Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Ni sawa, ila:

1. Ushawishi huna.
2. Platform huna.
3. Chama wala mfuasi huna.
4. Cheo huna.
5. Hata ccm wanakuona useless.
 
Hakuna hata mtu ana muda wa kusoma hilo gazeti lako. Ni hivi, hakuna uwezekano wa kutetea muungano huu kwa hoja. Hapa unapoteza muda wako bure. Tumechoka na muungano wenye kero zisizotatulika.
Jambo la kushangaza ni gazeti na Wahariri kutokuwa na muda wa 'fact check''
Hivi unakuwaje na Federation ya Tanzania na Zanzibar?

Yaani ni kama kusema kuna federation ya USA na California! na wamechapa kwenye gazeti!

Halafu anasema baada ya Muungano majina yalibadilishwa. Hana ushahidi ni lini au kwa sheria gani iliyobadili majina hayo.

For the sake of disussion tukubaki tu kwamba kulikuwa na Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.
Halafu anaendelea kusema Zanzibar ikaendelea kuwepo kwasababu za ''uadhimu na uadimu wa mUUngano''

Ukishasikia maneno hayo ujue hapo ni hoja muflisi, yaani hana namna ya ku defend

Alichokusudia ni kusema Zanzibar ipo, Tanganyika ilikufa lakini hawezi kusema hivyo kwsababu atajifunga.

Alichokifanya ni ku 'insinuate' Bara na Viswiani halafu akairudisha Zanzibar ili mbele ya safari atengeneze Federation yake ya Tanzania na Zanzibar. Hii ndio elimu ya Uraia tunayoambiwa itolewe! nope hakuna elimu hapa watu wanatafuta vipindi tu maisha yaendelee

Lakini mhariri wa gazeti anasikitisha, anawezaje kuacha ubabaishaji! utamalaki
 
Hapa ulisahau kwamba kuna aya uliyosema ''siku za karibuni kumekuwa na ubaguzi''
Ubaguzi wa Wazanzibar ni wa siku nyingi sana kinachotokea sasa hivi ni Watanganyika wamechoshwa

Watanganyika wamechoka kukaa kimyaa wakiwa na zigo la Muungano na kamzigo ka SMZ mgongoni na mkononi.
Swali wanalojiuliza ni kwamba ni kwa 'return gani' . Wanajua hawana cha kupoteza na wala hawana sababu za kuwazuia Wazanzibar kuvunja muungano! Akunyimae kunde kakupunguzia mashuzi
 
Hadi hapa sioni sababu ya kuendelea kusoma Hii hekaya yako. Inawezakana vipi mkubaliane "kufuta" majina ya zamani LAKINI mwingine aendelee na jina lake kwasababu eti kwa sababu ya "uadimu" na "uadhimu" wake? Hauko serious kabisa Ndugu. Kuna hoja za msingi kabisa, zinapaswa kuwa addressed na Sio hili andiko lako.
 
Hakuna hata mtu ana muda wa kusoma hilo gazeti lako. Ni hivi, hakuna uwezekano wa kutetea muungano huu kwa hoja. Hapa unapoteza muda wako bure. Tumechoka na muungano wenye kero zisizotatulika.
Aliandika akiwa amelewa
 
1. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.
Hiki ndicho nilikieleza, kwamba, Pascal alisema majina yalikufa na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.
Hakuishia hapo kwa njia za ubabaishaji akarudisha Zanzibar na siyo tena Tanzania Visiwani.

Hapo juu anasema Tanganyika nafasi yake imechukuliwa na '' Nchi mpya ya Tanzania Bara''
Hata katika ububusa tukubaliane kwamba kuna nchi ya Tanzania Bara.
Asichoeleza pascal ni kwamba serikali ya hiyo nchi ya Tanzania Bara ipo wapi?

