Umesema hayo mambo mengine ni ufahari wa kidunia tu ila kwako muhimu ni Tanzania kuwa na kiti umoja wa mataifa ndiyo nimekuuliza huko umoja wa mataifa ni mbinguni siyo duniani? Hata hivyo nisikutwishe mzigo usiyohumudu maana inawezekana tunajadili vitu viwili tofauti.Ndio kielelezo cha utaifa wa Tanzania kinapotambulika kimataifa. Kwani Tanganyika na Zanzibar zipo mbinguni?.
Neno!Unajua ndugu Pascal Mayalla mzee kama wewe ikifikia mahali mtu akakuita "mjinga" na Kitambakwiri" labda itakuwa ni kukukosea heshima na adabu...
Lakini inakuwaje kama wewe mwenyewe umejipa hiyo sifa ya UJINGA na UPUMBAVU?
Bila shaka atakeyeitikia na kukufukuzia kwa tabia yako hiyo hatakuwa amekuvunjia heshima yoyote..
Mpaka hatua hii, bila shaka yoyote ni kuwa WEWE Pascal Mayalla ndiye hasa uliye MJINGA na KITIMBAKWIRI unayestahili kuelimishwa na kufundishwa kusikiliza na kuelewa mawazo ya watu wengine..
Na pia muungano huo uwe na faida kwa pande zote. Mfano, Tanzania inapokuwa na MoU na mataifa kama Marekani, UK, Ufaransa , China n.k. utajiuliza ni kwa vipi? Uchumi wa Miji ya Beijing, New York , California n.k. ni mkubwa kuliko wa Tanzania! swali ni kwanini wanatuhitaji? Jibu ni rahisi kuna kitu kinaitwa ''mutual benefit'.Tunautaka muungano. Tunataka ushirikiano na watu au nchi zingine. Lakini muungano huo ni lazima uwe wenye usawa na kuheshimiana kwa pande zote zilizokubali kuunga/kushirikiana..
Makosa ni kudhani kwamba wataweza kuendelea na ulaghai huo daima milele.KWA HIYO: Sio UJINGA wala u - TIMBAKWIRI watu kuzisema kasoro hizi kwa malengo ya kurekebisha. Ujinga na u - timbakwiri ni kule kung'ang'ania kuishi ktk makosa au kasoro. Na huyo mtu ni wewe na wenzako wote huko CCM...
' The train has just left the train'' fursa ilikuwa kupitia Tume ya Warioba, wakaihujumu.Swali ni moja tu: Mataweza kuwafanya Watanganyika kuishi ktk ujinga wenu hadi lini?
Hilo halikubaliki na ni LAZIMA TUCHUKUE HATUA KUREKEBISHA..
Mkuu nakuelewa sanaMkuu Nguruvi3, unapoteza muda. Kwa bahati mbaya watu aina ya Pascal Mayalla wamejaaliwa kuwa na akili kubwa lakini zisizo za kawaida. Mtu kama huyu akiwa mwizi na akabahatika kuishi ndani ya taifa hili la wajinga ataiba hadi avimbiwe hadi kupasuka!
Wizi kama huu hujulikana kama wizi usio na staha. Yaani mtu anaanza kwa kuiba vya nje na ikiisha anaanza kufanya kufuru. Atawaibia ndugu zake, atawaibia wazazi wake, atamwibia mkewe, atawaibia watoto wake na mwisho ataanza kujiibia yeye mwenyewe.
Naam ndivyo walivyo na mimi binafsi nasita sana kuwa na mnakasha na watu wanaojiita wenye akili hizo huku wakitetea mambo ya kipuuzi na ya kijinga. Hizo si akili ni ugonjwa unaosababishwa na vitu vingi lakini viwili vikubwa ni tamaa na ulafi...tamaa na ulafi ni kama pete na kidole!
Lakini inapewa mapato kuliko Morogoro au Tabora! mapato yanayotoka Morogoro na Tabora.Zanzibar ni ndogo sana kiasi cha kuzisumbua akili za watu wengi wa bara wakaacha kutafuta mkate wao wa kila siku na kuanza kuiwazia. Ni sawa na wilaya mbili tu za mkoa wa Morogoro au Tabora.
