Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Hoja za Utanganyika na Uzanzibari ni Hoja Muflis za Ujinga wa Ukosefu Elimu ya Uraia. Tuwatoe Ujinga Huu Kwa Elimu ya Uraia au Tuwaache na Ujinga Wao?

Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.

Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.

Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081

Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.

Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.

NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.

Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.

Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,

1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.

2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.

Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.

Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.

Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.

Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.

View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4
Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.

Paskali

Hoja unayo but unamumunya mambo. Ukweli utakuweka huru. Uadimu na uadhimu wa Muungano wetu opo wapi? Kwanini Zanzibar ibaki na utawala wake wa ndani na Tanganyika ipoteze utawala wake wa ndani? Na kwanini utambulisho wa Uzanzibar ubaki? watu wanataka mambo yaliyonyooka; Ni ama Serikali moja kama ilivyo makusudio ya vyama vilivyoungana (TANU na ASP)au Serikali tatu (Serikali ya Zanzibar na Tanganyika zikiwa na mamlaka za ndani tu na Serikali kuu ikisimamia masuala yote ya ulinzi, uraia, mambo ya nje n.k). Ni mambo madogo tu yanayokera ktk muundo huu wa Muungano.
 
Hoja Kwanini Zanzibar ibaki na utawala wake wa ndani na Tanganyika ipoteze utawala wake wa ndani? Na kwanini utambulisho wa Uzanzibar ubaki? watu wanataka mambo yaliyonyooka; Ni ama Serikali moja kama ilivyo makusudio ya vyama vilivyoungana (TANU na ASP)au Serikali tatu (Serikali ya Zanzibar na Tanganyika zikiwa na mamlaka za ndani tu na Serikali kuu ikisimamia masuala yote ya ulinzi, uraia, mambo ya nje n.k).
Zanzibar imebaki na utawala wake wa ndani kwasababu ni the minority. Tanganyika haikufa, bali ni serikali ya Tanganyika ndio imeubeba muungano, hata kule UN, kimefutwa kiti cha Zanzibar tuu, Balozi wa Zanzibar UN akawa rendered jobless, Balozi wa Tanganyika UN, aliendelea, na serikali ya Tanganyika ikajigeuza serikali ya muungano, katiba ya Tanganyika, ikageuzwa katiba ya muungano, Rais wa Tanganyika, akawa rais wa muungano. Kilichotokea ni jina tuu la Tanganyika kugeuka Tanzania, everything else remains the same!, hivyo ni Tanganyika ndio imeendelea kuubeba huu muungano wetu adhimu hadi leo.

Na mwisho hilo la serikali moja, nakuunga mkono, mimi ni muumini wa serikali moja!.
P
 
Berlin conference surveyor aliyechora ramani ya africa ni nani? Tumeshindwa kabisa kubadili mipaka
 
Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.
Mwalimu ni binadamu kama mwingine yeyote yeye siyo Mungu kusema kwamba kila anachosema au kukifikiria ndiyo sahihi,yeye anasema kitu kwa utashi wake na uelewa wake.
Huwezi kusema eti kwa vile Watanganyika au Wazanzibar wanaohoji baadhi ya mambo katika huu Muungano ni wabaguzi sijui ubaguzi ni kama kula nyama ya mtu sijui nini! Sio kweli kwanza Watanganyika na Wazanzibar sio ndugu hivyo ikitokea mmoja kamkataa mwenzie huo sio ubaguzi,Watanganyika na Wazanzibar ni marafiki tu hivyo ikitokea wakashindwa kupatana na wakavunja urafiki wao hapo hakuna ubaguzi wowote.
Tuache tabia ya kumuona Nyerere ndiyo Mungu wetu huko ni kumkufuru muumba wa kweli kama Mungu angetaka Watanganyika na Wazanzibar tuwe ndugu Zanzibar ingekuwa ndani ya Tanganyika kama ilivyo Mafia,Ukerewe na visiwa vingine vilivyojaa ndani ya nchi yetu Tanganyika na tuache kuwa makondoo ya kuja kutawaliwa na Wazanzibar hadi vijijini huko,
Kama Tanganyika na Zanzibar ingekuwa nchi moja basi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania angekuwa na mamlaka hadi kule Zanzibar lakini kwa sasa hana mamlaka yoyote huko Zanzibar.
Muungano gani eti "Sio kila Mtanzania ni Mzanzibar"(Wazanzibar wanalisema sana hili) lakini kila Mtanzania ni Mtanganyika yaani Wazanzibar wao ni Watanzania, Wazanzibar na ni Watanganyika lakini Mtanganyika yeye ni Mtanganyika tu maana hata huo Utanzania wake ni kama haujulikani ndiyo maana leo hii kuna Wazanzibar wanakuja na hoja ya kuwataka Watanganyika waingie kwa pasipoti Zanzibar, sasa hapo kuna udugu?
 
