga kabisa kupeleka kwa nchi ya karne tano!


Umesahau ni wamoja kwasbabu ya adui Tanganyika. In fact wanataka mamlaka kamili hawataki muungano.

Hatuwezi kuishi kwa fikra tu kama unavyosema! jibu hoja moja baada ya nyingine
Nimekuuliza Tanganyika ina nini cha kupoteza ikiwa watapewa mamlaka kamili!
Nimekuuliza mchango wa Zanzibar kwa Tanganyika ni upi
Kwanini wanapewa hadhi ya raia daraja la kwanza wakati wakichangia sifuri katika Muungano
 
walidai wanaeneo lao mkuranga TANGANYIKA
Uliziba maskio hukuona hatari bandari kupewa mwarabu kwa mkataba wa kimangungo
Inakuwa vipi mwanaume kuwa chawa wa mwanamke tena si waAsili yake mwenye kujitapa waarabu ni wajomba zake
wanaume kama mabinti malaya
 
chuki zipo wapi? Jibu hoja
Huna hoja mkuu Zanzibar ina ukubwa wa wilaya mbili za huku bara, hicho kinachopelekwa huko kimeanza kwenda jana au juzi?.

Unapalilia chuki na madhara yake yanaweza kabisa kuja kuwa sumu kama sio leo basi hata muongo mmoja ujao.
 
Hapana! Ubaguzi wameanza wao! kwani si miaka yote wanasema Tanganyika imevaa koti la Muungano?
Husikii wakisema wao siyo Watanzania! Huwasikii wakidai Watanganyika waende kwao na passport

Akisema Mtanganyika ni tatizo, akisema Duni, Jussa na OMO ni halali! huu upuuzi umefika mwisho.
Tunawaambia wazi bila kumung'unya maneno, wao ndio wanauhitaji Muungano! shut up or put up

Hatuhitaji malumbano yasiyo na mwisho, Zanzibar inachukua rasilimali nyingi sana kuliko mkoa wowote na haichangi chochote. Tunahitaji kusonga mbele, hatuwezi kuishi kwa ku please watu milioni.
Tunachukua resources Simiyu, Geita na Njombe mikoa michanga kabisa kupeleka kwa nchi ya karne tano!


Umesahau ni wamoja kwasbabu ya adui Tanganyika. In fact wanataka mamlaka kamili hawataki muungano.

Hatuwezi kuishi kwa fikra tu kama unavyosema! jibu hoja moja baada ya nyingine
Nimekuuliza Tanganyika ina nini cha kupoteza ikiwa watapewa mamlaka kamili!
Nimekuuliza mchango wa Zanzibar kwa Tanganyika ni upi
Kwanini wanapewa hadhi ya raia daraja la kwanza wakati wakichangia sifuri katika Muungano
Hekima, umoja na amani na hizi ni ngao zetu Afrika na watu wake - maneno ya wimbo wa Taifa walioyatunga wana akili na waliona watu wenye fikra kama za kwako.

Huwezi kila kitu ukakipima kwa mali au kwa mchango wa kiuchumi, mara nyingi data hizo ni taarifa tu za kujengea hoja kwenye vikao au mikutano kiuhalisia hazina nguvu kuliko utashi wa wanaoungana,

Hizi chuki dhidi ya Muungano na wazenji zinazaliwa siku zote wakati Rais akiwa ni wa huko kizimkazi akiwa wa huku Chato na mkatoliki mwenzetu hayupo hata mmoja mwenye kuidai Tanganyika. Msingi wa kuzaliwa kwa Tanganyika ni roho ya kisasi dhidi ya Uzenji, huo utanganyika pia hauwezi kuwa na maisha marefu.
 