Inapewa mapato? haina vyanzo vyake vya mapato unataka kusema?. Tunajaribu kushusha thamani Zanzibar kwa maarifa yetu ambayo upatikanaji wake una walakini.Lakini inapewa mapato kuliko Morogoro au Tabora! mapato yanayotoka Morogoro na Tabora.
Hulioni tatizo hapo?
Lini Wananchi wa Morogoro na Tabora waliwahi kulipiwa umeme na JMT? Zanzibar wanalipiwa. Huoni tatizo?
Nafasi za ajira za Morogoro na Tabora zipo wapi? Zanzibar wanazo!
Nafasi za elimu ya juu na mikopo za Tabora na Morogoro ziko wapi? Zanzibar wanazo! huoni tatizo?
Unaweza ku ignore ukatafute mkate lakini bei ya mkate huo ni pamoja na bill ya umeme ya watu waliopunzika ufkweni Zanzibar! Ni pamoja na mishahara ya Wazanzibar wanaolala pale Mjengoni wakisema si Watanzania. Kwahiyo katafute mkate na maji ili ujaze ndoo inayovuja
Kupewa mapato ni makubaliano ya kikatiba yaliyoandikwa miaka mingi iliyopita. Nafasi za ajira za bara zipo nenda kwenye raasisi za kiserikali zinazotoa ajira watakupa mgawanyo wa kila eneo la Tanzania.Lakini inapewa mapato kuliko Morogoro au Tabora! mapato yanayotoka Morogoro na Tabora.
Hulioni tatizo hapo?
Lini Wananchi wa Morogoro na Tabora waliwahi kulipiwa umeme na JMT? Zanzibar wanalipiwa. Huoni tatizo?
Nafasi za ajira za Morogoro na Tabora zipo wapi? Zanzibar wanazo!
Nafasi za elimu ya juu na mikopo za Tabora na Morogoro ziko wapi? Zanzibar wanazo! huoni tatizo?
Unaweza ku ignore ukatafute mkate lakini bei ya mkate huo ni pamoja na bill ya umeme ya watu waliopunzika ufkweni Zanzibar! Ni pamoja na mishahara ya Wazanzibar wanaolala pale Mjengoni wakisema si Watanzania. Kwahiyo katafute mkate na maji ili ujaze ndoo inayovuja
Yes! tuonyeshe bajeti ya ulinzi, mambo ya ndani, nje katika bajeti ya SMZ.Inapewa mapato? haina vyanzo vyake vya mapato unataka kusema?. Tunajaribu kushusha thamani Zanzibar kwa maarifa yetu ambayo upatikanaji wake una walakini.
Tuonyeshe na utushawishi kwamba Tanganyika inahitaji Muungano! hebu tushawishi ni kwa lipi au faida gani.Muungano una faida zake za pande mbili tatizo unapofikiria kuhusu hasara ukitumia nguvu nyingi unapoteza uwezo wa kuuona upande wa faida.
Tuonyeshe wapi katika katiba imeelezwa hiyo!Kupewa mapato ni makubaliano ya kikatiba yaliyoandikwa miaka mingi iliyopita.
Hkusikia wanataka passport kuingia Zanzibar! huo si ubaguziNi hulka zile zile za uchoyo, ubaguzi na umaskini pia.
Karibu "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikilizaNarudia tena tuonyeshe au tueleze, kwanini Tanganyika inahitaji Muungano! ni kwasababu au faida gani
Natumaini umeelimikaKwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.
Anasema Zanzibar inafaidika sana na muungano, kisiasa, kiuchumi na kijamii, ikiwemo kufaidika kielimu, wakati wa muungano, Zanzibar haikuwa na chuo kikuu chake hivyo Wanzanzibari wote wa enzi hizo waliofika elimu ya vyuo vikuu, wamesomea bara.
Mama Samia amesema watu waachiwe kuujadili muungano kadri watakavyo na hata kutema nyongo kuhusu muungano, na serikali inazitumia hizo hoja zinazolalamikiwa kuimarisha muungano, akasema ni heri watu wafunguke na kusema hivyo kuyatoa madukuduku yao, kuliko kunyamaza na madukuduka ndani yao, siku wakilipuka moto utawaka, hivyo watu waachwe waseme.