Kama Tanzania Visiwani iimebaki kuwa Zanzibar, Tanganyika imebadilika kuwa Tanzania Bara, wapi ilipo serikali ya Tanzania Bara? Tunasema hivi kwasababu kukiwa na serikali ya Tanzania Bara na kisha Zanzibar lazima uwe na Serikali ya pamoja ya Tanzania. Na tukikubaliana na pascal kwa kujifanya hatuna akili, Federation itakuwa kati ya Tanzania Bara na Zanzibar siyo Tanzania na Zanzibar

Ukiangalia mkanganyiko huo halafu ukaambiwa ndio elimu ya Uraia, naomba nisihudhurie au kusoma hata kipande cha elimu hiyo. Hiyo siyo elimu ni ubabaishaji na upotoshaji wa kutumia ''mass' kupata vipindi vya TV.

Hapana! stop exploitation , watu wetu wanahitaji tuwasiaidie si kuwapotosha.
 
Nafikiri mada yako ingejikita kwanini wanasiasa wanatumia hoja ya utanganyika na Zanzibar.
Kasome bandiko #6, ameandika si kwa minajili ya kuamsha fikra au majadiliano. Ni wazi kuna 'kazi' anafanya hasa pale anaposema '' tunawamudu na tutawanyoorosha'' Ni kwasababu hiyo article yake yote imejaa 'fallacy and misleading information'' ili kutimiza azma ya kunyooorosha, si kwa mtazamo wa uwakili au uandishi!
Hoja kuu aliyotumia mwalimu Nyerere kuzima hoja ya G55 mwaka 95 ni kwa sababu wale walikuwa wabunge wa ccm, na sera ya CCM ilikuwa serikali mbili hivyo hoja yao ilikuwa batili kwani ilitakiwa ianzie ndani ya chama.
Nyerere hakukataa Serikali 3, alikataa utaratibu uliotumika bila kupitia chama kwa wakati ule
Kwanini watanganyika wanadai serikali yao?
Sababu kuu ni uvunjanji wa katiba unaofanywa na viongozi wakati CCM ambayo inaunda serikali imejaa kimya.
Hili lilianza na OIC ya Marehemu Mwinyi, kukawa na mambo ya ajabu ajabu kama yanayoendelea kuhusu kuchota rasilimali za Tanganyika, kukiuka katiba n.k. G55 wakasema tunahitaji Tanganyika
Hivi rais wa Zanzibar anapata wapi mamlaka ya kugawa uraia.
Halafu Pascal anasema hii ni nchi moja na Uraia ni wa nchi moja. Ni wapi kikatiba Rais wa SMZ ana uwezo wa kugawa Uraia. Lakini si hilo tu, Rais wa Zanzibar kuna wakati anakuwa '' Deputy Amir Jeshi Mkuu'' wakati huo huo anapigiwa mizinga 21 kama Amir Jeshi Mkuu. Wapi kwenye Federation hilo linatokea
Rais Samia alitumia vigezo vipi kuongeza kiwango cha asilimia ya misaada kwenda Zanzibar .
Siyo ,misaada ni pesa zilizoitwa za kibajeti
Kwanini serikali ya Zanzibar haichangii gharama za kuendesha muungano lakini wakati huo huo wanapata asilimia 2 ya mapato ya muungano, wanapata mapato ya payee ambayo hawachangii hata senti tano.
Kwa mujibu wa Katiba wa CCM wa Zanzibar bw Mbeto kiwango kimeongezwa kutoka 4.5% hadi 9% na Rais SSH.
Kwamba kila kodi ya Mtanganyika kuna kiwango kinakwenda Zanzibar !
Kwanini wazanzibar wanaajiriwa kwenye nafasi zisizo za muungano Kama mkuu wilaya, waziri wa uchukuzi na katibu wake na wameshiriki kuuza bandari za Tanzania bila kuzigusa za Zanzibar.
Ni kwasababu wana nafasi 21% na hizo hazitoshi wao katika mambo ya Muungano. Siku hizi RAS , DC Wakurugenzi wa Tanganyika ni Wazanzibar ! kule Zanzibar huwezi kuingiza hata kipande cha ndizi achilia mbali ajira
Time ya Nyalari, tume ya jaji Kissanga na tume ya Warioba zote zilipendekeza serikali tatu nao walikuwa wajinga.
Pascal Mayalla anawaita hawa wazee Vitimbakwiri
Kwanini Tanganyika ndio ibebe gharama ya muungano zaidi wakati Zanzibar ndio wanufaika wakubwa.
Hili nalo ni neno na jambo la kujiuliza, ni kwa faida ipi
Zanzibar waliondoka kinyemela swala la gesi na mafuta kinyemela baada ya kuhisi wao Wana vitu hivyo na uongozi wa rais wa muungano atakuwa mtanganyoka Ila tumeona Samia mkataba wake wa kwanza akiwa rais wa muungano ulikuwa wa gesi kwenda Kenya.
Siyo hilo tu kuna video ya Mzee Warioba akiongea na Buholela wa ITV, alishangaa na kuuliza jinsi mambo yalivyoondolewa na Zanzibar ! Yaliyobaki ni Tanzania a.k.a shamba la bili
Ni swala la muda serikali ya Tanganyika kurudi ndio maana jaji Warioba alisema ni heri watanganyika wakapewa serikali yao kabla ya kuidai.
Na kama hawatarudisha, Muungano utafikia hatma katika muda mrefu

