Home Shopping Centre wazusha taharuki Kariakoo

Home Shopping Centre wazusha taharuki Kariakoo

maishapopote

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2009
Posts
3,408
Reaction score
6,094
Wadau,kuna habari za uhakika chini kutoka kwa wadau wangu wa karibu kuwa hali ya mfanyabiashara said wa home shopping center si nzuri kibiashara...
kama thread moja iliyowahi kuandika habari zake humu ndani,inasemekana zaidi ya makontena 860 yamezuiwa bandarini kwa kile kinachoelezwa kufanya uchunguzi zaidi,mengi ya makontena haya yamewekwa bidhaa nyingine huku documents zikionyesha bidhaa nyingine.

hv karibuni amekuwa na ugomvi na mfanyabiashara mwingine Said salim bakhresa,na pia ameshagombana na Manji na yule muhindi mwingine tajiri zakaria,pia amekorofishana na subhashi Patel pale alipoanza kuingilia biashara ya mabati yanayofanana na ya kiwanda cha subash.

kuna wachina kama mia mbili hv nao mizigo yao iko kwenye hiyo ya huyu bwana so sad,kumbe na wao wanakwepa kodi

ukwepaji kodi huu wa Said,unajulikana wazi na kila mtu,hata serikalini,sijafahamu hasa kwann this time wameamua kumgeuka mwenzao! labda ndio yale maneno ya magufuli kuwa anaeweza kumtoa ni rais tu,maana huyu jamaa keshahamisha maafisa wa tra kama mia na hv!

my take:crime doesn't pay
 
Tetesi zainasema kuwa Home Shopping Centre ni mali ya mkuu wa kaya (tz) na ndio sababu mara nyingi makontena yake yamekuwa yakipita bandarini bila kutozwa ushuru wakati watanzania wa hali ya chini ambao wamempa dhamana wanaumizwa kwa kucheleweshewa mizigo yao bandarini kisa hakuna hela hazina.
Tetesi zinaendelea kusema kuwa hivi sasa kuna container zipatazo 30 bandarini zilizofojiwa detail kuwa zina vyandarua na kumbe sio. na badala yake zimegudnulika kuwa zina vitenge. (no wonder they are the cheapest shopping centre in TZ)
Ingawa sisuport fujo za Mtwara lakini tafakarini kama wananchi wa tanzania wanaojulikana ni waoga au niseme (waerevu wa kijinga) leo wanadhubutu kupambana na polisi kweli ni kwasababu ya Gas tu. Wananchi wamesikia mengi wamechoka na wamechoka sasa.

Naomba mwenye detail zaidi juu ya hili ambalo linasememkana lina uhusiano mkubwa na kikao cha leo wizara ya fedha atuhabarishe zaidi.
 
Hapa kuna issue nyeti...itaiva siku siyo nyingi. Hayo ya HSC na Ikulu yamesemwa mara nyingi sana, hata gazeti moja, bila shaka ni Mwanahalisi ilishaandika sana jinsi kampuni hii ilivyo na uhusiano wa karibu na Mama Salma na Riz...na jamaa huwa wanaingia Ikulu kama kwao na hakuwa wa kuwahoji..
- na huwa ma-container yao huwa hayaruhusiwi kuguswa na wakaguzi wa pale bandarini. na pia kuna wafanyabiashara wa mikoani walishakubali kusafirishiwa bidhaa zao kwa bei chee kupitia kampuni ya HSC ya clearing na Forwarding then bidhaa zao zilipofika Dar, huwa hawapewi BL na vibali vingine halisi, kwa kuwa hawakuwa na vibali toka kwa HSC waliishia kupoteza bidhaa zao kwa kukamatwa na ndio walikasirika na kupasua majipu na uozo wa hawa jamaa...wanaenda ikulu kila mara ndio wanaenda kujadili deals.
- Kkoo wameotesha nyumba kama upepo...mojawapo ni jumba linalotazamana na Ben Mkapa Sec
- wanamiliki Benki (Amana Bank) na wanafanya kila biashara sasa...!
 
