Hoja za Waitara - Je, CHADEMA watajibu?

Hoja za Waitara - Je, CHADEMA watajibu?

Huwaga wapo kwenye kambi ya waziri mkuu huwa wanabana vitu lakini vinahishia kutopata urais wanawake wao:

1. Malecela
2. Majaliwa
3. Pinda
4. Lowasa
5. Msuya


Tawezekana hawakuoa wanawake wenye dharau hapo zamani ulikuwa handsome na ulikuwa na fedha nyingi na vingora hadi nyumbani baby


Ndiyo walivyo saizi hatujui nani ni nani maana kama walituletea uongozi wa kuridhi itakuwa fursa kwa hisani ya watu wa marekani

1. Watoto na mke wa Nyerere
2. Watoto na mke wa mwinyi
3. Watoto na mke wa mkapa
4. Watoto na mke wa kikwete
5. Watoto na mke wa magufuli

Kukaa ikulu raha lazima siri zitavija ukiweka toy la urais,,

Lazima wawagawe wanawake
Kama kuna mtu atakua amekuelewa ulichoandika hapa atakua na kipaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani Wewe ni mgeni humu jamvini. Siku zote hoja inayoletwa humu kama ni nzito lazima itakua na idadi kubwa ya wachangiaji. Kama ni mchango unaoungwa mkono lazima uwe na likes za kutosha. Na huwezi kuungwa mkono kama huna facts. Sema siku hizi tu JF imeingiliwa unaweza ukapiga porojo na ukapata likes za kutosha. Lakini wewe hata hilo limeshindikana kwenye hoja yako. Inabidi unishukuru hata mimi niliekujibu.

Anyway turudi kwenye hoja yako. Sasa hivi msahafu wa CDM kumsafisha mwenyekiti wenu mbowe ni hati safi za CAG. Kumbuka CAG anakagua mahesabu tu kwa maana ya matumizi ya fedha zilizototolewa na Serikali Lakini maamuzi wa hizo fedha zinatumika vp hawezi kuingilia ni maamuzi ya chama na hapo ndo mbowe anapowapigia. Kwa mfano, chama kilikua na madeni na inaonekana kwenye mahesabu hayo madeni yamelipwa na stakabadhi zipo, unadhani CAG atasemaje? Lakini watu wanachohoji ni uhalali wa hayo madeni. Lakini vipi kuhusu michango na misaada ambayo chama inapokea nani anakagua?

Tuhuma za mbowe kuhusu ubadhirifu wa fedha za chama hazikuanza Leo wala jana. Chacha Wangwe aliongea, Zitto Kabwe aliongea, Mwigamba aliongea, Kitila aliongea. Na sasa wanaongea wabunge kina lijualikali na Waitara. Hawa wote wanamsingizia mbowe? Toka gizani fungua akili yako. Utajikuta unatetea kitu usichokijua kutokana tu na mahaba uliyonayo kwenye hicho chama.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tupunguze ulimbukeni na likes, tafuta mada za Fahami Matsawili zote ni nzito za kujadili mustakabali wa taifa mfano sera ya elimu, sera ya uwekezaji lakini hutoona comment wala like hta moja then urudi hapa kusema HOJA ndio huzaa likes. Trust me unaweza andika mada kusifia miradi ya awamu ya tano ila comment ya kwanza ikiwa "kachukue buku 7" hapo utakuta likes hadi 100. Nachosema ni JF ya sasa imejaa ushabiki sio kujibu hoja, ndio maana wewe ukaishia kunikejeli tu badala ujibu hayo maswali yangu.

1. Nmekwambia kuthibitisha sijaona hta uki upload hapa Financial statement ya CHADEMA ila umerudi na porojo kma waitara.

2. CAG kupitia NAO hakagui tu financial reports bali hadi procurement procedures, anakagua mali za chama pia, pamoja na madeni!! Sasa akifika kwenye deni atauliza hii 50M hapa ya Mbowe evidence yake ikwapi? Alikopesha lini kwa wiring ipi? Kma hamna document hapo anaweka querry hivyo haiwezi kuwa hati safi tena.

3. Issue hapa sio kelele za Mwigamba au Zitto, obvious kwa siasa za TZ kila anayehama lazima atoe tuhuma lakini shida uthibitisho. Sasa waitara ni waziri kwanini asitumie hayo mamlaka kuamuru Mbowe akaguliwe hadi akaunti binafsi ili mambo yawe wazi? Kwanini hajaleta financial statements za chama ama biashara za Mbowe ili atafute huo wizi wake?