Hizi mbinu za kutuma watu wapotoshe Federation ya Tanzania na Zanzibar hazitafanikiwa
 
TUPIGE KURA tuulizwe,kama uendelee au tuachane nao,,Hilo nalo mtakataa
 
Magufuli alimsoma siku nyingi huyu mtu na kusema Mayala mtu ni njaa kwa mtu mwenye akili huhitaji nguvu nyingi hata kuliona hili na kumpuudha hoja zake ila historia itamuhukumu siku moja kwa haya anayoandika.

Ki ukweli Muungano ni mzuri ila kuna mapungufu tu address mapungufu tutafute solution tuende mbele sio kuuvunja hilo hapana halikubaliki.

Mayala wewe ni wakili naomba jibu la hili swali Kati ya katiba ya Muungano na ya Zanzibar ni katiba ipi ipo juu ya mwenzake ukijibu hili nitakuuliza swali la pili...
 
Hawezi kuwa na jibu la maana, atuambie mtanganyika ananufaika vipi na huu muungano?
 
Ni mjinga pekee anaweza kudhani tuna muungano huku watanganyika tunanyonywa
 
Ni mjinga pekee ambaye hadai Tangayika huku tukinyonywa na Zanzibar
 
ni muhimu zaidi kuwatoa ujinga vitimbakwiri hawa. Kuacha kufanya hivyo ni kuwatelekeza, jambo ambalo si zuri, watazaliana na ujinga wa kibaguzi kudai kitu kisichokuepo utaongezeka zaidi 🐒
Unaandika kama aliyepata ajira wakati wa samia
 
Ntarudi kuchangia maana ndo natoka hapa arusha the hub lounge .Ukweli kuna mzanzibar nilikutana nae last week zanzibar nina kitu alinieleza ntashare.mada za msingi kama hizi sio za kuchangia na hangover.
 
mi swali langu ni kama Tanganyika ilifutwa kwanini zanzibar haikufutwa ili ibaki Tanzania? na kwanini kuwe na zanzibar ukaaz na hakuna tanganyika ukaaz? kwanini zanzibar wana katiba wana rais ambayo ni serikali kamili lakini tanganyika haipo? kwann mzanzibar anaruhusiwa kumiliki ardhi tanganyika lkn mtanganyika haruhusiwi kumiki ardhi? kama zanziba wana serikali yao kwanini tanganyika haina serikali yake?? naomba na mimi nitoe ujing ili nielewee urai vzr
 
Unaandika kama aliyepata ajira wakati wa samia
jambo la muhimu na maana zaidi ni kufuatilia vipindi na makala vya masula ya uraia na sheria ambavyo muungwana comrade Pascal Mayalla anakusudia kuitoa for free to the paplics....

hii ingine,
ya ajira si jui ya nani ilikua lini, ni mihemko tu ya kawaida out of point. Tafadhali usikate tamaa, hapana kususa wala kuzira katika kutafuta ufahamu na uelewa zaidi juu ya mambo haya muhimu zaidi kwa maslahi mapana kwa usalama, umoja na mshikamano wetu kama Taifa 🐒
Twende pamoja bila mihemko.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…