Amesema Zanzibar ni visiwa hivyo viko wazi pande zote, hivyo faida kubwa kabisa ya muungano ni ulinzi usalamax amani na na utulivu wa Zanzibar, bila muungano, ilikuwa ni rahisi sana kuivamia Zanzibar na Zanzibar ikivamiwa ni rahisi sana kuivamia bara, hivyo muungano umeimarisha sana ulinzi na usalama, amani na utulivu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kuna kitu Mama Samia amekisema sikuwahi kukijua!. Kumbe Wizara ya Mambo ya Nje ilipokiwa ikiitwa Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa ndio ilikuwa ya Muungano iki handle issues zote za Zanzibar kimataifa, lakini , ilipobadilishwa jina na kuitwa Wizara ya Mambo, ya Nje na Ushirikiano wa Africa Mashariki, sasa ina handle mambo ya Zanzibar ndani ya Africa Mashariki tuu, lakini kimataifa, kwa yale mambo ambayo sio ya muungano, SMZ ya Zanzibar imepewa uhuru wa kunegotiate ufadhili, misaada, na mikopo na mikataba ya kimataifa kwaniaba ya Zanzibar, ila kwenye kutiliana saini, anayetia saini ni serikali ya JMT, kwasababu Zanzibar haina sovereignty, sovereignty ni moja tuu ambayo iko kwenye JMT pekee!.
Hili sikuwahi kulijua, hivyo kumbe sasa Zanzibar inaweza kupata misaada na mikopo ya kimataifa, sasa kwavile uwiano wa kugawana misaada ya kutoka nchi wafadhili na wahisani, Zanzibar inastahili kupata asilimia 4.5% ya misaada yote kwa Tanzania, sasa kwa vile Zanzibar nayo inaweza kuomba ufadhili wa kimataifa, jee hii misaada ya kimataifa ya Zanzibar inayoomba, Tanzania bara pia tunapewa ule mgao wa asilimia 95.5% ya misaada ya Zanzibar, au misaada ya Tanzania tuu, ndio Zanzibar inapaswa kugaiwa asilimia 4.5%, lakini kwa misaada ya Zanzibar, then misaada hiyo ni ya Zanzibar pekee?.
Mama Samia amezungumzia kero za muungano na kusema kero nyingi zimeisha tatuliwa ila utekelezaji ndio unasua sua, na kutolea mfano deni lililokuwa la umeme la Tanesco, deni hilo lilisababishwa na double taxation, kwa Tanesco kuwachaji SMZ VAT huku shirika la umeme la Zanzibar, Zesco nalo likiwachaji kodi ya ongezeko la thamani Vat, wateja watumiaji wa umeme zao nao wakilipishwa Vat, kero hiyo imetatuliwa kwa Tenesco hawaichaji tena Vat kwa SMZ, hivyo Zanzibar haidaiwi tena deni lolote la umeme na Tanesco.
Ninachokumbuka kwenye deni la umeme la Zanzibar, lilitokana na Tenesco kuuza umeme kwa bei ya juu kwa Zesco, halafu Zesco wanauza umeme huo kwa bei ya chini Zanzibar, kumbe ilikuwa ni issue ya VAT!.
Pia amezungumzia kero za muungano kadri zinavyotatuliwa, kero nyingine zinaibuka, hivyo issue za kero za muungano ni issue endelevu.
Amezungumza mengi na kumalizia kwa kusisitiza Muungano ni jambo jema, tuulinde na kuuenzi.
Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?. Hili mnalionaje?.
Paskali
Punguza chuki na roho mbaya. Zanzibar ni sehemu ndogo sana kulinganisha na ukubwa wa Bara.Yes! tuonyeshe bajeti ya ulinzi, mambo ya ndani, nje katika bajeti ya SMZ.
Onyesha mikopo wanayopewa kama sehemu yao wapi wanarudisha wenyewe kama si JMT
Makusanyo ya kodi ya SMZ ni bilioni 60 kwa mwezi sawa na chini ya bilioni , bajeti ya 2023/2024 ni 2.4T!