Issu sio Mbowe kuiba ama lah issue ni FACTS, kma hamna mie siwezi kuamini. Huyo waitara kma alishajua Mbowe mwizi kwanini aligombea kupitia CHADEMA toka 2010? Hawa wanasiasa wapo kimaslahi tu mkuu sio kupinga ufisadi wa Mbowe.
 
With due respect, naona kuna tatizo kubwa pahala. Waziri anapata wapi muda wa kumshambulia mtu badala ya kudeal na mambo ya wizara yake ambayo ina changamoto lukuki.

Watanzania tuna tatizo kubwa sana kwenye bongo zetu, kwa namna hii hatutaenda kokote. Waziri kabisa kabisa anatumia muda wetu walipa kodi kijinga nmna hii? Imenikerehesha sana.

Nimeanza kukubaliana na kauli za prof. Watson juu yetu watu weusi. Waziri wetu anatuhutubia ujinga huu bila hata soni, waziri kabisa? Badala ya kuja na mambo ya sera na utekelezaji anatuhutubia mambo ya Mbowe?

Hati chafu au safi za CCM na CHADEMA hazina manufaa kwetu. Pengine abadilishiwe nafasi apelekwe kwenye uongozi wa chama.

Waziri kabisa kabisa hapo na wewe uñajiona mchapakazi? Watanzania tujitafakarini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hivi ushawahi kuona mtu mwenye akili timamu anajibizana na chizi ?...!!
 
Propaganda tu nilidhani ana nyaraka kumbe anatutuma kwa Gwajima!!

Anadai Mbowe ametapeli pesa za kampeni ilihali Waitara bado alikubali kugombea kupitia CHADEMA!!

Hvi tuhuma nzito hivi unadhani Dr Slaa asingezimwaga siku anasepa ama Zitto?

Dr Mashinji alikua katibu mkuu hajayasema hya sembuse hyu aliyekua subordinate tu.

Ifike mahala hawa waropokaji wafaiwe nyaraka kuthubitisha maana kma CAG anakagua mahesabu afu haoni huu ubadhirifu ila wanasiasa ndio wanauona basi nchi yetu ina matatizo mazito zaidi.

CCM jaribuni zaidi, Kma Dr Slaa alifeli sidhani kuna press conference ya kuivunja CHADEMA.

Kuna yule Naibu waziri alisema CHADEMA walimdhuru Lissu nashangaa polisi haijamuita kusaidia upelelezi na kosa la kuiba evidence eneo la tukio.
Mkuu, hata Ile kunyanyua mdomo wako kusema mambo ya jambazi sugu ni ujasiri uliopitiliza, Kwa Maana ni kujitoa mganga wewe mwenyewe
 
Mkuu, hata Ile kunyanyua mdomo wako kusema mambo ya jambazi sugu ni ujasiri uliopitiliza, Kwa Maana ni kujitoa mganga wewe mwenyewe
Ukiwa serikali huwezi ogopa jambazi sugu sababu unaweza amrisha hta JWTZ nzima imsake ila ukiwa huna jeshi kma wapinzani ndio lazima uogope kumsema "jambazi" sababu atakutumia wasiojulikana na wewe huna JESHI la kukulinda.

Sasa ikitokea waziri aogope jambazi nani sasa atakua mjasiri kuanika uhalifu?
 
Count down has started to the October elections, less than 150 days.
 
Tupunguze ulimbukeni na likes, tafuta mada za Fahami Matsawili zote ni nzito za kujadili mustakabali wa taifa mfano sera ya elimu, sera ya uwekezaji lakini hutoona comment wala like hta moja then urudi hapa kusema HOJA ndio huzaa likes. Trust me unaweza andika mada kusifia miradi ya awamu ya tano ila comment ya kwanza ikiwa "kachukue buku 7" hapo utakuta likes hadi 100. Nachosema ni JF ya sasa imejaa ushabiki sio kujibu hoja, ndio maana wewe ukaishia kunikejeli tu badala ujibu hayo maswali yangu.

1. Nmekwambia kuthibitisha sijaona hta uki upload hapa Financial statement ya CHADEMA ila umerudi na porojo kma waitara.

2. CAG kupitia NAO hakagui tu financial reports bali hadi procurement procedures, anakagua mali za chama pia, pamoja na madeni!! Sasa akifika kwenye deni atauliza hii 50M hapa ya Mbowe evidence yake ikwapi? Alikopesha lini kwa wiring ipi? Kma hamna document hapo anaweka querry hivyo haiwezi kuwa hati safi tena.

