Home of AC Milan, Official Thread

Home of AC Milan, Official Thread

Milan itabaki kuwa Milan...
Forza Milan

Babu unaongea the golden era ya mchezo wa soka na watoto ambao by that time bado walikua viunoni mwa baba zao au kwenye matumbo ya mama zao, wengine hawakua hata na akili za kucheza kombolela

Waache waendelee kubishana nani bora kati ya Christina na Nesi, Naima na Suzrez, wewe kaifanyie abracadabra team yako irudishe japo makali kama ya Bianconeri maana hali zetu mabuluda ni mbaya

Forza Serie A
 
Babu unaongea the golden era ya mchezo wa soka na watoto ambao by that time bado walikua viunoni mwa baba zao au kwenye matumbo ya mama zao, wengine hawakua hata na akili za kucheza kombolela

Waache waendelee kubishana nani bora kati ya Christina na Nesi, Naima na Suzrez, wewe kaifanyie abracadabra team yako irudishe japo makali kama ya Bianconeri maana hali zetu mabuluda ni mbaya

Forza Serie A

wakongwe tutarudi tu
 
Haya futa povu uende jukwaa la mapishi...wenzako wanakusubiri huko
Gang chomba katika ubora wako na rosoneri yako.Kiukweli kuna historia nzuri hapo kwa miamba iliopitia milan hilo halipingiki lakini kila zama na kitabu chake chomba siwezi kuibeza milan ila kurudia mafanikio hayo inabidi mjifunge kibwebwe kweli.
 
Gang chomba katika ubora wako na rosoneri yako.Kiukweli kuna historia nzuri hapo kwa miamba iliopitia milan hilo halipingiki lakini kila zama na kitabu chake chomba siwezi kuibeza milan ila kurudia mafanikio hayo inabidi mjifunge kibwebwe kweli.

wanasema hata ndoja lilikuwa vigo...so tutakaa sawa tu
 
Sitaki niumize vidole vyangu Ac Milan ni sawa na akina liverpool na barca klabu boora milele ni Real Madrid UCL mara 10 wkt Milan mara 5, hii haiitaji elimu na ujuzi kujua ipi ni bora.
 
Hah hah ha hah ahaaah dah nianze kwa kicheko kilichojaa dharau na kebehi kisha nashushia na Bia aina ya Peroni inayopatikana kila Bar au Night Club au sehemu yoyote ya anasa katika jiji la Milan.

kikubwa kinachonichekesha ni kitendo cha makusudi cha washabiki wa soka wa siku hizi kujitia uzezeta na kutoa maneno ya kipumbavu ambayo kwa siku za karibuni wamezidi kuambukizana hivyo matapishi hayo wanayoongea yanatapakaa kila kona.

mwanzo niliposikia nikasema labda niliemsikia alitoka chooni bila kuchamba, lakini kwa sasa mambo ni tofauti.

soka lina misingi yake, soka lina sheria zake, lakini soka lina kitu kimoja muhimu mno ambacho hicho ndio kinaleta ladha halisi, kitu kicho ni historia.

unapozungumzia Historia ya Soka kwa ngazi za vilabu basi hutaacha kuitaja klabu yenye mafanikio zaidi hapa ulimwenguni, hapa naizungumzia AC Milan, ambayo pia ndio klabu iliochezewa na nyota wengi zaidi kuliko klabu yoyote mpaka sasa.

basi wakati nafungua Peroni ya 4 huku nikivuta shisha nikawa navuta kumbukumbu huku natafakari kauli kauli za wakurupukaji hawa wanaodai eti AC Milan ni katimu kadoogo sana, tena huwa wanakwenda mbali zaidi kwa kusema eti katimu haka hakana lolote.

ukiwauliza vilaza hawa watakwambia kwao timu bora ni Barcelona, Manchester, Madrid, Chelsea eti na hata Arsenal nayo imo

sasa wakati nilipokuwa na Peroni ya 9 huku moshi wa Fleva ya Minti ukiingia mpaka kwenye Bandama na kupanda hadi kwenye mishipa midogo inayoingia ndani ya Ubongo nikarejea tukio la kusisimua na kuchekesha ndani yake.

nilikumbuka tukio la tarehe 19/04/1989 mwendo wa saa mbili na na nusu usiku, katika usiku huu usiosahaulika na Los blancos ulikuwa ni wa mechi ya nusu fainali ya marudiano ya AC Milan dhidi ya Real Madrid, ikumbukwe ktk mechi ya kwanza iliofanyika katika dimba la El Santiago Bernabeu, Madrid walilazimisha suluhu ya goli 1-1.

