Hongera ndugu zetu Waislamu. Wakristo tujifunze kwa hili kutoka kwa ndugu zetu

Hongera ndugu zetu Waislamu. Wakristo tujifunze kwa hili kutoka kwa ndugu zetu

Hoja Mfu huwezi lazimisha au shawishi watu kufuata imani nyingine kisa kufunga. Kila mtu anafunga kwa imani yake alafu wewe ni mvaa kobazi ila hapa umeigiza tu.
We itakuwa ni shabiki wa Makolo tu.
 
Nadhani ile dhana ya ukombozi wa bure bila matendo ya Sheria inawapa kiburi Wakristo..
Pia influence ya mawazo ya kupinga amri za Mungu za kimagharibi, zinazomtoa Mungu kwenye maisha ya kawaida ya mtu imechangia sana!

Fundisho kama Kila kiingiacho hakimtii mtu unajisi..
Hivi seriously mtu anaweza kula hata nyama ya binadamu mwenzake kwa kuwa ni kiingiacho?
 
IMANI HIZI ZINATOFAUTIANA, UISLAM NA UKRISTO NI MBINGU NA ARDHI IJAPOKUWA WOTE TUNAWAZA KUWA KUNA SIKU YA KIYAMA/HUKUMU
hautanielewa, sema nategemea matusi na kejeli.
 
Hamna jambo jepesi duniani, wewe ulishawahi kuenda leba wakina mama wanavo jufungua ni shurt kichwa sehemu ndogo kichwa cha mtoto kikumbwa lazima apite tu
Shurti lazima iwepo ili jamii ikae kwenye mstari. Nilikua nafafanua tu sababu ya waislamu kuonekana wamenyoka zaidi ya wakristo. Wakristo nao waki-apply mbinu kama za waislamu mfano kupiga watu wanaokula kipindi cha kwaresma, kujilipua kwa mabomu ya kujitoa muhanga, kuanzisha vikundi vya kigaidi kushinikiza dini yao ifuatwe n.k uenda dini yao pia inaweza kufuatwa kwa utiifu
 
Kwaresma pia ipo kwenye vitabu vya wakatoliki, kwani wamesema vitabu vyao ni biblia tuu?
Then ondoa neno "Ukristo" kwenye uzi wako, sema Wakatoliki, Wakristo wana madhehebu mengi, RC being one of them so sio kila Mkristo ni Mkatoliki though Wakatoliki wote ni Wakristo, sijui ntakua nimekuchanganya?
 
Kumbe usisali jpili...wala usisherehekee krismas...lakini hata pasaka yenyewe...na hata calendar walioweka ni wakatoliki hawa hawa
Jumapili na Pasaka vipo kwenye Biblia, wanao pinga ni Wasabato pekee yao kwa kuipotosha historia, Christmas ni kweli kabisa, haina uhusiano na Ukristo
 
Covax toka lini ukawa mkristo? Acha kudanganya uma..sema umekuja hapa kuipa promo dini yako
 
Kumbe wakristo ni matajiri tu ndio wameoa[emoji2297][emoji2297][emoji2297]
Mkuu hapo taswira nzima ni kwamba gharama ya ndoa ya kiislamu ni ndogo sana kiasi kwamba kuoa ni kuepesi sanaa hata bila kupitisha michango kwa ndgu na marafiki.
 
Wasalaam

Ndugu zetu waislamu wameanza mwezi mtukufu tangu tar 2...wanatimiza moja kati ya nguzo muhimu katika imani yao

Chanda chema huvishwa Pete...tangu wenzetu wameanza mwezi mtukufu,mwamko unauona ni mkubwa sana,watu wa kada mbalimbali,wakubwa kwa watoto,hata wale tunaowaweka kwenye makundi hatarishi kama wahuni,nao wakionekana kujitahidi...heko

Wakristo tunaanza Mfungo Jtano ya majivu ya wiki hii (hasa wakatoliki)
Ajabu muitikio wa kufunga huwa mdogo...huwa tunasingizia kufunga sio mpaka chakula kufunga ni matendo mema...sote tunajua kufunga ni namna tunayouadhibu mwili kwa kuukatalia vikali katika yale ambayo ungedai ni haki yake kama...vyakula,vinywaji,ashki,mazoea tunayoyapenda mfano burudani na michezo

Haya wakati mwingine yametusonga kiasi tumekosa tafakari kwa Mungu...mungo husaidia waliowahi kufunga mashahidi