3. Issue hapa sio kelele za Mwigamba au Zitto, obvious kwa siasa za TZ kila anayehama lazima atoe tuhuma lakini shida uthibitisho. Sasa waitara ni waziri kwanini asitumie hayo mamlaka kuamuru Mbowe akaguliwe hadi akaunti binafsi ili mambo yawe wazi? Kwanini hajaleta financial statements za chama ama biashara za Mbowe ili atafute huo wizi wake?

Issu sio Mbowe kuiba ama lah issue ni FACTS, kma hamna mie siwezi kuamini. Huyo waitara kma alishajua Mbowe mwizi kwanini aligombea kupitia CHADEMA toka 2010? Hawa wanasiasa wapo kimaslahi tu mkuu sio kupinga ufisadi wa Mbowe.
Mkuu zitto junior, hakika wewe na wanaokupa "likes" mmeamua, bila kupepesa macho na kumng'unya maneno, kutetea uovu unaofanywa na Mbowe na genge lake. Wanao mshutumu Mbowe ni viongozi wenzake waliokihama chama kwa sababu ya udhaifu wake kiuongozi. Je, hata huyu naye utamkosoa kwa lipi?

 


========
Mh. Waitara amesema kuwa baada ya wabunge wa CHADEMA kutangaza kuwa watahamia CCM na wengine wataenda NCCR Mageuzi basi wameshambuliwa sana na hasa Mh, Lijualikali.

Amesema kuwa miongoni mwa watu ambao anawafahamu ni pamoja na Lijualikali, anadai alipoenda Mlimba na Kilombero wakati Lijualikali anagombea udiwani na Lijualikali hakuwa mtumishi wa CHADEMA ila alikuwa ni mwanachama wa CHADEMA.

Anadai kuwa wakati huo yeye ndie aliekuwa mtu wa sera na utafiti na alifanya utafiti nchi nzima hivyo kusema Lijualikali hana nguvu Kilombero sio kweli kwa kuwa alichaguliwa kugombea kati ya wengi waliokuwa wanataka kugombea.

Anasema kwenye siasa ukitaka kushinda, chama cha siasa kinapomchangua mgombea mwenye sifa basi wanahesabu asilimia 30 kuwa tayari wameshashinda.

Anasema katika nchi hii mtu ambaye amebahatika kukaa kwenye siasa mda mrefu lakini ni tapeli wa kisiasa na alipaswa afungwe kwenye ile timu ya wahujumu wa Uchumi ni Mh. Mbowe lakini Mungu wake ni mkubwa sana.

Anadai kuwa kwenye matumizi ya pesa Mh. Mbowe anatumia pesa za chama kwa matumizi yake binafsi na hakuna maendeleo ya chama kama ofisi nk.

Anadai Kuna pesa ambazo CHADEMA ilipewa kutoka Japani kwa ajili ya kusaidia mchakato wa kampeni mwaka 2014 lakini pesa hizo hazijulikani ziliwekwa kwenye akaunti gani wala matumizi yake ni yapi na Mh. Mbowe hajatoa majibu kuhusu pesa hizo.

Anasema kuwa watu wanahama chama kwa kuwa wanagundua madhaifu yaliyopo kwenye mfumo wa kiuongozi wa Mh Mbowe kwa maana Mh Mbowe ndie anae fanya manunuzi peke yake na yeye ndie mwenye maamuzi ya mwisho na ikitokea mtu amelalamika au kusema kuhusu jambo lolote lisilo kuwa sawa kwa upande wa Mh. Mbowe basi anachukuliwa hatua kali.

Mbowe anatumia pesa za ruzuku kwa shughuli binafsi na kuwachangisha wabunge wake kila mwezi kwa matumizi binafsi. Huyu ni Dictator mkubwa sana wakati hata Ofisi ameshindwa kujenga licha ya kuwa Chama kinapata pesa nyingi.
Mbowe na Chadema hawana muda mchafu kujibizana na mataahira ya CCM yaliyolewa mataputapu.
 
Mkuu zitto junior, hakika wewe na wanaokupa "likes" mmeamua, bila kupepesa macho na kumng'unya maneno, kutetea uovu unaofanywa na Mbowe na genge lake. Wanao mshutumu Mbowe ni viongozi wenzake waliokihama chama kwa sababu ya udhaifu wake kiuongozi. Je, hata huyu naye utamkosoa kwa lipi?


Ole Medeye alikua CCM maisha yake yote ni lini amekua kiongozi wa CHADEMA?