Kwa machache ninayo jua mimi....home shopping center ni mmiliki wa silent ocean,inayosafirisha mizigo kutoka nchini china pamoja na dubai kwa bei ya kutupa,inafikia hatua mpk wewe uneenda kutuma mizgo yako ama kontena lako huendi tena tra kushughulikia kontena lako bali unaenda chukua mzgo wako warehouse,na kama utahofia kusumbuliwa na police wana magari yao ya HSC yanakuletea mzgo wako mpaka mlangoni kwako,wakwepa ushuru wengi na masikini wanaitumia sana kampuni hii.

HSC ndiyo wanaoingiza hapa nchini cement ya lucky toka pakistan kwa kibari maalumu,wao na mwenzao mmoja mwenye kiwanda cha mafuta na mifuko mbagala.

HSC ndiyo waliopanga lile jengo lilikuwa nikitumiwa na tra pale samora enzi hizo na hapo kuna office zao za silent ocean.

kwa leo ni hayo tu,siku hizi humu watu tunatoa infor za watu afu usalama wanazitumia kujipatia kipato sababu issue nyingi zinakuwa ni 100%.

NOTE: Kampuni hii imesaidia masikini wengi kuwa matajiri nchini,pamoja na kukwepa kwake kodi ila inarudisha kwa jamii kwa style ya kutoa misaada.kazi kwako kuihukumu ama kuisupport
 
No researched data, no right to tarnish, dig deep and come out with tangible evidence.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.

Aloyaandika ndivyo ilivyo na kwa sasa HSC wapo kwenye kaa la moto la TRA, mizigo yao mingi imekuwa 100% verification kwani kampuni za CLEARING FORWARDING AGENT(LONDON FREIGHT) zimekuwa suspended kutokana na ukwepaji kodi.Hao walikuwa wanatoa mizigo mingi ya wafanyabiahara Kariakoo na huwa walikuwa hawapewi listi.Fanya tafiti juu ya hilo.
 
No researched data, no right to tarnish, dig deep and come out with tangible evidence.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.

Mkuu Mtoi ndivyo ilivyo hali ni mbaya bandarini baada ya container za HSC kukamatwa zikiwa wame declare
vyandarua na wayamesh wakati ndani kuna vitenge na makapeti,hata saa hii kuna mkutano kati ya waziri wa
fedha Mgimwa na madirector wa makampuni ya Clearing and forwarding kinaendelea kwenye ofisi za wizara ya
fedha.Na document zao zilikuwa zinapigwa direct Release zote hazikuwa zinakaguliwa,baada ya ofisa mmoja wa
TRA kushtuka akaamua kukagua ndio balaa lilipoanzia na container zao nyingi zimekuwa seized bandarini,na
kumekuwa na shinikizo toka kwa wakubwa serikalini kwamba container ziachiliwe,lakini hongera kwa commissioner
wa customs ndugu Masamaki amewagomea kuzitoa.Issue ndio kwanza iko hot'
 
kwa kifup tu hawa jamaa mimi nimefanya nao kaz tangu mwaka 2007 wananisafirishia mizigo yangu toka china na dubai. ukwel kama alivyosema jamaa mmoja hapo juu ni kwamba kwa kias flan wanawasaidia Wtz masikin kupata hela na matajir pia ila njia anazotumia kuwapa utajir ni kwa kukwepa kodi kwa kusaidiana na baadhi ya watumish wa TRA wale wakubwa. wakat huo yeye kwa kuwaweka watu kati huko juu anapiga hela nyingi mno yaan unaibiwa mwenye mzigo na serikali hasa serikal. conteiner la nguo ni TshsMilion 17 kwa futi 20 lakn yeye anakuambia ni milion 19 au 20 lakn unatolewa on the sport ikifika. so kinachojitokeza serikalin wanabadilisha document wakishirikiana na watu wa TRA conteiner la nguo linabadilishwa linakuwa la cement so analipia milion 5 mpaka 7 za juu anawapa kidogo watumish nyingine zake. huu mchezo ameuanza cku akisaidiwa na Zakhia Megi kipindi akiwa wazir wa fedha. walichofanya wamemuuzia Riz 0ne hisa so wanaiba hela nyingi ni Mungu anajua. ingawaje ukwel mwingine mchungu ni kwamba kampun yake ndio inasuply karibu mizigo yote kkoo na posta so kumfungia ni kusababisha ombwe la mizigo sokon na pesa kupungua serikaln ushahd ni juz mwakiembe kakamata conteiner zake mia moja leo hii wamezuiliwa kutoa mizigo wk hiz mbili tu tayar imebid wazir wa fedha awaite wafanyabiashara aongee nao tatizo liko wapi. coz hazina haisomeki. na kwa kuwatonya nasikia hata mtoto wa mshua wakat anakamatwa china kama ni kweli hawa jamaa ofic yao ya china ndio iliratibu mazungumzo ya kuachiwa kwao.
 