na ktk mechi iliofuata sasa na kushuhudiwa na washabiki 73112 waliofurika Sansiro, Real Madrid walicharazwa goli 5-0 huku magoli ya Milan yakifungwa na Carlo Ancelotti, Frank Rijkaard, Ruud Gulitt, Marco Van Basten na Roberto Donadoni na hatimae Milan kutinga fainali.

kama hio haitoshi May/24/1989 milango ya saa mbili na robo usiku ktk dimba la Camp Nou ambapo mashuhuda wapatao 97,000 walishuhudia Milan wakiifunga Steau Bucharesti kwa jumla ya magoli 4-0 magoli yaliowekwa kimiani na Ruud Gullit aliefunga 2 na Marco Van Basten alietupia goli mbili pia na kuchukua tuzo ya mfungaji bora akiwa na jumla ya magoli 10.

eti watu wanajisahaulisha hayo pamoja na kujitoa akili kabisaa na kuishi bila kukumbuka kuwa hata msimu uliofuata baada ya hapo ilikuwa ni AC Milan pia iliobeba ndoo hio na rekodi hio hakuna alieweka mpaka sasa.

hivi leo hii nani hajui kuwa Milan ilitengeneza timu bora ambayo haitakuja kutokea ktk historia ya Soka?

hivi ni strikers gani wangeweza kupita beki imara ilioongozwa na Franco Baresi huku akisaidiwa na Alesandro Billy Costacurta, Paolo Maldini na Mauro Tasotti?

hivi ni nani alietimamu ambae anaweza kusahau kipigo cha Mbwa koko ndani ya uzio walichokipata Barcelona iliowahi kuwa bora kuliko Barcelona yoyote ile katika mechi ya fainali ya ligi hiohio ya mabingwa mwaka 1994?

kama mnajisaulisha well naomba kesho muanze kuvaa suruali kisha juu mvae chupi. ila mimi nawakumbusha kuwa Milan waliwasasambua Barca jumla ya goli 4-0 goli zilizopachikwa na Savicevic, Daniele Masaro, Roberto Donadoni na mkoba Marcel Desailly ktk mechi iliopigwa tarehe 18/04/1994 ktk dimba la Olimpico hapo Athens jumla ya watazamaji 70000 walishuhudia Pep Guardiola na Romalio wakishindwa kugusa mpira takriban dakika 30 za mwisho.

cha kuchekesha zaidi Milan walicheza bila top striker Van basten wala nahodha Franco Baresi na bila mchezaji ghali duniani kwa wakati huo yaani Gianluigi Lentini...hivi ni kipi Milan wafanye ili muwashimu?

je mlikuwa wadogo kipindi George Wear anatwaa tuzo ya mwanasoka bora wa Dunia, Ulaya na Africa? je hamkumbuki alikuwa striker wa timu gani?

hivi kweli mnajisahaulisha ukuta bora kwa karne hii umeundwa na Dida, Cafu, Maldini, Stam na Nesta?

niwaweke kundi gani kama mnashindwa kuheshimu triple R toka Brazil yaani Rivaldo, Ronaldo na Ronaldinho kuwa wote walicheza Milan?

sawa Seedorf, Rui Costa, Boban na Pirlo hamuwaheshimu, basi hata Redondo?

eti mtu alieitwa Super pipo hamumtambui, je Mtakatifu Baggio nae? au mnataka Mbwana Samatta acheze Milan ndio muiheshimu?

Bayern walishapigwa goli 4 Sansiro wakaonekana hawajui, je nani asiekumbuka kuwa washabiki wa Man UTD waligoma kurudia kuangalia kipindi cha pili baada ya wachezaji wao kuusaka mpira takriban dakika 45 za mwanzo huku Gatusso akibweka na kumficha Christiano?

kama hayo hayatoshi basi nikupe habari toka Mbinguni. huko mbinguni wanaamini kuwa kila mshabiki wa Soka ni mshabiki wa AC Milan.
MARK AND BIND IT.