Unajua ni kiasi gani 4.5% sasa ni 9% ya Bajeti ya JMT inakwenda Zanzibar! Morogoro na Tabora wanapata kiasi gani
Tuonyeshe wapi mapato ya TRA yamevuka kutoka SMZ kuja hazina Dar
Tuonyeshe wale Wabunge 80% wanalipiwa na bajeti ipi ya SMZ?
Kwanini mfuko wa Mbunge wa uende Zanzibar wakati hawana mchango wowote katika katika JMT
Kwanini Mbunge anayechaguliwa na watu 3,000 awe na haki sawa na Mbunge anayechaguliwa na watu 400,000
Kwanini wao wawe na kipaumbele zaidi ya raia mlipa kodi wa Tanganyika.
Tuonyeshe na utushawishi kwamba Tanganyika inahitaji Muungano! hebu tushawishi ni kwa lipi au faida gani.
Tanganyika kwa sababu ya hasira ya uzanzibari haitadumu huo ni wosia wa Mwalimu Nyerere. Tusijione eti tupo salama sana kuweza kuwa peke yetu.Tuonyeshe wapi katika katiba imeelezwa hiyo!
Kumbuka wao ndio wanataka formaula ya kugawana rasilimali za Tanganyika! kama ipo kikatiba ni wapi?
Hkusikia wanataka passport kuingia Zanzibar! huo si ubaguzi
Hukuwasikia Wazanzibar hawataki Utanzania kwasababu ni Wazanzibar, huo si ubaguzi
Unashindwa kuelewa kwamba Ubaguzi wa Wazanzibar ndio chanzo cha matatizo na sasa ubaguzi huo itakula kwao. Watu wanaitaka Tanganyika yao ili Zanzibar ipate mamlaka kamili
Tunahitaji Tanganyika tusimamie mambo yetu, hatuna muda wa kubembelezana kila siku!
Ikiwa wanataka Muungano watasema wao , Tanganyika haina cha kupoteza wala kunufaika!
Narudia tena tuonyeshe au tueleze, kwanini Tanganyika inahitaji Muungano! ni kwasababu au faida gani
chuki zipo wapi? Jibu hojaPunguza chuki na roho mbaya. Zanzibar ni sehemu ndogo sana kulinganisha na ukubwa wa Bara.
Hapana! Ubaguzi wameanza wao! kwani si miaka yote wanasema Tanganyika imevaa koti la Muungano?Tanganyika kwa sababu ya hasira ya uzanzibari haitadumu huo ni wosia wa Mwalimu Nyerere. Tusijione eti tupo salama sana kuweza kuwa peke yetu.
Umoja ndio kila kitu kwa nchi hizi za kiafrika, huu usalama wa Tanganyika ni kwa sababu tupo ndani ya muungano nje yake kuna ubaguzi mwingine unaokwenda kuzaliwa baina yetu sisi kwa sisi.
Tupunguze hasira na akili za kukomoana, hata Baba na Mama wanaoishi miaka 70 pamoja haina maana siku zote kwao ni sherehe tu, tupunguze hizi jazba zina madhara kwetu sis wenyewe tunaojiona tuna kila haki.
Huna hoja mkuu Zanzibar ina ukubwa wa wilaya mbili za huku bara, hicho kinachopelekwa huko kimeanza kwenda jana au juzi?.chuki zipo wapi? Jibu hoja
Hekima, umoja na amani na hizi ni ngao zetu Afrika na watu wake - maneno ya wimbo wa Taifa walioyatunga wana akili na waliona watu wenye fikra kama za kwako.Hapana! Ubaguzi wameanza wao! kwani si miaka yote wanasema Tanganyika imevaa koti la Muungano?
Husikii wakisema wao siyo Watanzania! Huwasikii wakidai Watanganyika waende kwao na passport
Akisema Mtanganyika ni tatizo, akisema Duni, Jussa na OMO ni halali! huu upuuzi umefika mwisho.
Tunawaambia wazi bila kumung'unya maneno, wao ndio wanauhitaji Muungano! shut up or put up
Hatuhitaji malumbano yasiyo na mwisho, Zanzibar inachukua rasilimali nyingi sana kuliko mkoa wowote na haichangi chochote. Tunahitaji kusonga mbele, hatuwezi kuishi kwa ku please watu milioni.