Tusifunge pale tunapokuwa tumebananishwa na hali ngumu kama uchumi,maradhi na kadhia mbali mbali kubwa au ndogo

Tuweke uwe ni utaratibu wa kujiunganisha na Mungu...kumbuka pamoja na dini zetu...bado binadamu anatakiwa ku connect kwa namna ya pekee na Mungu wake

Hongera waislamu wakristo tuige na tubadilike

NB:Shetani akimghiribu mtu anampa na kisingizio kuhalalisha ughiribu wake...wako watakuja na hoja...ooh waislamu hawafungi wanabadili ratiba ya kula...owk basi ninyi mnajua kufunga...tuwaoneshe wenzetu

Ukweli funga yao ni nzuri na Mungu anaipokea
Daah! Sawa mwarabu wa mahenge... yaani ni mkereketwa wa utamaduni wa waarabu zaidi ya waarabu wenyewe...
 
Tukisema ukweli bils kua na upendeleo kipi katika masuala ya dini, wakristo wameziidi hao wavaa kobazi (waislamu)
Kwenye mazishi wako excellent kwenye ndoa hata masikini muislamu ano oa, kwenye ibaada wana swali mara tano kwa siku, kwenye kutoa zakat masikini hujaa nyumba zao za ibaada kwa sababu wanajua wanatoa pesa na chakula, likija suala la kufunga mwezi wao hata muislamu mlevi mvuta bagi atafunga au atajificha,

je sisi wakuristo hao watu tuna wazidi nini kwenye dini? Au tuseme dini yao ina uhalisia.
Mkuu y kobazi
 
Kasilimu acha blah blah....
Wakristo hatuna mfungo wa pamoja, kila mtu anafunga kwa wakati wake na kwa hitaji lake. Hiyo kwa resma ni ya wakatoliki. Hamna maandiko yaliyoweka mfungo wa pasaka ni lazima
Na pasaka unayosherehekea utaratibu aliweka nani...au mna utaratibu wenu
 
Topic ni kufunga, tumefunga 40 January
Na pasaka mtasherehekea lini au september...unajua hata hiyo January wameweka wakatoliki?unaijua Gregorian Calender?au ndio ile nakunywa mchuzi wa nguruwe kipande cha nyama sili?
 
Kwani na sisi wakristo huwa tunafunga? Sisi si huwa tunapumzika kula baadhi ya vyakula? Mwaka jana rafiki yangu alifunga kula nyama tukakaribishwa sehemu wamepika sambusa za nyama yeye akatoa nyama zote ndani ya sambusa akala maganda ya nje ili asiharibu funga yake.

Sisi wakristo tukifunga tunafunga kwa imani ni kati yetu na mungu maana hata tukifunga huwezi kuona maana muda wote tunakula ila rohoni tumefunga
 
Mkristo halisi huwa hafungi kwa kujionesha kwa watu... Kwa taarifa yako kuna wakristo hutenga siku 7 za kufunga kila mwezi ndani ya miezi 12...

Hayo mamifungo ya kwaresma na Ramadan hufanywa na wanafiki mara moja kwa mwaka...

Utakatifu hsuji kwa mifungo kama hiyo ya kinafiki.

Bila shaka na wewe u mmoja wa wanafiki
'Wanafiki' mkuu unapata wapi ujasiri wa kuwaita wenzako wanafiki?ni mafundisho ya imani yako unayojivuna ni bora kuliko nyingine?kama haijakubadilisha na kuwa kama Kristo Yesu kweli...basi tuna mashaka...

Kristu hakuhukumu...

Yohana 8 | Biblia Kwenye Mtandao | Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

” Yesu akasema: “Wala mimi sikuhukumu kuwa na hatia. Ondoka uende zako ... Ninyi mnahukumu kulingana na mwili;+ mimi sihukumu mtu yeyote hata kidogo.+ ...
https://www.google.com/url?q=https:...Qjjh6BAgXEAE&usg=AOvVaw2VqQtH3MfkOVCfr7hHBoQd
Nani alikwambia wakatoliki wamekatazwa wasifunge hizo siku nyingine...
 
Na pasaka mtasherehekea lini au september...unajua hata hiyo January wameweka wakatoliki?unaijua Gregorian Calender?au ndio ile nakunywa mchuzi wa nguruwe kipande cha nyama sili?

Hapo unataka turudi kwenye mabishano ya dini na usahihi wa ukatoliki bla bla bla, I don’t have time for that nonsense
 
Back
Top Bottom