Hongera CP Hamduni Salum kwa kumpigia simu Elioth Lyimo na kuagiza maafisa wa TAKUKURU mkoani Kilimanjaro wafungue jalada la uchunguzi

Hongera CP Hamduni Salum kwa kumpigia simu Elioth Lyimo na kuagiza maafisa wa TAKUKURU mkoani Kilimanjaro wafungue jalada la uchunguzi

Napenda kutumia fursa hii kumpongeza kwa dhati Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, CP Salum Hamduni kwa kumpigia simu mzee Lyimo na kuagiza maafisa wa TAKUKURU mkoani Kilimanjaro wafungue jalada la uchunguzi.

Mzee Lyimo ni mfanyabiashara ambaye aliporwa TZS 25M na aliyekua Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya. Inaelezwa kuwa Sabaya alikua na desturi ya kufuatilia akaunti za wafanyabiashara wakubwa na kujua kiasi walichonacho bank.

Baada ya kufuatilia akaunti ya mzee Lyimo na kujiridhisha kuwa ana "mzigo wa kutosha" bank, alimvamia nyumbani kwake akiwa na mabaunsa, pamoja na askari polisi wa kituo cha polisi Bomang'ombe. Askari hao walibaki nje ya geti wakiwa kwenye gari. Inadaiwa Sabaya aliambatana na Juma Rahibu ambaye kwa sasa ni Meya wa Moshi.

Waliingia ndani wakiwa na mabegi mawili. Walitoa silaha na kuwaweka chini ya ulinzi familia nzima. Kisha wakamchukua mzee Lyimo na kuzungumza nae. Sabaya akamwambia "nahitaji 25M sasa hivi, ama nikukabidhi haya mabegi yawe yako"

Akafungua kumuonesha begi moja lina bangi na jingine lina mirungi. Mzee Lyimo akaona anatengenezewa kesi ya madawa ya kulevya ambayo haina dhamana. Na ukizingatia umri wake anaweza kufia gerezani. Basi akakubali kutoa kiasi hicho cha pesa.

Sabaya akaagiza polisi waliokua nje na "difenda" wamsindikize bank, ambapo alienda kutoa kiasi hicho cha pesa na kuja kumkabidhi Sabaya. Matukio yote yalirekodiwa kwenye CCTV za nyumbani kwa mzee Lyimo lakini Sabaya wala hakujali. Alijua mamlaka inayomlinda ni kubwa sana.

Hata hivyo mzee Lyimo hakuridhika na akaamua kutafuta haki yake kimyakimya. Akaenda kuripoti TAKUKURU lakini hawakumsaidia, akaripoti polisi hawakumsaidia. Baadae akamwambia Godbless E.J. Lema ambaye alilifikisha kwa Waziri mkuu lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa.

Sasa baada ya Sabaya kukamatwa, Lema akaamua kuandika tweet ya kukumbushia haki ya mzee Lyimo. Baada ya kuona tweet hiyo mamlaka zimeanza kuchukua hatua. CP Hamduni amempigia simu mzee Lyimo na tayari TAKUKURU Kilimanjaro wameshafungua jalada. Hongera sana Hamduni, naamini mzee Lyimo atapata haki yake.

View attachment 1818470
Hakuna utendaji kazi wa hivo mkuu acheni siasa za hivo malalamiko huwa yanawakilishwa kwenye ofisi husika ofisi hazipo daresalaam tu hata mikoan kama alikuwa mfanyabiashara hawezi kushindwa kuwasilisha malalamiko yake kwenye vyombo husika siyo habari za kwenye tweeter za lema acheni chuki zisizo na msingi na cp hamd na amini hawezi fanya upumbavu wa na namna hiyo, mtoa taarifa kupitia tweeter yupo ukimbizini anaandika namba za simu za mlengwa na maana mlengwa mwenyewe hawez fikisha malalamiko yake sehemu husika; hizo biashara yeye anazifanyaje kama anaweza shindwa kufanya hayo hadi awatumie wanasiasa uchwara
 