Anadai cjui aliahidiwa kiti CC, je anaweza prove hayo madai? Hana Copy ya MoU? Eti yye ndio alikua anakidhamini chama wakienda mikoani?

Unajua kutoa tuhuma ni rahisi ila kuthibitisha ndio mtihani.

Ssa kituko watu hamfuatilii mnachukua maneno kma yalivyo then tunajiita great thinkers

Mbowe angekua fisadi kma mnavyompaka hapa CCM wangeshampa kesi ya uhujumu uchumi kitambo tu
 
Ole Medeye alikua CCM maisha yake yote ni lini amekua kiongozi wa CHADEMA?

Anadai cjui aliahidiwa kiti CC, je anaweza prove hayo madai? Hana Copy ya MoU? Eti yye ndio alikua anakidhamini chama wakienda mikoani?

Unajua kutoa tuhuma ni rahisi ila kuthibitisha ndio mtihani.

Ssa kituko watu hamfuatilii mnachukua maneno kma yalivyo then tunajiita great thinkers

Mbowe angekua fisadi kma mnavyompaka hapa CCM wangeshampa kesi ya uhujumu uchumi kitambo tu

Hakuna anaye mpaka Mbowe tuhuma. Tuhuma zinazosemwa dhidi yake na genge lake ni nzito na zinatolewa na viongozi waliokuwa naye CHADEMA.

Maisha ya Ole Medeye CHADEMA amesimulia nwenyewe, kwenye hiyo video, akhojiwa maswali mazito, siyo yangu.

Wanaotoa tuhuma naamini wanao ushahidi, la, watuhumiwa wangekuwa au wanaweza kuwachukulia hatua. Ukimya wao ni dhahiri wamekubali tuhuma. Usiwasemee ya moyoni mwao.

Siwezi kufuatilia tuhuma ambazo hazikuelekezwa kwangu. Anayechafuliwa huwajibika kujisafisha.

CCM ni chama cha Siasa, kama CHADEMA, hivyo basi, kinashughulika kulinda na kutetea Katiba yake.

Tuhuma za ufisadi wa mali ya umma, km ruzuku, TAKUKURU imekwishaanza mchakato. Kuna tetesi ya Mbowe kuingia mini kujaribu kuharibu ushahidi. Chonde chonde, ninyi watetezi wake, msije kung'aka tena, ushahidi ukipatikana akapelekwa mahakamani kujibu tuhuma.
 
1591133532206.png
 
Hakuna anaye mpaka Mbowe tuhuma. Tuhuma zinazosemwa dhidi yake na genge lake ni nzito na zinatolewa na viongozi waliokuwa naye CHADEMA.

Maisha ya Ole Medeye CHADEMA amesimulia nwenyewe, kwenye hiyo video, akhojiwa maswali mazito, siyo yangu.

Wanaotoa tuhuma naamini wanao ushahidi, la, watuhumiwa wangekuwa au wanaweza kuwachukulia hatua. Ukimya wao ni dhahiri wamekubali tuhuma. Usiwasemee ya moyoni mwao.

Siwezi kufuatilia tuhuma ambazo hazikuelekezwa kwangu. Anayechafuliwa huwajibika kujisafisha.

CCM ni chama cha Siasa, kama CHADEMA, hivyo basi, kinashughulika kulinda na kutetea Katiba yake.

Tuhuma za ufisadi wa mali ya umma, km ruzuku, TAKUKURU imekwishaanza mchakato. Kuna tetesi ya Mbowe kuingia mini kujaribu kuharibu ushahidi. Chonde chonde, ninyi watetezi wake, msije kung'aka tena, ushahidi ukipatikana akapelekwa mahakamani kujibu tuhuma.
Huu ni unafiki wa wanasiasa wa TZ, kwanini walipokua CHADEMA hawakusema au angalau wangeiba taarifa wapelekee polisi ili wamkamate Mbowe? Kukaa kimya huku pesa zinaibwa miaka yote ina maana na ww ulikua mnufaika.

At least Zitto yeye alipambana hesabu zao zikaguliwe akiwa bado CHADEMA ila hawa wengine wakitoka ndio matusi bila ushahidi.

Mkuu mie nikwambie tu maadam haya wanayosema CAG hajawahi thibitisha itabaki ni kelele tu. Ilipaswa waje na nyaraka maana si wapo serikalini hawawezi nyimwa.

Mfano wanaposema Mbowe anajilipa madeni, basi wangekuja na financial statement za CHADEMA kuonyesha kweli Mbowe huwa anaidai CHADEMA mbona simple tu ingemuumbua asubuhi tu.

