Hongera na pole Balozi Siwa. Je, utaiweza TISS au TISS itakuweza?

Hongera na pole Balozi Siwa. Je, utaiweza TISS au TISS itakuweza?

Je Unafikiri uteuzi DG MPYA TISS kila wakati una maslahi kwa USALAMA wa TAIFA?

  • Ndio

    Votes: 46 22.1%
  • Hapana

    Votes: 162 77.9%

  • Total voters
    208
Moyo wa nchi unapitia magumu mengi. Idara haijawahi kufanyiwa mabadiliko ya kiwango hiki. Tumuombee mzee Siwa airudishe nchi kwenye mstari. Hawa wazee wanaweza kumsaidia mama, let's hope tunaweza kuanza kuona mabadiliko
Mtu mwenyewe ni mzee aliyesahaulika kustaafu!! Ana zaidi ya miaka 64!! Naona angeteuliwa Dr Slaa tu kwenye kitengo hiki!! Hiki kitengo kinadai uzalendo wa hali ya juu sana!!
 
Paragraph ya kwanza umekataa kwamba hawakuhofia siri KUVUJA, kisha ukasema aliponzwa na kumpa siri nzito mzee Mrema [emoji16][emoji16][emoji16]naomba niseme tu kwamba huna AKILI
Jamaa alitaka kuwa mkurugenzi akihamishwa au kuondolewa kazini labda ili kuhofia asitoe siri ni kuwa auwawe au kuwekwa kizuizini,na akatolea mfano kifo cha nimran kombe .
Ndio nikamuelewesha yule kifo chake kilichangia kwa kuhofiwa alikuwa anampa mrema siri kipindi hicho.
 
Hivi ukiwa spy master huwezi kuzidiwa kete na kuomba umwachie mwingine ? Mbona kama mnawafanya hawa watu kama Roboti, hivi kuwa hawana mapungufu , au wao wanadunia yao ya kutokuwa na mapungufu au kukosea ?
 
Muu,sijasema usimtoe nimesema hao sio MADC ambao unawatoa tu.Spy Master Akizingu unampa kitu kizito kama Vladmir Puttin kwa yule boss wa Wagner.ILA hakikisha amezingua kweli sio Kakataa ujinga wako then useme itakuwa Rahisi kwako kumuondoa....
Mmmh utawafanyia hivyo wangapi ? Pia wateuliwa wote na watenguliwaji wanajua sheria na miiko ya kiapo Chao kabla na baada ya kazi hiyo na kwenda kinyume na hilo sheria zipo na nchi haijalala ujue hivyo.?
 
Muu,sijasema usimtoe nimesema hao sio MADC ambao unawatoa tu.Spy Master Akizingu unampa kitu kizito kama Vladmir Puttin kwa yule boss wa Wagner.ILA hakikisha amezingua kweli sio Kakataa ujinga wako then useme itakuwa Rahisi kwako kumuondoa....
Mmmh utawafanyia hivyo wangapi ? Pia wateuliwa wote na watenguliwaji wanajua sheria na miiko ya kiapo Chao kabla na baada ya kazi hiyo na kwenda kinyume na hilo sheria zipo na nchi haijalala ujue hivyo.?
 
Ukimsoma mleta mada analalamikia wakuu wa tiss wanatolewa kwa sababu ya fitna na majungu.

Anaweza akawa ni mmoja wa waathirika wa hilo jambo au akawa ni sehemu ya hilo tatizo la fitna na majungu.

Hii Taasisi tatizo lao wameathiriwa sana na siasa. Na aliyeharibu hii taasisi ni Rais wa Awamu ya 5.


Kuteuliwa kwa huyu kachero wa siku nyingi inaweza kuwa moja ya njia ya kulitafutia dawa hili suala.

All in all. Hakuna shida yeyote. Wakuu wa CIA wanabadilishwaga mara kwa mara na bado taifa la Marekani linaendelea kuwa imara bila kutetereka. General Patreous alikuwa mkuu wa CIA kwa miaka isiyozidi 3 na hata aliyemtangulia hakuzidi miaka 3.

Patreous sababu zake zinajulikana alinogewa na penzi akaanza kumshirikisha mchepuko mambo ambayo hakupaswa kushiriki. Vipi kuhusu huyu ambaye miezi 8 hajafikisha sababu ni ipi zaidi ya kutolinda maslahi ya mama na wajomba zake?
 
Patreous sababu zake zinajulikana alinogewa na penzi akaanza kumshirikisha mchepuko mambo ambayo hakupaswa kushiriki. Vipi kuhusu huyu ambaye miezi 8 hajafikisha sababu ni ipi zaidi ya kutolinda maslahi ya mama na wajomba zake?
Angalia orodha ya wakurugenzi wa CIA. Wengi wanakaa madarakani mwaka 1, miaka 2 hadi 3.
Screenshot_20230828_225426_Chrome.jpg
 
Angalia orodha ya wakurugenzi wa CIA. Wengi wanakaa madarakani mwaka 1, miaka 2 hadi 3. View attachment 2732480

Kuwalinganisha na huku kwetu ni uongo na si sahihi. Mbona hio list yako inaonekana wamekaa more than 1 year wengi wao na hata hao waliokaa muda mchache kuna sababu yakuondolewa kwao na ina mashiko zaidi.

Huku kwetu miezi 8 ? Hata acting Dg wanakaa zaidi ya hio miezi 8 sababu ya kutolewa huku ni ipi zaidi ya kutoendana na matakwa ya aliyeko juu.