Muungano gani eti "Sio kila Mtanzania ni Mzanzibar"(Wazanzibar wanalisema sana hili) lakini kila Mtanzania ni Mtanganyika yaani Wazanzibar wao ni Watanzania, Wazanzibar na ni Watanganyika lakini Mtanganyika yeye ni Mtanganyika tu maana hata huo Utanzania wake ni kama haujulikani ndiyo maana leo hii kuna Wazanzibar wanakuja na hoja ya kuwataka Watanganyika waingie kwa pasipoti Zanzibar, sasa hapo kuna udugu?
Siku hizi imekuwa slogan '' Kila Mzanzibar ni Mtanzania lakini si kila Mtanzania ni Mzanzibar''
Hapa wanataka kutumia Utanzania katika kupata rasilimali za Tanzania lakini wao si Watanzania kwa imani yao kama alivyokana Mbunge wa Zanzibar ndani ya Bunge la JMT

Tuta debunk hii hoja, na ukweli ni kwamba hiyo slogan inachochea sana hasira za Watanganyika.
Hakuna sababu ya kupigazana kelele , tunahitaji Tanganyika

Pascal Mayalla anasema tuna '' Federation ya Tanzania na Zanzibar'' bado najiuliza kwasababu hii elimu ya Uraia sinayo kabisa. Kwamba kuna nchi ya Tanzania tofauti na nchi ya Zanzibar zimefanya Federation sijui inaitwaje.
 
Siku hizi imekuwa slogan '' Kila Mzanzibar ni Mtanzania lakini si kila Mtanzania ni Mzanzibar''
Hapa wanataka kutumia Utanzania katika kupata rasilimali za Tanzania lakini wao si Watanzania kwa imani yao kama alivyokana Mbunge wa Zanzibar ndani ya Bunge la JMT

Tuta debunk hii hoja, na ukweli ni kwamba hiyo slogan inachochea sana hasira za Watanganyika.
Hakuna sababu ya kupigazana kelele , tunahitaji Tanganyika

Pascal Mayalla anasema tuna '' Federation ya Tanzania na Zanzibar'' bado najiuliza kwasababu hii elimu ya Uraia sinayo kabisa. Kwamba kuna nchi ya Tanzania tofauti na nchi ya Zanzibar zimefanya Federation sijui inaitwaje.
Huyo jamaa anajifanya mahiri sana kwa uchambuzi lakini ninachokiona anajitia aibu tu,yeye anamuona Nyerere yupo sahihi kwa kila kitu maana kila siku Nyerere kasema,Nyerere kasema!
 
Pascal Mayalla anasema tuna '' Federation ya Tanzania na Zanzibar'' bado najiuliza kwasababu hii elimu ya Uraia sinayo kabisa. Kwamba kuna nchi ya Tanzania tofauti na nchi ya Zanzibar zimefanya Federation sijui inaitwaje.
Karibu kwenye elimu ya uraia kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu,
2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wanchi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.
Paskali
Natumaini umeelimika
P
 
Huyo jamaa anajifanya mahiri sana kwa uchambuzi lakini ninachokiona anajitia aibu tu,yeye anamuona Nyerere yupo sahihi kwa kila kitu maana kila siku Nyerere kasema,Nyerere kasema!
Sijifanyi mahiri, mimi ni mwandishi wa habari kwa miaka zaidi ya 30, na pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, hivyo nina umahiri fulani kwenye baadhi ya maeneo.

Mwalimu Nyerere ni mtu sahihi sana, na kuna vitu vingi Nyerere kasema, nitaendelea kuwaletea Nyerere alichokisema.
P
 
Karibu kwenye elimu ya uraia kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu,
Natumaini umeelimika
P
Hapana sijaelimika kwasababu sijui federation inatoka wapi
Nimeangalia Federal gov zote kuanzia East hadi West hakuna mahali nchi inaungana na jimbo au state

Kwa mfano, hakuna Federation ya USA na California au state yoyote. Kuna Federal gov ya state 50 za Marekani kufanya USA.

Nimeangalia Australia ambayo ni Federal state, sikuona mahali Australia imetengeneza federation na state zake

Orodha inaendelea.