Tunachukua resources Simiyu, Geita na Njombe mikoa michanga kabisa kupeleka kwa nchi ya karne tano!
Umesahau ni wamoja kwasbabu ya adui Tanganyika. In fact wanataka mamlaka kamili hawataki muungano.
Hatuwezi kuishi kwa fikra tu kama unavyosema! jibu hoja moja baada ya nyingine
Nimekuuliza Tanganyika ina nini cha kupoteza ikiwa watapewa mamlaka kamili!
Nimekuuliza mchango wa Zanzibar kwa Tanganyika ni upi
Kwanini wanapewa hadhi ya raia daraja la kwanza wakati wakichangia sifuri katika Muungano
Hakiuna kulipa kisasi, Tanganyika ni dude kubwa sana haliwezi kulingana na Zanzibat. Kinachotokea sasa hivi ni kuchoshwa na kelele na madai ya kipuuzi ya Wazanzibar. Mfano, wameondoa Uhamiaji katika mambo ya Muungano, unaelewa hilo? Zanzibar wanapokuwa juu ya katiba ya JMT na kuwa raia wa daraja la I kwa upendeleo wakati hawana mchango wowote kwa maendeleo ya Tanganyika inakera! Tunahitaji muda wa kufikiri mambo muhimu si kaeneo ka watu laki 5 milioni 1 wakiishi Tanganyika.Naelewa nguvu inayokuwa nyuma za hoja ya utanganyika kwamba ni kutaka kulipa kisasi kwa yanayosemwa na hao wa upande wa pili. Sioni uhai wa Tanganyika ikisimama yenyewe na ikadumu.
Yes tulimpinga kwasababu alifanya hayo na mfano mmoja ni Uwanja wa Chato ambao ni hasara.JPM alishambuliwa kwa zkuendekeza ukanda na wasukuma wakabaguliwa humu JF kisa hulka binafsi za JPM huo ni ushahidi wa sisi watanganyika kuja kugeukana huko mbele ya safari, hatuna kibali cha kutenda dhambi ya ubaguzi sisi kwa sisi na kisha tukasalimika.
Kwahiyo unadhani kama hayo yapo Wanaozuia ni Wazanzibar!Tutaanza kuwanyooshea vidole wahaya kisa wamesoma na kujiendeleza. Tutaanza kuwanyooshea kidole wachagga tukiwaita watafutaji wa utajiri waliopitiliza, tutaanza kujenga hoja za kuvunja huu umoja wetu tunaodhani tunao eti kwa sababu ya kupambana na hulka mbovu za wazenji.
Hapana tumewavumilia na sasa ni kero kwetu, tunahitaji muda wa kufikiri namna ya kushirikiana na nchi zinazotuzunguka zenye population ya 100M. Kila siku wao wanataka hawana cha kuwajibika! hapanaMstaarabu huvumilia na hutafuta namna za kumaliza kero zinazosumbua uhusiano wake na jirani yake wa karibu. Hakuna kisichoweza kutatulika kwa maongezi.
Yes tunaungana kwasababu za Uchumi1 matatizo mengi duniani yanatokea kwasababu za uchumi.Huwezi kila kitu ukakipima kwa mali au kwa mchango wa kiuchumi, mara nyingi data hizo ni taarifa tu za kujengea hoja kwenye vikao au mikutano kiuhalisia hazina nguvu kuliko utashi wa wanaoungana,
Hakuna chuki ni hisia zako. Maalim Seif alidai mamlaka kamili miaka zaidi ya 20, mbona hujasema ni chukiHizi chuki dhidi ya Muungano na wazenji zinazaliwa siku zote wakati Rais akiwa ni wa huko kizimkazi akiwa wa huku Chato na mkatoliki mwenzetu hayupo hata mmoja mwenye kuidai Tanganyika. Msingi wa kuzaliwa kwa Tanganyika ni roho ya kisasi dhidi ya Uzenji, huo utanganyika pia hauwezi kuwa na maisha marefu.