Waliokaa madarakani mwaka 1 ni wawili tu na kuna sababu kwanini walikaa mwaka 1
 
D
Nyerere alikuwa kidume. Nakumbuka nikiwa mtoto. Jumbe akatua uwanja wa Musoma. Hata akusalimia kamati ya ulinzi mkoa aliwapungia tu mkono na kuingia garini kuelekea Butiama.

Nakumbuka alionekana mtu mwenye mawazo sana. Muda mwingi alikuwa amejiinamia. Japo na utoto wangu nikajiuliza kwanini huyu amekuja kwa ghafla na dhararu wakati ni Makamu wa Rais na pia Rais wa Zanzibar?
Kikawaida wakati ule kila kiongozi anae fika Musoma. Alipokelewa na chipukizi na kuvishwa skafu pia kukabidhiwa mauwa.

Nikiwa wakati huo miongoni mwa chipukizi wa kudumu kupokea wageni wa kitaifa na kimataifa. Nilisogea karibu na kamati ya ulizi na usalama ili kupata umbea.

Wengi hawakuwa na furaha, nilipata habari kuwa anaweza ondolewa au kuvuliwa Urais. Nilirejea zangu nyumbani. Kilichoendelea Butiama hakikuwa cha kufurahisha. Abdu Jumbe aliondoka kimya kimya. Na kurudi Dar. Na ilitangazwa kuwa si tena Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, na wala si Makamu wa Rais. Ndipo Ally Hassan Mwinyi akateuliwa.

Abdu Jumbe akazuiwa asiende popote. Na kubaki Kigamboni.
Nirudi kwenye mada, kiusalama hasa wa Ikulu na usalama wa Rais, si rahisi na si vizuri kubadili mkurugenzi wa usalama wa Taifa kama ilivyo kwa viongozi wa kisiasa.

Mkurugenzi wa Usalama ndiyo mtu wa kwanza wa karibu kabisa na Rais ambaye anajua mengi si tu usalama bali mfumo mzima wa nchi ulivyo na unavyo kwenda.
Mkurugenzi huyu chini yake ana ma RSO na ma DSO na watumishi wengine vificho kibao. Swali je ameimarikaje ktk kujenga mitandao yake kwa hawa walio chini yake?
Mkurugenzi anawatu wake mpaka huko nje ya nchi balozini. Anawatu wake jeshini, polisi, magereza, na ofisi za umma na hata mashirika binafsi.

Mkurugenzi wa Usalama si mtu mdogo. Uwezi fanya mapinduzi ktk nchi bila kushirikisha watu wa usalama na hasa walio Ikulu.

Hivyo Rais awe makini, aisondoe mtu kisa tu kakataa kukubaliana na unachotaka. Viongozi wetu wanajisahau kuwa Usalama hawapo kutekeleza matakwa ya Rais. Bali wapo kwa matakwa ya nchi na raslimali zake. Watakulinda kiongozi wa nchi kwa sababu upo kulinda maliasili za nchi na kutetea maslahi ya Taifa.

Unapokwenda kinyume na maslahi ya Taifa, au kukiuka Katiba. Wanauwezo wa kutumia namna yoyote kukumaliza au kukuondoa madarakani.

Jumbe aliagiza watu wa usalama kwa mamlaka yake. Lakini hao hao ndo walio mnyang'anya passport na kumuweka chini ya ulinzi. Na kuzuiwa kigamboni.

Rais uwezi ukapewa kila kitu cha TISS. Utapewa habari ile wao watakayo amua ujulishwe. Lakini wanapokuchunguza wewe Rais uwezi pewa taarifa zako. Hizo ni zao wao wenyewe.

Trump aliondolewa na haohao watu wa usalama.

Mama Rais wetu, nakuona unavyojimwambafai, ukidhani huko salama saana. Ukidhani waokupa ushauri wanajua kila kitu. Kuwa makini.

Mageuzi uletwa na watu wa chini kabisa hata kama ni wanajeshi uwa si wale wajuu wenye vyeo, bali wa ngazi ya chini. Na hao wakubwa wanapata info zote toka kwa hawa wa nchini.

Utawabadili sana hao wakurungezi wa TISS, ila fahamu humo humo TISS mama umechokwa. Kwanza unaupendeleo. Kuna namna fulani unawatu wako unao wapa kipaumbele. Kuna watu hawafurahii. Usije muondoa mtu amabe alikuwa kesha jenga mifumo yote vizuri, na pengine ndo angekuwa msaada wako mkuu. Unapo mtoa kuna baadhi watabaki na vinyongo na hasa waliokuwa wanamsujudu.

Si kweli kwamba mtu akistaafu au kuachishwa ndo kwaheri hapati info. Ha ha ha! Hawa watu kumbuka wamekaa wakajijenga wanaelewa nini kinaendelea. Uwezi koswa wafuasi.

Magufuli alipomuondoa Kipilimba roho tu iliniuma ghafla. Nikajiuliza huyu alikuwa tayari kesha jenga mizizi. Anae kuja ni mgeni kwenye ofisi. Mpaka aanze kujijenga, lolote au chochote chaweza tokea. Penye mabadiliko ndo mara nyingi kunakuwa na mianya ya chochote. Matokeo uwa ni baadae.
Dogo nimeacha kusoma makala yako maana si kweli kuwa Aboud Jumbe alivuliwa madaraka Butiama, bali Dodoma.
Aliyekuhadithia mwambie anyooshe maneno.
 
Back
Top Bottom