Hii Federation ya Tanzania na Zanzibar inawezekanaje? Hii ndiyo elimu ngumu ninayohitaji,
Hapa tufafanulie sisi wenye vichwa vyepesi, Tanzania ni ipi na inafanyaje federation na Zanzibar ambayo ni sehemu ya Tanzania. !!!
 
Mwalimu Nyerere ni mtu sahihi sana, na kuna vitu vingi Nyerere kasema, nitaendelea kuwaletea Nyerere alichokisema.
P
Baada ya muda wake wa Urais Nyerere aliulizwa kuna kosa gani anafikiri alitenda akiwa madarakani

Mwl alisema ' Kosa kubwa lilikuwa kuua vyama vya Ushirika'' sasa usahihi unaousema wewe yeye kasema haupo
Pili, Nyerere aliua mfumo wa vyama vingi 1965 na kisha ''kusimamia' kwa remote urejeshwaji wake mwaka 1990
Usahihi upo wapi?

Ni kwamba alikuwa na maono, lakini kama binadamu alikuwa na mapungufu! si kosa ni ubinadamu

Hata hili la mkanganyiko wa Federation ya Tanzania na Zanzibar unalozungumzo ni mapungufu.
Nyerere hakuwahi kukataa uwepo wa Tanganyika ! Watoa elimu ya Uraia wanamsingizia
 
Tunahitaji elimu ya Uraia sisi vitimbakwiri

'' Federation ya Tanzania na Zanzibar ipoje'' ?
Muungano wetu adimu na adhimu ni muungano wa kitaifa na kimataifa. Kimataifa ni muungano wa union ya nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar kuungana na kuunda nchi moja ya JMT.

Lakini kitaifa ndani ya muungano, ni muungano wa federation ya nchi mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar.

Ni very unique duniani kote hakuna muungano kama huu, na kitu kikubwa kumhusu huu muungano wetu adhimu ni dhima ya muungano, ni muungano wa milele, hakuna any legal provisions za kuuvunja muungano!.

Kiukweli kabisa elimu hii ya uraia kuhusu muungano wetu ninayoitoa hapa, itasaidia sana kuwaelimisha wengi kuhusu muungano wetu adimu na adhimu, wakiwemo vitimbakwiri.
P
 
Wanabodi

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.

Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.

Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081

Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.

Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.

NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.

Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.

Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,

1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.

2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.

Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.

Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.

Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.

Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.

Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.

View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4
Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.

Paskali

Waache na ujinga wao hao manyumbu.

Just imagine ikiwa Tanganyika Mimi ndio itaniongezea hela?
 
Muungano wetu adimu na adhimu ni muungano wa kitaifa na kimataifa. Kimataifa ni muungano wa union ya nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar kuungana na kuunda nchi moja ya JMT.
Nakubaliana nawe 100%
Lakini kitaifa ndani ya muungano, ni muungano wa federation ya nchi mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar.
Hakuna nchi ya Tanzania Bara, kuna Tanganyika na Zanzibar.
Kama kuna Federation ya Tanganyika na Zanzibar ipo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Iko wapi Serikali ya Tanganyika?

Kumbuka unapokuwa na 'conflict' kati ya state au Province zinazounda Federal gov, msuluhishi ni Federal gov.
Lakini conflict hizo zitahusu mambo yaliyokubaliwa kuwa ni ya Federal gov.

Kukiwa na conflict zinazitwa kero za Wazanzibar (state) ikilalamikia Tanganyika (state) msuluhishi ni Tanzania (Federal gove). Swali kwa Pascal , katika meza ya majadiliano SMZ inawakilishi Zanzibar, iko wapi Serikali inayowakilisha Tanganyika! ili Zanzibar na Tanganyika zikae meza moja chini ya msuluhishi Tanzania?

Ni very unique duniani kote hakuna muungano kama huu, na kitu kikubwa kumhusu huu muungano wetu adhimu ni dhima ya muungano, ni muungano wa milele, hakuna any legal provisions za kuuvunja muungano!.
P

Kwani mkataba wa Muungano wa 1964 ulikuwa legally binding au la?
 
Nimesema nukibahatika kuwa rais Kaz ya Kwanza kufanya Ni kufunja huu muungano ndani ya siku tatu narejesha serekali ya tanganyika
 
Nakubaliana nawe 100%
Hakuna nchi ya Tanzania Bara, kuna Tanganyika na Zanzibar.
Kama kuna Federation ya Tanganyika na Zanzibar ipo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Iko wapi Serikali ya Tanganyika?
Ndio maana nimesema kunahitajika elimu ya uraia kuhusu huu muungano wetu. Muungano wetu ni wa nchi mbili, Tanganyika na Zanzibar na kuunda serikali moja ya JMT. Ni kweli hakuna nchi inayoitwa Tanzania Bara, wala Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar, hizi sio nchi, ni sehemu ya JMT. Tanzania Bara ni ile sehemu iliyokuwa Tanganyika, jina la Tanganyika limefutwa na nafasi yake kuchukuliwa na Tanzania Bara.