Gang Chomba
umeongea kiunaz sana ila uju hao kina van basten wangekutana na barca ya messi wangepigwa 9-0
 
Milan watarudi tu. Mm mdau wa serie a naumia sana kuiona milan ikiwa vile. Ila soon itarudi na europe tutaishika tu. Forza juventus.
 
mi sio mpenzi wa AC Milan ila barca anayoizungumzia hapo unaijua lakini mkuu??
nimuelewa mkuu,yeye anaamin hiyo ac milan ya kipindi hicho ndo timu bora kuwah kutokea katika ulimwengu wa soka nami nimemjibu hiyo 9-0 ni mfano tu,na maana hicho kizaz cha kina van basten si lolote kwa hii barca ya kizaz hiki
 
nimuelewa mkuu,yeye anaamin hiyo ac milan ya kipindi hicho ndo timu bora kuwah kutokea katika ulimwengu wa soka nami nimemjibu hiyo 9-0 ni mfano tu,na maana hicho kizaz cha kina van basten si lolote kwa hii barca ya kizaz hiki
HAPANA hujanielewa, nachokuuliiza je unaifaham hiyo barca iliyopigwa 4-0 ilikua ni barca ya namna gani???
kwa taarifa yako tu ni kuwa hiyo barca ya kipindi hicho ndio ilikuwa inaitwa The dream Team ambayo ilichukua ubingwa wa ligi ya hispania mara nne mfululuzo, Ilikua ni Balaa

kuna midahalo inaendelea kuwa ni kipi kikos bora kati ya Barcelona ya 1991-94 ya Johan cruyff, kikosi cha Guardiola 2008 - 2011 na hiki cha Luis Enrique cha sasa..

kwa hiyo kama unaijua hiyo Barca basi unaweza kuimagin hiyo AC Milan ilikuwaje
 
Hakuna kikosi bora Milele kila Timu na zama zake ukizungumzia UEFA Madrid ndio miamba na makombe 10 ukizungumzia makombe mengi kama Klabu Barcelona ndio wanaongoza kifupi zama za ligi ya serie A kua juu zimepita na kwa sasa La Liga ndio ligi bora
 
HAPANA hujanielewa, nachokuuliiza je unaifaham hiyo barca iliyopigwa 4-0 ilikua ni barca ya namna gani???
kwa taarifa yako tu ni kuwa hiyo barca ya kipindi hicho ndio ilikuwa inaitwa The dream Team ambayo ilichukua ubingwa wa ligi ya hispania mara nne mfululuzo, Ilikua ni Balaa

kuna midahalo inaendelea kuwa ni kipi kikos bora kati ya Barcelona ya 1991-94 ya Johan cruyff, kikosi cha Guardiola 2008 - 2011 na hiki cha Luis Enrique cha sasa..

kwa hiyo kama unaijua hiyo Barca basi unaweza kuimagin hiyo AC Milan ilikuwaje
hiyo dream team iliyopigwa 4 ilikuwa haina lolote ukilinganisha na barca ya kizaz kipya,kwanza huo ubingwa mara 4 mfululizo iliopata ilitegemea sana bahati ndo mana mara 3 kati ya hizo walimalizamechi za mwisho wakitegemea wapinzani wao wapoteze na bahati ikawa kwao,
tukirudi kwa hiyo milan ndio ilikuwa bora, lakini mpira wao ulikuwa nguvu nyingi tu ufundi kidogo lakini barca hii naipa credit sababu they have taken football back to its root mi naamin hata hivyo vizaz bora vilivyopita vya milan na barca wanafurah kuitazama barca hii kizaz hiki cha kina iniesta ndo haswa kinaujua mchezo wa soka kuliko timu zingine zozote zile zilizolowahi kutawala dunian
 
Frank Wanjiru Gang Chomba mnaonekana mmefurahi sana ila huyu mleta mada hamnazo HIVI UNAIZUNGUMZIA ACMILAN ILIYOPIGWA 4 NA SOSUOLO ha ha ha ha mna miaka mingap uefa hamjashiriki hiv uefa mmechukua mara ngap??
alafu mleta mada BARCELONA usiifananishe na milan yani ww unazungumzia goli 4 umesahau milan tushampiga 5 pale camp nou SS NDIO BARCELONA MABINGWA Aleyn kiboko ya timu zote kubwa duniani
 
Sitaki niumize vidole vyangu Ac Milan ni sawa na akina liverpool na barca klabu boora milele ni Real Madrid UCL mara 10 wkt Milan mara 5, hii haiitaji elimu na ujuzi kujua ipi ni bora.
mkuu tutake radhi BARCELONA huwez ifananisha na milan wala na liverfool pia huwez ifananishwa na timu kila msimu inabadil kocha KIUFUP BARCELONA HAIFANANISHWI NA TIMU YEYOTE ILE DUNIANI VIVA WAZEE WA TREBO
 
Siwataki radhi kwani tunachotazama ni makombe mangapi makubwa mmeshinda hivyo hata iweje hamuwezi karibia mafanikio ya Real Madrid na sio nyinyi tu hata nyingine yoyote km ipo duniani haikaribii RM.
 