Ndiyo maana kuna mtu kule tweeter hamkubali kabisa mzee wa kusini, ni mnafiki na mbinafsi sana, aliona watu wa hai hawamhusu shame
 
Sabaya alikuwa Ni jambazi, ila magufuli aisee,ona hata waziri mkuu alipelekewa malalamiko juu ya Sabaya,lakini akashindwa kuyafikisha kwa jiwe,aliogopa nayeye asije akapigwa chini,maana Magufuli watu dizaini ya Sabaya na matendo yao,yeye ndio alikuwa chaguo lake
Halafu watu kama Mwendazake huwa hawakosi makanisani...na viongozi wa dini walikuwa wanamkubali sana , Duh dunia hii
 
Bank inakuwaje kutoa taarifa za mgonjwa! Maajabu hayajakwisha Tz

Nadhani ulitaka kuandika mteja.Ilifika mahali wafanyabiashara waliamua kuweka fedha majumbani Bank hapakuwa sehemu salama.
 
Former Hai District Commissioner Lengai Ole Sabaya will on Friday appear in court for the second time to answer to six charges facing him.
However, the Tanzania Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) in Kilimanjaro Region says it is investigating seven other accusations facing him.
The new charges come after prominent businessman Elioth Lyimo lodged complaints to PCCB’s Director General Salim Hamduni.
Mr Hamduni told The Citizen over the phone that he had already sent his men to investigate the businessman’s claim of being robbed of Sh25 million by Sabaya.
Apart from that, the head of PCCB in the region, Ms Frida Wikesi, spoke of seven other accusations facing Sabaya and that they have already launched investigations.
Ms Wikesi said there were some people who were mentioned to have been accomplices of Sabaya in committing crime in the region including Moshi Municipal Mayor Juma Raibu, who is also under investigation and that if proved he was involved in the crime he would also be arraigned.
“As you heard, there are various unearthed accusations facing former Hai District Commissioner Lengai Ole Sabaya.
“Investigations into his accusations are ongoing in Kilimanjaro Region and when completed and proved to be true he will be taken to court for justice to take its own course,” said Ms Wikesi.
According to her, investigations against all those, who have been mentioned to cooperate with Sabaya to commit crime in the region, are ongoing so that justice can be done for the victims.
“It is true His Lord Mayor of Moshi Municipality, Juma Raibu, has also been mentioned. Investigations into the accusations facing him are ongoing and if he is proved to be involved, then he will be taken to court to answer to the charges facing him,” said Ms Wikesi.
Speaking about the businessman, the PCCB regional boss admitted that he had gone to her office and queried over the matter and that evidence about the complaints was still being collected by the Bureau’s officers.
“We have already taken statements from this businessman and evidence is still being collected as investigations will reveal the truth of the matter,” insisted Mr Wikesi.
When sought, the businessman admitted to having been robbed of his cash by Sabaya and that he had already submmited all of his exhibits to PCCB including his bank statement showing he withdrew the money on February 2, 2020.
“It is true Sabaya took my money totalling Sh25 milioni as I have my bank documents that show transactions took place on February 2, 2020 and I have already presented my bank slips to PCCB. For now I can’t talk anything because all the information about how the incident took place I have already handed it over to PCCB,” said Mr Lyimo
On June 4, this year, Sabaya and his five accomplices were for the first time appeared before the Arusha Resident Magistrate’s Court where six charges were read out against them before the court’s two different magistrates.
The charges, which included armed robbery, money laundering, economic sabotage and seeking and receiving bribe, are unbailable.
Credits: The Citizen
 
Kwann hao maaskari na OCD wa Hai wasiongezwe kwenye kesi kama hawakuwa wanagawana waliruhusu vipi sabaya atambe kwa uhalifu
 
Hivi ina maana huko PCCB hakuna aliyekuwa analijua hili? shame!!!SSH tuletee wazenj zaidi huku haya mengine ya huku bara ni majizi na manafiki tu.
Aisee kweli bora tuongozwe na wazenji wana hofu ya mungu kweli kweli uku kwetu bara wasanii wengi make hayo ya sabaya tu je na hao wengine tu tumeumia sana ndo mana mungu katuokoa
 
Mungu amjaalie mama na watumishi wake akiwemo kamanda Hamduni.
 