Naelewa nguvu inayokuwa nyuma za hoja ya utanganyika kwamba ni kutaka kulipa kisasi kwa yanayosemwa na hao wa upande wa pili. Sioni uhai wa Tanganyika ikisimama yenyewe na ikadumu.
Hakiuna kulipa kisasi, Tanganyika ni dude kubwa sana haliwezi kulingana na Zanzibat. Kinachotokea sasa hivi ni kuchoshwa na kelele na madai ya kipuuzi ya Wazanzibar. Mfano, wameondoa Uhamiaji katika mambo ya Muungano, unaelewa hilo? Zanzibar wanapokuwa juu ya katiba ya JMT na kuwa raia wa daraja la I kwa upendeleo wakati hawana mchango wowote kwa maendeleo ya Tanganyika inakera! Tunahitaji muda wa kufikiri mambo muhimu si kaeneo ka watu laki 5 milioni 1 wakiishi Tanganyika.
JPM alishambuliwa kwa zkuendekeza ukanda na wasukuma wakabaguliwa humu JF kisa hulka binafsi za JPM huo ni ushahidi wa sisi watanganyika kuja kugeukana huko mbele ya safari, hatuna kibali cha kutenda dhambi ya ubaguzi sisi kwa sisi na kisha tukasalimika.
Yes tulimpinga kwasababu alifanya hayo na mfano mmoja ni Uwanja wa Chato ambao ni hasara.
Tulimpinga kwa kauli zake za kipuuzi kuhusu watu wa kanda fulani ''watusubiri'
Watu wote waliompinga ni wale wanaotaka umoja. Na hata Kikwete Tulimpinga kwa kuendekeza ufisadi.
Mkapa tulimpinga kwa kupallilia ufisadi. Mwinyi tulimpinga kwa sera zake hasa za uchumi.
Nyerere tunamsema kila siku na mimi ni mmoja wao hasa kuua vyama ya ushirika na ujamaa
Samia atapingwa without exception!
Tutaanza kuwanyooshea vidole wahaya kisa wamesoma na kujiendeleza. Tutaanza kuwanyooshea kidole wachagga tukiwaita watafutaji wa utajiri waliopitiliza, tutaanza kujenga hoja za kuvunja huu umoja wetu tunaodhani tunao eti kwa sababu ya kupambana na hulka mbovu za wazenji.
Kwahiyo unadhani kama hayo yapo Wanaozuia ni Wazanzibar!
Mstaarabu huvumilia na hutafuta namna za kumaliza kero zinazosumbua uhusiano wake na jirani yake wa karibu. Hakuna kisichoweza kutatulika kwa maongezi.
Hapana tumewavumilia na sasa ni kero kwetu, tunahitaji muda wa kufikiri namna ya kushirikiana na nchi zinazotuzunguka zenye population ya 100M. Kila siku wao wanataka hawana cha kuwajibika! hapana

Nimekuuliza, tushawishi hapa jamvini kwanini Tanganyika inahitaji Muungano kiasi cha kutoa rasilimali nyingi kiasi hicho. OMO kasema 54% ya bajeti ya Zanzibar inategemea pesa za Tanganyika, na bado wanataka kupewa zaidi.
 
Huwezi kila kitu ukakipima kwa mali au kwa mchango wa kiuchumi, mara nyingi data hizo ni taarifa tu za kujengea hoja kwenye vikao au mikutano kiuhalisia hazina nguvu kuliko utashi wa wanaoungana,
Yes tunaungana kwasababu za Uchumi1 matatizo mengi duniani yanatokea kwasababu za uchumi.
Ni uchumi tu! Tunahitaji mshiriki wa Muungano. Zanzibar wanadai hadi inakera! Sasa hivi wanataka eti kuwe na formula ya kugawana rasilima za Tanganyika. Wao kila siku ni kugawana hutawasikia wakishiriki kuchangia au kujenga.
Hizi chuki dhidi ya Muungano na wazenji zinazaliwa siku zote wakati Rais akiwa ni wa huko kizimkazi akiwa wa huku Chato na mkatoliki mwenzetu hayupo hata mmoja mwenye kuidai Tanganyika. Msingi wa kuzaliwa kwa Tanganyika ni roho ya kisasi dhidi ya Uzenji, huo utanganyika pia hauwezi kuwa na maisha marefu.
Hakuna chuki ni hisia zako. Maalim Seif alidai mamlaka kamili miaka zaidi ya 20, mbona hujasema ni chuki
Jussa , OMO na Duni kila siku wanatukana Muungano mbona hujaona ni chuki
Sasa hivi wanataka twende Zanzibar kwa passpor, hujaona ni chuki
Wanasema wao si Watanzania huoni kama ni chuki
Wazanzibar wanamtukana Mwl Nyerere wakisema ''Laanatullah' kila siku huoni ni chuki
Hawataki hata ndizi ivuke bahari lakini mkono wa tembo kutoka Mombasa ni sawa, huoni ni chuki
Wana vitambulisho vya kuwabagua Watanganyika, huoni kama ni chuki

Kwa taarifa yako waliorudisha neno Tanganyika wakisema '' Watanganyika wamelala' ni Wakoloni weusi , wanaiba rasilimali (wanaiba zero) ni Wazanzibar!

Kwanini Mtanganyika akisema yaishe mnasema ni chuki! Yaani yote hapo juu hukuwahi kuyasikia.
Hapana, wapewe mamlaka kamili sisi tunahitaji Tanganyika. Ikiwa watataka muungano ni wao waje waombe, Tanganyika haina cha kupoteza
 
Back
Top Bottom