Zanzibar 2020 Hongera Dkt. Mwinyi panapo nia utaitibu Zanzibar

Zanzibar 2020 Hongera Dkt. Mwinyi panapo nia utaitibu Zanzibar

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana pana taarifa za upepo mwema kuanza kuvuma kule pande za Zanzibar.

Tulikotoka, tulikopita na tulipo kote kunafahamika. Kwamba uchaguzi ule ulikuwa na mzengwe usiofaa kurejewa? Hata mtoto mdogo anajua.

Kwa bahati mbaya pana watu wameumia na hata wengine kupoteza maisha kwenye harakati hizi huko Zanzibar.

Kwa hakika hao wote hawakuumia wala kupotea bure. Wote hao ni muhimu kuwepo katika hadidu rejea za maridhiano.

Pana nafasi kubwa ya Dk. Mwinyi katika maridhiano ya namna hii kujiweka katika nafasi muafaka ya kukubalika zaidi kote visiwani na hata bara iwapo tu atatanguliza haki mbele.

Amani Karume kupitia maridhiano aliiacha Zanzibar ikiwa moja na yeye kuweza kukubalika zaidi kama kiongozi aliyekuwa mwenye busara haswa.

Mwinyi kuridhiana na upinzani na hata ikibidi kuendesha uchaguzi mpya utakaokuwa huru, wa haki na wenye kuaminika hakutampunguzia lolote. Zaidi ya kuwa kwa matokeo yeyote yale, yeye ndiye atakayekuwa mshindi.

Mwinyi anaweza hata kushinda tena na sasa ikiwa katika uchaguzi utakaokuwa wenye uwazi unaokubalika.

Wamepata zawadi za nobeli kwenye jitihada kama hizi wengi. Baadhi yao ni kina De Clerk na kina Mandela. Kina Aung San Suu Kyi, na wengine wengi.

Mwinyi sasa hivi ndiye rais. Mustakabala mwema wa wanzibari upo mikononi mwake zaidi kuliko mtu mwingine yeyote.

Aungwe mkono Mwinyi na wapenda amani wote ili kumwezesha kufanya maamuzi hata kama yatakuwa magumu mno kwa mustakabala mwema wa watu wa Zanzibar.

"Shime Dk. Mwinyi historia iko upande wako kuitendea mema nchi hii."

Walisema waungwana mwanzo wa ngoma ni lele na mwanzo wa safari ndefu ni ile hatua ya kwanza.
 
Hata sijui umempa hongera ya nini? Aliyesema kujitekenya na kucheka hakukosea!

Mwinyi anatawala hilo koloni kwa niaba ya walioko Dodoma. Hawezi badilisha chochote. 2015 Shein alikuwa amekwisha kubali kushindwa. Walioko Dodoma wakamlazimisha kuendelea kuwa Rais.
Mabibi na mabwana pana taarifa za upepo mwema kuanza kuvuma kule pande za Zanzibar.

Tulikotoka, tulikopita na tulipo kote kunafahamika. Kwamba uchaguzi ule ulikuwa na mzengwe usiofaa kurejewa? Hata mtoto mdogo anajua...
 
Hata sijui umempa hongera ya nini? Aliyesema kujitekenya na kucheka hakukosea!

Mwinyi anatawala hilo koloni kwa niaba ya walioko Dodoma. Hawezi badilisha chochote. 2015 Shein alikuwa amekwisha kubali kushindwa. Walioko Dodoma wakamlazimisha kuendelea kuwa Rais.

Paragraph hii hapa inajibu hoja yako mkuu:

"Mwinyi sasa hivi ndiye rais. Mustakabala mwema wa wanzibari upo mikononi mwake zaidi kuliko mtu mwingine yeyote."

Benefit of doubt, sasa hivi yeye ndiye mwenye mamlaka hata ya kupiga "ajua" uchaguzi mzima ikibidi.

Maridhiano yapi kama si kurudia uchaguzi katika mazingira yanayokubalika?
 
Your are just hypothetical. All decisons are made in Dodoma. He is just a puppet. He can change nothing. All power is with Magufuli. Akileta fyoko, Kamati Kuu ya CCM inamwondoa kabla jua halijachomoza.
Paragraph hii hapa inajibu hoja yako mkuu:

"Mwinyi sasa hivi ndiye rais. Mustakabala mwema wa wanzibari upo mikononi mwake zaidi kuliko mtu mwingine yeyote."....
 
Paragraph hii hapa inajibu hoja yako mkuu:

"Mwinyi sasa hivi ndiye rais. Mustakabala mwema wa wanzibari upo mikononi mwake zaidi kuliko mtu mwingine yeyote."

Benefit of doubt, sasa hivi yeye ndiye mwenye mamlaka hata ya kupiga "ajua" uchaguzi mzima ikibidi.

Maridhiano yapi kama si kurudia uchaguzi katika mazingira yanayokubalika?

Kama unaamini Mwinyi anaweza kuitisha uchaguzi mpya Zanzibar na eti akashinda mwenye kustahiki kushinda basi cheki tena tafakari yako.

Mwinyi ni Nyapara wa kusimamia maslahi ya Tanganyika huko Zanzibar. Atatumika muda wake ukiisha Tanganyika itaweka nyapara mwingine. Na akijifanya kiti amekizoea sana na kisha kujaribu kwenda kinyume cha maslahi ya Tanganyika, atashughulikiwa kama alivyoshughulikiwa Jumbe.

Mwinyi ni kama TV tu, Remote iko Dodoma
 
Inaonekana Seif ameshakubali kuparamia fupa alilorushiwa na CCM, saivi wamebaki CDM peke yao wanapiga miayo, Tz kuna wajasiaria siasa na sio upinzani.
 