Hakuna utendaji kazi wa hivo mkuu acheni siasa za hivo malalamiko huwa yanawakilishwa kwenye ofisi husika ofisi hazipo daresalaam tu hata mikoan kama alikuwa mfanyabiashara hawezi kushindwa kuwasilisha malalamiko yake kwenye vyombo husika siyo habari za kwenye tweeter za lema acheni chuki zisizo na msingi na cp hamd na amini hawezi fanya upumbavu wa na namna hiyo, mtoa taarifa kupitia tweeter yupo ukimbizini anaandika namba za simu za mlengwa na maana mlengwa mwenyewe hawez fikisha malalamiko yake sehemu husika; hizo biashara yeye anazifanyaje kama anaweza shindwa kufanya hayo hadi awatumie wanasiasa uchwara
Screenshot_20210616-235341.png


Soma hapo mkuu CP Hamduni mwenyewe anasema kuna vyanzo vingi na yeye alitoa habari mtandaoni
 
TAKUKURU imesema inachunguza tuhuma nyingine saba zinazomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ikiwemo ya kuchukua TZS milioni 25 za mfanyabiashara Elioth Lyimo.

Aidha, taasisi hiyo inawachunguza wanaodaiwa kushirikiana naye akiwemo Meya wa Moshi, Juma Raibu.

Sources:

 
Juma raibu umefata mkumbo ndugu yangu sasa inaenda kula kwako mazima.
 
Juma raibu umefata mkumbo ndugu yangu sasa inaenda kula kwako mazima.

Juma Raibu ni ndugu yake na Diwani wa Sombetini Mh Bakari ambaye alikumbana na kipigo cha Sabaya.
 
Hakuna utendaji kazi wa hivo mkuu acheni siasa za hivo malalamiko huwa yanawakilishwa kwenye ofisi husika ofisi hazipo daresalaam tu hata mikoan kama alikuwa mfanyabiashara hawezi kushindwa kuwasilisha malalamiko yake kwenye vyombo husika siyo habari za kwenye tweeter za lema acheni chuki zisizo na msingi na cp hamd na amini hawezi fanya upumbavu wa na namna hiyo, mtoa taarifa kupitia tweeter yupo ukimbizini anaandika namba za simu za mlengwa na maana mlengwa mwenyewe hawez fikisha malalamiko yake sehemu husika; hizo biashara yeye anazifanyaje kama anaweza shindwa kufanya hayo hadi awatumie wanasiasa uchwara

Kwahiyo unabisha na taarifa rasmi ya PCCB au umeamua kujitoa ufahamu !.
 
Haya ni mambo ya Hovyo sana kwa Mtumishi wa Umma kutajwa nayo.
Nasikitika vyombo vya usalama vipo kimya kabisaa kuthibitisha hili kwa umma maana inasemekana alitumia
1. Jeshi la polisi na vifaa vyao
2. Alilipotiwa polisi na mzee lyimo inamaana kuna jalada, halafu wamepiga kimya KUTHIBISHA au KUKANUSHA
3. Aliwasilisha TAKUKURU mkoa napo hakuna andiko la lalamiko lake

Mwisho Inatumika TWEET ya Lema kama Ushhidi na Kamishna Takukuru kupiga simu

Inamaana serklini kooote hakuna alama?

Aibu ya Kitaifa hii
 
Back
Top Bottom