Shida mnakuja na maneno wakati ni serikali, bora hao TAKUKURU wafanye uchunguzi I hope watakuja na data za kueleweka kuliko hizi kelele bila nyaraka. Hazisadii kitu.

GT hupaswi kuamini maneno bila ushahidi, nakumbuka tuliambiwa CHADEMA wanalipwa na wazungu kumdhoofisha Magufuli ila mbona wakienda CCM wanapokelewa na kupewa uwaziri? Leo Mbowe akienda CCM na kupewa uwaziri utaweka wapi sura yako mkuu? Usikubali kupotoshwa na wanasiasa fanya tafiti zako binafsi.
 
Huu ni unafiki wa wanasiasa wa TZ, kwanini walipokua CHADEMA hawakusema au angalau wangeiba taarifa wapelekee polisi ili wamkamate Mbowe? Kukaa kimya huku pesa zinaibwa miaka yote ina maana na ww ulikua mnufaika.

At least Zitto yeye alipambana hesabu zao zikaguliwe akiwa bado CHADEMA ila hawa wengine wakitoka ndio matusi bila ushahidi.

Mkuu mie nikwambie tu maadam haya wanayosema CAG hajawahi thibitisha itabaki ni kelele tu. Ilipaswa waje na nyaraka maana si wapo serikalini hawawezi nyimwa.

Mfano wanaposema Mbowe anajilipa madeni, basi wangekuja na financial statement za CHADEMA kuonyesha kweli Mbowe huwa anaidai CHADEMA mbona simple tu ingemuumbua asubuhi tu.

Shida mnakuja na maneno wakati ni serikali, bora hao TAKUKURU wafanye uchunguzi I hope watakuja na data za kueleweka kuliko hizi kelele bila nyaraka. Hazisadii kitu.

GT hupaswi kuamini maneno bila ushahidi, nakumbuka tuliambiwa CHADEMA wanalipwa na wazungu kumdhoofisha Magufuli ila mbona wakienda CCM wanapokelewa na kupewa uwaziri? Leo Mbowe akienda CCM na kupewa uwaziri utaweka wapi sura yako mkuu? Usikubali kupotoshwa na wanasiasa fanya tafiti zako binafsi.

Nakubaliana na wewe huenda zikawa porojo za kisiasa kama hizo za viongozi wa upinzani, wanachama na wafuasi wao, wanazozipaza kwa viongozi wa CCM na Serikali yake.

Kwa kuwa tunaelekea Uchaguzi Mkuu, tuhuma hizi zikipuuzwa, zitatumiwa na wapinzani wa CHADEMA. Athari zake ni kwa wagombea wa CHADEMA kutumia muda mwingi wa kampeni kumsafisha Mbowe, na chama chake kwa ujumla, badala ya kunadi sera za chama.

Isitoshe msimamo na mtazamo wa viongozi wa CHADEMA kuhusu masuala mazito ya kitaifa km ujenzi wa miundo mbinu, moja ya nguzo za kukuza uchumi na uboreshaji wa huduma za jamii, kukejeli kuwa ni maendeleo ya vitu, pia ni chsngamoto kwa wagombea kutetea hoja ya chama kuwa maendeleo ya watu ni demokrasia.

Kwamba, viongozi wa CHADEMA, kwa vitendo walijifungia kama njia sahihi ya kudhibiti maambukizi ya COVID-19, pia itawapa shida kujitetea. Km iwapo Jeshi la Polisi, ambalo naafisa wake hukabiliana na jamii kila mara, lingamua nao wajifungie siku 14, usalama wa raia na mali zao ungekuwaje?

Kwa hiyo, Mkuu zitto junior, usichukulie shutuma hizo kama unafiki wa wanasiasa wa TZ. Hakika viongozi wa CHADEMA wanakabiliwa na mengi ya kujibu ikiwa ni pamoja na fedha za ruzuku kutokujenga hata ofisi moja ya chama, kama ukumbusho. Kumbuka awamu hii ya utawala wa nchi hii, chama kilipata wabunge wengi na kuongoza halmashauri za miji mikubwa nchini, hivyo kuwa na uwezo mkubwa kifedha na donge nono la ruzuku. Kama viongozi wake wameshindwa kufanya hivyo, kamwe chama kitakuwa na ofisi hata ya chumba kimoja.

Tunahitaji vyama vya siasa vyenye viongozi wenye kubeba dhamana ya wanachama kwa maendeleo yao na ya mama Tanzania.
 
Back
Top Bottom