Mwinyi kuridhiana na upinzani na hata ikibidi kuendesha uchaguzi mpya utakaokuwa huru, wa haki na wenye kuaminika hakutampunguzia lolote. Zaidi ya kuwa kwa matokeo yeyote yale, yeye ndiye atakayekuwa mshindi.
Hivi nyinyi mtaamka lini muache kuota ndoto za mchana? C'mon dude, move on, imeshatoka hiyo, ikirudi pancha!
 
Kama unaamini Mwinyi anaweza kuitisha uchaguzi mpya Zanzibar na eti akashinda mwenye kustahiki kushinda basi cheki tena tafakari yako.

Mwinyi ni Nyapara wa kusimamia maslahi ya Tanganyika huko Zanzibar. Atatumika muda wake ukiisha Tanganyika itaweka nyapara mwingine. Na akijifanya kiti amekizoea sana na kisha kujaribu kwenda kinyume cha maslahi ya Tanganyika, atashughulikiwa kama alivyoshughulikiwa Jumbe.

Mwinyi ni kama TV tu, Remote iko Dodoma

Iko namna hii, kushinda draft hakuna maana ya kumzuia opponent kuingia kingi.

Kupambana na Mwinyi hakuna maana ya kumkomalia kuwa hawezi kushinda uchaguzi. Maneno matupu yaliwahi kuvunja mfupa?

Kuwasaidia wengine kufanya maamuzi magumu ndani ya wakati ngumu ni sehemu ya mchezo.

Amini nakwambia huwezi waona mataga na malb7 kwenye uzi huu. Ni msiba!

Kumbuka Karume against the odds alikubali SUK.
 
Hivi nyinyi mtaamka lini muache kuota ndoto za mchana? C'mon dude, move on, imeshatoka hiyo, ikirudi pancha!

It's known that it takes efforts to see beyond one's nose.

Wanasema kila king'aacho si dhahabu dude!
 
Inaonekana Seif ameshakubali kuparamia fupa alilorushiwa na CCM, saivi wamebaki CDM peke yao wanapiga miayo, Tz kuna wajasiaria siasa na sio upinzani.

Maridhiano si kuparamia mfupa jombi. Hadidu za rejea ndiyo ngoma!
 
Your are just hypothetical. All decisons are made in Dodoma. He is just a puppet. He can change nothing. All power is with Magufuli. Akileta foko, Kamati Kuu ya CCM inamwondoa kabla jua halijachomoza.

But Karume prevailed against all the odds. A puppet? Yes, it is known. But the kitchen is too hot for him.

Wakimwondoa Mwinyi kama Jumbe wakati kesha onyesha nia ni sawa.

Roma haikujengwa siku moja.

Hadi pale kitakapochemka sawa sawa ndipo chakula kitakapowiva!
 
Huyu kijana alikuwa ni waziri wa ulinzi, ndiye aliyewatuma askari wafanye kile kilichofanyanyika, dhuluma ya utu, udhalioishaji usi mithilika ili tu awe rais kwakuwa hakuwa na ushawishi.
Bosi wake nae akamletea Warundi ili waue na wachinje bila huruma Kila atakayekuwa akitamka neno haki.
Mnataka maridhiano ya kishetani, watu waridhie Nini?
Endeleeni kuogelea kwenye huo mfereji wa damu za watu wasio na hatia
 
1604823309371.png

But Karume prevailed against all the odds. A puppet? Yes, it is known. But the kitchen is too hot for him.

Wakimwondoa Mwinyi kama Jumbe wakati kesha onyesha nia ni sawa.

Roma haikujengwa siku mmoja.

Hadi pale kitakapochemka sawa sawa ndipo chakula kitakapowiva!
 
Zanzibar kila uchaguzi askari kutoka bara wanakuja wanaua ndugu zenu mpo mpo tu!
 
Huyu kijana alikuwa ni waziri wa ulinzi, ndiye aliyewatuma askari wafanye kile kilichofanyanyika, dhuluma ya utu, udhalioishaji usi mithilika ili tu awe rais kwakuwa hakuwa na ushawishi.
Bosi wake nae akamletea Warundi ili waue na wachinje bila huruma Kila atakayekuwa akitamka neno haki.
Mnataka maridhiano ya kishetani, watu waridhie Nini?
Endeleeni kuogelea kwenye huo mfereji wa damu za watu wasio na hatia

Mkuu ndiyo maana huwa kuna wokovu. Misahafu inasema hata ijapokuwa ni nyekundu kuliko bendera zitakuwa nyeupe kuliko theluji.

Hadidu za rejea sahihi zilizo ndani ya muda (mfupi) unaofahamika ni muhimu sana.

Mstari wa chini ni uchaguzi kurejelewa katika misingi huru, haki na yenye kuaminika.

Haiko rahisi, lakini Sheitwani akiyakubali hayo kwa nini wandugu?

Bila ya kuwasahau wahanga wote wa madhila yaliyotokea.
 

Yanaeleweka hayo mkuu.

Kaomba maridhiano, apewe hadidu za rejea badala ya terms and conditions. Bottom line:

1. Uchaguzi kurudiwa within a short and specified timeframe.
2. Waliothirika na madhila ya yaliyotokea waangaziwe vilivyo.

Ni wazi kuwa haitakuwa rahisi na hata mafanikio ni slim. Lakini something is better than nothing.

Avenue hii bado ilikuwa labda ndiyo iliyo bora kabisa iliyopo kwa sasa kwa pande zote mbili.
 
Back
Top Bottom