Muungano wetu ni very unique, Zanzibar ndio yenye utawala wake wa ndani wa SMZ, lakini kwa Tanzania, serikali ya JMT, ni serikali ya muungano ambayo pia imevaa koti ya serikali ya Tanganyika kwa mambo ambayo sio ya muungano.
P.
 
Kwani mkataba wa Muungano wa 1964 ulikuwa legally binding au la?
Kulipaswa kuwe na mkataba wa kimataifa wa muungano ambao ni legally binding, but it's very unfortunately, kitu kilichopo ni zile Articles of Union, ambazo ni hati za muungano, japo zinaitwa mkataba, but in reality sio mkataba, ni just an agreement which is not legally binding kwasababu unapungukiwa na moja ya sifa muhimu za mikataba ya kisheria, inayoitwa "privity to contract" ni kila mkataba wa kisheria lazima uwe na kipengele cha privity kinacho onyesha jinsi ya kuuvunja huo mkataba. Kwenye articles of union, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja muungano, hiyo ndio dhima ya muungano ni for life!.

Karibu pande hizi Je, Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu ya Muungano? na hizi Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria (De Jure) Bali ni De Factor?! na Swali: Hivi Muungano Tanzania Upo Kweli?! au ni Dhana Tuu?!. (Ufuatiliaji Muungano Sehemu ya I)
P
 
Hapana sijaelimika kwasababu sijui federation inatoka wapi
Nimeangalia Federal gov zote kuanzia East hadi West hakuna mahali nchi inaungana na jimbo au state

Kwa mfano, hakuna Federation ya USA na California au state yoyote. Kuna Federal gov ya state 50 za Marekani kufanya USA.

Nimeangalia Australia ambayo ni Federal state, sikuona mahali Australia imetengeneza federation na state zake

Orodha inaendelea.

Hii Federation ya Tanzania na Zanzibar inawezekanaje? Hii ndiyo elimu ngumu ninayohitaji,
Hapa tufafanulie sisi wenye vichwa vyepesi, Tanzania ni ipi na inafanyaje federation na Zanzibar ambayo ni sehemu ya Tanzania. !!!
Huu ndio umuhimu wa elimu hii, muungano wetu adhimu ni very unique kwasababu kwa kimataifa ni muungano wa union ya nchi mbili kuungana na kuunda nchi moja ya JMT.

Lakini kitaufa ni muungano wa federation ya nchi mbili, za JMT na Zanzibar. Federal state ni serikali ya JMT, local states ni SMZ na Serikali ya JMT kwa mambo yasiyo ya muungano. Serikali ya JMT imevaa koti la serikali ya Tanganyika kwa mambo yasiyo ya muungano at the same time ndio federal state ya serikali ya muungano kwa mambo ya muungano. Kimataifa muungano wetu ni union ya nchi moja tuu ya JMT na Zanzibar kimataifa sio nchi, ni sehemu ya JMT lakini Kitaifa ni muungano wa federation ya nchi mbili, JMT na Zanzibar. Huu ni muungano very unique duniani na hatuhitaji kufanana na muungano mwingine wowote, tungekuwa ni watu wazuri kwenye international promotion, marketing na branding, tunge i promoti Tanzania kwa kuifanyia branding ya union promotion watu dunia nzima wangemiminika Tanzania kuja kushuhudia muungano wa ajabu wa union on one side and federation on the other side, tunge make millions!.

Sasa jambo kubwa zuri kama hili hatuwezi kuliacha likabezwa na vitimbakwiri, lazima tutokee watu Wazalendo wa kuitetea, tena sasa chini ya rais Mtanzania kutoka upande wa pili, Zanzibar, this is the most opportune moment to solidify the union into one solid government. Tumemshauri Rais Samia kwanza kwa kuuliza Je, umefika wakati kutimiza Uzalendo wa kweli wa kwenda kwenye Serikali moja? kisha kwa kushauri Pongezi za Miaka 60 ya Muungano: Twende Kwenye Muungano Kamili wa Ukweli wa Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja? Kero Zote za Muungano Zitayeyuka!

P
 
Back
Top Bottom