Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Nani anasema kuna kuvunja Muungano? Wanaosema ni WazanzibarMpango mzima ni kuungana, kwanini Tanzania tufikirie kuungana na Sudan Kusini walio kilomita zaidi ya 3000 halafu tufikirie wakati huo huo kutengana na Zanzibar?. Ni somo lenye kuhitaji hekima nyingi sana kuliko jazba na visasi.
Tueleze ni kwa namna gani Zanzibar inaweza kuwa na mamlaka kamili bila kuvunja Muungano
Hata elimu ya mtaani tu inatuambia kwamba unapokuwa na ushirika na mtu au watu wengine lazima utoe sehemu.
Tanganyika imebeba Muungano na kuibeba Zanzibar kwa miaka zaidi ya 60. Kinachoonekana ni Zanzibar kudhani ni sehemu ''special' ya Muungano na wana umuhimu sana. Well, kila kitu wanataka kiwe na ' Uzanzibar'
Kwa sehemu kubwa inatuathiri ndio maana tunasema turudi katika makubaliano ya Muungano kwa kuanza na Tanganyika. Hili litawasaidia Wazanzibar kupata mamlaka (sehemu) na itawapunguzia gharama Watanganyika.
Kwa mfano, Wazanzibar wanalalamika kuongezwa mambo ya Muungano na kwamba ni kuwaonea.
Hoja yao ni nzuri sana, solution ni moja kuondoa mambo yote yaliyoongezwa kutoka 11 hadi 22 wanayodhani Tanganyika inanufaika nayo
Mfano
Tuondoe Elimu ya Juu
Tuondoe hali ya hewa
Leseni za viwanda
Taasisi kama mawasiliano
Kwa mifano hiyo mitatu, nieleze Tanganyika inanufaika na nini kwa hali ya hewa kuwa jambo la muungano! unaweza kuona ni kelele tu kwa kukosa elimu. By the way wote wanaolalamika elimu ya juu kuwa muungano wamesoma Tanganyika katika vyuo vya Tanganyika tena BURE.
Kuondoa mambo ya muungano hakuna athari yoyote kwa Tanganyika kwasababu hakuna kitu pale!
Tunachohitaji mambo hayo yaondolewe kwa staha na heshima na si ujanja na ulaghai
Kwa mujibu wa Makamu wa Rais OMO, Uhamiaji wameondoa katika Muungano! guess what Wafanyakazi wa Uhamiaji na majengo yaliyojengwa miaka 2 tu yanatoka Hazina Dar es Salaam.
Lakini si hayo tu, tunahitaji kuona Wazanzibar wanachangia Muungano kama ilivyo Mikoa michanga ya Geita, Simiyu, Njombe. Hatuwezi kuwa na ushirika wakati Zanzibar wanadai tuu hatuwaoni katika huduma za Muungano!