Ndoto ya mchana hiyo. Huna watu , huna wapiga kura utaiondoaje CCM. Unawapiga debe tu ndani ya JF wanaotumia PC za Shemeji zao.
 
Wonders shall never end in Tanzania. Mwezi wa kumi na mbili 2012 nilikuwa China kwenye jimbo la Guangzhou nilibahatika kufika katika ofisi ya HSC katik jimbo hilo. Ukweli mambo yanayoendelea pale ndo utajua Tanzania ni nchi ya viongozi mazuzu! Mtu anapeleka container pale amepakia vitu tofauti lakini wale jamaa wanadiklea vitu fotauti. Mfano, jamaa alikuwa na container 40 ft la vifaa vya umeme na decorations za nyumba. Wale HSC wakamwambia yeye atapokea mzigo wake katika yard yao Dar es salaam na kulipia siku hiyo ya kuondoka na mzigo. Wakamuuliza yule jamaa anachotaka ni kupokea mzigo au ni kusoma kwenye karatasi nini kimeandikwa! Wao wanajua mzigo utapita wapi, kwa nani, kwa bei gani hadi kwenye yard. Jaama alilipia chini ya nusu ya bei ya kawaida kwani alishaingiza mzigo km huo miezi kama 3 kabla ya tukio hilo. Hii ndo Tanzania.
 
HSC wanakampuni kibao za Clearing bandarini pale, wafanyabiashara wanalazimika kuwatumia hawa jamaa kutokana na kuwa na mkono TRA na wakubwa wa wizara ya fedha.

Ukijifanya unatumia kampuni nyingine kwa wafanyabiashara wa nguo, viatu, pazia na vinginevyo utapigwa ushuru wa kufa mtu. Ila ukitumia HSC container la nguo au kitenge unalipa mil.28 tunaambiwa jamaa yeye anacheza na wakubwa wa TRA anasema container lina Tooth pick au toilet paper yeye analipa TRA mil.7 dah kumbe zigo linathamani ya dola 170,000/= ishu ya Mwakyembe kuanza kukagua container imeanza kumuumbua bwana HSC na wakubwa wa TRA imesababisha taharuki kwa wafanya biashara k.koo mizigo imezuiliwa na biashara imesimama.

Serikali imepoteza sana mapato juu ya hawa jamaa HSC wanakula pia na polisi wanasindikiza toilet paper kumbe nguo au vitenge au tv au friji.
 
Unganisheni dot msaada wa wahanga wa mafuriko.
 
Tanzania ku win lazima ufanye mazabe zabe,kuna uzi ulishaletwa hapa jf juu ya ufisadi huo,ila vyombo vya dola vinaingalia cdm tuu
 
Tanzania ku win lazima ufanye mazabe zabe

Mizigo ya wafanyabiashara imezuiwa HSC waliandika vitu tofauti na vilivyomo nguo zinaandikwa Tissues au toilet paper sasa Mwakyembe kashtukia dili hilo amewakwamisha wafanya biashara na HSC huwa anatumia Canter zake kusambaza mzigo.
 
Hao jamaa Dar wanauza vitu kwa bei chee lakini nje ya Dar wanauza bei ghali kufidia hasara.
 
Back
Top Bottom