Siwataki radhi kwani tunachotazama ni makombe mangapi makubwa mmeshinda hivyo hata iweje hamuwezi karibia mafanikio ya Real Madrid na sio nyinyi tu hata nyingine yoyote km ipo duniani haikaribii RM.
ingekuwa ni ngumu BARCA kuchukua UEFA kipind hiko sababu hata ww ulukuwa hujazaliwa pia jua kuwa klabu yenye mafanikio kupita zote duniani ni FC BARCELONA
 
HAPANA hujanielewa, nachokuuliiza je unaifaham hiyo barca iliyopigwa 4-0 ilikua ni barca ya namna gani???
kwa taarifa yako tu ni kuwa hiyo barca ya kipindi hicho ndio ilikuwa inaitwa The dream Team ambayo ilichukua ubingwa wa ligi ya hispania mara nne mfululuzo, Ilikua ni Balaa

kuna midahalo inaendelea kuwa ni kipi kikos bora kati ya Barcelona ya 1991-94 ya Johan cruyff, kikosi cha Guardiola 2008 - 2011 na hiki cha Luis Enrique cha sasa..

kwa hiyo kama unaijua hiyo Barca basi unaweza kuimagin hiyo AC Milan ilikuwaje
Mimi kukuelewa nilikuelewa ijapokuwa hujaniquote mimi ila niseme tu kuwa hiyi Milan ingekutana na ile Barca ambayo ilimpiga Man U 2-0 pale france, ingeweza kumtandika huyo Milan hata hizo bao 9.
Kuna kitu kimoja kwa Barca, Barca hana tabia ya kukamia kukufunga nyingi, isipokuwa anataka tu akusumbue uwanjani kwa style yake achezayo. Kungekuwa na uwezekana hiyo squad ya Milan ikarudishwa na kukutana na Barca ya 2016 kila timu ktk ubora wake basi dunia nzima tungeandamana kuwa Barca amekiuka haki za kimpira kwa kuidharirisha Milan.
 
Hakuna Joshua bora Milele kila Timu na zama zake ukizungumzia UEFA Madrid ndio miamba na makombe 10 ukizungumzia makombe mengi kama Klabu Barcelona ndio wanaongoza kifupi zama za ligi ya serie A kua juu zimepita na kwa sasa La Liga ndio ligi bora
Jamaa ni mgumu kukubali ukweli, anachojisifia yeye ni Historia, hajasema anguko lao ni lipi utadhani anafurahia vile au hajui chanzo cha timu yake kushuka.
 
hiyo dream team iliyopigwa 4 ilikuwa haina lolote ukilinganisha na barca ya kizaz kipya,kwanza huo ubingwa mara 4 mfululizo iliopata ilitegemea sana bahati ndo mana mara 3 kati ya hizo walimalizamechi za mwisho wakitegemea wapinzani wao wapoteze na bahati ikawa kwao,
tukirudi kwa hiyo milan ndio ilikuwa bora, lakini mpira wao ulikuwa nguvu nyingi tu ufundi kidogo lakini barca hii naipa credit sababu they have taken football back to its root mi naamin hata hivyo vizaz bora vilivyopita vya milan na barca wanafurah kuitazama barca hii kizaz hiki cha kina iniesta ndo haswa kinaujua mchezo wa soka kuliko timu zingine zozote zile zilizolowahi kutawala dunian
Tena hii Barca ya Luis Enrique kidoogoooo imepoteza kale karadha na hii imechangiwa na mambo kadhaa!
1. Xavi Kustaafu na kipindi cha nyuma kidogo alikuwa hapati namba baada ya ujio ya Ivan Rakitic
2. Messi kurudi ktk main position yake, yaani Winga ya kulia, kumbuka Messi alikuwa akichezaga kama 9 na alikuwa akichukua sana mipira kati na kupeleka mbele. Akiwa anarudi pale kati kulikuwa na burudani tosha kabisa akiwa na mafundi wa tik taka akina Iniesta, Sergio Busquets na Xavi Hernandez
 
Back
Top Bottom