Hongera jukwaa la siasa kuinuka tena. Ama kwa hakika huu ni mwanzo mpya

Hongera jukwaa la siasa kuinuka tena. Ama kwa hakika huu ni mwanzo mpya

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Mimi binafsi na watu kama kina Pascal Mayalla ni watu ambao tulijiweka kando kabisa na mada za kisiasa baada ya uchaguzi mkuu 2020. Hata hivyo nilikuwa nikipita ndani ya jukwaa hili kimya kimya na ilibidi tuchangie pale tunapojisikia. Mimi ni moja wa watu humu ambaye huenda ningepotea kabisa kama mwendazake angebaki hadi 2025 na kisha kuongeza muda kama ilivyokuwa imepangwa.

Nina furaha jukwaa letu pendwa limerudisha afya. Nilipokuwa napita humu kimyakimya na kuangalia mada zilizopo siyo sawa na sasa. Tumepta afya na tujipongeze kwa hilo.

Aidha ni furaha sana pia hata wale MATAGA wameanza kurudi kwenye mstari na hivyo mada za kuchangamsha jukwaa zimewadia upya. Leo tunashuhudia hata kina Kigwangala wameamua kutema ndoano ya kuabudu, wananena ukweli.

Itoshe kusema ukweli kuwa Mungu anaipenda Tanganyika, anawaonea huruma watu wake ambao walilala na kuamkia vitisho vya "Ole wenu mjaribu" Ninasema Mungu ashukuriwe.

Kuimaliza 2025 na giza lillilokuwa linafuatia kabla ya muda wenyewe ni muujiza. Lolote litakalonenwa sasa ni kuwa ukweli ni kwamba kuna "relief" na inaonekana wazi wazi.

Hutaki unaacha!
 
Najiuliza hivi kwanini watu ni wabinafsi sana ?

kwanini watu hawana umoja?

Mfano mtu mmoja tu anatengeneza mtazamo wake binafsi wa kutawala watu milioni 60 na anafanikiwa kwa kutumia haohao watu anao watawala kuendelea kuwa na nguvu

Kama umewahi kuona simba mmoja katikati ya maelfu ya nyumbu na bado simba akawa ni shujaa kwa kufanya anavyotaka kwa mafanikio kabisa hiyo ikafanya uwadhara wanyama nyumbu inabidi waombe radhi kwa dhati kabisa kwa kuwa wale ni bora mara elfu kuliko sisi ambao kwa mamilioni yetu na utashi wetu lakini tumekuwa under control na kichwa kimoja tu
 
jiwe alipandikiza hofu na uoga kwa kila mtu.

kwa hapa jf hofu na uoga haukuishia tu kwetu sisi members bali mpaka watendaji wanaofanya kazi ya ku moderate mijadala (moderators).
 
Afadhali wewe ni kuanzia 2020. Mimi tangu 2015 niliachana na haya mambo ya hili jukwaa. Kwa kipindi chote sikuwahi kununua wala kusoma gazeti, kusikiliza habari au TV wakati wa taarifa ya habari au kusikiliza radio za kimataifa kama BBC, VOA na DW.

Kiufupi ilikuwa giza tupu. Watu tulikuwa tunalazimika kuabudu na kusikiliza kauli ya mtu mmoja.

Binafsi sina chuki na mwenda zake. Hiyo ilikuwa style yake ya Uongozi na aliichagua hiyo kwa kuwa aliona ndio inafaa.

Tumwache apumzike kwa amani.
 
Kwa katiba hii hata angetaka kulawiti wanaume wote hapa uwanja wa Mkapa angeweza, na bado wangetokea watu wakamsifia. Ndani ya hii miaka mitano nchi yetu ilikuwa mikononi mwako shetani.
Huu ni upuuzi na kukosa hekima.
 
P. L. O. Lumumba chungulia dirishani usikie wenye nchi wanavyosema kisha upime sifa zako kwa mwendazake, najua wewe ni mpita njia tu hauna cha kupoteza.

Labda na Mimi BAN za MODS zitapungua.
 
Bora mwendazake aondoke tu, kunamfumo fulani wa kijinga sana alikua anataka kuutengeneza nashukuru Mingi katuepushia hilo. Ilifikia mahali hata polepole anakuwa na kauli za kipuuzi kwa Wananchi. Mama pangua sukuma gang yote washamba watupu waliotaka kutuingiza shimoni
 
P. L. O. Lumumba chungulia dirishani usikie wenye nchi wanavyosema kisha upime sifa zako kwa mwendazake, najua wewe ni mpita njia tu hauna cha kupoteza.
Labda na Mimi BAN za MODS zitapungua.
Mtu mmoja hawezi kuwa mwenye nchi.
 
Back
Top Bottom